Imekuwa kazi yangu kubwa hapa kijiweni kujaribu kuwashusha watu munkari ili wapate kujitazama wenyewe kwanz akabla ya kuzungumzia matokeo ya Kijana kukojolea Kuruan na uchomaji moto wa makanisa. Nawaomba jitazameni nyie wenyewe wala sio matukio na mtakuta ya kwamba mna CHUKI baina yenu...Maneno mnayoandika humu aidha kwa kuegemea upande mmoja au kukosoa upande mwingine ni dalali ya kuitaka haki upande unao kuhusu - WHY?..
Hadithi ya Mjengwa inaonyesha hekima kubwa ya mtume na mfano bora kwetu wa kuigwa lakini ukweli ni kwamba sisi sote sio MITUME wala hatuna hekima walopewa mitume hata kwa Ukaribu mdogo. Mantiki ya hadithi ile ni kuonyesha Uongozi bora, busara inayoweza kutumiwa na viongozi wetu pale wananchi wanapotaka kutumia hasira zao ktk swala ambalo wanaliona ni kinyume cha mila na tamaduni zao..Na kama hadithi ile inavyosema wale waumini wote wa Uislaam walitaka kumpiga yule mlevi, wao hawakuona Ulevi wake wala kutokujua kwake kuwa sababu isipokuwa kitendo cha kukojolea msikiti kilikuwa dharau kubwa na sio ustaarabu. Na kikubwa zaidi eleweni yule mtu aliitwa Bedui kwa maana asili yao hawa Mabadui walikuwa hawana ustaarabu na kawaida yao kukojoa, kuchuma dawa mahala popote wanapoona kama Baniani na kujamba au kutema makohozi.
Udini nchini kwetu umepandikizwa mbegu mbaya wala sio magugu yanayoota yenyewe na yanahitaji kupaliliwa. Ukipanda mbigiri bila shaka tutavuna Mbigiri na ndicho kilichotokea hivyo watoto wetu wanapokuja zikanyaga na kulia kwa maumivu hapo ndipo tunaanza kunyoosheana vidole. lakini UDINI nchini umetokana na nini haswa - Jibu lake rahisi sana - SIASA na UTAWALA. Toka siku tuloruhusu Dini kuwa sehemu ya Siasa za nchi yetu tukahalalisha waraka, mihadhara na mafundisho ya dini na hata viongozi kuongoza ufunguzi wa ibada, sala na mikutano ya dini kuwa sehemu ya ujenzi wa mandeleo nchini ndipo tulipokuwa tukipanda mbegu za UDINI.
Mwalimu Nyerere alipambana na UDINI kwa kuhakikisha hakuna mahusiano baina ya serikali na dini. Kwa waislaam waliona wanakwazwa kwa sababu haikuwa kawaida serikali kutoshirikiana na viongozi wa dini. Kweli waliomba mambo mengi sana na yakapigwa chini lakini vile vile hakuruhusu Upande wa imani yake wafaidike kwa lolote. Serikali yake ikachukua jukumu kubwa la kupambana na maadui wetu watatu yaani UMASIKINI, UJINGA na MARADHI na kuifanya haki ya kila Mtanzania bila kujali dini zao. Alipambana na Ukoloni mamboleo kwa kutowapa nafasi wageni kututawala kiuchumi. Nyerer aliwajuwa maadui wetu na hivyo kuweka misingi imara ya kulinda umoja wetu.. Huu ndio ulikuwa Uongozi wenye DIRA wenye mwongozo ambao hata mtume aliufuata kwa sababu alikuwa na mission, malengo na azma ya kuufikisha ujumbe kwa hawa mabedui wasioamini, sio viongozi wetu leo hii.
Toka Mageuzi ya Kiuchumi mwaka 1985 tanzania tumekuwa tunajiendesha kama gari bovu.. Umaskini, Ujinga na Maradhi haikuwa tena sababu ya vita ya kitaifa kuwakomboa wananchi hivyo mwenye uwezo aliweza kujipenyeza na kukamata nguzo hizo kibiashara. Na toka mwaka huo Ukoloni Mamboleo haukuwa tena maadui wetu wa nje isipokuwa tegemezi letu. Kwa hiyo Unapoutazama UDINI nchini nawaomba pia mtazame jinsi Ubeberu ulivyorudi nchini. Na wala msije walalamikia kina Barricks au Richmond isipokuwa sisi wenyewe ndio tumeruhusu mambo haya yafikie hapa tulipo. Tumewaruhusu wawekeze tukalegeza masharti yetu ili wapate kukamata njia za uchumi sasa leo tunawalalamikia nini?
Tanzania imepoteza SIASA SAFI na UONGOZI BORA, hivyo ni nchi inasokuwa na DIRA..Hao WATU na ARDHI vitabakia kuwa watumishi na shamba la utawala ulokosa ubunifu tukapanda mbegu hizi na hakika tutavuna tulichopanda..
Hadithi ya Mjengwa inaonyesha hekima kubwa ya mtume na mfano bora kwetu wa kuigwa lakini ukweli ni kwamba sisi sote sio MITUME wala hatuna hekima walopewa mitume hata kwa Ukaribu mdogo. Mantiki ya hadithi ile ni kuonyesha Uongozi bora, busara inayoweza kutumiwa na viongozi wetu pale wananchi wanapotaka kutumia hasira zao ktk swala ambalo wanaliona ni kinyume cha mila na tamaduni zao..Na kama hadithi ile inavyosema wale waumini wote wa Uislaam walitaka kumpiga yule mlevi, wao hawakuona Ulevi wake wala kutokujua kwake kuwa sababu isipokuwa kitendo cha kukojolea msikiti kilikuwa dharau kubwa na sio ustaarabu. Na kikubwa zaidi eleweni yule mtu aliitwa Bedui kwa maana asili yao hawa Mabadui walikuwa hawana ustaarabu na kawaida yao kukojoa, kuchuma dawa mahala popote wanapoona kama Baniani na kujamba au kutema makohozi.
Udini nchini kwetu umepandikizwa mbegu mbaya wala sio magugu yanayoota yenyewe na yanahitaji kupaliliwa. Ukipanda mbigiri bila shaka tutavuna Mbigiri na ndicho kilichotokea hivyo watoto wetu wanapokuja zikanyaga na kulia kwa maumivu hapo ndipo tunaanza kunyoosheana vidole. lakini UDINI nchini umetokana na nini haswa - Jibu lake rahisi sana - SIASA na UTAWALA. Toka siku tuloruhusu Dini kuwa sehemu ya Siasa za nchi yetu tukahalalisha waraka, mihadhara na mafundisho ya dini na hata viongozi kuongoza ufunguzi wa ibada, sala na mikutano ya dini kuwa sehemu ya ujenzi wa mandeleo nchini ndipo tulipokuwa tukipanda mbegu za UDINI.
Mwalimu Nyerere alipambana na UDINI kwa kuhakikisha hakuna mahusiano baina ya serikali na dini. Kwa waislaam waliona wanakwazwa kwa sababu haikuwa kawaida serikali kutoshirikiana na viongozi wa dini. Kweli waliomba mambo mengi sana na yakapigwa chini lakini vile vile hakuruhusu Upande wa imani yake wafaidike kwa lolote. Serikali yake ikachukua jukumu kubwa la kupambana na maadui wetu watatu yaani UMASIKINI, UJINGA na MARADHI na kuifanya haki ya kila Mtanzania bila kujali dini zao. Alipambana na Ukoloni mamboleo kwa kutowapa nafasi wageni kututawala kiuchumi. Nyerer aliwajuwa maadui wetu na hivyo kuweka misingi imara ya kulinda umoja wetu.. Huu ndio ulikuwa Uongozi wenye DIRA wenye mwongozo ambao hata mtume aliufuata kwa sababu alikuwa na mission, malengo na azma ya kuufikisha ujumbe kwa hawa mabedui wasioamini, sio viongozi wetu leo hii.
Toka Mageuzi ya Kiuchumi mwaka 1985 tanzania tumekuwa tunajiendesha kama gari bovu.. Umaskini, Ujinga na Maradhi haikuwa tena sababu ya vita ya kitaifa kuwakomboa wananchi hivyo mwenye uwezo aliweza kujipenyeza na kukamata nguzo hizo kibiashara. Na toka mwaka huo Ukoloni Mamboleo haukuwa tena maadui wetu wa nje isipokuwa tegemezi letu. Kwa hiyo Unapoutazama UDINI nchini nawaomba pia mtazame jinsi Ubeberu ulivyorudi nchini. Na wala msije walalamikia kina Barricks au Richmond isipokuwa sisi wenyewe ndio tumeruhusu mambo haya yafikie hapa tulipo. Tumewaruhusu wawekeze tukalegeza masharti yetu ili wapate kukamata njia za uchumi sasa leo tunawalalamikia nini?
Tanzania imepoteza SIASA SAFI na UONGOZI BORA, hivyo ni nchi inasokuwa na DIRA..Hao WATU na ARDHI vitabakia kuwa watumishi na shamba la utawala ulokosa ubunifu tukapanda mbegu hizi na hakika tutavuna tulichopanda..