Yahusu kuchanjiwa muku

Yahusu kuchanjiwa muku

Class mate wangu alishiriki vita ya Uganda, aliporudi alinihadithia aliyoyaona ni balaa,
Naamini Nyerere alikuwa na lengo zuri sana kuzuia "UMANGARIBI" haya ma TV ndio yametufanya tuone utamaduni ni ushamba, tungeendeleza yetu si ajabu leo tusingekuwa na magonjwa ya ajabu ajabu hivi.. Unaenda kuongea na babu anakupa dawa mambo yanakuwa fresh, siku hizi mpaka mionzi, na unakufa
 
Naamini Nyerere alikuwa na lengo zuri sana kuzuia "UMANGARIBI" haya ma TV ndio yametufanya tuone utamaduni ni ushamba, tungeendeleza yetu si ajabu leo tusingekuwa na magonjwa ya ajabu ajabu hivi.. Unaenda kuongea na babu anakupa dawa mambo yanakuwa fresh, siku hizi mpaka mionzi, na unakufa
Dawa nyingi zinatokana na miti shamba, binafsi natumia remedies tu maishani ni tiba asilia mpaka wanangu
 
napenda kufahamu kama ukichanjiwa unaweza ukatolewa au kuiondoa mwilini mwako
 
mshana jr test ya muku haiishii kwenye majambia tu,; ni visu, nyembe, sindano, misumari na risasi ya ukweli ukweli lazima idufue mwili wako tena inalengwa kifuani!
Hutakiwi kuwa muoga siku ya kuchanjwa na kwenye tukio la test vinginevyo ukitestiwa inaingia mazima na risasi itakuuwa!!

Huko kigoma hii kitu inaitwa "VIDONO"
Na wakaguru wanaipata kwa mtemi wao anaitwa "JENGA" inapatikana wilaya ya Gairo kijiji cha Idibo- hakatizi maasai hapo kijijini na ikitokea kakatiza huchinjwa kama kuku na jeshi kuu la "MWANO"
Kule kanda ya ziwa inaitwa "BHULABHUKA"
Ilishawahi kututesa hii kitu mwaka juzi bibi alipofikia kufa ktk umri wake wa miaka 100+ alitusubirisha mpaka wiki mbili hafi huku mwili ukiwa umeoza ila bado angali anapumua!!!

Mwishoni alikuja mdogo wake akaamuru tutoboe juu ya paa na mwiba wa nungunungu!!!

Dunia ina maajabu acha kabisa!!
Mkuu umenikumbusha kisa cha bibi yangu mzaa baba, alikufa kifo cha mateso sana!! Alianza kuugua 2004 akafa mwaka jana 2015... Cha ajabu wakati yupo hospitali ameoza upande mmoja hatamaniki baba akaota ndoto aende kijijini kwao kuna kitu kipo kwenye sanduku la huyo bibi akakichome moto...
Kweli alikwenda na kukikuta alipokichoma moto tu huku akapigiwa simu toka mbeya mjini bibi kakata roho!! Japo hakuwahi tusimulia ni nini hasa alichoma but hali ndo hiyo.
 
yaani hii thread nimeipita mara nyingi, na kila nikipita hilo neno muku nilikua naliona tofauti...
hahahaha....aisee.kuna wengine nadhani wameshajaribu kuligeuza ili kuona kama litaleta maana waitakayo.
nimeshaisikia sana habari za watu kuchanjwa dawa za kujikinga na kifo na wengine kuwa na hirizi zinazo uhai.
 
Mkuu umenikumbusha kisa cha bibi yangu mzaa baba, alikufa kifo cha mateso sana!! Alianza kuugua 2004 akafa mwaka jana 2015... Cha ajabu wakati yupo hospitali ameoza upande mmoja hatamaniki baba akaota ndoto aende kijijini kwao kuna kitu kipo kwenye sanduku la huyo bibi akakichome moto...
Kweli alikwenda na kukikuta alipokichoma moto tu huku akapigiwa simu toka mbeya mjini bibi kakata roho!! Japo hakuwahi tusimulia ni nini hasa alichoma but hali ndo hiyo.
Lakini pia hii ya kuugua mpaka kuoza lakini mtu hafi inatokana na maagano nadhiri na viapo hasa na nguvu za giza...huyo mtu hafi mpaka atengue hayo mambo
 
Mwaka 1991 pale Lushoto huku chuo cha mahakama by then chuo cha ccm kuna jamaa maarufu sana Muuza mitumba wa enzi hizo almaarufu kama Mahmoud...huyu jamaa alipigwa karibu na daraja moja usiku na kichwa chake kinapondwa na mawe
Wale wabaya wake wakidhani wamemaliza kazi jamaa aliokotwa alfajiri akiwa bado hai na kupelekwa hospital ya Lushoto, pale alikutwa na skull fracture 11, akawahishwa KCMC Moshi ambako alikaa miezi mitatu...kesi yake ni mojawapo ya maajabu kule Lushoto miaka ile....Mahmoud alikuwa kachanjiwa muku
Ukizaliwa Ocean road ukasoma Bunge sekondari Tambaza chuo kikuu UDSM kazini Ips haya mambo utaona ni story za kusadikika
Mkuu natamani niseme kitu lakin mdomo unakuwa mzito....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom