VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Kuna sintofahamu kubwa kati ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini(DPP) na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam juu ya suala la Mkuu wa Idara ya Usalama wa CHADEMA,Winfred Lwakatare ambaye anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kuandaa mipango ya kijasusi ya kudhuru watu.
Chanzo cha kuaminika toka ndani ya Ofisi ya DPP kinadai kuwa DPP amelitaka Jeshi la Polisi kukusanya ushahidi zaidi ili kuweza kumtengenezea Lwakatare makosa ya kisheria na kumsomea mashtaka kesho. Pia,amewataka Polisi kuamua,kwa kuainisha sababu mujarabu,kama Bwana Joseph Ludovick naye ashtakiwe pamoja na Lwakatare au la.
Vuta-nkuvute hiyo ilianza jana baada ya DPP na Wasaidizi wake kushinda Ofisini kuyapitia 'mafaili' ya Lwakatare na Ludovick yaliyotoka Polisi ili kujiridhisha na uchunguzi wa awali na makosa yanayoainishwa na uchunguzi huoili kuandaa Hati za Mashtaka dhidi ya Washukiwa hao.
'DPP alifika mahali haelewi kosa la kuwashtaki akina-Lwakatare kwa ushahidi uliopo.Akawataka Polisi wajiridhishe na kurudishe 'mafaili ' kwake hadi ifikapo saa kumi na mbili na nusu ya Jumatatu' kilidokeza chanzo hicho toka Ofisi za DPP
Kesho Jumatatu,Lwakatare anatarajiwa kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayomkabili. Bado haijulikani,atashtakiwa kwa mashtaka yapi hasa na kwa mujibu wa Sheria gani za nchi hii. Kesho,kutakuwa na taarifa zaidi na kamili.Tuvute subira.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam
Chanzo cha kuaminika toka ndani ya Ofisi ya DPP kinadai kuwa DPP amelitaka Jeshi la Polisi kukusanya ushahidi zaidi ili kuweza kumtengenezea Lwakatare makosa ya kisheria na kumsomea mashtaka kesho. Pia,amewataka Polisi kuamua,kwa kuainisha sababu mujarabu,kama Bwana Joseph Ludovick naye ashtakiwe pamoja na Lwakatare au la.
Vuta-nkuvute hiyo ilianza jana baada ya DPP na Wasaidizi wake kushinda Ofisini kuyapitia 'mafaili' ya Lwakatare na Ludovick yaliyotoka Polisi ili kujiridhisha na uchunguzi wa awali na makosa yanayoainishwa na uchunguzi huoili kuandaa Hati za Mashtaka dhidi ya Washukiwa hao.
'DPP alifika mahali haelewi kosa la kuwashtaki akina-Lwakatare kwa ushahidi uliopo.Akawataka Polisi wajiridhishe na kurudishe 'mafaili ' kwake hadi ifikapo saa kumi na mbili na nusu ya Jumatatu' kilidokeza chanzo hicho toka Ofisi za DPP
Kesho Jumatatu,Lwakatare anatarajiwa kupandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka yanayomkabili. Bado haijulikani,atashtakiwa kwa mashtaka yapi hasa na kwa mujibu wa Sheria gani za nchi hii. Kesho,kutakuwa na taarifa zaidi na kamili.Tuvute subira.
VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa wa Lumumba Dar es Salaam