denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,511
- 68,141
Unataka wapinzani waende mahakama ipi madai yao yakasikilizwe? au hizi za kuwafundisha mawakili wa serikali nini waseme? na kuwalinda kina Kingai?Point tatu za msingi
1. CCM hawajaanza kuiba kura 2019 wala 2020. Wizi wa kura upo kwenye DNA ya CCM. Waliiba kura 1995, 2000 (na kusababisha mauaji Zanzibar), 2005 (mtandao wa jk kazini), 2010 (kitengo wakalazimika kukanusha hadharani kuwa hawajaiba kura), 2015 (hapa kosa kubwa lilikuwa kwa upinzani kumsimamisha kada wa CCM Lowassa) na hiyo 2019 na 2020. Na wataiba kura tena 2025.
2. Mtu anapoibiwa halafu anaishia kulalamika tu kuwa ameibiwa, haina tofauti na anayekaa kimya baada ya kuibiwa. Wapinzani waeleze wamefanya wamefanya nini dhidi ya wizi huo mfulilizo?
3. Mapungufu ya CCM sio uimara wa upinzani. Moja ya sababu za CCM kibaki madarakani miaka mingi ijayo, apart from huo wizi wa kura, ni kukosekana kwa credible opposition. Let's face it, chama ambacho ukipishana nao tu mtazamo inakuwa halali kwao kutukana, kikikabidhiwa dhamana ya nchi kitakuwa na tofauti gani na CCM?
Wakidai Katiba Mpya unasema hawajui wanachopigania, wao ni kikundi kidogo cha watu, sijui unataka madai yao yaanzie wapi ambapo wengi wataibuka kwa pamoja.