Yanayojiri bungeni Dodoma leo 08 Julai 2015

Yanayojiri bungeni Dodoma leo 08 Julai 2015

Mhe. Kigwangallah ameomba mwongozo wa mwenyekiti bungeni leo,akimwomba aitishe kikao cha kamati ya uongozi na kamisheni ya bunge ili kuona namna ya kuliepusha bunge na aibu inayoweza kutokea kesho wakati wa kuhitimisha na kuvunja bunge,kutokana na minong'ono iliyosambaa hapo bungeni.

Mhe.kigwangallah hakutaja minong'ono hiyo wala kusema ni aibu gani itakayotokea,mimi pia taarifa hii ni mpya kabisa masikioni mwangu,naomba wadau wanaoujua watujulishe ili tuchangie mawazo yetu.
 
Minong,ono ni aibu ya rais kuvunja bunge alilozindua likiwa na wabubunge 350 anavunja likiwa na wabunge 40
 
Sasa wanaogopa nini?Wangemshauri Bi Mkora kuifuta ile adhabu yake immediately baada ya kuitoa.Sasa wamepitisha madudu ndiyo wanawakumbuka?

Pamoja na matusi yote waliyowatukana wapinzani wakirudi hao wapinzani nitawaona wapumbavu kabisa.
 
Watu wengi hawaelewi nini maana ya kofi kwenye mishahara ya wafanyakazi.Kwa mfanyakazi anayelipwa shilingi 720,000 au zaidi kodi ni 30%.Mshahara wa milioni moja unatakiwa ukatwe kaki 3 za kodi.Kodi inayopunguzwa kila mwaka,mfano mwaka huu kutoka 12% hadi 11% ni kwa wale wanaolipwa mshahara usiozidi laki 360.Ikiwa na maanda kuwa watapata unafuu wa TSh 1,900 kila mwezi.Sasa jiulize unafuu huo kwa wafanyakazi uko wapi?Serikali basi ipunguze 30% angalau hadi 25% au 20%
 
Kama serikali inatia aibu, kuna ajabu gani kwa bunge kutia aibu
 
Mbali na makampuni ya simu, kwani serikali ikiamua kukata 20% tu ya matumizi ya magari (V8's) si itaokoa mara hamsini zaidi ya hizi!? (Kumbuka kuna ripoti ilisema magari tu yanatumia trillion 5). Alafu anavyoongea utadhani yeye sio mfanyakazi wa serikali na hiyo kodi haimhusu!
Ni bora kuwa na mawaziri kwa profile zao kama rasimu ya Warioba inavyotaka badala ya hizi nafasi kutumiwa kuzawadiwa na kuponya magomvi ya familia.

Hawa jamaa wamechoka dawa pekee iliyobaki ni kuwapiga chini tu Oktoba.
 
UKAWA wapo wame mtuma Leticia awawakilishe na ameuliza swali kwa niaba ya UKAWA!
Sasa lile tamko la Mbowe lilikuwa la nini wakati kuna mbunge wa Chadema yupo bungeni akiendelea na vikao.
 
sijui kesho kutatokea nini kuna thread nimeisoma inamuhusu membe na pm
 
Sasa wanaogopa nini?Wangemshauri Bi Mkora kuifuta ile adhabu yake immediately baada ya kuitoa.Sasa wamepitisha madudu ndiyo wanawakumbuka?

Pamoja na matusi yote waliyowatukana wapinzani wakirudi hao wapinzani nitawaona wapumbavu kabisa.

Majembe hayawezi kulamba matapishi, hiyo ni aibu yao
 
Kwani adhabu ya kutohudhuria vikao vitano na vyote vilivyobaki imeisha?
 
Kuna wabunge kadhaa wanataraj kujivua uanachama wa ccm

Sty tuned..

Aibu nyingine.n.raisi kufunga bunge bila upinzani..hahaaaaa
 
... Waendelee Na Bunge Lao Wenyewe, Ukawa Wanawahusu Nin
 
kunamfanyakazi kila mwezi anakatwa 400000/= ni hatari ccm.tukutane oktober

Enzi nipo mtumwa,kwa mwaka nilikuwa nakatwa kodi kati ya 4.2m mpaka 5.0m wakati mkinga wa k/koo mwenye ghorofa tano analipa laki 7 kwa mwaka...mie nakatwa fedha kabla hata sijanunua sabuni wakati mkinga anakatwa ile faida baada ya kutoa kila kitu..serikali iangalie hilo.
 
Back
Top Bottom