Habarini za asubuhi ndugu zangu naombeni ushauri wenu wa dhati maana niko njia panda sijui lipi la kufanya,mimi naishi Arusha nina mke na watoto wawili sasa hivi karibuni kama miezi 5 iliyopita nilipata mgeni pale nyumbani kwangu ni binti kama wa miaka 20 ni ndugu yake na wife.yule binti kwakweli ni mrembo sasa shetani alinipitia nikajikuta natembea nae, hako ka mchezo hua nakafanyia hapohapo nyumbani mda labda wife hayupo na msichna wa kazi sometime hayupo .sasa msichana wangu wa kazi alishtukia huo mchezo ndipo alipomweleza wife kila kitu, wife nae akambana yule ndugu yake hadi akakubali kua ni kweli hua na duu na baba mda ukiwa haupo,yaliyo nikuta nikwamba nimewekwa kikao na binti akaongea yoote mbele ya kadamnass ndugu zangu ni aibu maana majirani wanajua hadi watoto wanajua sasa niko njia panda sijui nianzie wapi nahisi ndoa yangu ndoa bass tena ,emebidi nitoke home kwa mda niko kwa washkaji angalau labda hasira ya wife itapungua