political monger senior

JF-Expert Member
Nov 26, 2020
1,802
5,788
MAPINDUZI YA NIGER YANA MASILAHI MAPANA KWA URUSI NA HASARA KUBWA KWA NCHI ZA MAGHARIBI.

Yawezekana ukawa miongoni mwa wanaojiuliza ni kwanini ECOWAS, Ufaransa na Marekani wanatolea macho mapinduzi ya Niger?

Leo nitakupatia madini. Kumbuka makala hii ni ndefu hivyo usiwe mvivu. Jitahidi usome mwanzo hadi mwisho na kwa utulivu wa hali ya juu utapata madini. Na ili uweze kunielewa vizuri, inabidi uwe mtaalam wa kuunganisha "dots".

Ni hivi;- mapinduzi ya Niger yana masilahi mapana kwa Urusi na washirika wake (Afrika, Eurasian, China, Iran na North Korea) na hasara kubwa kwa nchi za Magharibi ikiwemo Ufaransa.

Kivipi?! Twende taratibu. Mimi ni Mwalim na kazi yangu ni kufundisha.

Kwanza ifahamike kuwa haya si mapinduzi ya kwanza kutokea tangu Niger kupata uhuru 1960. Nchi hiyo kutoka ukanda wa Sahel (Sahel Regions) imeshuhudia mapinduzi mara tano katika nyakati tofauti tofauti. Mapinduzi ya 1974 (Kanal Seyni Kountche), 1996 (Mahamane Ousman), 1999 (Kanal Ousman - anauawa), 2000 (Mahmadou Tandja), 2010 (Supreme Council wawakamata Tandja na Mawaziri wake), 2023 (General Tchiani)

Kwa maana hiyo haya si mapinduzi ya kwanza kutokea nchini Niger, lakini jiulize ni kwanini awamu hii Ufaransa, Marekani na Umoja wa Nchi za Kiuchumi kutoka Magharibi (ECOWAS) wameyavalia njuga?!

Marekani na Ufaransa kupitia Black Water, na Urusi kupitia Wagner wana majeshi yao nchini Niger. Marekani ana "base" mbili nchini humo, moja ikiwa kwenye mji mkuu wa Niamey. Kisingizio kikubwa cha uwepo wa majeshi hayo ni vita dhidi ya ugaidi. Ajabu ni kwamba, wala hawashirikiani katika vita hivyo. Kila nchi inapambana kivyake.

Je, ni kweli nchini Niger kuna ugaidi?!

Hili ni swali nyeti na linahitaji chapisho maalumu kulijibu. Lakini kwa kifupi tu ni kwamba, nchi zenye nguvu kijeshi zimekuwa zikitumia kisingizio cha UGAIDI kama njia ya kuhalalamisha uvamizi wao katika nchi ambazo wana maslahi nazo. Ukweli ni kwamba, wao ndio huunda makundi ya kigaidi, huku wakigawa silaha pande zote mbili (upande wa serikali na upande wa magaidi). Lengo lako ni kuondoa utulivu katika nchi hizo. Wakati zikiwa katika misuko suko ya kupambana na ugaidi, wao hutumia mwanya huo kupora rasilimali kama vile;- dhahabu, mafuta nk. Huu ndio ukweli uliofichwa.

Sasa tuangalie, mapinduzi haya yana masilahi gani kwa Urusi?! Na hasara gani kwa nchi za Magharibi ikiwemo Ufaransa?!

Ufaransa; ni miongoni mwa nchi zilizoathirika kwa kiasi kikubwa kwenye upande wa "geopolitics" kutokana na mapinduzi yanayoendelea kwenye nchi za ukanda wa Sahel. Nchi nne za ukanda huu (Chad, Mali, Burkina Faso na sasa Niger) zimewatimua Ufaransa. Na baada ya mapinduzi ya Niger Rais Macron anasema kwamba, iwapo maslahi ya Ufaransa yataaathiriwa na mapinduzi ya nchini Niger, hawatosita kuchukua hatua.

Hebu tuangalie, ni maslahi gani ya Ufaransa anayozungumzia Rais Macron ambayo yapo kwenye ardhi ya Niger?!

Niger ni miongoni mwa nchi zenye utajiri mkubwa wa Urenium. Asilimia zaidi ya 60 ya umeme unaotumika nchini Ufaransa unategemea Urenium kutoka Niger. Lakini pia Niger ni miongoni mwa nchi zenye umasikini mkubwa, ikishika nafasi ya saba katika nchi masikini duniani. Wakati ambapo Ufaransa anategemea 60% ya umeme kupitia Ureniam inayopatikana Niger, zaidi ya 80% ya raia wa Niger wanaishi bila umeme.

Sasa tuangalie Urusi wana maslahi kwenye mapinduzi haya?!

Kama nilivyosema hapo awali, inabidi uwe mtaalam wa ku-connet dot. Sasa twende pamoja. Hebu tazama kwa umakini (ramani) kwenye hizo picha mbili. Tuanze na picha ya kwanza ambayo inaonyesha nchi za ukanda wa Sahel. Kwanza, utagundua hizo nchi zote ziliwekwa rangi zinatawaliwa kijeshi. Kati ya hizo nchi zote ni nchi moja tu (Niger) ndio ilikuwa katika utawala wa Kidemokrasia, nayo imaefanya mapinduzi na kuingia katika utawala wa kijeshi.

Pili, utagundua kuwa hizo nchi (zenye rangi) zipo katika mpangilio ambao unaweza kusema ni kama unatengeneza njia. Ndioooo, hiyo ni njia ya kibiashara kutoka Senegal hadi Eritrea. Njia hiyo inatengenezwa na Urusi kama mbadala wa njia inayotumika hivi sasa.

Sasa ili unielewe nachomaanisha, hebu twende kwenye picha ya pili.

Katika mfumo wa njia za kibiashara, kuna "Choke Point" mbili ambazo ni muhimu sana duniani, nazo ni;- Suez Canal (Egypt) Bosporus Strait (Turkey). Njia ya kwanza ni Suez Canal;- ndio hiyo yenye msitari wa rangi ya blue. Hiyo ndio njia ya kibiashara inayotumika hivi sasa ambapo kitu kinapotoka Urusi ni lazima kipite kwenye nchi za Finland, Sweden, UK, kisha kizunguke hadi France, Spain, kije kwenye Mediterranean Sea, kipite kwenye "Swiss Canal" alafu ndio kiende India au kwenye nchi za Afrika.

Njia ya pili ni Bosporus Strait: Kitu kitoke Urusi kipite Black Sea, kisha kipitie Uturuki (Bosporus Strait) ambapo ngano yote kutoka Ukraine na Urusi ni lazima ipitie hapo, kisha kiende hadi Swiss Canal (Egypt) alafu ndio kiingie India na kwingineko ikiwemo Afrika. Na "Choke Point" zote hizi, zipo chini ya "control" ya nchi za Magharibi. Kwahiyo wanazitumia kama fimbo katika kuhakikisha matakwa yao yanafuatwa.

Angalia msitari wenye rangi ya chenza au kwa urahisi njano: Hiyo ndio njia mpya inayochongwa na Urusi. Baada ya kufanikiwa kuunganisha njia ya "SAHEL REGIONS", maana yake mzigo utatoka St Petersburg - Urusi, utapita kwenye bandari ya Astrakhan, kisha utapita Caspian Sea, na utakwenda hadi Tehran nchini Iran. Ukifika hapo unachukua njia ya reli na utakwenda moja kwa moja hadi Chabahar Port. Ukishafika hapo utaingia kwenye Arabian Sea na utaweza kufika mahali popote pale duniani.

Je, Urusi anahusika na mapinduzi haya?!

Bila shaka jibu ni ndio. Na ili kuthibitisha hilo hebu turejee kwenye mkutano wa Putin na viongozi wa nchi za Afrika. Mkutano huo Putin aliupa jina la "New World Multpolar Structure". Na kwa wasifahamu "Multpolar" mifumo tofauti tofauti ya kiungozi isiyotegemea mfumo mmoja. Inaweza kuwa miwili, mitatu au zaidi. Katika mkutano huo Rais Putin aliwaambia viongozi wa Afrika kwamba, lengo lake ni kumtaka kuwakomboa dhidi ya ukoloni wa kisasa. Yaani Afrika isiwe tegemezi kwa nchi Magharibi.

Kwenye mkutano huo viongozi wa nchi 49 kati ya nchi 54 za Afrika walihuduria. Rais Putin alitoa msahama wa deni la US Dollar Bilioni 23 kwa nchi Afrika. Huu ni msamaha mkubwa kuwahi kutokea tangu dunia kuumbwa. Pamoja na msamaha huo, pia aliahidi msaada upande wa teknolojia, kilimo, jeshi, mawasiliano, huku ahadi kubwa ikiwa ni;- kuzikwamua nchi za Afrika katika ukoloni (decolonization).

Katika nchi 5 ambazo hazikuhudhuria mkutano wa Putin, mbili ya hizo ni Nigeria pamoja na Rais Muhamed Bazoum wa Niger kabla ya hajapinduliwa. Kumbuka Nigeria ndio kiongozi wa ECOWAS. Na baada ya mapinduzi nchini Niger ECOWAS iliongozwa na Nigeria wakatishia kuivamia kijeshi Niger. Guinea ambayo nayo ni mwanachama wa ECOWAS wakasema kwamba hawatoshiriki katika kuingiza jeshi nchini Niger. Mali na Burkina Faso wakatamka wazi wazi kwamba kuivamia Niger kijeshi ni sawa na kutangaza vita na sisi. Wakati huo huo Algeria akatoa tamko kwamba hatokuwa kimya akiona jirani yake (Niger) anashambuliwa. Jana ECOWAS wametoa tamko la kubadili uwamuzi wa kuvamia kijeshi Niger.

Nadhani sasa utakuwa umeelewa, ni kwa kiasi gani mapinduzi ya Niger yana maslahi mapana kwa Urusi na hasara kubwa kwa upande wa Magharibi. Na ili usiwe na shaka juu ya "analysis" hii nakushauri, nenda kasome kitu kinachoitwa "How Iran-Russia railway deal cold be game-changer for global transit".

Kumbuka;- "if you don't have research no right to speak".

...political monger senior.
View attachment 2718239View attachment 2718240
 
Mwalimu, US ananufaika vipi na bokoramu?.
Swali moja la kujiuliza NIGERIA wanachimba mafuta lakini mpaka leo hii hawana Refinery yaani kiwanda cha kuyatengeneza ayo mafuta kutoka kuwa kwenye barrel yaani mafuta ghafi kuja kwenye mafuta safi kwaajili ya matumizi.. USA anahakikisha NIGERIA wasiwe na Amani kwa kum keep busy na vita dhidi ya Boko haram uku yeye akija kama msaidizi wa kukusaidia kuwatokomeza uku Akichukua Raslimali zako kama malipo ya Ulinzi wake ..
 
Swali moja la kujiuliza NIGERIA wanachimba mafuta lakini mpaka leo hii hawana Refinery yaani kiwanda cha kuyatengeneza ayo mafuta kutoka kuwa kwenye barrel yaani mafuta ghafi kuja kwenye mafuta safi kwaajili ya matumizi.. USA anahakikisha NIGERIA wasiwe na Amani kwa kum keep busy na vita dhidi ya Boko haram uku yeye akija kama msaidizi wa kukusaidia kuwatokomeza uku Akichukua Raslimali zako kama malipo ya Ulinzi wake ..
Mwalimu,nimeuliza marekani ananufaika vipi na bokoharamu?
Ukinijibu ili huo ufafanuzi mwingine unaojaribu kuutoa will fall in a place itself.
 
.
20230408_220002.jpg
 
Swali moja la kujiuliza NIGERIA wanachimba mafuta lakini mpaka leo hii hawana Refinery yaani kiwanda cha kuyatengeneza ayo mafuta kutoka kuwa kwenye barrel yaani mafuta ghafi kuja kwenye mafuta safi kwaajili ya matumizi.. USA anahakikisha NIGERIA wasiwe na Amani kwa kum keep busy na vita dhidi ya Boko haram uku yeye akija kama msaidizi wa kukusaidia kuwatokomeza uku Akichukua Raslimali zako kama malipo ya Ulinzi wake ..
Waalimu wa tanzania wengi ni Guruguja.ndiyo maana CCM inawatumia then Inawa- dustbin.
Kitendo cha kusema Nigeria haijawi kuwa na refinery kumeshapoteza umaana wa post yako.
Ulichokindika ni porojo tupu za kufanya mazombi(maafrika) yajisikie Amani bandia kwa kudhani shida walizonazo chanzo ni mataifa ya nje.
Bure kabisa.
 
Mwalimu,nimeuliza marekani ananufaika vipi na bokoharamu?
Ukinijibu ili huo ufafanuzi mwingine unaojaribu kuutoa will fall in a place itself.
Unajua NIGERIA inasemekana ndio nchi yenye uchumi mkubwa AFRICA? ngoja nikuelezee kidogo How this BIG BOYS DO(WEST) Nigeria bila kuwa ma migogoro ya ndani kwa ndani mpaka muda huu ingekuwa mbali sana kiuchumi kuzipita karibu nchi nyingi za ulaya..USA na washirika wake wanajua kabisa kitendo cha kukuacha kuwa na uchumi mkubwa ni kuwa threat kwao kwakuwa utaweza kujitegemea almost kwa kila kitu means utakuwa na power ya kufanya mambo yako bila wao kuitajika 1st watapoteza ushawishi kwako 2nd utakuwa kama darasa kwa wengine kufanya kama ulivyofanya wao na wao kupoteza makoloni yao(neo colonialism) na kingine ni wao kukosa cheap energy au resources kutoka kwako ndio mahana mafuta yanachimbwa NIGERIA yanaenda kusafishiwa USA or INDIA then unakuja kuuziwa tena wewe mwenyewe why wasijenge Refinery apo kwako au kukuacha ujenge Refinery apo kwako? Kulikuwa na tetesi kuwa dangote anataka kujenga Refinery apo NIGERIA ikaja kugundulika kuwa ni siasa tu na wala hakuna kitu kama icho...niitimishe Boko haram wapo pale ili nchi ikose utulivu na wewe usiweze kupiga hatua zaidi na kuweza kutumia resources zako vizuri uku wao wakinufaika na mikataba ya ulinzi na misaada wanayokupa.
 
MAPINDUZI YA NIGER YANA MASILAHI MAPANA KWA URUSI NA HASARA KUBWA KWA NCHI ZA MAGHARIBI.

Yawezekana ukawa miongoni mwa wanaojiuliza ni kwanini ECOWAS, Ufaransa na Marekani wanatolea macho mapinduzi ya Niger?!

Leo nitakupatia madini. Kumbuka makala hii ni ndefu hivyo usiwe mvivu. Jitahidi usome mwanzo hadi mwisho na kwa utulivu wa hali ya juu utapata madini. Na ili uweze kunielewa vizuri, inabidi uwe mtaalam wa kuunganisha "dots".

Ni hivi;- mapinduzi ya Niger yana masilahi mapana kwa Urusi na washirika wake (Afrika, Eurasian, China, Iran na North Korea) na hasara kubwa kwa nchi za Magharibi ikiwemo Ufaransa.

Kivipi?! Twende taratibu. Mimi ni Mwalim na kazi yangu ni kufundisha.

Kwanza ifahamike kuwa haya si mapinduzi ya kwanza kutokea tangu Niger kupata uhuru 1960. Nchi hiyo kutoka ukanda wa Sahel (Sahel Regions) imeshuhudia mapinduzi mara tano katika nyakati tofauti tofauti. Mapinduzi ya 1974 (Kanal Seyni Kountche), 1996 (Mahamane Ousman), 1999 (Kanal Ousman - anauawa), 2000 (Mahmadou Tandja), 2010 (Supreme Council wawakamata Tandja na Mawaziri wake), 2023 (General Tchiani)

Kwa maana hiyo haya si mapinduzi ya kwanza kutokea nchini Niger, lakini jiulize ni kwanini awamu hii Ufaransa, Marekani na Umoja wa Nchi za Kiuchumi kutoka Magharibi (ECOWAS) wameyavalia njuga?!

Marekani na Ufaransa kupitia Black Water, na Urusi kupitia Wagner wana majeshi yao nchini Niger. Marekani ana "base" mbili nchini humo, moja ikiwa kwenye mji mkuu wa Niamey. Kisingizio kikubwa cha uwepo wa majeshi hayo ni vita dhidi ya ugaidi. Ajabu ni kwamba, wala hawashirikiani katika vita hivyo. Kila nchi inapambana kivyake.

Je, ni kweli nchini Niger kuna ugaidi?!

Hili ni swali nyeti na linahitaji chapisho maalumu kulijibu. Lakini kwa kifupi tu ni kwamba, nchi zenye nguvu kijeshi zimekuwa zikitumia kisingizio cha UGAIDI kama njia ya kuhalalamisha uvamizi wao katika nchi ambazo wana maslahi nazo. Ukweli ni kwamba, wao ndio huunda makundi ya kigaidi, huku wakigawa silaha pande zote mbili (upande wa serikali na upande wa magaidi). Lengo lako ni kuondoa utulivu katika nchi hizo. Wakati zikiwa katika misuko suko ya kupambana na ugaidi, wao hutumia mwanya huo kupora rasilimali kama vile;- dhahabu, mafuta nk. Huu ndio ukweli uliofichwa.

Sasa tuangalie, mapinduzi haya yana masilahi gani kwa Urusi?! Na hasara gani kwa nchi za Magharibi ikiwemo Ufaransa?!

Ufaransa; ni miongoni mwa nchi zilizoathirika kwa kiasi kikubwa kwenye upande wa "geopolitics" kutokana na mapinduzi yanayoendelea kwenye nchi za ukanda wa Sahel. Nchi nne za ukanda huu (Chad, Mali, Burkina Faso na sasa Niger) zimewatimua Ufaransa. Na baada ya mapinduzi ya Niger Rais Macron anasema kwamba, iwapo maslahi ya Ufaransa yataaathiriwa na mapinduzi ya nchini Niger, hawatosita kuchukua hatua.

Hebu tuangalie, ni maslahi gani ya Ufaransa anayozungumzia Rais Macron ambayo yapo kwenye ardhi ya Niger?!

Niger ni miongoni mwa nchi zenye utajiri mkubwa wa Urenium. Asilimia zaidi ya 60 ya umeme unaotumika nchini Ufaransa unategemea Urenium kutoka Niger. Lakini pia Niger ni miongoni mwa nchi zenye umasikini mkubwa, ikishika nafasi ya saba katika nchi masikini duniani. Wakati ambapo Ufaransa anategemea 60% ya umeme kupitia Ureniam inayopatikana Niger, zaidi ya 80% ya raia wa Niger wanaishi bila umeme.

Sasa tuangalie Urusi wana maslahi kwenye mapinduzi haya?!

Kama nilivyosema hapo awali, inabidi uwe mtaalam wa ku-connet dot. Sasa twende pamoja. Hebu tazama kwa umakini (ramani) kwenye hizo picha mbili. Tuanze na picha ya kwanza ambayo inaonyesha nchi za ukanda wa Sahel. Kwanza, utagundua hizo nchi zote ziliwekwa rangi zinatawaliwa kijeshi. Kati ya hizo nchi zote ni nchi moja tu (Niger) ndio ilikuwa katika utawala wa Kidemokrasia, nayo imaefanya mapinduzi na kuingia katika utawala wa kijeshi.

Pili, utagundua kuwa hizo nchi (zenye rangi) zipo katika mpangilio ambao unaweza kusema ni kama unatengeneza njia. Ndioooo, hiyo ni njia ya kibiashara kutoka Senegal hadi Eritrea. Njia hiyo inatengenezwa na Urusi kama mbadala wa njia inayotumika hivi sasa.

Sasa ili unielewe nachomaanisha, hebu twende kwenye picha ya pili.

Katika mfumo wa njia za kibiashara, kuna "Choke Point" mbili ambazo ni muhimu sana duniani, nazo ni;- Suez Canal (Egypt) Bosporus Strait (Turkey). Njia ya kwanza ni Suez Canal;- ndio hiyo yenye msitari wa rangi ya blue. Hiyo ndio njia ya kibiashara inayotumika hivi sasa ambapo kitu kinapotoka Urusi ni lazima kipite kwenye nchi za Finland, Sweden, UK, kisha kizunguke hadi France, Spain, kije kwenye Mediterranean Sea, kipite kwenye "Swiss Canal" alafu ndio kiende India au kwenye nchi za Afrika.

Njia ya pili ni Bosporus Strait: Kitu kitoke Urusi kipite Black Sea, kisha kipitie Uturuki (Bosporus Strait) ambapo ngano yote kutoka Ukraine na Urusi ni lazima ipitie hapo, kisha kiende hadi Swiss Canal (Egypt) alafu ndio kiingie India na kwingineko ikiwemo Afrika. Na "Choke Point" zote hizi, zipo chini ya "control" ya nchi za Magharibi. Kwahiyo wanazitumia kama fimbo katika kuhakikisha matakwa yao yanafuatwa.

Angalia msitari wenye rangi ya chenza au kwa urahisi njano: Hiyo ndio njia mpya inayochongwa na Urusi. Baada ya kufanikiwa kuunganisha njia ya "SAHEL REGIONS", maana yake mzigo utatoka St Petersburg - Urusi, utapita kwenye bandari ya Astrakhan, kisha utapita Caspian Sea, na utakwenda hadi Tehran nchini Iran. Ukifika hapo unachukua njia ya reli na utakwenda moja kwa moja hadi Chabahar Port. Ukishafika hapo utaingia kwenye Arabian Sea na utaweza kufika mahali popote pale duniani.

Je, Urusi anahusika na mapinduzi haya?!

Bila shaka jibu ni ndio. Na ili kuthibitisha hilo hebu turejee kwenye mkutano wa Putin na viongozi wa nchi za Afrika. Mkutano huo Putin aliupa jina la "New World Multpolar Structure". Na kwa wasifahamu "Multpolar" mifumo tofauti tofauti ya kiungozi isiyotegemea mfumo mmoja. Inaweza kuwa miwili, mitatu au zaidi. Katika mkutano huo Rais Putin aliwaambia viongozi wa Afrika kwamba, lengo lake ni kumtaka kuwakomboa dhidi ya ukoloni wa kisasa. Yaani Afrika isiwe tegemezi kwa nchi Magharibi.

Kwenye mkutano huo viongozi wa nchi 49 kati ya nchi 54 za Afrika walihuduria. Rais Putin alitoa msahama wa deni la US Dollar Bilioni 23 kwa nchi Afrika. Huu ni msamaha mkubwa kuwahi kutokea tangu dunia kuumbwa. Pamoja na msamaha huo, pia aliahidi msaada upande wa teknolojia, kilimo, jeshi, mawasiliano, huku ahadi kubwa ikiwa ni;- kuzikwamua nchi za Afrika katika ukoloni (decolonization).

Katika nchi 5 ambazo hazikuhudhuria mkutano wa Putin, mbili ya hizo ni Nigeria pamoja na Rais Muhamed Bazoum wa Niger kabla ya hajapinduliwa. Kumbuka Nigeria ndio kiongozi wa ECOWAS. Na baada ya mapinduzi nchini Niger ECOWAS iliongozwa na Nigeria wakatishia kuivamia kijeshi Niger. Guinea ambayo nayo ni mwanachama wa ECOWAS wakasema kwamba hawatoshiriki katika kuingiza jeshi nchini Niger. Mali na Burkina Faso wakatamka wazi wazi kwamba kuivamia Niger kijeshi ni sawa na kutangaza vita na sisi. Wakati huo huo Algeria akatoa tamko kwamba hatokuwa kimya akiona jirani yake (Niger) anashambuliwa. Jana ECOWAS wametoa tamko la kubadili uwamuzi wa kuvamia kijeshi Niger.

Nadhani sasa utakuwa umeelewa, ni kwa kiasi gani mapinduzi ya Niger yana maslahi mapana kwa Urusi na hasara kubwa kwa upande wa Magharibi. Na ili usiwe na shaka juu ya "analysis" hii nakushauri, nenda kasome kitu kinachoitwa "How Iran-Russia railway deal cold be game-changer for global transit".

Kumbuka;- "if you don't have research no right to speak".

...political monger senior.
View attachment 2718239View attachment 2718240
Siamini kama hata wewe mwenyewe unaelewa ulichoandika.
 
Unajua NIGERIA inasemekana ndio nchi yenye uchumi mkubwa AFRICA? ngoja nikuelezee kidogo How this BIG BOYS DO(WEST) Nigeria bila kuwa ma migogoro ya ndani kwa ndani mpaka muda huu ingekuwa mbali sana kiuchumi kuzipita karibu nchi nyingi za ulaya..USA na washirika wake wanajua kabisa kitendo cha kukuacha kuwa na uchumi mkubwa ni kuwa threat kwao kwakuwa utaweza kujitegemea almost kwa kila kitu means utakuwa na power ya kufanya mambo yako bila wao kuitajika 1st watapoteza ushawishi kwako 2nd utakuwa kama darasa kwa wengine kufanya kama ulivyofanya wao na wao kupoteza makoloni yao(neo colonialism) na kingine ni wao kukosa cheap energy au resources kutoka kwako ndio mahana mafuta yanachimbwa NIGERIA yanaenda kusafishiwa USA or INDIA then unakuja kuuziwa tena wewe mwenyewe why wasijenge Refinery apo kwako au kukuacha ujenge Refinery apo kwako? Kulikuwa na tetesi kuwa dangote anataka kujenga Refinery apo NIGERIA ikaja kugundulika kuwa ni siasa tu na wala hakuna kitu kama icho...niitimishe Boko haram wapo pale ili nchi ikose utulivu na wewe usiweze kupiga hatua zaidi na kuweza kutumia resources zako vizuri uku wao wakinufaika na mikataba ya ulinzi na misaada wanayokupa.
Mwalimu/Rabi.ficha porojo zako.nimekuuliza swali dogo tu umebaki kuzunguka tu huku ukitaja taja mavitu mengi mengi yasiyo na maana katika hili somo lako.
Nigeria Ina Refinery nyingi ila zilifungwa wakati wa Kolona baada ya uzalishaji kudolola hivi juzi Tinubu katoa zaidi ya $25 billion kuzifix ili zianze kazi.
Furthermore US haihitaji mafuta ya Nigeria,wanunuzi wakuu wa mafuta ya Nigeria kwa Africa ni Dangote ni upandr wa nje ya Africa ni Spain na India.Sasa sijui ni kwanini US atengeneze ugaidi Nigeria alafu mnufaika awe India na Spain?.
Vikundi Virginia vya kigaidi Africa vinatengenezwa na nchi za mashariki ya Kati.si kwamba nyie waalimu hamuijui fact hii,mnaijua ila walimu uwongo ni sehemu ya taaluma yenu ndiyo maana hupo hapa kudanganya.
 
Mwalimu/Rabi.ficha porojo zako.nimekuuliza swali dogo tu umebaki kuzunguka tu huku ukitaja taja mavitu mengi mengi yasiyo na maana katika hili somo lako.
Nigeria Ina Refinery nyingi ila zilifungwa wakati wa Kolona baada ya uzalishaji kudolola hivi juzi Tinubu katoa zaidi ya $25 billion kuzifix ili zianze kazi.
Furthermore US haihitaji mafuta ya Nigeria,wanunuzi wakuu wa mafuta ya Nigeria kwa Africa ni Dangote ni upandr wa nje ya Africa ni Spain na India.Sasa sijui ni kwanini US atengeneze ugaidi Nigeria alafu mnufaika awe India na Spain?.
Vikundi Virginia vya kigaidi Africa vinatengenezwa na nchi za mashariki ya Kati.si kwamba nyie waalimu hamuijui fact hii,mnaijua ila walimu uwongo ni sehemu ya taaluma yenu ndiyo maana hupo hapa kudanganya.
Ulichokiandika ni porojo ni kama una chuki binafsi na mto mada.

Maendeleo hayana chama
 
MAPINDUZI YA NIGER YANA MASILAHI MAPANA KWA URUSI NA HASARA KUBWA KWA NCHI ZA MAGHARIBI.

Yawezekana ukawa miongoni mwa wanaojiuliza ni kwanini ECOWAS, Ufaransa na Marekani wanatolea macho mapinduzi ya Niger?

Leo nitakupatia madini. Kumbuka makala hii ni ndefu hivyo usiwe mvivu. Jitahidi usome mwanzo hadi mwisho na kwa utulivu wa hali ya juu utapata madini. Na ili uweze kunielewa vizuri, inabidi uwe mtaalam wa kuunganisha "dots".

Ni hivi;- mapinduzi ya Niger yana masilahi mapana kwa Urusi na washirika wake (Afrika, Eurasian, China, Iran na North Korea) na hasara kubwa kwa nchi za Magharibi ikiwemo Ufaransa.

Kivipi?! Twende taratibu. Mimi ni Mwalim na kazi yangu ni kufundisha.

Kwanza ifahamike kuwa haya si mapinduzi ya kwanza kutokea tangu Niger kupata uhuru 1960. Nchi hiyo kutoka ukanda wa Sahel (Sahel Regions) imeshuhudia mapinduzi mara tano katika nyakati tofauti tofauti. Mapinduzi ya 1974 (Kanal Seyni Kountche), 1996 (Mahamane Ousman), 1999 (Kanal Ousman - anauawa), 2000 (Mahmadou Tandja), 2010 (Supreme Council wawakamata Tandja na Mawaziri wake), 2023 (General Tchiani)

Kwa maana hiyo haya si mapinduzi ya kwanza kutokea nchini Niger, lakini jiulize ni kwanini awamu hii Ufaransa, Marekani na Umoja wa Nchi za Kiuchumi kutoka Magharibi (ECOWAS) wameyavalia njuga?!

Marekani na Ufaransa kupitia Black Water, na Urusi kupitia Wagner wana majeshi yao nchini Niger. Marekani ana "base" mbili nchini humo, moja ikiwa kwenye mji mkuu wa Niamey. Kisingizio kikubwa cha uwepo wa majeshi hayo ni vita dhidi ya ugaidi. Ajabu ni kwamba, wala hawashirikiani katika vita hivyo. Kila nchi inapambana kivyake.

Je, ni kweli nchini Niger kuna ugaidi?!

Hili ni swali nyeti na linahitaji chapisho maalumu kulijibu. Lakini kwa kifupi tu ni kwamba, nchi zenye nguvu kijeshi zimekuwa zikitumia kisingizio cha UGAIDI kama njia ya kuhalalamisha uvamizi wao katika nchi ambazo wana maslahi nazo. Ukweli ni kwamba, wao ndio huunda makundi ya kigaidi, huku wakigawa silaha pande zote mbili (upande wa serikali na upande wa magaidi). Lengo lako ni kuondoa utulivu katika nchi hizo. Wakati zikiwa katika misuko suko ya kupambana na ugaidi, wao hutumia mwanya huo kupora rasilimali kama vile;- dhahabu, mafuta nk. Huu ndio ukweli uliofichwa.

Sasa tuangalie, mapinduzi haya yana masilahi gani kwa Urusi?! Na hasara gani kwa nchi za Magharibi ikiwemo Ufaransa?!

Ufaransa; ni miongoni mwa nchi zilizoathirika kwa kiasi kikubwa kwenye upande wa "geopolitics" kutokana na mapinduzi yanayoendelea kwenye nchi za ukanda wa Sahel. Nchi nne za ukanda huu (Chad, Mali, Burkina Faso na sasa Niger) zimewatimua Ufaransa. Na baada ya mapinduzi ya Niger Rais Macron anasema kwamba, iwapo maslahi ya Ufaransa yataaathiriwa na mapinduzi ya nchini Niger, hawatosita kuchukua hatua.

Hebu tuangalie, ni maslahi gani ya Ufaransa anayozungumzia Rais Macron ambayo yapo kwenye ardhi ya Niger?!

Niger ni miongoni mwa nchi zenye utajiri mkubwa wa Urenium. Asilimia zaidi ya 60 ya umeme unaotumika nchini Ufaransa unategemea Urenium kutoka Niger. Lakini pia Niger ni miongoni mwa nchi zenye umasikini mkubwa, ikishika nafasi ya saba katika nchi masikini duniani. Wakati ambapo Ufaransa anategemea 60% ya umeme kupitia Ureniam inayopatikana Niger, zaidi ya 80% ya raia wa Niger wanaishi bila umeme.

Sasa tuangalie Urusi wana maslahi kwenye mapinduzi haya?!

Kama nilivyosema hapo awali, inabidi uwe mtaalam wa ku-connet dot. Sasa twende pamoja. Hebu tazama kwa umakini (ramani) kwenye hizo picha mbili. Tuanze na picha ya kwanza ambayo inaonyesha nchi za ukanda wa Sahel. Kwanza, utagundua hizo nchi zote ziliwekwa rangi zinatawaliwa kijeshi. Kati ya hizo nchi zote ni nchi moja tu (Niger) ndio ilikuwa katika utawala wa Kidemokrasia, nayo imaefanya mapinduzi na kuingia katika utawala wa kijeshi.

Pili, utagundua kuwa hizo nchi (zenye rangi) zipo katika mpangilio ambao unaweza kusema ni kama unatengeneza njia. Ndioooo, hiyo ni njia ya kibiashara kutoka Senegal hadi Eritrea. Njia hiyo inatengenezwa na Urusi kama mbadala wa njia inayotumika hivi sasa.

Sasa ili unielewe nachomaanisha, hebu twende kwenye picha ya pili.

Katika mfumo wa njia za kibiashara, kuna "Choke Point" mbili ambazo ni muhimu sana duniani, nazo ni;- Suez Canal (Egypt) Bosporus Strait (Turkey). Njia ya kwanza ni Suez Canal;- ndio hiyo yenye msitari wa rangi ya blue. Hiyo ndio njia ya kibiashara inayotumika hivi sasa ambapo kitu kinapotoka Urusi ni lazima kipite kwenye nchi za Finland, Sweden, UK, kisha kizunguke hadi France, Spain, kije kwenye Mediterranean Sea, kipite kwenye "Swiss Canal" alafu ndio kiende India au kwenye nchi za Afrika.

Njia ya pili ni Bosporus Strait: Kitu kitoke Urusi kipite Black Sea, kisha kipitie Uturuki (Bosporus Strait) ambapo ngano yote kutoka Ukraine na Urusi ni lazima ipitie hapo, kisha kiende hadi Swiss Canal (Egypt) alafu ndio kiingie India na kwingineko ikiwemo Afrika. Na "Choke Point" zote hizi, zipo chini ya "control" ya nchi za Magharibi. Kwahiyo wanazitumia kama fimbo katika kuhakikisha matakwa yao yanafuatwa.

Angalia msitari wenye rangi ya chenza au kwa urahisi njano: Hiyo ndio njia mpya inayochongwa na Urusi. Baada ya kufanikiwa kuunganisha njia ya "SAHEL REGIONS", maana yake mzigo utatoka St Petersburg - Urusi, utapita kwenye bandari ya Astrakhan, kisha utapita Caspian Sea, na utakwenda hadi Tehran nchini Iran. Ukifika hapo unachukua njia ya reli na utakwenda moja kwa moja hadi Chabahar Port. Ukishafika hapo utaingia kwenye Arabian Sea na utaweza kufika mahali popote pale duniani.

Je, Urusi anahusika na mapinduzi haya?!

Bila shaka jibu ni ndio. Na ili kuthibitisha hilo hebu turejee kwenye mkutano wa Putin na viongozi wa nchi za Afrika. Mkutano huo Putin aliupa jina la "New World Multpolar Structure". Na kwa wasifahamu "Multpolar" mifumo tofauti tofauti ya kiungozi isiyotegemea mfumo mmoja. Inaweza kuwa miwili, mitatu au zaidi. Katika mkutano huo Rais Putin aliwaambia viongozi wa Afrika kwamba, lengo lake ni kumtaka kuwakomboa dhidi ya ukoloni wa kisasa. Yaani Afrika isiwe tegemezi kwa nchi Magharibi.

Kwenye mkutano huo viongozi wa nchi 49 kati ya nchi 54 za Afrika walihuduria. Rais Putin alitoa msahama wa deni la US Dollar Bilioni 23 kwa nchi Afrika. Huu ni msamaha mkubwa kuwahi kutokea tangu dunia kuumbwa. Pamoja na msamaha huo, pia aliahidi msaada upande wa teknolojia, kilimo, jeshi, mawasiliano, huku ahadi kubwa ikiwa ni;- kuzikwamua nchi za Afrika katika ukoloni (decolonization).

Katika nchi 5 ambazo hazikuhudhuria mkutano wa Putin, mbili ya hizo ni Nigeria pamoja na Rais Muhamed Bazoum wa Niger kabla ya hajapinduliwa. Kumbuka Nigeria ndio kiongozi wa ECOWAS. Na baada ya mapinduzi nchini Niger ECOWAS iliongozwa na Nigeria wakatishia kuivamia kijeshi Niger. Guinea ambayo nayo ni mwanachama wa ECOWAS wakasema kwamba hawatoshiriki katika kuingiza jeshi nchini Niger. Mali na Burkina Faso wakatamka wazi wazi kwamba kuivamia Niger kijeshi ni sawa na kutangaza vita na sisi. Wakati huo huo Algeria akatoa tamko kwamba hatokuwa kimya akiona jirani yake (Niger) anashambuliwa. Jana ECOWAS wametoa tamko la kubadili uwamuzi wa kuvamia kijeshi Niger.

Nadhani sasa utakuwa umeelewa, ni kwa kiasi gani mapinduzi ya Niger yana maslahi mapana kwa Urusi na hasara kubwa kwa upande wa Magharibi. Na ili usiwe na shaka juu ya "analysis" hii nakushauri, nenda kasome kitu kinachoitwa "How Iran-Russia railway deal cold be game-changer for global transit".

Kumbuka;- "if you don't have research no right to speak".

...political monger senior.
View attachment 2718239View attachment 2718240
Umeongelea kwa undani na mm binafsi nimekuelewa kabsa. Hivyo kama tumeyafaham haya matatizo yanayozikumba nchi zote za Africa, hivyo kipi kifanyike??? Ukijua solutions utagundua mambo si rahisi kama yalivyo
 
Swali moja la kujiuliza NIGERIA wanachimba mafuta lakini mpaka leo hii hawana Refinery yaani kiwanda cha kuyatengeneza ayo mafuta kutoka kuwa kwenye barrel yaani mafuta ghafi kuja kwenye mafuta safi kwaajili ya matumizi.. USA anahakikisha NIGERIA wasiwe na Amani kwa kum keep busy na vita dhidi ya Boko haram uku yeye akija kama msaidizi wa kukusaidia kuwatokomeza uku Akichukua Raslimali zako kama malipo ya Ulinzi wake ..
Kama ni kweli, basi tumpe pongezi US maana anatumia akili zake vizuri.
 
Waalimu wa tanzania wengi ni Guruguja.ndiyo maana CCM inawatumia then Inawa- dustbin.
Kitendo cha kusema Nigeria haijawi kuwa na refinery kumeshapoteza umaana wa post yako.
Ulichokindika ni porojo tupu za kufanya mazombi(maafrika) yajisikie Amani bandia kwa kudhani shida walizonazo chanzo ni mataifa ya nje.
Bure kabisa.
Matatizo mengi ya afrika chanzo ni sisi wenyewe
 
Back
Top Bottom