Yaliyonikuta na Basi la Kilimanjaro Express

Yaliyonikuta na Basi la Kilimanjaro Express

Hata BM labda ukibahatisha DYE, DZQ, EBL, DXN, DVM hapa utaenjoy sana.
Hiyo BM DXN. Kuna moja nilipanda siti zimebanwa kama daladala za kwenda kange kasera. Walisema ni luxury, hata kiyoyozi hakijawashwa tuna kazi ya kujifuta jasho tu. Humo ndani ni biashara zinaendelea kama kariakoo. Hujakaa vizuri kapita wa biskuti, ukigeuka hivi kapita wa korosho, ukinyoosha mguu kaingia wa machungwa ya kuonja na kununua. Vurugu tu, mnaingia hotelini dakika 10 ni pale dereva anapomaliza kula. Uluxury pekee niliouona kwenye BM siku hiyo ni kutokupakiza wale watu wa dawa za promotion na kusimamisha abiria.
Tanga to Arusha kuna kampuni inaitwa Raqeeb. Luxury unalipa 23,000 iwe unashuka Arusha au Moshi. Inasimama kila kituo na kupakia abiria tofauti yake na dalala ni ukubwa wa umbo la gari Ila huduma ni kama daladala tu. Inasimamisha abiria, hakuna ac, movie za mkojani na singeli yani kelele tu. Wanajitahidi makondakta wao kwa kuwa na hekima. Ukitaka luxury hapa Tz wewe safiri na gari yako binafsi tu
 
Tiari si ana hotel jamani chips yai 9000
Silagi chochote kwenye hizo hotel zaidi ya maji labda na juice na biscuit eat some more kuboost sukari nisisikie njaa.

Kama unataka Dar unaenda Arusha ya nini kuchafuwa tumbo lako wakati unapokwenda ndio makao makuu ya vyakula.

Kuna safari nilitokea Moshi na familia nilinunuwa mitetea ikachinjwa siku moja kabla ya safari tukakaanga wenyewe tukasafiri na vitoweo vyetu, kufika kwenye hotel zao za kitapeli unanuwa chips kavu tu za moto maisha yanaendelea.

Hii ni system yangu mpaka leo, nikisafiri na familia tunabeba msosi wetu flied food, sipendi kabisa Utapeli wa vyakula njiani halafu mafuta siyo ya kuyaamini.
 
Tatizo Abood hizo anazipa route fupi tu ya moro.
Au atawachukua mpk moro anawatupa ngarangara mnapiga ndefu
Moro to Arusha kaweka zile DJP ambazo zilikua zinapiga route ya Dar Moro. Sema wana jamaa anaekatisha ticket pale msamvu Mhidini mtu peace sana yule
 
Kwa safari za kaskazini Basi langu ni Sai Baba tu, na kusini ni Majinja, hayajawahi niangusha haya mabasi
 
Wakati mwingine jaribu Extra Luxury Coach Mkuu...

Utanishukuru..
Wanajitahidi, japo wanakatabia ka kuongeza abiria 1 au 2 wa kusimama. Watawaweka pale mbele. Mmoja atakaa kiti cha konda na mwingine pembeni. Makonda wa kike na kiume nao ujibanza maeneo hayo. Wakikalibia check point wanakuja sumbua abiria kubanana na hao nyongeza. Sijui kama tajiri anajua hili.
Napandaga sana hili bus, kimuundo ni mazuri, wanajitahidi kwenda na muda, ila kasoro yao ndio hiyo
 
Choo chake pia Mtu akitoka ni harufu inasikika ndani ya Bus…Aah nishasemaga Kilimanjaro na Dar lux sintopanda!!!

Bus ambazo hua naenjoy kwa Huduma Bora, Seat nzuri na Kukufanya Usiboreke ni Marangu, Extra luxury au BM .
 
Wanajitahidi, japo wanakatabia ka kuongeza abiria 1 au 2 wa kusimama. Watawaweka pale mbele. Mmoja atakaa kiti cha konda na mwingine pembeni. Makonda wa kike na kiume nao ujibanza maeneo hayo. Wakikalibia check point wanakuja sumbua abiria kubanana na hao nyongeza. Sijui kama tajiri anajua hili.
Napandaga sana hili bus, kimuundo ni mazuri, wanajitahidi kwenda na muda, ila kasoro yao ndio hiyo
Mimi wameshawahi kunipandisha hiyo sehemu, ilikuwa tarehe 24 December, usafiri mgumu kinoma
 
Back
Top Bottom