Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini...

Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini...

Mtoi na kundi lako, nadhani umemezeshwa propaganda zinazoenezwa na maadui juu ya lile tukio. Waislamu si wajinga kama mnavyotaka watu wafikri. Issue ni kuwa baada ya mama mmoja wa kiislamu kuripoti hii habari ya kokojelea masahafu kwa mama wa ' bedui'. Yule mama alijibu kwa jeuri 'si makaratasi tu hayo'

Hiki ndicho chanzo cha kadhia nzima ambacho watu hawataki kukizungumza badala yake wanalilia guitar na 'whisky' zilizomwagwa altereni!

Dharau za hawa ndugu zako hazivumiliki, hata humu JF unaona mwenyewe, wako hivyo!
Endelea nao, lakini ufahamu walivyo!

Nunua i pad weka msahafu wako kwenye i pad. Ama hujui i pad ni nini?
 
Mtazunguka mbuyu wee wakati aliyepanda mbegu ya haya yote yupo na anafahamika! Na mbaya zaidi yupo kimya tu kama vile haoini na hasikii
 
Mtoi na kundi lako, nadhani umemezeshwa propaganda zinazoenezwa na maadui juu ya lile tukio. Waislamu si wajinga kama mnavyotaka watu wafikri. Issue ni kuwa baada ya mama mmoja wa kiislamu kuripoti hii habari ya kokojelea masahafu kwa mama wa ' bedui'. Yule mama alijibu kwa jeuri 'si makaratasi tu hayo' Hiki ndicho chanzo cha kadhia nzima ambacho watu hawataki kukizungumza badala yake wanalilia guitar na 'whisky' zilizomwagwa altereni! Dharau za hawa ndugu zako hazivumiliki, hata humu JF unaona mwenyewe, wako hivyo! Endelea nao, lakini ufahamu walivyo!
Hata kama mama wa 'Bedui' alijibu kwa ujeuri juu kitendo cha yule mtoto amabacho si cha kiungwana, ilitakiwa yeye mwenye kosa ndiye ahukumiwe kwa kosa lake BINAFSI. Iweje kosa la watu wawili liwahusishe watu wengine wasiohusika? Usijaribu kuhalalisha uovu uliofanywa na hao Waislamu kwa sababu ambazo hazina mashiko. Tafadhali soma kwa makini ujumbe wa Mjengwa ambaye pia ni Mwislamu utapata kitu cha kukusaidia . Punguza jaziba na Mungu atakusaidia.Amen
 
Sasa nani ataweza kunishawishi niondoe dhana yangu kwamba uislamu ni NGO iliyojengeka kwenye misingi ya vurugu? Kila mahali duniani utasikia vurugu za waislam dhidi ya dini zingine. Maggid keshasema Boss wa Uislam hakuwa na pupa, labda alisahau kuwaambia watu wake wafanyeje likitokea tena hilo, au aliwaambia lakini kwa kuwa msahafu umeandikwa kwa lugha wasiyoijua wengi hawasomi, na wanaosoma wamekariri hawajui maana yake, wanaojua wanawatumia wafuasi wao kukamilisha malengo tofauti na Mtume wao. Mtume atawakana siku ya siku, maana hinaonyesha hakubaliani na vurugu. Maana yake wanaofanya vurugu ni wahuni tu na wala hawana dini mioyoni mwao. Kisasi ni cha Mungu na wala binadamu hawezi kumsaidia Mungu sababu Mungu huyo anao uwezo wa kufanya chochote apendavyo.
 
Ndugu umenena sahihi,ila suala la msingi sio umri wa yule mtoto bali ni kuvumiliana,hata angefanya mtu above 18 years.Nimehudhuria mara nyingi mihadhara ya waislam huwa wanachoma biblia na wakristo wakiwa around bila reaction yeyote,na huu ndo uvumilivu wa aina tunaohitaji.Swali fupi,kwanini hiyo hasira haikuelekezwa kwa yule mama aliyesema hayo ni makaratasi tu? kwanini ielekezwe kwenye makanisa? individual issue handled as community issue? is that right.elimu dunia duni.
 
Kaka Maggid umenena kitu kizuri sana waislamu wajaribu kupitia hi kitu natumaini watafaidika sana na somo litawaingia ikiwezekana hata misikiti humo wapelekee hili neno ulilolinena hapa tena uanze na Ponda!
 
A very educated Muslim indeed. Thank you Maggid! May the God of us all bless you today and the days to come!

Ndugu zangu,

Moja ya hadithi za Mtume Muhammad S.A. W ni pale Mtume Muhammad alipokuwa msikitini na maswahaba wake. Mara akaingia msikitini mtu wa kabila la Mabedui na kuanza kukojoa. Maswahaba wa Mtume wakasimama kwa hamaki kutaka kumwadhibu Bedui yule.

Mtume akawasihi maswahaba wake wasifanye jambo lolote litakalomdhuru Bedui yule. Hapo ikavutwa subira. Bedui yule akakojoa na akamaliza. Mtume Muhammad alipomuhoji Bedui yule ikabainika kuwa alikuwa ni mtu wa hovyo na wala hakujua kuwa alimokuwa ni msikitini. Bedui yule akaelimishwa, akaelewa. Akarudi kwenye ustaarabu.

Ndio mkojo ule ulifutwa kwa maji na amani ikawepo. Wahenga walinena; Subira yavuta heri. Siku zote, hamaki si jambo jema. Kwa kutanguliza subira na kutumia hekima Mtume Muhammad aliivuta heri na kuepusha shari.

Maana, kama Mtume alisingewaasa maswahaba wake kuvuta subira, basi, makubwa matatu yangetokea ndani ya msikiti ule; Mosi, zingezuka vurugu na watu kuumizana na hata kutoana roho. Pili, mkojo wa Bedui yule ungesambaa msikitini kwa vile alishaanza kukojoa na isingekuwa rahisi kwake kukatisha mkojo wake. Tatu, Mkojo una madhara ya kiafya pia.

Naam, kwa mwanadamu, ni muhimu kuwa na subra na kutafakari kabla ya kufanya maamuzi. Kwa ndugu zangu Waislamu, tunaona Mtume Muhammad ameweza kuonyesha hilo. Na kwa ndugu zangu Wakristo, kuna mifano pia ya Yesu Kristo kuonyesha subra.

Ndio, Uislamu, kama ilivyo kwa Ukristo na dini nyingi za humu duniani, msingi wake ni amani na upendo. Kitendo cha mtoto yule wa Mbagala kukojolea korani kitazamwe kwa sura ya kitendo kilichofanywa na mtoto .

Na kama ilivyokuwa kwa Bedui yule, kama pale Mbagala subira na hekima vingetangulizwa, basi, yumkini tungebaini kuwa mtoto yule hakujua madhara ya kitendo chake. Naye angekanywa kama tuwakanyavyo watoto wetu. Na hata kitendo hicho kingefanywa na mtu mzima, bado tulikuwa na haja ya kutanguliza subira na hekima kumhoji aliyetenda, yaweza akawa kama Bedui yule kwenye msikiti alimosali Mtume na maswahaba wake.

Na kwa kuangalia picha zile za Mbagala naiona hatari iliyopo sasa, kuwa tuna vijana wengi wasio na kazi; Wakristo kwa Waislamu. Vijana wasio na dogo. Ni kama moto uliofifia. Akipatikana kwa kuchochea kuni wanalipuka.

Ni vijana wanaopatikana wakati wowote na mahali popote. Hata jambo likianza saa tatu asubuhi wao wapo. Hawana ofisi wala bosi wa kumwomba ruhusa ya kwenda kuandamana na kurusha mawe. Ndio hawa wanaonekana wamevaa ' Kata kiuno' na wengi wao hawajahi hata kuingia misikitini au makanisani.

Inakuawaje kijana wa kweli wa Kiislamu achome kanisa na kuiba kompyuta. Inakuawaje kijana na muumini wa kweli wa Kiislamu aonekane saa mchana wa jua kali akivamia baa na kukimbia na kreti za bia? Ni maswali yanayotutaka tutafakari kwa makini.

Maana, ninavyoamini mimi, uchumi na elimu duni ndio hasa vinavyochochea vurugu za kijamii, iwe za kidini au kisiasa, na hususan inapohusisha vijana. Vijana wetu hawana misingi mizuri ya elimu, na wengi hawana ajira pia. Haya ni sawa na makombora yasiyo na gharama kubwa kuweza kutumiwa na wanasiasa wasio waadilifu na hata viongozi wa kidini wenye mitazamo mikali. Ni makombora yaliyoanza kutulipukia. Tuliziona ishara, tukazipuuzia.

Leo Kuna vijana watakaotumiwa au kutumia fursa hiyo kutenda maovu kwa kisingizio cha dini. Ni hawa wataoshiriki kuchafua taswira za dini husika pia. Tujiadhari, kabla ya hatari kubwa inayotujia. Hatujachelewa.

Na hilo ni Neno La Leo.

Maggid Mjengwa,

Iringa.

0788 111 765
 
Mtoi na kundi lako, nadhani umemezeshwa propaganda zinazoenezwa na maadui juu ya lile tukio. Waislamu si wajinga kama mnavyotaka watu wafikri. Issue ni kuwa baada ya mama mmoja wa kiislamu kuripoti hii habari ya kokojelea masahafu kwa mama wa ' bedui'. Yule mama alijibu kwa jeuri 'si makaratasi tu hayo'

Hiki ndicho chanzo cha kadhia nzima ambacho watu hawataki kukizungumza badala yake wanalilia guitar na 'whisky' zilizomwagwa altereni!

Dharau za hawa ndugu zako hazivumiliki, hata humu JF unaona mwenyewe, wako hivyo!
Endelea nao, lakini ufahamu walivyo!

ulikuwepo katika hilo eneo ukasikia hiyo kauli? au umesikia tu na unashuhudia kama uliyekuwepo katika tukio huyo mama akijibu utasemaje? na je ukiambiwa na mwingine haikuwa hivyo! maana issue hii kila mtu anasema alivyosikia, wengi si mashuhuda. ushabiki sio mzuri, kama unapenda haki basi usi-bias
 
Kwahiyo maswahaba huwa hawana subra!

Wewe nawe!! watu wanazungumza ya maana unaleta jokes zisizochekesha!! nyie ndio siku zoite mnapenda kushabikia udini-faida mtakayoipata ni ndogo sana ukilinganisha na hasara zake!!!

-Majid, nakushukuru kwa kuthibitisha kwamba Uislamu ni dini ya amani, tofauti na inavyoonyeshwa na baadhi yetu waislamu
 
TUngekuwa na Waislamu japo 10 ya Mjengwa hapa Tanzania, hakika nchi ingekuwa ya maana sana. Huyu ana akili. Si hawa wanaoleta vurugu. Swali kwa Mjengwa: Yule aliyekojolea Kuran kafikishwa mahakamani, je, yule aliyempelekea Kuran mbona kaachwa?

MJENGWA SIO Muislam. Huyu ni kafiri wa kutupwa. Hana mke. Ameweka hawara wa kizungu. Hawezi kujiita muislamu.
 
Nimependa maoni ya mwandishi, ni ukweli usiopingika kuwa dini zetu si kichaka cha kutenda maovu bali matendo mema, kuvumiliana, amani, upendo na utulivu na kumcha Mungu hivyo kikundi kinachofanya mambo yanayoharibu uhuru wa kuabudu wa mwingine huyo anafanya matendo ya kishetani nasi tuwaogope watu wanaoleta udini kama ukoma. Je kuna yeyote mwenye hakika kuwa dini yake ndio dini ya mwenyezi Mungu? Kitakachomwokoa mtu ni imani yake na matendo mema na si dini yake hivyo tuendelee kuvumiliana na kushirikiana maana chuki haitusaidii kwani wote ni waTz. Mungu ibariki Tz, Mungu tubariki waTz.
 
Maggid,

As much as I agree na unachokizungumza pia uelewa yule Bedui alikuwa amelewa. Hivyo basi hujaelezea uhalisia wa jambo lilivyokuwa. Binafsi yangu I do not believe in violence but rather busara na hekima. Ndio maana nasema hivi suala la waislamu na wakristo ni vema likaangaliwa kwa macho mawili na uangalifu mkubwa. Niliwahi kushauri zamani kuwa iwepo TRUTH AND RECONCILIATION COMMITTEE. Watu wakanibeza but ukweli wa mambo ni kwamba waislamu wana joto lao moyoni linawauma. Waislamu wengi wanaamini Nyerere alitumika kuukandamiza uislamu (refer to Mohamed Said books). Vile vile baadhi ya mambo yanayofanywa na wakristo kukandamiza waislamu mfano wanapokejeli ati wao wamepeleka mwanzo MOU wakati sio kweli waislamu walipeleka mwanzo MOU ikapigwa chini (refer to Mohamed Said books), kunapelekea kuona waislamu wanaonewa.

Tukirejea suala la huyu kijana nadhani maggid you are misleading kwa sababu huyu ni kijana wa miaka 14 (inamaana ana fahamu zake na akili timamu kwasababu umri huo mara nyingi vijana wa kiume wanabelehe) hivyo basi anajua fika kitu anachokifanya na kwanini anafanya. Usimfananishe na mtoto wa miaka 7 ambaye hata kuoga hajui. Hapo Maggid unakosea. Vile vile mtume alitumia busara kuwaambia masahaba wamuachie yule bedui kwasababu alikuwa kwanza amelewa na pili hajui anafanya nini. Kisheria tunasema he is in the state of unsound mind. Hata kwenye macho ya kisheria ukiuwa katika hali hiyo unakuwa unapewa punishment pungufu kwasababu wanachukulia hukuwa unafahamu unachokifanya. Sasa huyu kijana alikuwa anajua fika analolifanya na sio kuwa alikuwa amelewa au hafahamu.

Hivyo nakushauri siku nyengine unapogusa suala la waislamu kuwa na ufahamu kidogo wa kitu unachokizungumzia. Yes hekima na busara ni muhimu katika jambo hili but GET YOUR FACTS RIGHT !!!!!

Nilikuwapo!!!!

Mkuu
Huwa najiuliza kwa nini mwalimu aliwanyang'anya wamissionari shule zao na kuzifanya za serikali, kisha kila mtanzania
bila kujali dini yake wakasoma. Huwa najiuliza endapo asingefanya hivyo nadhani taifa hili lingekuwa limeangamia maana tusingewapata angalau akina mjegwa ambao wanaweza kutafakali.

Ni jambo la aibu na la kusikitisha tunapofumbia macho uhalifu kwa kisingizio cha kulinda dini. Kwanza hiyo dini niya nani? mimi naami kwamba dini zote zina wakuu wake sinaminishi mitume nazungumzia kama dini ni ya shetani mkuu wa dini hiyo ni shetani na kama ni ya Mungu Mungu ndo mkuu wa dini hiyo. Je kama dini ni ya Mungu huyo mungu anayetetewa na mwanadamu ni mungu yupi huyo.

Hicho ndicho ninachokiona kwa wakristo wanaomjua Mungu wao kwamba hana sababu ya kutetewa na mtu au binadamu. napata kigugumizi ninapo ona baadhi ya dini na hasa madhehebu ambayo yana msaidia mungu wako kujitetea huyo mungu wao kalala usingizi????. hata asijitetee, hebu tuwe wakweli tuache umamuma watu wajinga na wapumbavu tuwakemee bila kujali dini zao na tusiwaonee haya kuwapa ukweli wakati huohuo ukizingatia kuwa Usibishane na mpumbavu ukaja kuwa kama yeye.
 
Tuache mafundisho ya uogo hayata tusaidia, watoto wanajaribu mafundisho yetu je yapo sawa? kumbuka kila fundisho litajaribiwa na kizazi hiki hivyo tuwe makini na mafundisho yetu. je huyu mtoto mkristo aliitoa wapi qurani?
Mkuu hv uko dunia hii kweli..? Ina mana hujui hyo mtoto mkristo alipata wapi qurani..?
 
Waislam ubwabwa na biliani watakupinga tu Mjengwa
 
Kwa mujibu wa hadithi hii ya Mtume S.A.W inafundisha ustahimilivu bila kujali huyo Bedui alikuwa amelewa, alikuwa kichaa au vyovyote vile maana kinachosemwa ni kitendo cha kukojoa eneo takatifu bila kujua. Sheikh mkuu wa Mkoa wa Dar aliyasema maneno hayo siku ya tukio la Mbagala TBC alikuwa na Mkuu wa Mkoa na Kamanda Kova. Mwisho wa maneno yake akasema kuwa MAIMAMU wangelimaliza suala hilo kwa kuwaita watoto na kuwaelimisha juu ya vitabu vya MUNGU,lakini siyo kuchoma makanisa na kukusudia kuchoma kituo cha polisi. Watanzania ushabiki wa dini uliopitiliza ni mbaya sana tuwe wavumilivu na kuwafundisha vijana haki ya MUNGU WETU. Ahsante Maggid
 
Waislam tu wanapenda shari, yanayotokea Zanzibar yametkana na kukojolewa kitabu kitukutu?
 
Maggid,

Waislamu wengi wanaamini Nyerere alitumika kuukandamiza uislamu (refer to Mohamed Said books). Vile vile baadhi ya mambo yanayofanywa na wakristo kukandamiza waislamu mfano wanapokejeli ati wao wamepeleka mwanzo MOU wakati sio kweli waislamu walipeleka mwanzo MOU ikapigwa chini (refer to Mohamed Said books), kunapelekea kuona waislamu wanaonewa.
Nilikuwapo!!!!

Mkuu, ninahisi kwamba wewe ni muislamu kutokana na jinsi ulivyoandika.
Aidha unaonekana pia kwamba umebahatika kupata elimu nzuri tu. Lakini wasiwasi wangu ni kwamba elimu uliyoipata haijakuelimisha vya kutosha.

Umejaribu kutupeleka katika rejea za vitabu vya mtunzi mohamed Said, kutuaminisha mambo ya kusadikika ya kwamba ati Mwl Nyerere aliukandamiza Uislamu. Na kututaka tuamini kushindanishwa kwa dhana ati nani alipeleka kwanza MoU kwa serkali, kati ya waislamu na wakristu.

MoU ni nini?, ni sera?, hadi useme kikundi fulani kiliipeleka ya kwao kwanza kwa serikali ikakataliwa lakini ya kikundi cha pili ikakubaliwa?!!! Kama kulikuwa na MoU, lazima ilikuwa imeandaliwa kwa pamoja baina ya pande mbili zinazokubaliana kuwa na hayo maelewano.

Lakini vilevile elewa kwamba Tz, imeongozwa hadi sasa na marais wanne. Wakristu wawili na waisalamu wawili. Ina maana unataka kuwatukana waheshimiwa hao marais waislamu kwamba hawakujua kuongoza hadi wasijue kwamba ati kuna kitu kinachoitwa MoU kinachowakandamiza waislamu wenzao?

Tatizo ni kwamba badala ya kujadili hoja kwa mantiki watu wanaleta ushabiki wa kidini bila kutumia akili ipasavyo. Samahani kama nitakukwaza.
 
Wapo wachche wanaotamani hali fulani itokee nchini, lakini wapo wengi wanatamani hali fulani isitokee. Kwanini waislamu wachache wanataka kutufanya waislamu wengi hatuna akili kwa kufuata mkumbo, ambao unafaidisha watu wachache kwa malengoyangu wenyewe. Kama wanataka mapinduzi ya kidini wawapeleke Syria wakajione.. huu ni upuuzi jamani. GOMESA
 
Back
Top Bottom