Wizara ya Afya yamruka Manumba, wahoji alikoipata ripoti ya Mwakyembe!

Huu Msakata wa Mwakiembe na Sumu hauna Tofauti na Sakata za Posho za Wabunge, Huku wanasema approved na huku wanasema not yet na huku wanasema still pending ....Crzy
 
Mimi nilikwishazungumzia huko nyuma kuhusu hili jeshi letu la Polisi kwamba linahitaji kuundwa upya kabisa (from the scrach).

Tanzania hatuna jeshi la polisi lenye kufanya kazi yake kikamilifu bila uoga na kujituma. na hii ni kwa sababu ya mfumo uliopo ambao hauwapi nafasi.

Hili suala la uchunguzi juu ya ugonjwa unaomsumbua Dr Mwakyembe, halihitaji mijadala namna hii bali polisi walitakiwa wawe busy kushughulika na uchunguzi wa kina juu ya hali aliyonayo Dr Mwakyembe.

Ila ukweli unabaki palepale kwamba Tanzania yetu ya leo imezungukwa na kiza kinene chenye kutoa madudu mengi ya ajabuajabu ambayo yanamaliza kabisa jitihada zozote za wanaharakati.
Mkuu Richard samahani usiseme hatuna jeshi la Polisi Tanzania, sema ndani ya jeshi la Polisi kuna wababaishaji na wanatumiwa!!!! Kama kungekuwa hakuna jeshi la polisi, wewe usingelilala nyumbani mwako, panapostahili kusifia sifia, polisi wapo na wanafanya kazi zao vizuri tuu!!!!!

 
SCREW 'EM! Serikali moja, chama kimoja, utawala mmoja lakini wanafanya kazi utadhani nchi ya wagagagigikoko na wale wa mgonenagonago!

Rais hajui anachosema Wazrii Mkuu, Waziri Mkuu hajui anachosema Rais, Spika hajui Rais alisema nini, Waziri hajui Waziri mwenzie amesema nini! Sijui wakiingiaga kwenye hivyo vikao vyao wanafanyaje kwa kweli!

Nasikia JK anataka kubadilisha baraza la mawaziri. Najiuliza hivi tatizo ni mawaziri au ni RAIS mwenyewe?
 
Manumba pambaf kabisa. Hivi hili jamaa elimu yake ni kiwango gani? Natilia shaka sana elimu aliyonayo. YAWEZEKANA ANA VYETI VYA KUGUSHI huyu kihiyo.

Katika hili Manumba amekurupuka na kama alivyosema Dr. Mwakyembe jamaa ameingia kwenye hii issue kama jitu ambalo halijawahi kwenda shule(Non-PROFESSIONAL)!Director of Criminal Investigation(DCI) utaletewaje habari mezani wakti wewe ndiyo unatakiwa uende kwa mhusika(Dr. Mwakyembe) umhoji na ikiwezekana utume watu kwenda Hospitali ya Apollo kwenda kupeleleza kama kweli Naibu Waziri alilishwa sumu? Hili ni swala linahusu uhai na Afya wa mtu amabye ni Waziri!

Kichekesho ni pale WAZIRI MPonda anapokanusha kuwa Manumba aulizwe taarifa hiyo ameipata wapi! Kuonyesha umbumbumbu wake anasema TAARIFA HIYO AMEPEWA NA MADAKTARI,KWA HIYO KAMA NI YA UONGO WAULIZWE HAO MADAKTARI!!!!!??? Kweli DCI unaweza kuongea utumbo kama huu eti waulizwe madakatari????

Manumba anatakiwa ajiuzulu au huyo aliyemweka kwenye hiyo nafasi(Rais) amwondoe mara moja!
 
Akizungumza na Tanzania Daima jana kwa njia ya simu, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Haji Mponda, alisema suala hilo limezungumzwa na Manumba, hivyo ni bora atafutwe na kueleza ametoa wapi taarifa hiyo na kueleza kuwa wizara hiyo kwa sasa haina la kusema.

Ugonjwa wake umekuwa ukihusishwa na kulishwa sumu na mara kadhaa Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amenukuliwa akisema ugonjwa huo umetokana na kulishwa sumu na kusisitiza kuwa Jeshi la Polisi lina ushahidi.
Hivi huu mtindo wa viongozi wa nchi kuwa na double standard kwa kila kitu utahisha lini? Kauli mbilimbili tofauti toka kwa viongozi wakubwa wawili wa nchi ni aibu kwa nchi yetu jamani.Hivi kwanini hii serikali inashindwa namna ya kurekebisha hili? DCI Manumba kasema wizara ndio imewapa ripoti,ndani ya siku mbili Waziri mwenye dhamana ya afya anadai yeye hajui kuhusu hiyo report,Hii imekaaje wakuu?

Haya huku Waziri mwenye dhamana ya Afrika Mashariki anasema kuwa rafiki yake kalishwa sumu,lakini mamlaka nyingine ndani ya nchi inakataa hilo,tena bila hata ya kumshughulikia huyo aliyesema maneno wanayoyakanusha.Mtindo huu wa kuendesha nchi kihuni kama familia zenu unatumaliza watanzania.Hii ni dalili kuwa hakuna mahusiano mazuri kati ya viongozi wa chama na serikali yao.Na kama ikiendelea hivi,hii miaka mitatu iliyobaki tuna hali ngumu sana.Mungu tusaidie!!
 
.....Sure Mkuu, nami niliwaza hivyo kuwa baada ya mtoto huyo wa kigogo kuhitaji hiyo ripoti ya ugonjwa, wajanja wa wizara ya afya wakafyatua ripoti feki wakakamata mshiko wao. Na kwa vile kulikuwa na lengo la kuichapisha ripoti hiyo magazetini-hususani gazeti la Mtanzania (kama ilivyodai Thread hiyo) na wao Mtanzania kuhofia masuala ya kisheria na kimaadili juu ya kuichapisha, huenda plan B ikawa ni kuwapatia Polisi ili waitoe kama matokeo ya uchunguzi! Na kwa vile polisi wetu ni polisi jina, pasipo hata kuingia deep juu ya reliability ya taarifa hiyo (bila kuchanganya na zao), wakajiona tayari wamesha-win, wakakurupa (kama alivyosema Mwakyembe) kuhitimisha kuwa HAKUNA SUMU!
Na bado, lazima ataibuka Mkubwa mwingine kuongezea utata juu ya hili.

ha ha ha haaa! Kama ile movie ya posho eeh!
 
Mnamshangaa Manumba Kweli?
-Lile la Rais, Spika na Waziri Mkuu juu ya kupanda kwa posho je?
-Lile la Edward Hosea na sakata la Richmond na kamati ya Bunge je?
-Lile la Jairo, Luhanjo, CAG na kamati ya Bunge je?
Halafu, kule Marekani niliwahi kuona Bill Clinton akimkana Monica Lewinsky. Muhimili wa nne wa DOLA utusaidie katika hili. Mwakyembe naye alimalize hili. Taarifa yake mnayoishangilia humu haina tofauti na kauli ya Lowasa kwenye NEC ya CCM juu ya Richmond!
 
Sijui bado tunasubiri kitu gani kitokee ndipo WOTE tuseme kuwa serikali hii ni ya wahuni!
 
Kwa wasiofahamu nawafahamisha na wanaofahamu nawakumbusha;

Robert Manumba anatoka jimbo moja na Andrew Chenge;
Ndio maana kwenye sakata la rada wale jamaa wa SFO walipopanga kumhoji chenge kuhusu paundi 600,000 alizotoa kwenye akaunti yake iliyoko kisiwa cha Jersey na kumpa Dr Idrisa Rashid, Manumba alivujisha siri kwa Chenge na wakapanga chenge ajibu kuwa alimkopesha rafiki yake kwa ajili ya mtaji wa fenicha. Wazungu walidhani Manumba ana integrity! kumbe ana kichwa cha nazi.

Kwa suala la Mwakyembe polisi hawawezi kusema ukweli hata ukiwa mdogo kiasi cha punje ya haradali!
Mwakyembe atuambie yeye mwenyewe anachoumwa. Isitoshe kile alichotuficha kinaendelea kututesa yeye mwenyewe na watanzania kwa ujumla mpaka leo. Fyatuka Dr. watz tuamue kabla mambo hayajazidi kuharibika. Mwenzio EL alishalipuka kwenye kikao wewe lipuka hadharani.
 
lol kwa hiyo Manumba na "vijana wake" wametumia mbinu za kijasusi kuzipata ripoti za wizara ya afya bila wahusika wenye taarifa kuwapatia au kujua .
Hiyo nina mashaka DCI Manumba and team wamechomekewa na mtoto wa kigogo aliyesemwa hapa JF anatafuta riporti ya Mheshimiwa Mwakyembe KWA GHARAMA YA TSHS40,000,000/=!!!!

 
Mkuu Richard samahani usiseme hatuna jeshi la Polisi Tanzania, sema ndani ya jeshi la Polisi kuna wababaishaji na wanatumiwa!!!! Kama kungekuwa hakuna jeshi la polisi, wewe usingelilala nyumbani mwako, panapostahili kusifia sifia, polisi wapo na wanafanya kazi zao vizuri tuu!!!!!

Nakubaliana na wewe Mtumishi Wetu! Lakini fikiria uonevu unaofanywa na Jeshi hili. Hapa tunazungumza jinsi wanavyojikanyaga kuhusiana na WAZIRI! Je ingekuwa ni mwnanchi wa kawaida, si wanadharau tu! Ona ni kesi ngapi ziko mahakamani, tena za shutuma kali dhidi ya watu fulani fulani. Huyu Manumba na mwenzie DPP na yule Hosea walifanya usanii mkubwa kwenye kesi ya Richmond, EPA na hatuna uhakika sana kama wale walioko mahakamani na gharama kubwa za kesi zile kwamba ni wahusika. Kwa namna hii unashawishika kuamini hawa mapolisi wetu wanatumiwa na wababishaji- ndio maana nimekubaliana na hoja yako.

Sitaki niamini kuwa jeshi la Polisi ndio linanifanya nilale kwa amani! Ukipata shida ukapiga simu- watakuja kwa wakati wao, watauliza maswali ya kijinga! Usingizi wangu ninahakikishiwa na ulinzi shirikishi katika maeneo yangu na hawa makampuni ya binafsi! Polisi wanaua hovyo hovyo siku hizi, bora lifute- ni kama hatuna Jeshi la Polisi Tanzania!

Mungu Ibariki Tanzania
 
Nimeipitia hiyo habari mwanzo mpaka mwisho mara tatu, sijaona pahala Wizara ya afya ilipomruka Manumba.

Wacheni udaku.
 
Kama kawaida yao viongozi wa nchi,kila mtua hajui anachosema.Ndugu zangu picha linaendelea kae vizuri kwenye vitiwale walionje waiteni.
 
Manumba Kazi yake ni Kusubiri Ofisini Ujinga unaoletwa na Maaskari ambao tayari Mwakyembe alisema hawana sifa ya kushiriki katika uhalali wa kumfanyia Mahojiano kwa sababu ni Askari haohao wanao tuhumiwa Kumbambikia Mtoto wa Mengi Madawa tena ni Askari haohao wanaoshutumiwa kwa Mauaji
Morogoro!

Bado ushahidi wa Dr. Harrison Mwakyembe unatosha kumaliza picha ya Waziri Mkuu aliyejiuzuru Edward Lowasa na Mbunge wa wa Zamani Igunga Rostam Aziz kuwa ni Mafisadi na wezi Nchini.

Lowasa alisubiri Mwakyembe akiwa India katika Matibabu eti ndio akatoa Maneno ya yeye kujisafisha ndani ya Kamati Kuu CCM huku Kikwete akiwa ameundiwa Mkakati wa kung`olewa kipindi kile lakini baada ya Sita kugunduwa akakimbilia India Kumpa Ukweli Kamanda mwenzie namna ambavyo Mambo yanataka kufanywa!

Leo hii kupona kwa Mwakyembe ni Pigo Takatifu kwa IGP Said Mwema na DCI Manumba kwani hawa wote wanapokea Mshahara kwa Lowasa & Lostam kwa Kazi moja tu! Kuhakikisha Ushahidi unapotea na kamwe watanzania wasijue ukweli wa Mambo yalivyo!

Mwakyembe aliandika Barua ya Siri kwa IGP Mwema je ni nani aliyeandika kwenye Vyombo vya Habari kama si yeye IGP Mwema! Bado sisi Wananchi wa Tanzania tunasema Kusoma hatujui Kitabu chenu IGP na DCI hata Picha za Kitabu mmnaamini hatuzioni ?.

Juzi Bungeni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Mbowe alisema! Haya mambo ya Funika Kombe Mwanaharamu apite yatatugharimu Sana! Nami narudia usemi wake! IGP Mwema na DCI Manumba Watanzania tunajua Sinema yote kabla hamjaanza kuhadidhia hivyo muwe Makini sana hatua mnazochukua Maana Ukweli mbona uko wazi bayana juu ya Ninyi wawili kuhusika na Mafisadi.
 
Nimeipitia hiyo habari mwanzo mpaka mwisho mara tatu, sijaona pahala Wizara ya afya ilipomruka Manumba.

Wacheni udaku.
Soma na Mwananchi ya leo pia ingawa limepanda bei. Mwakyembe alimalize hili lisije likammaliza kama Richmond ilivyomgeuka sasa.
 
Watanzania tuko kimya, kazi yetu kushabikia tu. Wana mbeya na wana kyela na wanaharakati mko wapi? Wakati umefika sasa wakutoa tamko na maamuzi kwa serikali hii. Ndugu yetu dr. Mwakyembe anateseka kwa kosa gani? Kutetea maslahi ya umma. Nchi hii inakwenda wapi? Jeshi la polisi ni kwa ajili ya nani? Mshahara wanaopata pesa zinatoka wapi? Lazima swala la mwakyembe tulisimamie tuungane watanzania tuache unafiki, ushabiki, na ubinafsi. Tuki kaa kimya tutapoteza wapiganaji na tutakosa wapiganaji wapya. Waandishi wa habari mnapewa taarifa za uwongo mnamsikiliza tu na kuandika kama ilivyo hamna hata uchungu wa nchi yenu. Ingekuwa nchi nyingine msemaji wa polosi manumba asinge toka salama kwa kusema uwongo. Tujirekebishe
 
Back
Top Bottom