GAZETI
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 5,278
- 6,672
Nilikuwa maeneo ya upanga karibu na kituo cha polisi cha zamani ambacho kimehamishwa Ghafla ikasimama gari mbele yangu. Mtu mmoja mwenye mvi na kitambi kikubwa akateremka na kuanza kunifokea. Akaniambia "Fundi umefuata nini huku mi nakuitia kazi we unazurura tu!" Akanipatia bahasha huku akifoka akaniambia haraka sana kaanze kazi. Akaingia kwenye gari na kuondoka nilipofungua ile bahasha nimekuta kibunda cha noti za shilingi 10,000 1.milion. na kile cha shilingi 5000 laki tano. Kwa jinsi alivyoondoka haraka nimeshindwa kukanusha kuwa sio mimi.