Wamwshindwa kuweka mpango mathubuti ya kukusanya kodi toka kwa wafanyabiashara ambao ndio wenye kipato kikubwa,serikali yetu imekuwa ikiwagandamiza wafanyakazi zaidi kwa sababu wanakatwa toka kwenye source na hawana uwezo wa kutoa rushwa ili kodi ipunguzwe. Walichotakiwa kufanya ni kuweka mpango ulio bora na watoe elimu kwa umma na wasimamie kodi katika kuleta maendeleo na pia wapunguze warsha,semina na safari zisizokuwa na tija kwa taifa kuliko kujipangia posho ovyo ovyo na hiki ndo kinasababisha wafanya biashara kupiga dili na wafanya kazi wa TRA. Wafanyakazi hawana uwezo wa kugomea kodi lakini wananyonywa mno na serikali na hawana la kufanya. Kodi ni sawa kabisa kwa mfanyakazi kukatwa lakini si kwa kiwango hicho,mafanyakazi wa Tanzania mwenye Gross salary ya 6,000,000/=, kodi anayolipa kwa mwezi ni kodi inayolipwa na mfanya biashara mwenye mtaji wa milioni zaidi ya 100 kwa mwaka!
Wafanyakazi hawajielewi ila siku wakitoka usingizini watasema NO!!!