Leo asubuhi nikielekea Mwanza, nimekutana na kisa cha ajabu sana na Fastjet.
Kuna mtoto mdogo wa kiume miaka kama 14 aliyekuwa wa mwisho kwenye foleni kwenye check in kuelekea Mwanza. Ilipofika zamu yake, akafungiwa kwamba muda umepita. Huyu mtoto hakuelewa cha kufanya na kukosa ndege.
Matokeo yake kaambiwa aende kwenye desk iliyopo nyuma ya check in desks. Mbaya zaidi pale pia akaambiwa atoke nje ya Geti akabadilishe ticket. Kwa vile nilikuwa na muda, nililazimika kutoka naye nje. Huko nje pia kaambiwa alipie Tsh. 300,000. Kwa kipi, nilishindwa kuelewa kusema kweli.
Hii nchi inaendeshwa kana kwamba hakuna sheria. Mtu unanunua ticket kwa Shillingi 130,000 lakini hawajali, wana kuambia ulipie karibia mara tatu? TCAA na Ndugu Suleiman nadhani wamelala au kama wako macho, wameyafumbia macho haya.
Watanzania hii ya Fastjet tulipiganie. Huu ni wizi wa mchana kweupe!
Kuna mtoto mdogo wa kiume miaka kama 14 aliyekuwa wa mwisho kwenye foleni kwenye check in kuelekea Mwanza. Ilipofika zamu yake, akafungiwa kwamba muda umepita. Huyu mtoto hakuelewa cha kufanya na kukosa ndege.
Matokeo yake kaambiwa aende kwenye desk iliyopo nyuma ya check in desks. Mbaya zaidi pale pia akaambiwa atoke nje ya Geti akabadilishe ticket. Kwa vile nilikuwa na muda, nililazimika kutoka naye nje. Huko nje pia kaambiwa alipie Tsh. 300,000. Kwa kipi, nilishindwa kuelewa kusema kweli.
Hii nchi inaendeshwa kana kwamba hakuna sheria. Mtu unanunua ticket kwa Shillingi 130,000 lakini hawajali, wana kuambia ulipie karibia mara tatu? TCAA na Ndugu Suleiman nadhani wamelala au kama wako macho, wameyafumbia macho haya.
Watanzania hii ya Fastjet tulipiganie. Huu ni wizi wa mchana kweupe!