GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,647
- 109,036
Kabla ya kuchanja rasmi leo Chanjo yangu ya UVIKO-19 aina ya J&J nilijaribu kuwataarifu watu kadhaa, ila cha kushangaza wote waliishia kunitishia huku wengine waitaka ninunue kile cheti cha uthibitisho wa kupata chanjo kwa Tsh 30,000/= ila nisichanje kabisa, ila nikawakatalia na kuamua kuchanja na kupata cheti.
1. Nilitishwa nikichanja nitakufa hapo hapo cha kushangaza hadi muda huu napumua.
2. Nilitishwa nikichanja nitasikia kizunguzungu ila nashangaa hadi sasa sizunguki na kichwa changu.
3. Nilitishwa nikichanja nitasikia mno maumivu ya mwili ila hadi sasa sisikii maumivu yoyote zaidi tu ya hawa mbu wanaokesha nami usiku kucha.
4. Nilitishwa nikichanja tu nitaanza kujikuta naokota makopo (nadata mazima) ila hadi muda huu medulla oblangata yangu iko vyedi (vyema) kabisa.
5. Nilitishwa nikichanja tu nitakosa hamu ya kula na nashangaa mpaka muda huu nimeshafuta sahani tatu za ugali wa ulezi, mtama na kichuri na nimeomba nipikiwe mwingine.
6. Nilitishwa nikichanja uono wangu utakuwa hafifu (sitoona vizuri) ila ninaona vizuri kabisa
7. Nilitishwa nikichanja tu basi hapo hapo nyara baioloji yangu ya kufyatua watoto itazima mazima ila nikashangaa dakika 30 baada ya kuchanja imepitia majaribio na iko vizuri kabisa.
Asante sana Daktari uliyenichanja Chanjo ya UVIKO-19 leo na wale Majuha wote mnaotisha watu kuwa wasichanje kwakuwa itawaathiri acheni mara moja kufanya hivyo, ila wimbi la UVIKO-19 likija na kupukutisha ndugu zako usianze kusema kuwa umerogwa au una nuksi au Mwenyezi Mungu hakupendi.
1. Nilitishwa nikichanja nitakufa hapo hapo cha kushangaza hadi muda huu napumua.
2. Nilitishwa nikichanja nitasikia kizunguzungu ila nashangaa hadi sasa sizunguki na kichwa changu.
3. Nilitishwa nikichanja nitasikia mno maumivu ya mwili ila hadi sasa sisikii maumivu yoyote zaidi tu ya hawa mbu wanaokesha nami usiku kucha.
4. Nilitishwa nikichanja tu nitaanza kujikuta naokota makopo (nadata mazima) ila hadi muda huu medulla oblangata yangu iko vyedi (vyema) kabisa.
5. Nilitishwa nikichanja tu nitakosa hamu ya kula na nashangaa mpaka muda huu nimeshafuta sahani tatu za ugali wa ulezi, mtama na kichuri na nimeomba nipikiwe mwingine.
6. Nilitishwa nikichanja uono wangu utakuwa hafifu (sitoona vizuri) ila ninaona vizuri kabisa
7. Nilitishwa nikichanja tu basi hapo hapo nyara baioloji yangu ya kufyatua watoto itazima mazima ila nikashangaa dakika 30 baada ya kuchanja imepitia majaribio na iko vizuri kabisa.
Asante sana Daktari uliyenichanja Chanjo ya UVIKO-19 leo na wale Majuha wote mnaotisha watu kuwa wasichanje kwakuwa itawaathiri acheni mara moja kufanya hivyo, ila wimbi la UVIKO-19 likija na kupukutisha ndugu zako usianze kusema kuwa umerogwa au una nuksi au Mwenyezi Mungu hakupendi.