Kanifurahisha jinsi alivyofafanua suala la mahakama ya kadhi kuwekwa kwenye katiba ya Kenya,amesema Mombasa ilikuwa chini ya Sultani wa Zanzibar,Waingereza walipoitaka kwa ajili ya Bandari,walifanya makubaliano na Sultani akawapatia kwa Masharti kuwa kamwe wasifute mahakama ya kadhi,hivyo kaonya wanaotaka mahakama hiyo kwa Tanzania kwa kutolea mfano katiba ya Kenya waijue kwanza historia kwani kwa Tanzani ni ngumu kwani Waromani nao watadai mahakama ya canon laws ambayo nayo ikikubaliwa ni ngumu kwa Tanzania kwani rufaa za kesi ni kwa Papa huko Vatican,pia na dini nyingine zote nazo zinaweza kudai mahakama zao,hivyo ameshauri ilo suala lisiwepo kwenye katiba.