Ya Said Fella, Ruge na washindwa....

Ya Said Fella, Ruge na washindwa....

Dudu baya kajipambanua kwa kuwa muwazi ila kuna wengi wanalia kama samaki machozi yanaenda na maji. Rubi na wengine wengi kutoka THT walishalalamika sana juu ya mawingu media. Unaweza ukaona bifu kati ya WCB. Jide wengine walioachwa kwenye fiesta kisa waligomea ujira mdogo. Yanayofanywa na clouds media wanayajua wasanii. Sie wasikilizaji tutege masikio na macho.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nakupa hizi cases uzisome uzielewe vizuri wewe na wenzako:

1. Hivi nikiwa natafuta mafundi wa kunijengea nyumba yangu nikakutafuta unijengee ukakataa kwa kuwa malipo yangu ni mabaya, nikatafuta mafundi wengine wakakubali kujenga kwa malipo yale yale ambayo ni mabaya kwako, kuna haja ya kulia lia kuwa mimi ni mnyonyaji nawalipa mafundi hela kidogo??


2. Ukiomba kazi CRDB ukakubaliwa ukapewa mkataba ukausoma ukasaini ukaambiwa siku ya kuja kuanza kazi. Ukaenda kumwambia dada yako mshahara uliokubaliana na CRDB kwenye mkataba. Dada yako ambae yeye anafanya kazi Standard Chartered bank na analipwa hela kubwa sana hapo StanChart, akakwambia CRDB ni wanyonyaji usikubali kufanya nao kazi. Kesho wewe ukakataa kufanya kazi CRDB ukabaki nyumbani unalia njaa hauna kazi na huyo dada yako wa StanChart hakusaidii chochote utailaumu CRDB au dada yako aliekurubuni ujinga??

3. Ukiwa wewe ni msanii akapatikana promoter mmoja akakwambia nina show 1 nataka ukapige kwa sh million 5. Alafu akatokea promoter mwingine (mfano Ruge) akakwambia mimi nina shows 10 za Fiesta ila dau langu ni milioni 3 kwa kila show. Wewe na akili yako ya biashara utachagua kupiga show wapi??

Kutoka kwenye hizo cases jifunze vitu hivi vitatu:
1. Dunia ya soko huru iko wazi kwa kila mtu. Unapokataa kufanya kazi kwa ujira mdogo ujue kuna wenzako watakubali kuifanya kwa ujira ule ule. Kitendo cha kuikataa na ukaanza kulia lia kuwaaminisha watu kwamba muajiri analipa ujira mdogo hakizuii wenzako kuendelea kujenga maisha. Usilazimishe wengine waikatae kama wewe


2. Unapopata kazi/deal yotote ya kukuingizia pesa usiwe mtu wa kuwahi kushikwa masikio na waliofanikiwa. Huyo aliyefanikiwa atakushauri hiyo kazi malipo yake ni mabaya usiifanye wakati yeye ana uhakika wa kuingiza hela. Na siku ukiiacha hatakusaidia pesa ila atakusaidia kusambaza malalamiko kwa kuwa alikushauri yeye uamuzi mbovu. Yeye wakati anakushairi hivyo ukibahatika kujua historia yake alipopitia unakuta alishawahi fanya kazi za kunyanyaswa na malipo mabaya saaana kuliko hata hayo lakini ndo zimemjenga na kumfanya a grow hadi hapo alipo.

3. Kwenye biashara lazima uwe na akili ya kukokotoa revenue. Usidanganywe na mtu mmoja anaekulipa hela nyingi kwa deal moja wakati kuna mwingine angeweza kukulipa hela pungufu ila akakupa deal 10! Mil 5 x 1 = Mil 5 lakini mil3 x 10 =mil 30! Sasa wewe kataa kufanya kazi ya mil 3 ukisubiri ya mil5 unaishia kuwaona wenzio wanakubali kufanya hiyi ya mil 3 unawekeza nguvu zako katika kuwalaumu kwamba wanakubali kunyonywa mara ooh jamaa ni mnyonyaji, n.k wakati wenzio wana make money. Ruge alikuwa anajua anachokifanya hata bei ya vitu vya jumla ni ndogo kuliko bei ya reja reja kwa kitu kitu kimoja kimoja.

All in all Ruge alikuwa na mapungufu yake kama binadamu, sio busara kumsema vibaya wakati amepumzika. Tumuombee apumzike pema lakini tusiwe watu wa kujoin upande wa walalamikaji bila kuumiza kichwa kwanza!

Amefariki sasa tutawaona hao walalamikaji wanakuwa kwenye mafanikio makubwa sasa. Ha ha haaaa

R.I.P kyoma Ruge

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dudu baya amekosea sana ingawa hataji jina, ila watanzania tumeishajua anamlenga nani,mtu mzima kufurahia kifo sio poa kbs kwa hilo dudu amefeli, ilikuwa inatosha kbs alivyokuwa anamsema alivyokuwa hai sasa kuna ulazima gani wa kumdhihaki marehemu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa kwangu Mimi shida ni kwamba ni kosa kisheria au ni ile wanaita moral wrong ? Kwa kile alichofanya dudubaya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama kawaida , marehem zake ni sifa njema tu.
.
IMG-20190228-WA0112.jpeg


Jr[emoji769]
 
Hatimaye Ruge amelala kwa amani... Siku zake za mwisho hazikuwa rahisi... Amepambania uhai wake kwa nguvu zake zote... Yatasemwa mengi... Yataandikwa mengi... Lakini hatimaye yataisha na maisha kusonga mbele.... Ni wiki ya Ruge...

Kwenye haya maisha kuna makundi mawili.. Kundi la washindi na kundi la washindwa.... Huwa tunaaswa sana kujifunza toka kundi la washindi... Ogopa sana kundi la washindwa... Hili kundi la washindwa linaweza kukuzushia chochote.. Kisha wakakijengea uhalisia na kukitangaza hasa... Mara nyingi hawakuzushii mema bali mabaya.... Kundi hili lina fikra za ajabu kweli... Yani kushindwa kwao kwenye lolote wanakuhusisha na wewe
Mbali ya Ruge na wadau wengine waliofanya mengi kwenye mziki wetu wa kisasa na hata kuibua vipaji vingi ni Said Fella (mkubwa Fella) naye huyu ni mhanga kama Ruge [emoji1019] japo kwa asilimia tofauti
Miaka ya mwanzoni mwa 2000 alileta mapinduzi makubwa kwenye bongo fleva kwa kuwa na kundi la kwanza lililofanikiwa sana la TMK-WANAUME...
Kundi hili lilitikisa mno likiwakilisha Uswazi na ndio likawa chachu ya kuanzishwa kwa makundi mengine rasmi kama East coast nk... Vibao vya TMK vilikuwa moto wa kuotea mbali... Nani hakumbuki Dar mpaka Moro?
Vinara wa kundi kina Juma nature wakiwa ndio wanasikika sana, wakafitinishwa, wakajazwa maneno... Upeo wa kufikiri ukawa mdogo... Wakaambiwa Fella anawanyonya, anawatumikisha wakati yeye si msanii kwahiyo anakula jasho lao bure
Sumu hii ikawaingia baadhi na chini ya Juma nature kundi la TMK-WANAUME likagawika vipande viwili.... Wenye kuona mbali wakabaki na Fella... Wenye kuona karibu wakaondoka na kuunda kundi lingine kwa mbwembwe nyingi na kutoa kibao cha kwanza NDEGE TUNDUNI... wimbo huu ulikuwa masimango tupu kwa Fella...
Fella hakutaka majibizano... Alifahamu wakati ni hakimu mzuri..... Leo hii Fella ni nani na yuko wapi na Juma nature ni nani na yuko wapi! Washindi dhidi ya washindwa....!!!
Makubwa Ruge aliyoyafanya kwenye muziki wa bongo fleva hayaonekani kwa baadhi yetu... Anatuhumiwa, anabezwa, anatukanwa, anakejeliwa... Anaitwa mnyonyaji na kila aina ya jina baya... Lakini ukiangalia wanaofanya hivyo ni akina nani!? Ni kundi dogo la washindwa.

Ruge sio malaika, Ruge sio mkamilifu ni binadamu kama binadamu mwingine yeyote yule ana changamoto zake ana kushinda na kushindwa kwake.. Ni mpambanaji anayehitaji naye kutoka kimaisha... Alifanikiwa kwa kiasi chake... Akapata alichopata.... Kuna wengine kati yetu tungepata nafasi yake pengine tungekuwa wabaya zaidi yake....
Washindwa wamepata pa kutolea nyongo zao.. Yani ugumu wao wa maisha na kushindwa kwingi lawama zote ni kwa Ruge... Ruge alikuwa mjasiriamali angefanyaje kulinda kazi yake? Rip brother!
Basi sasa kwa washindwa... Ruge kaondoka, yule mnyonyaji tapeli.. Aliyekuwa kashikilia funguo za maisha yenu.... Tunataka tuone tofauti sasa... Tunataka kuwaona mkitoka kimaisha sasa kwakuwa kikwazo kimeondoka!!!!

KATIKA MAISHA OGOPA SANA KUNDI LA WASHINDWA!!! ALWAYS LEARN FROM THE BEST....

Jr[emoji769]

kiongozi nondo zako hua ni moto sana

nanukuuutuu;

Ruge sio malaika, Ruge sio mkamilifu ni binadamu kama binadamu mwingine yeyote yule ana changamoto zake ana kushinda na kushindwa kwake watanzania yawapasa kuifaham hii code(TUACHE UNAFIKI)
 
kiongozi nondo zako hua ni moto sana

nanukuuutuu;

Ruge sio malaika, Ruge sio mkamilifu ni binadamu kama binadamu mwingine yeyote yule ana changamoto zake ana kushinda na kushindwa kwake watanzania yawapasa kuifaham hii code(TUACHE UNAFIKI)
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]

Jr[emoji769]
 
Nadhani cha Kujifunza kwa ruge ni mambo mengi sana, yakujifunza. Lakni makubwa mawili

kwanza kuwathamini binadam wengine katika kila tulifanyalo, yaani utu. Wanaolalama ni watu pia tunaweza kuwasikiliza na kusympathize. Tuelewe hisia zao hatuwezi tu kuwapuuza. Tujifunze hata kwa hilo pia, wanaojitokeza waziwazi wamekua na ujasiri huo lakini wapo wengi wanayafanya pengine makubwa zaidi chinichini.

Pili ni kua maisha ya marehemu yanatufunza kuwa wenye juhudi, kujituma na kupambana pamoja na ubunifu mkubwa. Hayo ndio yaliyokuza sanaa yetu kupitia mpendwa marehem Ruge.
 
Game ni ya 2007 huko
Miaka ya mwanzoni mwa 2000 nilijaribu kuingia kwenye sanaa ya muziki na maigizo... Nilikuwa mtunzi wa nyimbo pia.. Binti mmoja jina la kisanii alijiita Lattoya aliondoka na daftari zima la nyimbo (nilimpatia) lakini halikurudi wajanja wa wakati huo walimpiga.. Mwaka 2003/4 nikazisikia baadhi ya nyimbo zikipigwa radio one, zilikuwa zimebadilishwa kidogo mashairi... Lakini sikuwa na ushahidi nikapotezea
Wasanii wa maigizo wakati huo walikuwa wanakuja kwangu kufanya shooting... Nilikuwa na sitting room moja matata sana... Shopping yake nilifanyia south Africa na game hapa kwetu... Hivyo yalikuwa mazingira mazuri ya kufanyia shooting ya maigizo yao
Nilikuwa na usafiri by then baloon GX 90 moja kali sana... Waliitumia sana hii gari kufanyia shooting T 800 ABJ... Vingi niliwasaidia bure kabisa na hata kuwapa misaada midogo dogo
Wasanii (na hii ni hulka ya watu wengi) wanapokuwa underground na ushamba ushamba wao huwa very humble, heshima na adabu kama zote, kila utakachomwambia habishi
Unambrand mpaka anatakata na kuanza kuonekana kwenye vyombo vya habari na majukwaani... Hapo ndio wengine humuona na kuanza kumharibu... Naye bila kutafakari ametoka wapi... Huanza dharau na kujiona bora na kujifanya anajua kuliko wewe......
Nafikiri umepata idea kidogo juu ya mimi

Jr[emoji769]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha longolongo wataje hao mabilionea matapeli.....p diidy alikuwa anamsimamia BIG lakini hyo sababu haikumfanya p didy kutumia hyo nafasi kujitajirisha huku BIG akibaki kuwa maskini....alichokifanya ni kuhakikisha wote kwa pamoja wanatusua maisha na hicho alichopaswa kufanya ruge!! Kwani ukifatilia almost 98% ya mafanikio ya ruge yamesababishwa na wasanii , sasa jiulize kwanini wasanii bado maskini huku ruge akipata utajiri wa kufuru?

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaufahamu vizuri lkn mfumo wa capitalism ?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah umetema madini ambayo sijawahi kuyaona toka nizaliwe...
Respect to you
Hatimaye Ruge amelala kwa amani... Siku zake za mwisho hazikuwa rahisi... Amepambania uhai wake kwa nguvu zake zote... Yatasemwa mengi... Yataandikwa mengi... Lakini hatimaye yataisha na maisha kusonga mbele.... Ni wiki ya Ruge...

Kwenye haya maisha kuna makundi mawili.. Kundi la washindi na kundi la washindwa.... Huwa tunaaswa sana kujifunza toka kundi la washindi... Ogopa sana kundi la washindwa... Hili kundi la washindwa linaweza kukuzushia chochote.. Kisha wakakijengea uhalisia na kukitangaza hasa... Mara nyingi hawakuzushii mema bali mabaya.... Kundi hili lina fikra za ajabu kweli... Yani kushindwa kwao kwenye lolote wanakuhusisha na wewe
Mbali ya Ruge na wadau wengine waliofanya mengi kwenye mziki wetu wa kisasa na hata kuibua vipaji vingi ni Said Fella (mkubwa Fella) naye huyu ni mhanga kama Ruge [emoji1019] japo kwa asilimia tofauti
Miaka ya mwanzoni mwa 2000 alileta mapinduzi makubwa kwenye bongo fleva kwa kuwa na kundi la kwanza lililofanikiwa sana la TMK-WANAUME...
Kundi hili lilitikisa mno likiwakilisha Uswazi na ndio likawa chachu ya kuanzishwa kwa makundi mengine rasmi kama East coast nk... Vibao vya TMK vilikuwa moto wa kuotea mbali... Nani hakumbuki Dar mpaka Moro?
Vinara wa kundi kina Juma nature wakiwa ndio wanasikika sana, wakafitinishwa, wakajazwa maneno... Upeo wa kufikiri ukawa mdogo... Wakaambiwa Fella anawanyonya, anawatumikisha wakati yeye si msanii kwahiyo anakula jasho lao bure
Sumu hii ikawaingia baadhi na chini ya Juma nature kundi la TMK-WANAUME likagawika vipande viwili.... Wenye kuona mbali wakabaki na Fella... Wenye kuona karibu wakaondoka na kuunda kundi lingine kwa mbwembwe nyingi na kutoa kibao cha kwanza NDEGE TUNDUNI... wimbo huu ulikuwa masimango tupu kwa Fella...
Fella hakutaka majibizano... Alifahamu wakati ni hakimu mzuri..... Leo hii Fella ni nani na yuko wapi na Juma nature ni nani na yuko wapi! Washindi dhidi ya washindwa....!!!
Makubwa Ruge aliyoyafanya kwenye muziki wa bongo fleva hayaonekani kwa baadhi yetu... Anatuhumiwa, anabezwa, anatukanwa, anakejeliwa... Anaitwa mnyonyaji na kila aina ya jina baya... Lakini ukiangalia wanaofanya hivyo ni akina nani!? Ni kundi dogo la washindwa.

Ruge sio malaika, Ruge sio mkamilifu ni binadamu kama binadamu mwingine yeyote yule ana changamoto zake ana kushinda na kushindwa kwake.. Ni mpambanaji anayehitaji naye kutoka kimaisha... Alifanikiwa kwa kiasi chake... Akapata alichopata.... Kuna wengine kati yetu tungepata nafasi yake pengine tungekuwa wabaya zaidi yake....
Washindwa wamepata pa kutolea nyongo zao.. Yani ugumu wao wa maisha na kushindwa kwingi lawama zote ni kwa Ruge... Ruge alikuwa mjasiriamali angefanyaje kulinda kazi yake? Rip brother!
Basi sasa kwa washindwa... Ruge kaondoka, yule mnyonyaji tapeli.. Aliyekuwa kashikilia funguo za maisha yenu.... Tunataka tuone tofauti sasa... Tunataka kuwaona mkitoka kimaisha sasa kwakuwa kikwazo kimeondoka!!!!

KATIKA MAISHA OGOPA SANA KUNDI LA WASHINDWA!!! ALWAYS LEARN FROM THE BEST....

Jr[emoji769]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakupa hizi cases uzisome uzielewe vizuri wewe na wenzako:

1. Hivi nikiwa natafuta mafundi wa kunijengea nyumba yangu nikakutafuta unijengee ukakataa kwa kuwa malipo yangu ni mabaya, nikatafuta mafundi wengine wakakubali kujenga kwa malipo yale yale ambayo ni mabaya kwako, kuna haja ya kulia lia kuwa mimi ni mnyonyaji nawalipa mafundi hela kidogo??


2. Ukiomba kazi CRDB ukakubaliwa ukapewa mkataba ukausoma ukasaini ukaambiwa siku ya kuja kuanza kazi. Ukaenda kumwambia dada yako mshahara uliokubaliana na CRDB kwenye mkataba. Dada yako ambae yeye anafanya kazi Standard Chartered bank na analipwa hela kubwa sana hapo StanChart, akakwambia CRDB ni wanyonyaji usikubali kufanya nao kazi. Kesho wewe ukakataa kufanya kazi CRDB ukabaki nyumbani unalia njaa hauna kazi na huyo dada yako wa StanChart hakusaidii chochote utailaumu CRDB au dada yako aliekurubuni ujinga??

3. Ukiwa wewe ni msanii akapatikana promoter mmoja akakwambia nina show 1 nataka ukapige kwa sh million 5. Alafu akatokea promoter mwingine (mfano Ruge) akakwambia mimi nina shows 10 za Fiesta ila dau langu ni milioni 3 kwa kila show. Wewe na akili yako ya biashara utachagua kupiga show wapi??

Kutoka kwenye hizo cases jifunze vitu hivi vitatu:
1. Dunia ya soko huru iko wazi kwa kila mtu. Unapokataa kufanya kazi kwa ujira mdogo ujue kuna wenzako watakubali kuifanya kwa ujira ule ule. Kitendo cha kuikataa na ukaanza kulia lia kuwaaminisha watu kwamba muajiri analipa ujira mdogo hakizuii wenzako kuendelea kujenga maisha. Usilazimishe wengine waikatae kama wewe


2. Unapopata kazi/deal yotote ya kukuingizia pesa usiwe mtu wa kuwahi kushikwa masikio na waliofanikiwa. Huyo aliyefanikiwa atakushauri hiyo kazi malipo yake ni mabaya usiifanye wakati yeye ana uhakika wa kuingiza hela. Na siku ukiiacha hatakusaidia pesa ila atakusaidia kusambaza malalamiko kwa kuwa alikushauri yeye uamuzi mbovu. Yeye wakati anakushairi hivyo ukibahatika kujua historia yake alipopitia unakuta alishawahi fanya kazi za kunyanyaswa na malipo mabaya saaana kuliko hata hayo lakini ndo zimemjenga na kumfanya a grow hadi hapo alipo.

3. Kwenye biashara lazima uwe na akili ya kukokotoa revenue. Usidanganywe na mtu mmoja anaekulipa hela nyingi kwa deal moja wakati kuna mwingine angeweza kukulipa hela pungufu ila akakupa deal 10! Mil 5 x 1 = Mil 5 lakini mil3 x 10 =mil 30! Sasa wewe kataa kufanya kazi ya mil 3 ukisubiri ya mil5 unaishia kuwaona wenzio wanakubali kufanya hiyi ya mil 3 unawekeza nguvu zako katika kuwalaumu kwamba wanakubali kunyonywa mara ooh jamaa ni mnyonyaji, n.k wakati wenzio wana make money. Ruge alikuwa anajua anachokifanya hata bei ya vitu vya jumla ni ndogo kuliko bei ya reja reja kwa kitu kitu kimoja kimoja.

All in all Ruge alikuwa na mapungufu yake kama binadamu, sio busara kumsema vibaya wakati amepumzika. Tumuombee apumzike pema lakini tusiwe watu wa kujoin upande wa walalamikaji bila kuumiza kichwa kwanza!

Amefariki sasa tutawaona hao walalamikaji wanakuwa kwenye mafanikio makubwa sasa. Ha ha haaaa

R.I.P kyoma Ruge

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji1666][emoji1666][emoji1666][emoji1666]Safi mkuu umeonyesha vyema mfumo wa soko huria unavyofanya kazi

Pia kwa kuwakumbusha tu watu wengine wasije sahau kipindi ambacho dunia inapitia kwa Sasa kuwa ni soko huria. (capitalism) ambapo inaambatana na sifa zake zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kaharibu mambo mengi sana na kuchangia kuleta mabaya mengi. Kachuma pasipo huruma na kula pasipo kunawa, Mungu amuweke anakostahili.


Pesa aliyokuwa akitokwa na mate ili aipate kaiacha na Mungu hajamwacha afaidi, pesa haijazuia kifo na wala hatazikwa nayo, yameisha na vyote vinaishia mlangoni

Tujifunze ...pesa haitanunua uhai na siku ikifika hakuna mjanja wala pa kujificha
 
Back
Top Bottom