Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini...

hata kama angekuwa ni wa miaka 100, je msahafu unahalalisha kuchoma makanisa na kuiba mali za kanisa, je hilo ni suluhisho? kwani aliyefanya kitendo hicho ametumwa na makanisa yaliyovamiwa?
Mkuu wangu nitarudia kusema hivi yaliyotokea Mbagala ni mazao ya kile tulichopanda. Hawa watu wote ni maskini na wajinga ambao walipewa sababu ya kuvamia na kuchoma makanisa ilihali wao wenyewe wamejazwa ujinga kama yule mtoto alokojolea Msahafu.

Hekima haiwezi kutokea ktk kundi la wajinga sasa nyie wenye werevu na usikivu ndio mnaotakiwa kuitangaza kheri, amani na utumilivu lakini ikiwa nanyi mnashindwa kuelewa basi itakuwa kazi kubwa sana kuuondosha udini nchini. Mabadiliko huanza na sisi, wewe ulostaarabika mfunze mwenzako ustaarabu, wewe uloelimika mfunze yule ambaye hana elimu ili kesho naye akawafundishe wengine..

Leo hii ukianzisha lolote hata iwe kuua wahindi na matajiri basi sii waislaam wala wakristu watakaoshiriki maana tumewapa sababu ya kuwachukia wahindi na matajiri kwa kuwaweka wao ktk umaskini. Hivyo mnapokataa kosa la kukojolea msahafu hawa wenzenu hawatawaelewa na wala huwezi kupima kwa mtazamo wako, heshimuni imani yao ili nanyi mheshimiwe. Kifupi tuheshimiane kwanza.
 

Nukuu toka Quran

"Be tolerant, command what's right, pay no attention to foolish people" [7:199]


"And the servants of the Most Merciful are those who walk upon the earth easily, and when the ignorant address them [harshly], they say [words of] peace," [25:63]


"Invite to the way of your Lord with wisdom and good instruction, and argue with them in a way that is best. Indeed, your Lord is most knowing of who has strayed from His way, and He is most knowing of who is [rightly] guided." [16:125]
 
Dini hizi zitawafilisha mbali, at the end mtapigwa kebiriti wote.
 
Mkuu hukunielewa. Nimekuambia si kila kitu katika ukristo ni kizuri na naamini si kila kitu katika uislamu ni kizuri. Yaani mimi nakubaliana na criticisms za ukristo na nina criticisms zangu kwa huo ukristo. Kwa kifupi tu nikuambie madhara mengi ya dini yanaonekana pale inapokuwa na nguvu ya dola. Karne nyingi ukristo ilikuwa dola ya dunia. Katika kipindi hicho wamefanya unyama wa kutisha. Ile Vatican imejengwa kwa damu ya watu wengi ambao hawakuwa na hatia sawa sawa na Makkha ulivojengwa kwa damu nyingi za watu wasiokuwa na hatia kwa unyama wa kutisha ambao bado unatumiwa na wanadamu wanaonufaika na utawalala wa kisiasa kwa mgongo wa dini. Ndio maana nimekuambia si kwamba ukristo ni utakatifu. Mimi kwa uelewa wangu nnavochukulia dini na mwenendo wa historia inavyoonyesha dini zilitumika kusimika tawala za wanadamu. Ukianza kwa Musa, kwa Samwel, mpaka kwa Saul hadi Daudi na wafalme wengine waliofuata walijikita kwenye dini kili kutawala. Ambaye aliondoa dini kwenye utawala ni Yesu. Lakini alipoondoka tu watu wakajipachika uwakilishi wake na kuanza kutawala wanadamu wengine kwa mgongo wa dini. Hao ndio wanaitwa popes. Uislamu hausalimiki katika kosa hili mtume wake katumia dini kujijenga kisiasa na kupata umaarufu kisha kuwa mtawala.
Kwa hiyo mkuu mimi sisemi ukristo haujatenda dhambi. Marekani inasababu nyingi za kutokuwepo kwenye historia hiyo ya dini na utawala ndio maana Marekani kama nchi utasema ina hayo mabavu ya kukalia nchi nyingine lakini haina maana kuwa ni ukristo ila ni ufalme (yaani ni utawala) usiohusiana na dini.
Nilichotaka kusema ni kuwa Mungu hana vurugu, hana hasira za haraka, ni mvumilivu na hakurupuki, haui hovyo na vitendo vyovyote vinavyokinzana na hizo tabia za mwenyezi Mungu lazima tuzikatae. Kuhubiri chuki kati ya jamii zetu na kusema dini fulani ni maadui wetu tuzikatae na tuwaambie waziwazi viongozi wetu wa dini kama watakuja kutuhubiri hizi chuki misikitini au makanisani kwamba wanachokifanya ni ushetani na tuwakatae.
 

Lilikuwa ni suala la kuongea na mama yake au kuliripoti kwa mamlaka?

Makanisa ya madhehebu mbali mbali yamevunjwa, je huyo mtoto anasali kwote huko?
 
Mkuu na wewe una misimamo mikali sana na chuki sana,umepotea mida lakini naona umerudi.

Sasa ingelikuwa ni sharia,huyo mtoto aliyebalehe mngemfanya kitu gani?
 
Mkuu wangu nitarudia kusema hivi yaliyotokea Mbagala ni mazao ya kile tulichopanda. Hawa watu wote ni maskini na wajinga ambao walipewa sababu ya kuvamia na kuchoma makanisa ilihali wao wenyewe wamejazwa ujinga kama yule mtoto alokojolea Msahafu.
Watu wanasema eti tunakoelekea ni kubaya,mimi nasema tumeshafika kubaya.Wewe hupenda kumtetea Sheick Ponda.

Hayo unayoyasema hapo juu wewe na Mdondoaji kuhusu ukosefu wa ajira,ujinga na ukosefu wa elimu,munaandika tu bila kujuwa kwamba munasapoti misimamo ya Ponda kuhusu mfumo Kristo, hayo sijui ya Necta,kwamba waislam wanapenda shule ila wanazuliwa na wakristo.Kwamba hata kazi hawana kwasababu mfumo kristo ndiyo unawanyanyasa,hiyo ni chuki mbaya sana!Ni sawa na wale Hitler aliowaweka kambini ambao walikuwa hawajui wazazi wao,na baada ya kufundishwa jeshini,wakaambiwa wazazi wao waliuwawa na jews!

Mmesahawaonyesha hao vijana kuwa adui yao ni wakristo,na kwamba huo ufukara,ujinga na mengineyo,sababu ni wakristo.

Sasa mnataka kupakazia wengine.Chuki imepandwa na waislam wakiongozwa na kiongozi wa nchi.Hilo liko wazi.

Haijalishi maneno ya kwamba eti ni wahuni sijui eti mtoto aliyekojolea kuraan alijazwa ujinga.Ukweli ni kwamba mmezipanda hizo mbegu za chuki.Its a painfull truth.
 
Nimekuelewa vizuri sana lakini haya sii mafundisho ya Ukiristu wala Uislaam. Ukisoma vitabu hivi viwili utanielewa vizuri naposema Ukirstu au Uislaam sio WATU ama mkusanyiko wa watu (jamii) isipokuwa wale wanaofuata mafundisho ndio huitwa wakristu au waislaam. Kwetu sisi vitabu hivi ni kama toleo ya agizo la Mungu hivyo hakuna mbora zaidi ya Mungu mwenyewe.

Kwa hiyo sisi wote tuliozaliwa ktk Uislaam na Ukristu halafu tukafikiri sisi ni waumini, tunajidanganya wenyewe kutokana na kwamba hatufuati mafundisho. Na bahati mbaya kuna watu wanafikiri wanaweza wao kuwa na uchungu na dini hizi kuliko Yesu au Muhammad ambao ndio viongozi wetu kwa fokra ya kwamba wanaweza kuilinda dini ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo wale wote wanaoyafanya mambo haya kwa faida zao na kwa minajiri ya kupanua wigo la utawala wao hawana Uislaam wala Ukristu maana tumearishwa tu KUJILINDA pale tunapoingiliwa na kukwazwa ktk imani zetu. Kama vile mwanamke anayetaka kuwa rapped akajitetea hivyo hata akiua itakuwa amejilinda yeye na makosa ni ya yule alotaka kumwingilia..

Nikuchekeshe kidogo:- Tatizo la Dunia ya leo kimfumo ni kwamba atalaumiwa yule mwanamke kwa kuua kwa sababu kitendo cha kuwa rapped watamuuliza kama yeye bikira kama sio bikira kwani taabu iko wapi hadi afikie kuua?
 
kwa hiyo huko Pakistani, Afghanistani, Sudan, Somali, Mombasa, na kwingineko wote wanalalamikia MOU?
Analytical, hapo pekundu, umenikumbusha kisa cha kale ka-binti kanaitwa MALALA kutaka kuuwawa, eti msahafu haururusu wanawake kwenda shule/kupata elimu dunia, kinacho nitisha jinsi hawa jamaa wanavyopenda kuiiga mambo hii staili nayo wanaweza kuileta hapa TZ.
 
Mkuu wangu nimeandika hivi:- Mfumo Kristumaana yake ni pale serikali inaposhirikiana na kanisa kuendesha shughuli za AFYA na ELIMU... Je jambo hili halifanyiki nchini?.. Hili linafanyika sasa hivi na ndio uchcochezi ulipoanza kwa nini serikali isiliondoe, kun ugumu gani?.

Labda nikupe mfano mwingine serikali yetu ikitumia hukumu zinazoendana na Uislaam itakuwa kosa kwa Mkristu kusema tuna Mfumo wa Sharia law? halafu Waislaam wachukie wakati wanaona kweli unatumika?.. Mfano mwingine.. Leo hii serikali nyingi zina mfumo Dume mbona wewe mwanaume huchukii kusikia wanawake wanaposema tuna mfumo dume isipokuwa hapa kwenye Ukristu wakati unajua fika kwamba serikali yetu inashirikiana na makanisa kuhudumia wananchi ktk Afya na Elimu jambo ambalo waislaam hawalipendi..

Sasa ni nani anayeendeza udini na kuwapandisha waislaam chuki kama sio serikali. Hivi kuna tatizo gani ikiwa serikali haitashirikiana na kanisa? kwani nchi gani Makanisa walishindwa kuendesha shule na Hospital zao! kuna ulazima gani kuendeleza mfumo wa kikoloni ambao hata Nyerere aliupiga vita...
- Nasubiri majibu yako..
 
Sasa utasemaje hao waislam waliokosa elimu na ni mafukara wasiwashambulie wakristo kama msiamo wako ndo huo?Hivi unadhani ni kwanini wanachoma makanisa kwa sababu ya ukosefu wa elimu na ajira?
 
Sasa utasemaje hao waislam waliokosa elimu na ni mafukara wasiwashambulie wakristo kama msiamo wako ndo huo?Hivi unadhani ni kwanini wanachoma makanisa kwa sababu ya ukosefu wa elimu na ajira?
Nifikiri mimi tena au wewe ndio unatakiwa kufikiria na kunipa jawabu. Mkuu wangu ukisema Saudia Arabia au Iran wanatumia mfumo wa Sharia law na hatuutaki kabisa Tanzania, nitakubaliana na wee wala sintopinga wala kuona huwapendi Waislaam. Haya labda niulize miye kama napenda mfumo huo utumike nyumbani? -nitakujibu - Hell NO! Kwa sababu sisi ni taifa ambalo halina dini na wananchi wake ndio wanafuata imani za dini zao hakuna sababu ya kumlazimisha mtu imani, utaratibu ama sheria zako.

Sasa nashangaa sana wakristu wanajua fika kwamba mfumo huu uliopo nchini uliletwa na wakoloni kuja kuitawala Afrika wakitumia makanisa kuendesha shughuli za AFYA na ELIMU huku wao wakikwapua maliasili zetu. Wakiwanyima haki sawa Waislaaam na Waislaam wanajua madhara ya mfumo ule sasa wanapokuja kuilalamikia serikali mnashindwa vipi kuliona hili badala yake mnaitetea serikali ile ile mnayotaka kuindoa madarakani..

Hawa wa Mbagala ni matokeo ya kulea Mfumo kwa miaka 20 toka mwaka 1992 waislaam wamekuwa wakilalamika na wengine wachochezi wakimlalamikia Nyerere kwa sababu walifikiria wao ndio watakuwa na nguvu ya kuendesha nchi kwa sheria zao.. Hivyo binafsi yangu yanaona makosa pande zote mbili na nasema tuondokane na mfumo kristu tuweke mfumo bora zaidi wa ELIMU na AFYA nchini haya matatizo yataondoka laa sivyo jipu hili litaendelea kusambaa kesho litakuwa sehemu ambayo hatukutegemea kabisa..
 
hahahaha bahati mbaya MAJJID si mwislamu kama wengi wanavyofikiria, ni jina tu linashabihiana na majina ya kiislamu na kwa kuwa anao ndugu zake wengi waislamu maeneo ya kisarawe na kule iringa.
 

kwahiyo wewe pia ulienda kuchoma makanisa kwa kukasirishwa na hilo neno ni makaratasi.. wewe na wenzako ni watu wa ajabu sana.sasa kwa kuchoma makanisa unadhani kile ulichokusudia umepata????
 
Tofauti ni kuwa yule bedui alikuwa hafahamu kitu kuhusu uislam lakini hawa leo wanaujua vizuri uislam
 
Mkuu,siyo kwamba ninapinga hayo unayosema,ila ninachosema ni kwamba hayo ndiyo yametufikisha huku tulipo.So ni lazima mchukuwe responsiblity.

Marekani,UK,Australia na Canada ambapo waislam wana thrive na kuishi vyema kwa amani na kusoma kuna mfumo gani?

Hilo la mfumo krsito ndo mzizi wa fitina,na hapo ndipo waislam na wakristo hawataweza kuelewana hata kidogo.Kwa mantiki hiyo,hakuna maneno yatakayoweza kutufanya tuishi pamoja kwa amani tena.
 



Hii siyo dini.Zanzibar washaua askari.Ndiyo wanayofundishwa misikitini,
 

Hapo kwenye red; Unataka kusema leo hii mlevi akiingia msikitini akawa anakojoa na mpo waislamu kadhaa ndani, mtamuacha kwa sababu amelewa na hajui anachokifanya?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…