Mlatino Zeshalo
JF-Expert Member
- Sep 10, 2014
- 2,016
- 3,464
Habari zenu wana JF
Natumai mambo yanaenda vizuri ukizingatia leo ni siku ya mapumziko kwa wengi wetu.
Niende moja kwa moja kwenye mada, tar 16 mwez huu siku ya j3 nilifanya booking online kwaajili ya kupata chanjo ya covid 19. Nilitamani sana nipate hiyo chanjo siku ya ijumaa tar 20 mwez huu. Mipango yangu ilikuwa nikipata chanjo ijumaa, jmos niende home kusikilizia reaction ya chanjo mwilini ili ikizingua niwe karibu na ndugu.
Jana tar 20 nilijiandaa na mida ya saa 6 mchana nilikuwa nimeshafika kwenye kituo nilichofanyia booking kwaajili ya kupokea chanjo. Niliwapa ref number niliyopewa siku nimefanya booking. Baada ya hapo nilienda chumba cha sindano.
Kabla sijatoa shati, niliamua kumuuliza nurse kama hiyo chanjo inasababisha homa maana nilisikia kwa watu watatu tofauti kuwa ukichoma lazima homa ikuzingue. Nurse alijibu simple tu kuwa unaweza kupata homa kidogo tu na siyo wote wanaopata homa. Akanipa mfano ambao sikuutilia maanani sana kuwa yeye hakupata homa lakini wenzake walipata.
Basi nikatoa shati akanichoma sindano, baada ya kumaliza akaniambia nenda kapumzike pale kwenye bench. Nikajiuliza sana, kwanini nipumzike? Hiyo chanjo inakipi hasa cha kunifanya nikimaliza nipumzike, badae kuna jamaa mmoja alichoma baada ya mimi kumaliza, nae aliambiwa asisimame, akae kwani angeweza kudondoka.
Nilikaa pale mapumzikoni kama dakika 15, nikasepa getto. Ilikuwa mida ya saa nane mchana. Nikaandaa chakula nikala fresh. Jioni sikuwa na mpango wa kupika, ikabidi mida ya saa moja nikatafute chakula kwenye hotel flani, nilivaa jacket maana huku kwetu mvua ilinyesha mchana wakati nipo kwenye chanjo. Nilitoka kupata chakula cha jioni saa moja na dakika 45. Basi nikazama getto kufanya mambo mengine.
Usiku saa mbili nikampigia dogo simu (anaishi na aunty Dar) nikamweleza kuwa nimekamilisha zoezi la chanjo maana baada ya kufanya booking nilimwambia pia. Dogo akacheka sana akisema mziki wake utaujutia maana aunty aliumwa baada ya kuchomwa hiyo chanjo. Mimi sikujali, tukapiga story kidogo badae nikaanza kuhisi mwili unauma kwa mbali. Kadri muda ulivyozidi kwenda hali yangu pia ikaanza kuwa mbaya. Nikamcall tena dogo kumwambia kuwa hali yangu imechange, hapo ni saa nne usiku. Akanishauri nivumilie kesho nisepe home. Basi, kidume nikalala, saa sita na dakika 15 nikashtuka, nikapiga glass ya maji then nikalala. Hapo ilibidi nijihami tu kuwa na maji karibu labda yangesaidia chochote. Saa saba pia na dakika 28 nikaamka tena, nikanywa maji alaf nikaenda kukojoa, lakini muda huu hali ilikuwa mbaya sana maana nilianza kutetemeka sana. Ikabidi nivae full, huwa napenda kulala na boxer. Nikavaa soksi ndefu, pensi, tshirt na jacket. Nilipolala nikajifunika shuka na duvet kwa juu. Asee niliendelea kutetemeka hadi nikahisi hilo duvet halina maana. Wakati huo kichwa kinauma balaa, alafu mwili wote kuanzia miguuni hadi shingo vilikuwa hoi.
Nikajikaza huku nikisali maana nilijua asubuhibikifika ntaenda kulazwa. Ndani ninazo diclopa za maumivu lakini sikutaka kutumia maana sijui ingekuwaje. Nikalala hadi saa nane na nusu nikashtuka tena, nikanywa maji then nikauchapa. Saa tisa nikaamka tena hapo nilikuwa nahisi baridi imekata, nikavua soksi maana nilikuwa nahisi miguu imechemka sana, poa nikavua jacket.
Nikalala lakuni bado nilijifunika shuka na duvet. Asubuhi leo nimeshtuka saa tatu, nikaenda nje kuota jua kidogo then nikarudi ndani. Nikawa nahisi homa imepungua japo kichwa kinauma kwa mbali. Saa tano asubuhi nikachukua maji ya mvua, ya baridi sana nikaoga. Asee nilihisi raha sana maana mwili umwkuwa fit japo maumivu ya kichwa bado nayahisi.
Sijajua kwa wengine waliopata hii chanjo kama na wao wamepitia hii changamoto maana daah, usiku nimehangaika hadi kufikia muda nikajuta kuchomwa hiyo chanjo. Nimepatwa maswali mengi kichwani, kwamba, ni kweli hawa viongozi wamechoma hii chanjo? Mbona wao walikuwa fit tu, au wao afya zao ni bora zaidi?
Lakini namshukuru Mungu, maana naendelea vema japo kichwa ndio bado kinauma kwa mbali. Jioni ntaenda uwanjani nikajaribu kufanya mazoezi kidogo maana miguu usiku pia ilizingua sana hadi nikahisi nitaamka nikiwa nimepooza.
Natumai mambo yanaenda vizuri ukizingatia leo ni siku ya mapumziko kwa wengi wetu.
Niende moja kwa moja kwenye mada, tar 16 mwez huu siku ya j3 nilifanya booking online kwaajili ya kupata chanjo ya covid 19. Nilitamani sana nipate hiyo chanjo siku ya ijumaa tar 20 mwez huu. Mipango yangu ilikuwa nikipata chanjo ijumaa, jmos niende home kusikilizia reaction ya chanjo mwilini ili ikizingua niwe karibu na ndugu.
Jana tar 20 nilijiandaa na mida ya saa 6 mchana nilikuwa nimeshafika kwenye kituo nilichofanyia booking kwaajili ya kupokea chanjo. Niliwapa ref number niliyopewa siku nimefanya booking. Baada ya hapo nilienda chumba cha sindano.
Kabla sijatoa shati, niliamua kumuuliza nurse kama hiyo chanjo inasababisha homa maana nilisikia kwa watu watatu tofauti kuwa ukichoma lazima homa ikuzingue. Nurse alijibu simple tu kuwa unaweza kupata homa kidogo tu na siyo wote wanaopata homa. Akanipa mfano ambao sikuutilia maanani sana kuwa yeye hakupata homa lakini wenzake walipata.
Basi nikatoa shati akanichoma sindano, baada ya kumaliza akaniambia nenda kapumzike pale kwenye bench. Nikajiuliza sana, kwanini nipumzike? Hiyo chanjo inakipi hasa cha kunifanya nikimaliza nipumzike, badae kuna jamaa mmoja alichoma baada ya mimi kumaliza, nae aliambiwa asisimame, akae kwani angeweza kudondoka.
Nilikaa pale mapumzikoni kama dakika 15, nikasepa getto. Ilikuwa mida ya saa nane mchana. Nikaandaa chakula nikala fresh. Jioni sikuwa na mpango wa kupika, ikabidi mida ya saa moja nikatafute chakula kwenye hotel flani, nilivaa jacket maana huku kwetu mvua ilinyesha mchana wakati nipo kwenye chanjo. Nilitoka kupata chakula cha jioni saa moja na dakika 45. Basi nikazama getto kufanya mambo mengine.
Usiku saa mbili nikampigia dogo simu (anaishi na aunty Dar) nikamweleza kuwa nimekamilisha zoezi la chanjo maana baada ya kufanya booking nilimwambia pia. Dogo akacheka sana akisema mziki wake utaujutia maana aunty aliumwa baada ya kuchomwa hiyo chanjo. Mimi sikujali, tukapiga story kidogo badae nikaanza kuhisi mwili unauma kwa mbali. Kadri muda ulivyozidi kwenda hali yangu pia ikaanza kuwa mbaya. Nikamcall tena dogo kumwambia kuwa hali yangu imechange, hapo ni saa nne usiku. Akanishauri nivumilie kesho nisepe home. Basi, kidume nikalala, saa sita na dakika 15 nikashtuka, nikapiga glass ya maji then nikalala. Hapo ilibidi nijihami tu kuwa na maji karibu labda yangesaidia chochote. Saa saba pia na dakika 28 nikaamka tena, nikanywa maji alaf nikaenda kukojoa, lakini muda huu hali ilikuwa mbaya sana maana nilianza kutetemeka sana. Ikabidi nivae full, huwa napenda kulala na boxer. Nikavaa soksi ndefu, pensi, tshirt na jacket. Nilipolala nikajifunika shuka na duvet kwa juu. Asee niliendelea kutetemeka hadi nikahisi hilo duvet halina maana. Wakati huo kichwa kinauma balaa, alafu mwili wote kuanzia miguuni hadi shingo vilikuwa hoi.
Nikajikaza huku nikisali maana nilijua asubuhibikifika ntaenda kulazwa. Ndani ninazo diclopa za maumivu lakini sikutaka kutumia maana sijui ingekuwaje. Nikalala hadi saa nane na nusu nikashtuka tena, nikanywa maji then nikauchapa. Saa tisa nikaamka tena hapo nilikuwa nahisi baridi imekata, nikavua soksi maana nilikuwa nahisi miguu imechemka sana, poa nikavua jacket.
Nikalala lakuni bado nilijifunika shuka na duvet. Asubuhi leo nimeshtuka saa tatu, nikaenda nje kuota jua kidogo then nikarudi ndani. Nikawa nahisi homa imepungua japo kichwa kinauma kwa mbali. Saa tano asubuhi nikachukua maji ya mvua, ya baridi sana nikaoga. Asee nilihisi raha sana maana mwili umwkuwa fit japo maumivu ya kichwa bado nayahisi.
Sijajua kwa wengine waliopata hii chanjo kama na wao wamepitia hii changamoto maana daah, usiku nimehangaika hadi kufikia muda nikajuta kuchomwa hiyo chanjo. Nimepatwa maswali mengi kichwani, kwamba, ni kweli hawa viongozi wamechoma hii chanjo? Mbona wao walikuwa fit tu, au wao afya zao ni bora zaidi?
Lakini namshukuru Mungu, maana naendelea vema japo kichwa ndio bado kinauma kwa mbali. Jioni ntaenda uwanjani nikajaribu kufanya mazoezi kidogo maana miguu usiku pia ilizingua sana hadi nikahisi nitaamka nikiwa nimepooza.