Yamenikuta yakunikuta

Yamenikuta yakunikuta

Habarini za asubuhi ndugu zangu naombeni ushauri wenu wa dhati maana niko njia panda sijui lipi la kufanya,mimi naishi Arusha nina mke na watoto wawili sasa hivi karibuni kama miezi 5 iliyopita nilipata mgeni pale nyumbani kwangu ni binti kama wa miaka 20 ni ndugu yake na wife.yule binti kwakweli ni mrembo sasa shetani alinipitia nikajikuta natembea nae, hako ka mchezo hua nakafanyia hapohapo nyumbani mda labda wife hayupo na msichna wa kazi sometime hayupo .sasa msichana wangu wa kazi alishtukia huo mchezo ndipo alipomweleza wife kila kitu, wife nae akambana yule ndugu yake hadi akakubali kua ni kweli hua na duu na baba mda ukiwa haupo,yaliyo nikuta nikwamba nimewekwa kikao na binti akaongea yoote mbele ya kadamnass ndugu zangu ni aibu maana majirani wanajua hadi watoto wanajua sasa niko njia panda sijui nianzie wapi nahisi ndoa yangu ndoa bass tena ,emebidi nitoke home kwa mda niko kwa washkaji angalau labda hasira ya wife itapungua

Yani umekosa hivo halafu uko kwa washkaji??nyumba yako aitengeneze nani?manake kama ni wa kutoka nyumbani kupumua,ni mkeo sio wewe!..kwanza umejuta kweli?hicho ndo cha msingi.ukute unajuta kubambwa so umejifunza kucheat kwa umakini next time!..kama unajutia toka moyoni,first jiandae mfukoni ukae safi,coz making this up will be so costly,over unaoa upya. nenda kwa wakwe zako ukawaombe radhi coz umewatukana na wao.tena sana.ikibidi ujibebeshe pesa ukawapooze,tena uende na watu wazima kadhaa toka kwenu watakusaidia kuomba msamaha kimila.hapo hakuna kuficha tena,siri ishajulikana.najua ni aibu na ubabe wa kiume inabidi upungue,ila ndo ujue makosa yana gharama tena kubwa..pili rejea home,mpe mkeo likizo.make her feel like a queen.nakumbusha,ni ngumu na uanaume tupa kule,hii ni ndoa yako bana,itetee au iache iteketee.mruhusu mkeo aondoke nyumbani akakae nyumbani au kama unajiweza,aende to a hotel.let her do anachopenda.women tunapenda shopping,so let her.keep in touch,keep apologising na ndo iwe sms ya kwanza anayoikuta kila akiamka na kabla hajalala.(Mind u kama kakupenda,she won't cheat akiwa away).kaa karibu na watoto.kama hujui kupika,ndo ujue.kila kitu ukifanye wewe.mkeo akihave enough air,atarudi tu siku.hili halitakusaidia tu kurejesha ndoa,bali litakufundisha kuthamini familia.utatengeneza bond kubwa sana na watoto wasione you're that much of a beast ingawa umeshawaathiri kwa kiasi flani.pole kaka ingawa umeniudhi kwa uzembe wako..kikubwa,mpe mkeo muda to breathe,rudi nyumbani uwajibike.ukishajua how hard it is kutunza familia,hutokaa umvunjie mkeo heshima
tena!USIRUDIE TENA!!
 
Haya ndio mambo ambayo watu tunakemea daily humu MMU wewe umeoa kibungo wa nn???????? Halafu zikiletwa thread humu nyie ndo wa kwanza kuanza kusema ooooh mwanamke tabia,ila ndo vizuri watoto nao wamejua nina uhakika hawataweza kuja kurudia makosaa wataoa warembo kwelikweli damn
 
Dada kwani katembea na mwanaume mwenzake? we si unaona kamgegeda shemeji tena toka nikutoke na dadaye...
Hahahahahahahahahahahahahahahahahahhaha watu 8 unanivunja mbavu zangu hahahahhahahhahhahhahahahahhahahhahhahahahhahahaha
 
pole mzee mwenzangu duh1 hapo sasa naww inabidi uzuge unahasira mbay na kila mtu hii itapunguza maswli na wengne watjihc wamekukosea by the way hapo ni kwako bhan cyo kwa mwanamke

wanaume viumbe wa ajabu mno, kumbe unajifanya una hasira wakati ushenzi umefanya mwenyewe.! NINYI NI HOVYO SANA NA HANA UTU HATA CHEMBE
 
Wewe hayajakukuta ila yamemkuta mkeo
 
Never teach a person how to apologise..what if moyoni mwake hajajuta kweli na atarudia kumuumiza mkewe??ukute hajutii kosa,anajutia siri kufichuka.mwache mwenyewe ndo anjua atamlambaje mkewe miguu amsamehe.halafu sijui kwanini mtu anakosa halafu kikubwa anachojali ni jamii kujua badala ya extent aliomuumiza mwenzie.hapa mtoa mada anaogopa jamii na hasira za mkewe..sioni kama kajutia kosa.angempenda mkewe,asingemuaibisha kwenye hiyo jamii anayoiogopa.na wa kuogopa kukatisha kitaa should be mkewe ambae kutwa atanyooshewa vidole na kuonewa huruma..wanaume wengine sijui wana-assume wake zao wana mioyo ya plastiki!!!!nakereka mimi!mxiuuuu

mkuu umenena vizuri nami sina budi kukubaliana na wewe though hii thread niya muda kweli.............ukiachilia kuihofia jamii na mambo mengine kwangu mimi km mimi ndoa niya muhimu sana, nikimkosea wife mimi huwa niwa kwanza kuomba msamaha cuz nampenda sana mke wng pia naipenda sana ndoa yng, pia mkuu sio kwamba tunavyowasaliti wake zetu hatuwapendi? hapana ni tamaa tu ndio zinatuponza kwasababu sie sio wakamilifu hivyo in most cases tunakuwa subjected in lust na mambo mengine yanayofanana na hayo, km wewe upo kwenye ndoa kweli hujawahi kumsaliti mwenzio ata mara moja kweli, be honest zungumza ukweli.
 
akili za kiume sijui zikoje.

under yr roof?? bora hata ungeenda mbali aisee

ha ha cha kuiba ni kitamu jamani, ukienda mbali hufaidi kwa sababu unakua umejiandaa na uko na utulivu. sishauri kwa walio oa kama mimi. hii ni kwa vijana tu.
 
Kwanini ukubari kikao wakati unajijuwa we ndo mkosaji?
 
Pole sana kwa yaliyotokea japo nimechelewa kuisoma thread yako. Kwanza kabisa nakushauri umuombe mkeo msamaha kwa dhati kabisa na uache tabia hiyo kisha utubu kwa MUNGU hakika atakusamehe. Kosa moja hufutwa na mema mengi sana hivyo fanya yanayopendeza na yatakayomuonyesha mkeo kuwa umebadilika na kweli ulipitiwa kama unavyosema. Mkeo na wewe mlikosa busara ndiyo maana imefikia hata majirani na watoto kujua mambo yenu ya ndani tena ya aibu, aibu hii si kwako tu bali hata kwake na familiya nzima.
Kama kweli mkeo anakupenda na anajitambua atakusamehe japo inaweza kuchukua muda kutokana na namna aliyoumia.
Usichoke kumwomba msamaha, jiamini acha kuona ona aibu, hilo ni tatizo limetokea kukimbia nyumbani haitasaidia, unatakiwa ukae nyumbani ulitatue liishe na uache tabia hiyo.
Hakika ulimkosea mkeo ila bado una nafasi na kurudisha amani katika ndoa yako, kaa na mkeo faragha mzungumze myamalize kwani hata asipokubali bado kitu kishafanyika cha msingi ni kulinda kisirudie tena. Nawatakia mafanikio mema katika kutatua tatizo hili.
 
Back
Top Bottom