Yametimia: Tulichokisema...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
NIRA DHIDI YA WAANDISHI IVUNJWE - UHURU WETU ULINDWE
(Dhidi ya Mpango wa Serikali kulifungia/kuliadhibu Gazeti la MwanaHalisi)


Na. M. M. Mwanakijiji

Kwa mara nyingine tena serikali ya Kikwete inakabiliwa na changamoto moja kubwa nayo ni kama itaweza kuzikunja kucha zake ambazo tayari zimenoloewa, kutolewa na kunyoshwa kama simba aliyeona mawindo. Bahati mbaya tumeshawahi kuwepo hapa huko nyuma.

Lakini safari hii inaonekana hakuna mtu mwenye uwezo wa kutuliza wale wenye vichwa vya "moto" ambao wamedhamiria kutoa funzo moja, la wazi ambalo litakuwa ni onyo kwa vyombo vingine vinavyodiriki kuvuka "mpaka" na kuvunja sheria ya magazeti ya mwaka 1976.

Vyanzo vya uhakika kabisa vimedokeza kuwa Serikali imrkusudia kulifungia gazeti la MwanaHalisi kutokana na habari yake ya Jumatano iliyopita kuwa na mambo ya kichochezi, kichonganishi na ambayo haina maslahi ya umma bali iliyokusudia kuleta wasiwasi na kutishia hali ya "amani na usalama". Mpango huu kwa hisia zangu (kutokana na matakwa ya kisheria) hauwezi kukamilika hadi Gazeti la Serikali litoke na sina uhakika toleo jipya linatakiwa kutoka lini.

Sheria hiyo inaeleza wazi katika Ibara ya 31 kuwa kuna makosa yanayohusu uchochezi na kwa tafrisiri hiyo mtu atakuwa ana nia ya uchochezi endapo atafanya kati haya haya (kitu ambacho Mwanahalisi itatuhumiwa)

31.-(l)
(a) kuchochea. chuki au ufidhuli au uasi dhidi ya Jamhuri ya Muungano
au Serikali yake; au
(b) kuchochea wakazi wowote wa Jamhuri ya Muungano kujaribu
kuleta mapinduzi ya kijambazi ya jambo lo lote katika Jamhuri
ya Muungano, lililowekwa kwa mujibu wa Sheria;
(c) kuchochea chuki au ufidhuli au uasi dhidi ya utekelezaji wa
haki katika Jamhuri ya Muungano;
(d) kuchochea manung'uniko na chuki au uasi miongoni mwa wakazi
wa Jamhuri ya Muungano;
(e) kuchochea chuki na uhasama baina ya vikundi mbali mbali vya
wakazi wa Jamhuri ya Muungano.QUOTE]

Lakini ndani ya sheria hiyo hiyo ibara inayofuatia inasema kuwa mtu hatakuwa na hatia ya kuwa na nia ya uchochezi endapo atafanya mambo yafuatayo (Ibara 31):

(a) kuonyesha kwamba Serikali imepotoshwa au imekosea, katika shu-
Auli yake yo yote-, au
(b) kuonyesha makosa au hitilafu katika Serikah au Katiba ya Jamhuri
ya Muungano, kadri mambo hayo yalivyo kwa mujibu wa
Sheria, au katika Sheria za nchi au katika utekelezaji wa haki,
kwa madhumuni ya kusahihisha au kurekebisha makosa hayo au
hitilafu hizo; au
(c) kuwashawishi wakazi wo wote wa Jamhuri ya Muungano kujaribu,
kwa njia zilizo halali kwa mujibu wa Sheria, kuleta mabadiliko
ya jambo lo lote lililowekwa kwa mujibu wa Sheria;
(d) kuonyesha, kwa madhumuni ya kutaka yaondolewe, mambo yo
yote yanayochochea au yanayoweza kuchochea chuki na uhasama
baina ya vikundi mbali mbali vya wakazi wa Jamhuri ya
Muungano.

Sasa hapa unakabiliwa na tatizo. Kama mtu anafanya mambo ya ibara ya 31 ambayo yanatajwa kuwa ni halali lakini matokeo yake (kwa ni njema kabisa) yakasababisha hisia za chuki dhidi ya serikali au dharau kama ilivyo ibara ya 30 itakuwaje? Tutajuaje kuwa mtu anayefanya jambo hilo hana lengo baya hata kama analofanya ni halali? Sheria yetu mbovu ya magazeti inajichanganya kwa kujaribu kutoa jibu hapa (31:3)
(3) Katika kufikiria kama jambo lo lote lilitendwa, maneno yo yote
yalitamkwa au hati yo yote ilichapishwa na kutangazwa, kwa nia ya
kuchochea uasi, kila mtu atahesabika kuwa. ana jukumu kamili juu ya
matokeo yote ya vitendo vyake vyote vya makusud[/U]

hilo la kusema maneno hayo ni kupanua wigo wa uwezo wa serikali kufahamu nia ya mtu kiasi kwamba hakuna mazingira yoyote yale ambayo mtu anaweza kusema au kufanya kitu ambayo hayataangukia kwenye "vitendo vyake ya makusudi". Ni wangapi kati yetu wanafanya vitendo vya makusudi (visivyo vya bahati mbaya)?

Lakini kwenye suala la Mwanahalisi madai yatakayotolewa yataangukia katika vipengele hivyo lakini ni Ibara ya 36 ndiyo naamini itatumiwa kulifungia gazeti hilo au hata kuchukua hatua zaidi za kisheria. Ibara hiyo inasema hivi:

Mtu ye yote atakayetangaza au kueneza habarl yo yote
ya uwongo, Uzushi au taarifa ambayo yaweza kuwatia watu woga na
wasi wasi au kuchafua amani katika nchi atakuwa ametenda kosa na
akipatikana na hatia mbele ya mahakama atapaswa kuadhibiwa kwa
kutozwa faini isiyozidi shilingi elfu kumi na tano au kufungwa gerezani
kwa muda usiozidi miaka mitatu au kupewa adhabu zote mbili
(2) lwapo mtu ye yote atashtakiwa kwa kosa chini ya kifungu cha
(1) mahakama itabidi ikubali kuwa kuna utetezi wa kutosha ikiwa
mshtakiwa atathibitisha kwamba kabla ya kutangaza au kueneza habari
au taarifa ya aina iliyoelezwa katika kifungu cha (1) alichukua hatua
madhubuti za kuhakikisha ukweli wa mambo na kwamba matokeo
yake yalimfanya asadiki kwamba habari au taarifa hiyo ilikuwa ya kweli

Katika hilo la ibara ya 36 inaonekana suala hapa ni kwenda mahakamani. Lakini serikali haitaenda mahakamani kufungua mashtaka ya uchochezi. Wao watatumia kipengele cha sheria ambacho kinampa madaraka makubwa Waziri wa Habari.

Lakini kinachotisha zaidi siyo tu ukali wa sheria hiyo lakini zaidi uwezo wa Waziri mwenye dhamana ya Habari kufungua magazeti. Hebu tuangalie sheria hii inatoa nguvu za namna gani basi? Nitaweka ibara yote hapa:

25.-(l) Waziri akiona kwamba kwa ajili ya manufaa ya umma au
kwa ajili ya kudumisha amani na usalama inafaa afanye hivyo
aweza kutoa amri na kuitangaza kwenye Gazeti la Serikali ambayo itaeleza
kwamba gazeti lililotajwa katika amri hiyo litakoma kutolewa
tangu siku (ambayo katika fungu hili itaitwa ''tarehe ya kuanza kutumika'')
itakayotajwa katika amri hiyo.

(2) Kila amri iliyotolewa kwa mujibu wa kifungu cha (1) itataia-
(a) jina la gazeti linalohusika na amri hiyo;
(b) majina ya mwenye gazeti, mchapishaji na mtoaji wa gazeti hilo:
Isipokuwa kwamba hakuna amri kama hiyo iliyolewa kwa
mujibu wa kifungu cha (1) itakayokuwa batu kwa sababu ya
kukosa kutoa maelezo au kutoa maelezo yasiyo sahihi kuhusu mwenye
gazeti, mchapishaji au mtoaji wa gazeti au ye yote kati yao.
(3) Iwapo amri imetolewa kwa mujibu wa kifungu cha (1) kuhusu
gazeti lo lote-

(a) mtu ye yote ambaye, tangu tarehe ya kuanza kutumika. atachapisha
au kutoa au kuagiza lichapishwe au litolewe gazeti lo
lote lililotajwa katika amri hiyo, atakuwa ametenda kosa na
akipatikana na hatia mbele ya mahakama atapaswa - kuadhibiwa
kwa kutozwa faini isiyo,zidi shilingi elfu ishirini au kufungwa
gerezani kwa muda usiozidi miaka minne au kupewa
adhabu zote mbili pamoja;

(b) mtu ye yote ambaye, tangu tarehe ya kuanza kutumika, atauza,
atachuuza, atagawa, kuweka au kuagiza iwekwe hadhara ya
watu nakala yo yote au sebemu ya nakala ya gazeti lililotajwa
katika amri hiyo, iwe nakala hiyo au sehemu yake ilichapishwa
au kutolewa kabla ya tarehe ya kuanza kutumika au
sivyo, atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia mbele
ya mahakama atapaswa kuadhibiwa kwa kutozwa faini isiyozidi
shilingi elfu kumi au kutungwa gerezani kwa muda usiozidi
miaka miwili au kupewa adhabu zote mbili pamoja.

(4) Kwa madhumuni ya fungu hili ''hadhara ya watu'' ina maana
ya kawaida ya maneno hayo na pia ifahamike kuwa ni pamoja na
njia yo yote ambayo watu wana haki ya kupita, jengo, mahali au
chombo ambacho watu wana haki ya kukitumia ama bila masharti
au kwa malipo, na jengo lo lote au mahali po pote panapotumiwa
na watu kwa ajili ya ibada au mikutano au mahakama ambayo
watu wote wanakuwa huru kuhudhuria.

Katika ibara hiyo kuna mambo matatu ya kuangalia kwa ukaribu.

Kwanza, katika kufungia gazeti Waziri haitajiki kwenda mahakamani kupata amri ya mahakama kufanya hivyo. Yeye kutokana na wadhifa wake na kwa mujibu wa sheria hiyo ana uwezo wa kulifungia gazeti lolote alimradi kwamba "akiona kwamba kwa ajili ya manufaa ya umma au kwa ajili ya kudumisha amani na usalama inafaa afanye hivyo"

Hii ina maana kuwa katika suala la MwanaHalisi manufaa ya Umma ni nini? Tunapata kupata jibu kidogo katika majibu ya serikali (kupitia ndugu yetu Salva) kuwa Rais Kikwete anapendwa sana na anafanya mambo mazuri yanayosifiwa ndani na nje ya nchi yetu. Ina maana ya kuwa kama Mwanahalisi wameandika kitu ambacho kitamharibia sifa Rais na kumfanya asionekane bora au anayefaa au aliye makini basi "manufaa ya umma" yanadhurika! Yawezekana kitu kama hicho hicho ambacho ni wao wanajua manufaa ya umma ni nini hasa. Na katika hili wanaweza kuleta sheria za Usalama wa Taifa ya 1970, ya Taasisi ya Kijasusi ya 1996, Uhujumu uchumi na hata wakajaribu ile ya Madaraka ya Rais wakati wa Dharura ya 1986.

Kimsingi "manufaa ya umma" kinaweza kuwa kitu chochote cha kuwafurahisha watawala!

Jambo la pili la kuona katika ibara hiyo ya 25 ni kuwa ili wafikishane mahakamani ni mpaka pale ambapo Gazeti (Mwanahalisi katika mjadala wetu huu) iamue kukaidi agizo hilo la Waziri na kuchapisha gazeti hilo licha ya kufungiwa baada ya kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali (kitu ambacho nadhani wanakisubiri na sina uhakika linatoka lini). Endapo watatangaza (kumbuka kuwa Waziri hawezi kutangaza simamisho hilo hadi pale litangazwe kwanza kwenye gazeti la serikali vinginevyo litakuwa ni agizo batili) basi Mwanahalisi watakabiliwa na kukubali au kukaidi.

Kwa maneno mengine MwanaHalisi haliwezi kwenda mahakamani kupinga agizo la Waziri wa habari kwani Sheria haitoi nafasi hiyo (wanaweza kujaribu) kwani uwezo wa kulifungia gazeti uko mikononi mwa Waziri. Na zaidi ya yote Ibara ya 52 inasema hivi.

Hapana mtu ye yote anayeweza;kufungua mahakamani shauri lo
lote ]a madai dhidi ya mtumishi wa Serikali ye yote kwa ajili ya
jambo lo lote ambalo mtumishi huyo ametenda au ameacha kutenda
katika kutekeleza madaraka yake chini ya Sheria hii.

Wakikaidi serikali itavamia jengo la Mwanahalisi kuchukua vitu mbalimbali (kama ushahidi) na kuwapeleka mahakamani au kuwasumbua tu kama walivyofanya mapema mwaka huu.

Hili naamini ndilo linalopaswa kutokea kwani wakienda mahakamani ni serikali itatakiwa ithibitishe kuwa kilichoandikwa ni uchochezi, uchonganishi au kwa namna yoyote ile inavunja sheria ya 1976. Lakini uzuri wa kufikishana mahakamani ni kuwa kwa mara ya kwanza (katika kumbukumbu yangu) katika miaka ya karibuni sheria hii itawekwa kizimbani na uhalali wake Kikatiba utakuwa matatani hasa ukizingatia hili jambo la tatu nitakalolisema. Hivyo njia pekee ni kwa MwanaHalisi kukaidi agizo la kufungiwa litakalotangazwa kwenye Gazeti la Serikali.

Jambo la tatu ni kipengele cha mwisho kinachojadili "hadhara ya watu". Maana ya neno hilo kwa mujibu wa sheria hii ni mahali popote pale ikiwemo "jengo lo lote au mahali po pote panapotumiwa na watu kwa ajili ya ibada au mikutano au mahakama ambayo watu wote wanakuwa huru kuhudhuria" Hii ina maana gani?

Kwa kifupi baada ya Mwanahalisi kufungiwa ukikutwa na gazeti hilo (toleo la ukaidi) mahali popote iwe msikitini, kanisani, mahakamani au mahali popote pale ambapo panakidhi maana yao ya hadhara basi utakuwa na makosa na utatakiwa kulipa faini au kutumikia miaka 2 jela au vyote viwili.

Ninachosema ni kuwa endapo Serikali itakunjua kucha zake na kuwaparua mwanaHalisi, itakuwa ni wakati mbaya zaidi katika historia yetu ambapo vyombo vya habari kwa mara nyingine vinalazimika kufungiwa. Magazeti yamefungiwa huko nyuma mara nyingi tu na MwanaHalisi halitakuwa la kwanza.

Lakini magazeti hayo yote huko nyuma yamekuwa yakikubali amri hiyo bila kufanya civil disobedience. Ni matumaini yangu kuwa vyovyote wanavyotaka kufanya serikali wafanye, lakini MwanaHalisi litatoka hata kama itabidi litoke kwa njia nyingine kabisa lakini toleo hilo litatoka pamoja na hilo kufungiwa na kama kuna kwenda mahakamani basi wataenda mahakamani. Lakini hatuwezi kamwe kuacha sheria hii iendelee kuwepo na kuwa kama nira dhidi ya vyombo vya habari. Siyo sheria hii tu bali pia ya madaraka ya Rais wakati wa dharura ambayo sitoshangaa kama itatumiwa Tarime Jumapili , kama walivyoitumia Pemba 2001.

Tunatoa wito kwa serikali kuzikunja kucha zake, kukaa chini na kuzungumza vinginevyo badala ya kumuacha Waziri alifungie gazeti basi waende kwanza mahakamani kutoa shitaka dhidi ya MwanaHalisi kwa kutumia sheria hiyo au yoyote waliyonayo.

Hatuwezi kukaa kama watumwa ambao dakika yeyote nira ya mabwana zetu itashushwa kwenye shingo zetu. Endapo gazeti hilo litafungiwa kwa sababu Waziri kasema hivyo, ninaahidi kukaidi amri hiyo kwa njia ninazojua mimi.
 
Hivi kwani uamuzi wa kufungia gazeti ni wa mwisho? Aliyefungiwa hawezi kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo? Au kushitaki mahakamani kuwa kufungiwa kwake hakukuwa kwa haki?

Mimi naona Mwanahalisi asilie kufungiwa maana hiyo sasa itakuwa ndiyo fursa yake ya kulipeleka hilo suala mahakamani, ambako mambo yote yatawekwa hadharani.
 
Nimekupata vizuri mkuu, sina la kuongeza ngoja nisubiri hilooo tangazo la serikali
 
Hivi kwani uamuzi wa kufungia gazeti ni wa mwisho? Aliyefungiwa hawezi kukata rufaa dhidi ya uamuzi huo? Au kushitaki mahakamani kuwa kufungiwa kwake hakukuwa kwa haki?

Mimi naona Mwanahalisi asilie kufungiwa maana hiyo sasa itakuwa ndiyo fursa yake ya kulipeleka hilo suala mahakamani, ambako mambo yote yatawekwa hadharani.

hakuna rufaa. Hadi wakaidi amri ya kuchapisha kwani Waziri halazimiki kutoa maelezo ya kwanini amelifungia gazeti hilo. Hivyo hata kina Kubenea wakifungiwa wakienda mahakamani kesi hiyo itatupwa nje (without merit). Naamini njia pekee ni wao kukaidi amri hiyo au kufungua kesi ya Kikatiba dhidi ya sheria iliyotumika kuwafungia rather than kupinga uamuzi wa wao kufungiwa.
 
hakuna rufaa. Hadi wakaidi amri ya kuchapisha kwani Waziri halazimiki kutoa maelezo ya kwanini amelifungia gazeti hilo. Hivyo hata kina Kubenea wakifungiwa wakienda mahakamani kesi hiyo itatupwa nje (without merit). Naamini njia pekee ni wao kukaidi amri hiyo au kufungua kesi ya Kikatiba dhidi ya sheria iliyotumika kuwafungia rather than kupinga uamuzi wa wao kufungiwa.
Hatari ya kuchukua option ya kukaidi amri ni kwamba watashitakiwa kwa kosa lingine (la kukaidi amri), ambalo sijui watawezaje kujitetea kwa kumwaga habari tunazotamani kusikia bila kukiri kwanza kosa hilo (ambalo nadhani lina adhabu). Hii ndiyo shida tuliyo nayo kwa kuzinyamazia sheria kandamizi hadi pale zinapotuumiza, maana sheria kama hii ilipaswa kuwa imepingwa mahakamani tangu kitambo, maana inakiuka katiba na haki ya binadamu ya natural justice, kusikilizwa kwa haki kabla ya kuhukumiwa (Tuache hili, ni la siku ingine). Hakuna option bora kuliko hiyo?
 
Hatari ya kuchukua option ya kukaidi amri ni kwamba watashitakiwa kwa kosa lingine (la kukaidi amri), ambalo sijui watawezaje kujitetea kwa kumwaga habari tunazotamani kusikia bila kukiri kwanza kosa hilo (ambalo nadhani lina adhabu). Hii ndiyo shida tuliyo nayo kwa kuzinyamazia sheria kandamizi hadi pale zinapotuumiza, maana sheria kama hii ilipaswa kuwa imepingwa mahakamani tangu kitambo, maana inakiuka katiba na haki ya binadamu ya natural justice, kusikilizwa kwa haki kabla ya kuhukumiwa (Tuache hili, ni la siku ingine). Hakuna option bora kuliko hiyo?

Hapana wakikaidi amri sheria inatoa defence. Wakikaidi amri watailazimisha serikali kuwashtaki kwa kutotii amri ya Waziri na hivyo kuvunja sheria ya magazeti ya 1976. Wao wataenda mahakamani watasema sheria (kipengele) kinachompa Waziri mamlaka hayo makubwa ni kinyume na Katiba na hivyo kuligeuza hilo suala kutoka kuwa la kihalifu na kuwa la Kikatiba. Katika misingi hiyo Mahakama itatakiwa kuamua kama sheria iliyotumika haiko too vague kiasi kwamba Waziri anaweza kufanya lolote lile bila checks ya mahakama.

kwa hiyo kwangu sihofii sana hilo la kushtakiwa kwani ndio mtindo wanaotumia sana ACLU hapa kutafuta kile wanachokiita 'trial cases". Nadhani hii itakuwa ni trial case nzuri ya kupima mipaka ya uhuru wa habari. So I really would like to see the gvt wanalifungia MwanaHalisi kwa sababu likitolewa nakala yake na kuwekwa JF na Watanzania walioko nyumbani wakalisoma bila kulichapisha (online) na wakalisambaza bila kulipiga chapa (online) watakuwa wanavunja sheria ya kukaidi agizo hilo. Itakuwaje kama Watanzania hao wako nje ya nchi na ni anonymous?
 
Hapana wakikaidi amri sheria inatoa defence. Wakikaidi amri watailazimisha serikali kuwashtaki kwa kutotii amri ya Waziri na hivyo kuvunja sheria ya magazeti ya 1976. Wao wataenda mahakamani watasema sheria (kipengele) kinachompa Waziri mamlaka hayo makubwa ni kinyume na Katiba na hivyo kuligeuza hilo suala kutoka kuwa la kihalifu na kuwa la Kikatiba. Katika misingi hiyo Mahakama itatakiwa kuamua kama sheria iliyotumika haiko too vague kiasi kwamba Waziri anaweza kufanya lolote lile bila checks ya mahakama.

kwa hiyo kwangu sihofii sana hilo la kushtakiwa kwani ndio mtindo wanaotumia sana ACLU hapa kutafuta kile wanachokiita 'trial cases". Nadhani hii itakuwa ni trial case nzuri ya kupima mipaka ya uhuru wa habari. So I really would like to see the gvt wanalifungia MwanaHalisi kwa sababu likitolewa nakala yake na kuwekwa JF na Watanzania walioko nyumbani wakalisoma bila kulichapisha (online) na wakalisambaza bila kulipiga chapa (online) watakuwa wanavunja sheria ya kukaidi agizo hilo. Itakuwaje kama Watanzania hao wako nje ya nchi na ni anonymous?

Kwa ufafanuzi huo mkuu nakubaliana na maelezo na pendekezo lako. Sasa nasubiri kuona atakayefikishwa kwenye "check mate!"
 
Hatuwezi kukaa kama watumwa ambao dakika yeyote nira ya mabwana zetu itashushwa kwenye shingo zetu. Endapo gazeti hilo litafungiwa kwa sababu Waziri kasema hivyo, ninaahidi kukaidi amri hiyo kwa njia ninazojua mimi.[/[/COLOR]QUOTE]

Mkakati ulipo ni kuhakikisha kuwa kila mwenye kufungua mdomo au kunyoosha kidole dhidi ya uovu wa wakubwa anaonja maumivu.Mwanahalisi wamewindwa kwa muda sasa na inaelekea wamepata pa kugonga nyundo sasa.

Hata hivyo tuna changamoto kubwa ya kuhakikisha moto uliowashwa na wanamapinduzi hauzimwi na mafisadi wachache wasiowaza kesho ya watanzania itafananaje
 
Last edited:
Pengine huu ni wakati mwafaka wa kuangalia how weak/ineffective our civil society is.Mapungufu ya sheria hiyo yamekuwa yakijulikana for ages,so why wait until gazeti likumbwe na misukosuko ndio zije fikra za kuipinga sheria hiyo dhalimu?Yaleyale ya serikali kwamba hadi janga litokee ndio ichue "hatua za makusudi" badala ya "hatua za tahadhari."

Kiungo kati ya state na society ni kama hakipo.Tuna lundo la NGOs za kutetea wanyonge au waathirika wa utawala mbovu wa sheria lakini imekuwa kama desturi kwamba zinasubiri litokee la kutokea ndio zilipuke.Hivi hilo Jukwaa la Wahariri halioni kwamba sheria hiyo ya habari inaweza kulifanya lisi-exist (i.e. siku mashetani ya serikali yatakapoamua kufungia vyombo vya habari ambavyo wahariri wake ndio wanaounda jukwaa hilo)?Nimesoma mahala flani Jukwaa hilo linailalamikia serikali na kudai haina nia nzuri.Tangu lini serikali inayokumbatia ufisadi ikawa na mahusiano mazuri na vyombo vya habari?

Serikali inaweza kucheza mchezo mchafu zaidi kwa kutumuia sheria hiyhiyo dhalimu,nayo ni kupelekea kifo cha asili kwa gazeti hilo.Yaani Waziri alifungie,Mwanahalisi wakaidi,kesi ipelekwe mahakamani,kisha Serikali iiombe mahakama kwamba gazeti hilo lisichapishwa hadi hukumu ya kesi itapotolewa.Tukumbuke kwamba Mwanahalisi wanategemea mauzo ya magazeti yao ili ku-survive.Wakiwa kifungoni kwa muda mfupi tu inaweza kuwa ndio mwisho wa gazeti.

Kuna mbinu chafu zaidi zinazoweza kutumika zaidi ya hizo za kisheria,na mfano mzuri ni namna gazeti mahiri la Family Mirror "lilivyouawa."Wakati jitihada za kuligeuza Mwanahalisi kuwa kama Rai (yaani kutoka Rai la akina Ulimwengu into la akina Balile) zinaelekea kutofanya kazi,mafisadi kwa kuwatumia watwana wao serikalini wanakuna vichwa kuhakikisha kwamba gazeti hili halidumu.Wanaweza kufanikiwa kwani wanafahamu udhaifu wa Watanzania:watalalamika leo kesho watasahau.Watetezi wa uhuru wa habari watapiga kelele weee (pindi azma ya mafisadi kuona Mwanahalisi linawekwa korokoroni itapotimia) lakini muda si mrefu watarejea kwenye usingizi wao wa pono.
 
Uhuru ambao unatolewa kwa moyo wote kwa watanzania ni kuandika magazeti ya uroda na ya habari za uswahilini. Lakini magazeti kama RAI (real Rai sio hii fake ya sasa) au magazeti serious kama Mwanahalisi huwa hayatakiwi. Wanaolinda sera za habari na sheria za habari wanapenda kuona kapu la wajinga Tanzania, ambalo linafurahia habari za kijinga kijinga na za uswahilini.
Lakini ukiangalia kwa undani utaona kuwa magazeti ya uroda ndio more damiging than haya magazeti makini. NI vizuri kujua ni nani amefikia uamuzi huo..hakika sio rais, Rais hawezi kufanya ujinga huu kwa kisingizio cha sheria
 
Hapana wakikaidi amri sheria inatoa defence. Wakikaidi amri watailazimisha serikali kuwashtaki kwa kutotii amri ya Waziri na hivyo kuvunja sheria ya magazeti ya 1976. Wao wataenda mahakamani watasema sheria (kipengele) kinachompa Waziri mamlaka hayo makubwa ni kinyume na Katiba na hivyo kuligeuza hilo suala kutoka kuwa la kihalifu na kuwa la Kikatiba. Katika misingi hiyo Mahakama itatakiwa kuamua kama sheria iliyotumika haiko too vague kiasi kwamba Waziri anaweza kufanya lolote lile bila checks ya mahakama.

Mkuu,

Inawezekana hiyo approach ikawa siyo iliyo bora.

Kujitetea mahakamani kwa misingi ya ukiukwaji wa Katiba kunaweza kutupiliwa mbali kwa kigezo kwamba sio mahala pake.

Utakumbuka miezi michache iliyopita ex-Police Commissioner Zombe alivyo "pandisha mzuka Mahakamani" na kusema kwamba amekamatwa na anahukumiwa bila kusikilizwa, kinyume na Ibara ya 13 na 15 ya Katiba na mstari wa Yohana 7:51 wa msahafu, jaji alimwambia utetezi wa ki-Katiba aupeleke kwenye kesi ya Katiba.

Kwa mtaji huo, na huo tu, kwenye Mahakama za Tanzania, ukianza kujitetea ooooh mimi mnanionea kwa mujibu wa Katiba kipengele kile na hiki hapa, watakwambia kafungue kesi ya Katiba. By the time unafungua kesi ya Katiba uko jela tayari, kwa sababu, mind you, hii kesi yetu original bado ilikuwa inaendelea, na defense yako uliyoitegemea ya Katiba imetupwa. Kiufupi, utafungwa, na kesi ya Katiba hutakuwa na hamu nayo tena.
 
Mkuu,

Inawezekana hiyo approach ikawa siyo iliyo bora.

Kujitetea mahakamani kwa misingi ya ukiukwaji wa Katiba kunaweza kutupiliwa mbali kwa kigezo kwamba sio mahala pake.

Utakumbuka miezi michache iliyopita ex-Police Commissioner Zombe alivyo "pandisha mzuka Mahakamani" na kusema kwamba amekamatwa na anahukumiwa bila kusikilizwa, kinyume na Ibara ya 13 na 15 ya Katiba na mstari wa Yohana 7:51 wa msahafu, jaji alimwambia utetezi wa ki-Katiba aupeleke kwenye kesi ya Katiba.

Kwa mtaji huo, na huo tu, kwenye Mahakama za Tanzania, ukianza kujitetea ooooh mimi mnanionea kwa mujibu wa Katiba kipengele kile na hiki hapa, watakwambia kafungue kesi ya Katiba. By the time unafungua kesi ya Katiba uko jela tayari, kwa sababu, mind you, hii kesi yetu original bado ilikuwa inaendelea, na defense yako uliyoitegemea ya Katiba imetupwa. Kiufupi, utafungwa, na kesi ya Katiba hutakuwa na hamu nayo tena.

Adhabu ya kufungwa ni sehemu ya mchakato wa sheria. Na ndio maana kuna rufaa. Tukiogopa kufungwa na hivyo kushindwa kupinga sheria mbovu hatustahili kwenye mapambano haya. Lengo la kuikaidi sheria hiyo ni ili kulazimisha serikali ilazimishe sheria mbovu mahakamani.

Jana (Jumamosi) Polisi walimuita Kubenea aende makao makuu ya Polisi. Tukamwambia akatae ili kama Polisi wana sababu yeyote ya kutaka kumhoji aidha wawasiliane na wakili wake au waende mahakamani. Hatuwezi kuendelea kukubali utawala wa kibabe kwa sababu fulani ni polisi kuna ulazima wa kukaidi (civil disobedience).

Jumatatu (kama mambo yatakuwa ninavyosikia) gazeti la serikali (linalotarajiwa kutoka siku hiyo) litatangaza kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi kwa miezi mitatu. Hilo litategemea sana kama Kubenea atakubali kujitolea kuhojiwa na Polisi kabla ya siku hiyo na kutoa ufafanuzi wa habari iliyoandikwa.

Lakini sasa hivi uwezekano wa wao kufungiwa umepungua sana baada ya habari hii kutoka na tayari tumewasiliana na taasisi mbalimbali zinazotetea waandishi wa habari duniani na wote wamekaa mkao wa kula.

Lakini vyovyote vile gazeti la Mwanahalisi linapaswa kutoka Jumatano kwa namna yeyote ile.
 
Adhabu ya kufungwa ni sehemu ya mchakato wa sheria. Na ndio maana kuna rufaa. Tukiogopa kufungwa na hivyo kushindwa kupinga sheria mbovu hatustahili kwenye mapambano haya. Lengo la kuikaidi sheria hiyo ni ili kulazimisha serikali ilazimishe sheria mbovu mahakamani.

Jana (Jumamosi) Polisi walimuita Kubenea aende makao makuu ya Polisi. Tukamwambia akatae ili kama Polisi wana sababu yeyote ya kutaka kumhoji aidha wawasiliane na wakili wake au waende mahakamani. Hatuwezi kuendelea kukubali utawala wa kibabe kwa sababu fulani ni polisi kuna ulazima wa kukaidi (civil disobedience).

Jumatatu (kama mambo yatakuwa ninavyosikia) gazeti la serikali (linalotarajiwa kutoka siku hiyo) litatangaza kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi kwa miezi mitatu. Hilo litategemea sana kama Kubenea atakubali kujitolea kuhojiwa na Polisi kabla ya siku hiyo na kutoa ufafanuzi wa habari iliyoandikwa.

Lakini sasa hivi uwezekano wa wao kufungiwa umepungua sana baada ya habari hii kutoka na tayari tumewasiliana na taasisi mbalimbali zinazotetea waandishi wa habari duniani na wote wamekaa mkao wa kula.

Lakini vyovyote vile gazeti la Mwanahalisi linapaswa kutoka Jumatano kwa namna yeyote ile.

Bado polisi wanang'ang'ania Kubenea aende na yeye amesisitiza anawasiliana kwanza na Mwanasheria wake na kwamba yeye si Mhariri na suala hilo linashughulikiwa na maelezo kama wanataka maelezo waende maelezo. Inaonekana polisi wanafanya kazi kwa shinikizo kubwa kutoka wanakojua wao.

Hatari yake ni kwamba wanachokifanya sasa ni kumharibia Muungwana na huo ni mkakati mwingine wa kumchafulia kwa kumchonganisha na umma.
 
Wahariri wakisimama kidete hili litakwisha mapema. Lakini kama wataendekeza wivu wao kwa Mwanahalisi ndio itakuwa imetoka. Ingekuwa zamani ingekuwa rahisi sana kwa sababu Muungwana alikuwa hakubali kitu chochote kinachomwaribia sifa. Lakini siku hizi baada ya kugundua matundu yote ya kumwagiwa sifa yamezibwa, taratibu na yeye anaanza kuubeba umkapa, ambao ulikuwa na falsafa ya utawala wa kibabe.

Kwa kawaida uwezo mdogo wa uongozi humpelekea kiongozi kuwa dikteta, na ndiko anapoelekea JK maana atakuwa hana cha kumlinda zaidi ya maguvu ya dola. Aliyemdanganya kwamba angeuweza urais alimchuuza kwelikweli. Ningekuwa mshauri wake wa karibu ningemshauri sasa atengeneze mazingira ya kuachana na kazi ya urais kwa heshima ifikapo 2010, lakini wapi wajanja wanaofaidi urais wake watamdanganya kwamba mzee wananchi wanakupenda, unafanya kazi nzuri hata Bush anakusifia, wanampiga changa la macho!!
 
Wahariri wakisimama kidete hili litakwisha mapema. Lakini kama wataendekeza wivu wao kwa Mwanahalisi ndio itakuwa imetoka. Ingekuwa zamani ingekuwa rahisi sana kwa sababu Muungwana alikuwa hakubali kitu chochote kinachomwaribia sifa. Lakini siku hizi baada ya kugundua matundu yote ya kumwagiwa sifa yamezibwa, taratibu na yeye anaanza kuubeba umkapa, ambao ulikuwa na falsafa ya utawala wa kibabe.

Kwa kawaida uwezo mdogo wa uongozi humpelekea kiongozi kuwa dikteta, na ndiko anapoelekea JK maana atakuwa hana cha kumlinda zaidi ya maguvu ya dola. Aliyemdanganya kwamba angeuweza urais alimchuuza kwelikweli. Ningekuwa mshauri wake wa karibu ningemshauri sasa atengeneze mazingira ya kuachana na kazi ya urais kwa heshima ifikapo 2010, lakini wapi wajanja wanaofaidi urais wake watamdanganya kwamba mzee wananchi wanakupenda, unafanya kazi nzuri hata Bush anakusifia, wanampiga changa la macho!!

hata bush anakusifia
haaaapo basi si unawajuwa wakwe...?
 
Wakuu,
Utakumbuka miezi michache iliyopita ex-Police Commissioner Zombe alivyo "pandisha mzuka Mahakamani" na kusema kwamba amekamatwa na anahukumiwa bila kusikilizwa, kinyume na Ibara ya 13 na 15 ya Katiba na mstari wa Yohana 7:51 wa msahafu, jaji alimwambia utetezi wa ki-Katiba aupeleke kwenye kesi ya Katiba.
Hivi kuna mahakama yenye sheria tofauti na zile za Kikatiba!..Hizo tetezi za kikatiba husikilizwa wapi!
Nimechanganyikiwa kidogo kutokana na maelezo hapo juu...Naomba somo!
 
Wakuu,

Hivi kuna mahakama yenye sheria tofauti na zile za Kikatiba!..Hizo tetezi za kikatiba husikilizwa wapi!
Nimechanganyikiwa kidogo kutokana na maelezo hapo juu...Naomba somo!

Mkandara, Katiba yetu inasema kuwa "kutakuwa na Mahakama Maalum ya Katiba". Mahakama hii ni tofauti na mahakama nyingine kwani inaundwa na ina mandate tofauti. Mahakama hiyo inaitwa "Mahakama Maalum ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano" (Ibara ya 125)

Lakini uwezo wake au majukumu yake hauhusu mambo kama haya mengine ambayo yamo katika uwezo wa kawaida wa mahakama Kuu na ya Rufaa. Mahakama hii Maalum inaangalia mambo ya Kikatiba yale tu yanayohusu mgongano kati ya Serikali ya Muungano na Serikali ya Zanzibar (kama lile suala la nchi si nchi).

Kwa ufupi, masuala ya Kikatiba yanaweza kusikilizwa na mahakama nyingine lakini linapokuja suala la Kikatiba kuhusu Zanzibar na Muungano, basi Mahakama Maalum ndiyo inayoshughulikia na uamuzi wake ni wa mwisho.
 
Laiti watu wangepitia kidogo mada hii labda wangejua namna ya kujiandaa kidogo. Grrrrrrrrrrr
 
Back
Top Bottom