Yanga: Musonye atuombe radhi

Yanga: Musonye atuombe radhi

Lazima aumie,simba na yanga ni giants wa east Africa,halafu amepanic nini wakati kasema wameongezeka As Vita Motema Pembe na ZESCO,kombe lenyewe wanawania dola 30,000.
Mil kama 62,timu ikae Rwanda, mazoezi,gharama,na bado ikose hiyo hela na bado Club bingwa inawasubiri,nilitamani azam nao wangejito
Musonye lazima aumie.. tena ilitakiwa mashindano yake yawe hapa BONGO halaft timu zote zijitoe... tuone kama hata 9000 Mlangoni angepata
 
Mkuu pamoja na hali ya kipindi cha nyuma hatujawahi kupitisha bakuli... halafu yanga enzi za Manji mlijaza uwanja mkiambiwa bure bila kiingilio.
Simba mashabiki Timu ikiwa na hali mbaya mnaitelekeza,na Timu za Kkoo kama usipokuwa inafanya vizuri huwezi muona shabiki kiwanjani,sikweli kwamba uwanja ulijaa kwasababu ya manji bali timu bora,enzi izo Simba mnajifanya mnatumia vijana kumbe njaa mlikuwa mnajaza viwanja?
 
Kwanini awaombe radhi kwani hamkuwahi kufungwa goli 6-0 kule Morroco?
Kwani Mikia Fc hamjapigwa goli 15 mechi 3 ndani ya miezi 6.
Hiyo ulotaja ya mwaka 1998 tena Raja akiwa kwao ndo ya kutusumbua sisi?
Ninyi mmebakwa goli 5 5 mkaja na msemo kila mtu ashinde kwao mbona hamjiangalii?
 
Mkuu pamoja na hali ya kipindi cha nyuma hatujawahi kupitisha bakuli... halafu yanga enzi za Manji mlijaza uwanja mkiambiwa bure bila kiingilio.
Angalia timu ipi ilipata mapato mengi ya kiingilio kwa miaka mitatu iliyopita ndiyo utajua nani ana mashabiki wengi
 
Angalia timu ipi ilipata mapato mengi ya kiingilio kwa miaka mitatu iliyopita ndiyo utajua nani ana mashabiki wengi
Msimu uliopita

1.Simba
2.Yanga
3.Lipuli

Misimu miwili ya nyuma na msimu huu sijui
 
Hii kwa wanachama, mashabiki, wapenzi na wakereketwa wa Timu ya Yanga, mabingwa wa Ligi kuu bara mara 27.

Nicolas Musonye, umetukosea sana kwa maneno mabovu dhidi yetu, sababu za Yanga kujitoa ni dhahiri na haziepukiki.

Wito : Uombe radhi kwa Timu yetu kabla ya mwezi huu kuisha lasivyo sisi Yanga ukija Tanzania tutaitisha maandamano ya kukupinga kwa maneno yako mabaya na kejeli kama si dharau.
Huyo jamaa hata kwao kenya wamemchoka na ni wakumdharau tuu kwani tangu achukue uongozi CECAFA mvuto wote umepotea kutokana na tabia zake za kidikteta.
 
Huyo jamaa hata kwao kenya wamemchoka na ni wakumdharau tuu kwani tangu achukue uongozi CECAFA mvuto wote umepotea kutokana na tabia zake za kidikteta.
Ni mkora sana huyo Dingilai
 
Muda mfupi baada ya Yanga kutangaza kutoshiriki michuano ya kombe la Kagame, Katibu Mkuu wa Shirikisho la vyama vya Soka Afrika Mashariki (CECAFA), Nicholas Musonye amesema uamuzi huo wa Yanga hautaathiri chochote kwenye mashindano hayo kwa kuwa timu hiyo isingefanya maajabu

"Yanga ni timu ya ovyo. Hawakushiriki mashindano yaliyopita pia"

"Kumbuka wao sio mabingwa wa Tanzania, hatutawamiss. Acha wajitoe ndio maana wakishiriki mashindano ya CAF huwa wanafungwa mabao 5-0, 6-0, Hatujai kujiondoa kwao," Musonye amenukuliwa na mtandao wa GOAL

Kauli hiyo imewakera wadau wa soka nchini hasa Wanayanga kwani haikupaswa kutolewa na kiongozi wa ngazi ya juu kabisa kwenye soka la Afrika Mashariki

Wengi wamehoji kwa nini walitoa mwaliko kwa mabingwa hao wa Kihistoria kama walifahamu wasingeleta changamoto yoyote kwenye michuano hiyo?

Michuano ya kombe la Kagame imeendelea kupoteza umaarufu wake siku hadi siku kutokana na viongozi wa CECAFA kukosa ubunifu

Kwa miaka mingi zawadi zimeendelea kubaki hivyo hivyo huku waandaaji wake wakishindwa kuiboresha

Mfano mwaka huu ratiba ya michuano hiyo itaingiliana na michuano ya AFCON 2019 huko Misri

Ni wazi hakutakuwa na msisimko kwa kuwa mashabiki wengi watakuwa wanafuatilia michuano ya AFCON
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom