Yaliyotokea mpakani na Kenya, Zambia na Rwanda yanaonyesha haja ya umakini kwa Magufuli kuteua wakuu wa mikoa ya mipakani wenye uwezo wa kidiplomasia

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Nakumbuka katika kuteua wakuu wa mikoa muda fulani uliopita, Raisi Magufuli alisema kwamba alikuwa akiteua wakuu wa mikoa ya mipakani wengi wakiwa wanajeshi ili kusaidia katika suala la ulinzi mipakani. Lakini sasa, migongano na nchi jirani za Kenya, Zambia, Rwanda na hata Uganda zimetufundisha na kutupa onyo juu ya umuhimu wa kuhakikisha kwamba wakuu wa mikoa ya mipakani wanapaswa kuwa watu wenye uwezo mkubwa wa kidiplomasia.

Ukichukulia Tanga na Kilimanjaro kwa mfano, tumeshuhudia wakuu wa mikoa wakichochea badala ya kuzima moto wa jazba uliojitokeza kati yetu na Kenya, hadi kufikia hatua ya kuwakejeli viongozi wakuu wa nchi jirani! Sasa hii ni hatari sana, na tusipoangalia inaweza kuleta machafuko kufikia wananchi wa mipakani kuanza kupigana na watu wa nchi jirani na hata kuuana. Na mazingira kama hayo yanaweza kufikia hatua ya polisi au jeshi kuingilia kati, na hata risasi kupigwa dhidi ya nchi jirani na kuzua mpambano wa askari wenye silaha.

Sio vibaya kuweka wanajeshi kama wakuu wa mikoa ya mpakani, kwa kuwa wapo wanajeshi wanaojulikana kuwa mahili katika masuala ya diplomasia. Hata hivyo, kama ni suala la ulinzi mipakani ni vema kuwa na kambi za jeshi katika kila mkoa wa mpakani, na wakuu wa kambi hizi wakawa sehemu ya kamati za ulinzi za mkoa ambazo zinasimamiwa na wakuu wa mikoa.

Hata hivyo, kipaombele kiwe kuteua wakuu wa mikoa ya mipakani ambao ni raia na watu wenye uwezo mkubwa katika masuala ya diplomasia. Na ikibidi, wakuu wa mikoa ya mipakani wawe wanapitia mafunzo maalumu ya diplomasia kabla ya kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi.

Ningependa kushauri kwamba mabadiliko haya yafanyiwe kazi haraka iwezekanavyo.
 
Hao wamefundishwa kuuwa Kama njia ya kutatua tatizo na sio kuongea ( diplomasia Kama njia ya kutatua tatizo) wamefundishwa kutumia nguvu badala ya busara yaani Moto na Moto hivo diplomasia ni msamiati mkavu kwao.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hawa jirani zetu ni wa wahuni unatakiwa uende nao kihuni na hapa suala la diplomasia halipo. Kama wanataka diplomasia wakutane wa Waziri wa Mambo ya Nje. Watu wanatudhihaki eti tuna corona, wewe unasema diplomasia. Hakika nakuambia watu kama Wakenya wanataka aina hii ya Shigella na utawasikia wanakuja kuonba suluhu.
 
Hio ndio dawa yao. Ilibidi wakuu wote wa mikoa mipikani wafanye kama Tanga. Ingependeza sana.
Tuoneshane makali kidogo kidogo
 
Synthesizer , sidhani kama wakuu wa mikoa ni wajinga kiasi hicho kuchukua maamuzi makuba kama hayo. Siyo wajinga wakijua tabia ya boss wao! Nina uhakika wamempigia simu Kassim na kumomba ushauri. Kasimu naye hawezi kuchukua maamuzi kama hayo, atakuwa amempigia Boss wake na BOSS kutoa go ahead!
 
Hawa jirani zetu ni wa wahuni unatakiwa uende nao kihuni na hapa suala la diplomasia halipo. Kama wanataka diplomasia wakutane wa Waziri wa Mambo ya Nje. Watu wanatudhihaki eti tuna corona, wewe unasema diplomasia. Hakika nakuambia watu kama Wakenya wanataka aina hii ya Shigella na utawasikia wanakuja kuonba suluhu.
Hilo ndilo ninaloshauri kwamba watu wenye mtazamo kama wako kamwe wasije kuteuliwa kuwa wakuu wa mikoa ya mipakani - ni wazi watu wa aina yako mpo wengi!
 
Sio kila kitu diplomasia mkuu vitu vyengine ni kwenda navyo hivyohivyo tunachafuliwa kama nchi kitu ambacho si sahihi then wewe utake kukaa mezani tu!!
Zarau zilitaka kuzidi kipindi kile na Rwanda mkwere akaleta amsha amsha..
 
Hawa jirani zetu ni wa wahuni unatakiwa uende nao kihuni na hapa suala la diplomasia halipo. Kama wanataka diplomasia wakutane wa Waziri wa Mambo ya Nje. Watu wanatudhihaki eti tuna corona, wewe unasema diplomasia. Hakika nakuambia watu kama Wakenya wanataka aina hii ya Shigella na utawasikia wanakuja kuonba suluhu.
Shigela huyu huyu aliyesema eti Uhuru amefungia watu wake ndani lkn maambukizi yamekua makubwa zaidi wkt huku kwetu Magu hajafungia watu wake ndani na maambukizi yanaenda kuisha?

LORD HAVE MERCY.
 
Exactly! 🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾

Synthesizer , sidhani kama wakuu wa mikoa ni wajinga kiasi hicho kuchukua maamuzi makuba kama hayo. Siyo wajinga wakijua tabia ya boss wao! Nina uhakika wamempigia simu Kassim na kumomba ushauri. Kasimu naye hawezi kuchukua maamuzi kama hayo, atakuwa amempigia Boss wake na BOSS kutoa go ahead!
 
Synthesizer , sidhani kama wakuu wa mikoa ni wajinga kiasi hicho kuchukua maamuzi makuba kama hayo. Siyo wajinga wakijua tabia ya boss wao! Nina uhakika wamempigia simu Kassim na kumomba ushauri. Kasimu naye hawezi kuchukua maamuzi kama hayo, atakuwa amempigia Boss wake na BOSS kutoa go ahead!
Mkuu, umeongea jambo ambalo watu wengi sana wameniambia, kwamba reaction zote zilizofanywa na wakuu wa mikoa katika huu mtifuano lazima zilikuwa maagizo toka juu. Sitaki kabisa kuamini hilo, na labda basi mimi niko "naive" kufikiri kwamba hatuwezi kuwa na kiongozi asiye na busara kiasi hicho. Kama kweli huo ndio uongozi tulio nao, basi twapaswa kuogopa sana!
 
Kwamba wenyewe watujibu harshly halafu sisi tulete diplomasia....

Ewaaaa, hiyo ndio maana ya diplomasia - wao wanakujibu harshly wewe unaleta diplomasia. Si ndio hata vitabu vya dini vinasema, au tumekuwa taifa la wapagani, wote tumeshakuwa mashetani tayari?
 
Mkuu, umeongea jambo ambalo watu wengi sana wameniambia, kwamba reaction zote zilizofanywa na wakuu wa mikoa katika huu mtifuano lazima zilikuwa maagizo toka juu. Sitaki kabisa kuamini hilo, na labda basi mimi niko "naive" kufikiri kwamba hatuwezi kuwa na kiongozi asiye na busara kiasi hicho. Kama kweli huo ndio uongozi tulio nao, basi twapaswa kuogopa sana!
Synthesizer , haya ni maamuzi makubwa, hayawezi kuyafanya Mkuu wa Mkoa, NEVER on Earth! Hata PM peke yake hawezi kuthubutu! Ndiyo maana wakuu wote wa Nchi handling ya covid-19 inafanywa na WAKUU WA NCHI, pote duniani. Naangali all world TVs zoteni wakuu wa nchi wanaotoa mwongozo nini kifanyike (of course baada ya kushauriana na wataalamu wake) ! Kuwafungia ndani watu mwezi siyo kitu kidogo cha kufanywa na msaidizi wako bila consultation na wewe. Kufunga vyuo vyote siyo kitu cha kufanya na msaidzi wako!
 
Kumbe wakuu wa mikoa ya Tanga na Kilimanjaro ni wanajeshi,nilikuwa sijui hili
Nadhani Tanga, Kilimanjaro huyu mama sidhani kama alishakuwa mwanajeshi. Lakini hiyo ilikuwa kauli ya ujumla, hakuna tuliposema Mkuu wa mkoa Tanga na Kilimanjaro ni wanajeshi. Ila Magufuli alisema anataka kuweka wanajeshi mikoa ya mipakani kama Kigoma na Kagera ili wasaidie masuala ya ulinzi mipakani
 
Baba yetu haamini kwenye mambo ya professionalism,ndio maana una muona Mwiguru Nchemba mchumi by professional sasa ni Waziri wa sheria na katiba.
Mkuu Kwani umuhimu /uwepo wa makatibu wakuu katika wizara husika ni upi?,uwaziri haujalishi professional ya mhusika Maana waziri si mtendaji Bali msimamizi,kazi kubwa huwa iko kwa makatibu wakuu na the subjects

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ewaaaa, hiyo ndio maana ya diplomasia - wao wanakujibu harshly wewe unaleta diplomasia. Si ndio hata vitabu vya dini vinasema, au tumekuwa taifa la wapagani, wote tumeshakuwa mashetani tayari?
Walichopanda ndicho watakachovuna
 
Hawa jirani zetu ni wa wahuni unatakiwa uende nao kihuni na hapa suala la diplomasia halipo. Kama wanataka diplomasia wakutane wa Waziri wa Mambo ya Nje. Watu wanatudhihaki eti tuna corona, wewe unasema diplomasia. Hakika nakuambia watu kama Wakenya wanataka aina hii ya Shigella na utawasikia wanakuja kuonba suluhu.
Mimi naona Shigela amekuwa mpole ilitakiwa zaidi.
Jumuiya ya Africa mashariki ilikufa sababu ya unyang'au wa hawa watu.
Uweke diplomasia na watu walioshindwa kuunganisha makabila yao.
 
Back
Top Bottom