Hivi kwa nini wengi wanajifanya wana pesa nyingi sana humu JF? Wangekuwa na pesa ndefu wasingekuwa wanashinda JF kwa kueneza umbeya. Hebu endeleeni kusafisha vibibi vya kithungu kama BAK.
Hivi baba yako au babu yako akiizeeka na kutojiweza hiyo kazi ya kumuogesha hua anaifanya nani? Au wewe ukizeeka nani atakusafisha na kukusitiri? Acha kudhalau kazi za watu ndugu yangu... duniani humu, sote tunategemeana kwa namna moja au nyingine.
Hata ungekuwa Ginimbi wa Zimbabwe au Bill Gates, lazima tu utasafishwa muda wako ukifika... mfano , wewe ugua tu Malaria, hata mtu wa kukupa uji utamuona wa maana sana na mahela yako... kwa ufupi.
Humu JF watu wanatoa tu kero zao na najua wakubwa wanasomaga na kuzipatia kero majobu mujarabu.