Will Kikwete make this speech?

Will Kikwete make this speech?

Kumbuka Mzee Iddi alitushambulia mwaka 1972 kwa kile alichodai kuwa anashambulia majeshi ya msituni ya Obote. Nyerere alijiandaa na ile vita iliyoanza 1978 kwa muda mrefu sana. Hatukupata mkopo wala msaada wa maana katika vita ya Uganda. Tuliigharamia wenyewe. Hoja yangu sio kama tulipashwa kupigana vita au hapana. Ninachotaka kusema ni kuwa Nyerere alijiandaa muda mrefu kumuondoa Amin. Hata kabla ya hapo Nyerere alitambulika bayana kwa maamuzi yake ya kuamuru majeshi yetu kwenda kupigana Msumbiji na kakisiwa fulani huko Afrika. Mikakati ya kumuondoa Mzee Smith huko Zimbabwe, mapigano Angola, na vikwazo vya uchumi Afrika kusini. Hivyo basi, alipowaita wazee wa Dar na kuwaeleza "nia tunayo na nguvu tunazo" wazee walisisimka kwasababu walioanisha matendo yake ya nyuma tokea harakati za kumg'oa mkoloni mpaka siku alipokuwa anawahutubia. Waliamini kuwa ile ilikuwa dhati ya moyo wake na wakawa na imani na aliyokuwa akiyasema.

Mkuu Kyoma shukran kwa unyambulifu huo usiwe unapotea sana maana tunakosa mengi.

Hicho kipande nilichokipachika hapomjuu kwangu ni shule mpya nilikuwa sina elimu nalo.
 
Hotuba nzuri hutokana na yale uliyoyafanya na/au unayotarajiwa kuyafanya. Yote haya Rais wetu hana. Yeye urais ilikuwa ni accomplishment; it was an end rather than a means to achieve something. Sanasana atatoa hotuba ya kujipongeza kwa njia alivyohangaika na kui-invest katika kupata urais na kupondea wale wanaojaribu kumkosoa. Huko tunakoenda hana njia nyingine ya kunyamazisha kelele za watu wanaomkosoa zaidi ya kuwa dikteta. Ndiyo hivyo ameshaanza na Mtikila. Tutashuhudia mengi.
 
Kitila Mkumbo,
urais ilikuwa ni accomplishment; it was an end rather a means to achieve something.
Kuna ukweli mkubwa katika maneno hayo na hii ndio hali halisi ya viongozi wengi wa kiafrika!...
Watakapo weza kuona tofauti kati ya maneno hayo basi huyo rais ama Mtawala lazima atafanikiwa...
 
Kwa kifupi hakuna jipya bali ni hotuba ya yada yada yada yada yada! wakati ataendelea kula nchi na kuwakumbatia mafisadi, wala rushwa, wanaojilimbikizia mali na wanaosaini mikataba isiyo na maslahi kwa Tanzania wakati mamilioni ya Watanzania wakiendelea kutaabika na umaskini uliokithiri na huduma mbovu mahospitalini, mashuleni, kwenye huduma muhimu za usafiri upatikanaji maji, umeme n.k.
 
Kuna pointi mbili muhimu ambazo nimeziona na kwa namna fulani zinahusiana.

a. Kwanini Kikwete aliutaka Urais? Kitila naona amelijibu swali hilo kwa maneno machache lakini ukweli wake unaweza kujaza vitabu. Kikwete kuutaka Urais kama an end in itself, ni sawa sawa kabisa na bondia ambaye sifa zake, jinsi alivyotunisha misuli na anavyozungumza "dirty" juu ya wabaya wake anavyopania kuingia ulingoni. Wakati watu wanaamini kuwa bondia huyo anataka kuingia ulingoni ili kuuthibitishia umma kuwa yeye ni bondia bora kuliko wote, kumbe bondia huyo anataka kuingia ulingoni ili aweze kusema "alipanda katika ulingo wa fainali za ngumi duniani".

Na anapoingia ukumbini kwa kushangiliwa na kupigiwa miluzi bondia wetu anaanza kampeni yetu dhidi ya bondia ambaye jina lake hata halijulikani na hakuna chombo cha habari kilichomfuatilia. Kipenda kilipopigwa bondia watu akawa anajirusha rusha kwa mbwembwe na kabla hajakaa sawa Richmond puu! na kabla hafungua macho kuanglia kilichompiga Buzwagi puu!! na anabakia ameshikilia kamba akiweweseka..!!

Watu wanajiuliza kama sifa za bondia yule kabla ya kuingia ulingoni zilikuwa na msingi?

Hili linanileta kwenye hoja ya Kyoma. Kama bondia ana rekodi ya kupigana toka huko nyuma na kushinda basi hata apige porojo vipi watu wanaamini anaweze kuthibitisha maneno yake kwa vitendo, kwani watu wanajua anayo rekodi. Vinginevyo itakuwa kama kisa cha yule Bondia wa Uingereza Prince Naseem ambaye alikuwa na mbwembwe sana hadi siku ile alipokiona cha moto!

Hata hivyo hili linanipeleka kwenye point nyingine kuwa kuna wakati ambapo bondia hata asiye na rekodi ya kutisha anaweza kujijengea jina inapotokea nafasi ya kupambana na bingwa wa dunia! Douglas Douglas hakuwa anajulikana na hakupewa nafasi ya kufanya vizuri hadi pale alipombumunda (notthe same as mabumunda) Mike "Iron" Tyson! Kuna wakati ambapo mpigani uoneshe kuwa unasimama kwa nguvu zako mwenyewe na siyo ahadi, sifa, au majina ya kujipachika au kupachikwa.

Rais Kikwete amepewa nafasi nyingi ndani ya miaka hii miwili kuweza kuonesha kuwa he is a fighter! Suala la Richmond, Buzwagi, na mambo mengine yanayoendelea sasa zimekuwa ni nafasi zilizopotezwa na sidhani atapata nafasi nyingine ya kuonesha kuwa "hana ubia" katika Urais. Watanzania wamemshangilia na walifurahia yeye kuingia ulingoni, lakini hadi hivi sasa salamu za ushindi zimesitishwa, kwani watu wanamuona ni mpiga porojo. Hotuba yake ya Mkutano Mkuu yaweza kuwa ni defining moment, na akaziachia kamba za ulingo na kuanza kujibu mashambulizi, siyo dhidi ya wapinzani kama alivyofanya bali ndani ya serikali yake na watu wa karibu ambao wana sabotage his efforts.

Ni mpaka pale atakapoonesha kuwa anaweza kupigana katika ulingo wa Taifa letu, basi atabakia kuwa ni bondia mtarajiwa! na hii ni raundi ya kwanza, asipoangalia wananchi hawatataka arudi tena ulingoni kwenye raundi ya pili na ya mwisho 2010! Wakati timu yake inajiuliza kama ni bondia aliyestahili, ni lazima akumbushwe kuwa kuna wato wako gymn wanafanya mazoezi!!
 
Hata hivyo hili linanipeleka kwenye point nyingine kuwa kuna wakati ambapo bondia hata asiye na rekodi ya kutisha anaweza kujijengea jina inapotokea nafasi ya kupambana na bingwa wa dunia! Douglas Douglas hakuwa anajulikana na hakupewa nafasi ya kufanya vizuri hadi pale alipombumunda (notthe same as mabumunda) Mike "Iron" Tyson! Kuna wakati ambapo mpigani uoneshe kuwa unasimama kwa nguvu zako mwenyewe na siyo ahadi, sifa, au majina ya kujipachika au kupachikwa.

Mzee Mwanakijiji, heshima mbele mkuu!

kwanza nakubaliana na maneno machache ya Mzee Kitila Mkumbo kuwa kwa Kikwete "Urais ilikuwa ni accomplishment. Mzee Kitila made my day. Hakika, ukimuondoa Salim miongoni mwa waliokuwa wanautaka Urais mwaka 2005, ni Kikwete peke yake aliyekuwa ameranda randa dunia nzima na kukutana na viongozi wa mataifa yote duniani kuzidi mgombea mwingine yeyote. Binafsi, nilidhani kitendo cha kumchagua Kikwete kuwa Rais kingejenga imani miongoni mwa watanzania kuwa kiti chetu cha henzi kimekaliwa na Rais ambaye si limbukeni wa safari za nje ya nchi zinazowagharimu watanzania mamilioni ya fedha.

Rais wa Tanzania sio mtu binafsi bali ni Taasisi. Tungekuwa na ahueni tena mara dufu kama mtu binafsi aliyekalia taasisi ya Urais angekuwa na nia ya dhati kuwa kitendo cha kukalia hiyo taasisi in it and itself is an accomplishment. Basi tungemwombea ili amalize kipindi chake haraka sana so that we can move on. Lakini sheria ya asili inatutahadharisha. Wahenga walisema kuwa "nature abhors vacuum"-hulka huchukia hombwe. Hofu yangu kubwa sio kwa Kikwete anayefikirika kuiona Taasisi ya Urais as an accomplishment, and therefore a dead end. Hofu yangu ni wale wanaomtumia mtu aliyekalia Taasisi ya Urais wa nchi yetu in order to achieve something, ikizingatiwa kwamba mtu mwenyewe yupo kama hayupo.

Anyway, Mzee mwanakijiji unasema kuwa Douglas alikuwa hajulikani na hakupewa nafasi ya kufanya vizuri. Well, nadhani kujulikana sio sifa ya ubora bali ni sifa ya kutang'aa. Mara nyingi bidhaa inajulikana kwasababu ya matangazo. Kumbuka mapambano ya ngumi za uzito wa juu duniani ni miradi mikubwa kwa makampuni mengi ya kibepari. Mabondia wanauzwa kama bidhaa kabla ya mapambano. Biashara inayosifika kwa matangazo inahitaji umakini wa hali ya juu kutoka kwa wanunuzi. Bahati mbaya siasa za nchi yetu zimegeuka kuwa miradi mikubwa kwa makampuni ya kibeberu. Wanasiasa wanauzwa kama bidhaa.

Ni mkosi, ni nuksi, ni balaa, na ni bahati mbaya kuona biashara ya namna hii inafanyika katika nchi yetu. Nasema hivyo kwasababu watanzania baada ya uhuru hatukupewa nafasi ya kufanya mijadala ya wazi wazi kuhusu mambo ya siasa. Baada ya kukabwa kabali kwenye medani ya kisiasa, tulipumulia katika michezo. Mijadala ya michezo hasa mpira wa miguu ilishamiri mijini na vijijini katika virabu vya pombe, Migahawani, vituo vya mabasi, majumbani, mashuleni na vyuoni. Bahati mbaya tukazaa Mashabiki wengi wa mpira kuliko tulivyozaa wapenzi wa mpira.

Mshabiki ni yule anayependa kitu bila sababu. Mpenzi ni yule anayependa kitu akiwa na sababu za msingi. Wapenzi wanajadiliana kabla ya usajili wa wachezaji wa timu yao. Wanakosoana na kukubali makosa kabla ya mpira kuanza. Hata wakishindwa, wanakubali kwa dhati ya moyo wao kwasababu wanatambua udhaifu wa timu yao. Kwa wapenzi, kushindwa ni changamoto na wala sio nafasi ya kupigana mieleka. Ni fursa ya kuchanga bongo kwa lengo la kuondoa udhaifu na kujenga timu yenye kuleta ushindi.

Mashabiki wanafanya mambo kinyume na wapenzi. Hata timu yao ikimsajili golikipa ambaye ni kipofu, mashabiki watatetea huo uozo hata kwa ncha ya upanga. Wakifungwa watavulumushiana matusi, masumbwi, na kubwatabwata kwa sababu zisizo na kichwa wala miguu. Eti wameshindwa kwasababu uwanja ulikuwa na maji, kana kwamba timu iliyowafunga ilichezesha Samaki. Vitendo hivi vya kiushabiki ni mojawapo ya sababu zilizoigalgaza michezo yetu nchini. Sasa tunashabikia timu za Ulaya ambazo zina wapenzi wengi kuliko Mashabiki.

Nimeongelea suala la ushabiki na upenzi kwasababu baada ya kuruhusiwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa, ushabiki uliokuwa mpirani ulihamia kwenye duru za siasa. Ndio maana siku hizi ukichanganya mpira na siasa watu wanapata kiwewe. Lakini ukweli ni kwamba nchi yetu inakabiliwa na tatizo la kuwa na idadi kubwa ya mashabiki wa vyama vya siasa kuzidi idadi ya wapenzi wa hivyo vyama. Wengi wanavishabikia vyama bila sababu, na vikifanya usajili wakati wa kinyanganyiro cha kugombea nafasi za uongozi, ushabiki unatawala kuliko upenzi. Kumwaga tindikali kwenye kidonda, makampuni ya kibeberu yanakuja na mfumo wa matangazo ya kuwauza wanasiasa wetu kama bidhaa sokoni. Wananchi wanaishia kuchagua hizo bidhaa (wanasiasa) kutokana na hayo matangazo ambayo nyuma yake wamejificha mabeberu.

Ni kweli, Tyson alikuwa ni moto wa kuotea mbali wakati anapigana na Douglas. Alikuwa na wapenzi pamoja na Mashabiki wengi. Tyson alijijengea sifa kwa kuwakwida mabondia luluki. Umaarufu wake haukuwa na doa. Kwa mtu aliyejijengea jina kama Tyson, ni rahisi kwa kila kampuni ya kibepari kutaka kuwekeza kwenye jina lake. Mantiki ni kuwekeza mtaji wa fedha kidogo kwa faida kubwa. Lakini hiyo haimaanishi kuwa Tyson hakuwa na kasoro za msingi. Pia, si kweli kwamba Douglas hakuwa bondia bora kabla ya lile pambano. Ni kwamba hakuna kampuni iliyokuwa tayari kuwekeza fedha kwa utangaza ubora wa Douglas.

Kumbuka "wapenzi" wa kambi ya Tyson, kabla ya lile pambano walianza kuingiwa na wasiwasi kuwa hakuna bondia yeyote aliyewahi kumfikisha Tyson katika raundi ya kumi. Yalikuwepo majadiliano kuwa pamoja na ubora wa Tyson, hajawahi kupigwa ngumi nyingi na akaanguka chini alafu akainuka na kumtwanga mpinzani wake mpaka akashinda. Uso wake ulikuwa haujapigika na walikuwa hawajuhi uvumilivu wake wa masubwi ni wa kiasi gani kama angepata bondia wa kumfikisha katika hali hiyo. "Mashabiki" wa Tyson hawakulifikiria suala hilo kwasababu walijua kuwa konde moja la Tyson likimpata bondia yeyote anazilai na hawezi kuamka. Kama ilivyo adha, "Mashabiki" huwa hawana utamaduni wa kufikiri zaidi ya hapo.

Douglas aliigia kambini kwa muda mrefu akijiandaa kupigana raundi nyingi. Aliongea bayana kabla ya pambano kuwa Tyson hajawahi kupigana raundi nyingi hivyo yeye alijiandaa na hilo na hakuona sababu ya kushindwa lile pambano. Kuingia ulingoni na kupambana na Tyson halikuwa lengo la Douglas na wala isingekuwa accomplishment kwake. Alidhamiria muda mrefu kumtwanga Tyson. Kwa "wapenzi" wa ndondi, pambano la Tyson vs Douglas lilimalizika katika raundi ya sita/saba wakati Tyson alipomtwanga Douglas sumbwi moja la nguvu na Douglas akaanguka chini.

Lakini Mashabiki wa Tyson walijua Dougla hasingeamka tena, hivyo huo ndio ulikuwa mwisho wa mchezo. Ndio maana "Mashabiki" wa Tyson hawakuamini kilichotokea baada ya mechi kumalizika. Waliishia kulalama kuwa refa alikosea kwa kuhesabu mpaka 11 badala ya kuishia 10, hivyo kumpa Douglas nafasi ya kuamka. Kitendo cha Douglas kuamka kilikuwa ni pigo kubwa la kisaikolojia kwa Tyson. Naam! alitambua kuwa aliyokuwa akiyasema Douglas yametimia. Na "wapenzi" wa Tyson, walitambua kuwa huo ndio ulikuwa mwisho wa Tyson.

Kumbuka Mama yake kipenzi wa Douglas alikuwa amefariki muda mfupi kabla ya pambano. Douglas alishauriwa akubali kuhailisha pambano ili akamzike Mama yake lakini yeye alikataa ombi hilo. Aliwaambia washauri wake kuwa haitakuja kutokea siku katika maisha yake akajiandaa kupigana raundi nyingi kama alivyokuwa amejiandaa. Alisema Mama yake alikuwa shahidi mzuri wa jinsi alivyojiandaa na kama angekuwa hai angetaka ashinde lile pambano. Muda mchache kabla ya pambano, Douglas alisema anataka pambano lile liwe la kumhenzi Mama yake. Ni kweli, baada ya ushindi ule akaenda kutumia fedha yote kwenye matanuzi. Akawa na matatizo ya uzito mkubwa na huo ndio ulikuwa mwanzo na mwisho wa Douglas na Tyson pia. Lakini dhamiri ya douglas ya kumtwanga Tyson ilitimia.

Mzee Mwanakijiji ni vema umetoa mfano wa Douglas kwani tunaweza kujifunza mengi katika siasa zetu za bongo. Kitu cha kwanza ni kuwa kujulikana sio sifa ya ubora bali ni sifa ya matangazo. Kujulikana kisiwe kipimo cha kuwapima wagombea uongozi katika nchi yetu. Tuweke machujio ambapo kila mtu, anayejulikana na asiyejulikana atatakiwa kuchujwa. Hivyo basi, yatupasa tuache ushabiki katika masuala ya msingi, hasa tunapotakiwa kumchagua mtu wa kukalia Taasisi ya Urais wa nchi yetu ambayo ina madaraka makubwa kuzidi Taasisi zote. Rais wa nchi yetu ni kama Mungu mtu aliye juu ya sheria zote. Tuvipende vyama vya siasa badala ya kuvishabikia.

Tuwe wapenzi wa nchi yetu kwa kukubali makosa tuliyoyafanya badala ya kujipa matumaini ya kufikirika. Tukubali kwamba mwaka 2005 nchi yetu ilikuwa imekabwa kabali na mikataba mibovu. Tulikuwa na chaguo la kuiondoa nchi yetu kutoka katika hilo janga ili iweze kupumua lakini hatukufanya hivyo. Hatukuwauliza au kuwapigia makelele wagombea Urais ili watueleze jinsi gani wangeiondoa nchi yetu katika koromeo la mikataba mibovu. Bahati nzuri, mmoja wa wagombea ambaye alitokea kushinda uchaguzi alikuwa kiongozi wa Wizara ya Nishati na Madini. Tulitakiwa kumkaba koo ili atueleze alichoona na anachojua. Kwasababu alikuwa anautaka Urais kama accomplishment, na laiti angejua kuwa ndoto zake zisingetimia bila kutupatia majibu ya uhakika, basi angesalimu amri kwa wananchi kwa kutueleza ukweli. Leo hii tungekuwa tunaongelea mengine.

Lazima tujue kuwa Kikwete hakuwa na utajiri unaoonekana machoni mwa watanzania. Hata angekuwa nao, usingefua dafu kwa kiasi cha fedha kilichotumika wakati wa kampeni za kumuingiza madarakani. Hatukujiuliza wakati ule kuwa zile fedha ni za nani na zingerudishwa vipi? Hata hivyo, hilo halitukatazi kukubali ukweli sasa hivi kuwa zile fedha zilikuwa na wenyewe na lazima zirudishwe. Tukisha kubali huu ukweli, basi tuachane na ndoto za kutegemea hotuba yenye kuleta matumaini kutoka kwa Kikwete. Binafsi naona tutafakari jinsi ya kujinasua kutoka katika hiki kitanzi tulichojiwekea wenyewe. Kilichoko mezani kwetu ni nchi yetu ya Tanzania na wala sio wale waliotoa fedha za matangazo na hongo na wala Kikwete mwenyewe. Kwetu sisi, iwe ama zake ama zao. Tudai nchi yetu irudishwe mikononi mwa watanzania. Na ole wao watakao ingilia kati kwani watakiona cha mtema kuni.

Mwisho tukubali ukweli kuwa sio watanzania waliomuingiza Kikwete madarakani. Waliomuingiza Kikwete madarakani wametulia kama maji ya mtungi. Wanalia kivulini huku wakiwa wamekunja nne. Kama Urais ni accomplishment, basi hotuba zake zote zitawahenzi waliofanikisha hilo na sio wale walioenda kutumbukiza karatasi kwenye masanduku ya kura.
 
In business, it is great to make efforts, however it is the results that matters! as of now we have seen no results but tireless efforts to sell a product that in not consumable = loss of capital and production!

Measured Results on JK leadership and management are NIL/KAPA/PATUPU! we only see jitihada hewa!
 
Yombayomba,

Hotuba ilikuwa nzuri sana, sio kwa mtazamo wenu, ila ilikuwa nzuri. Kitendo cha kuwakemea mtandao kilikuwa cha kishujaa!
 
Yombayomba,

Hotuba ilikuwa nzuri sana, sio kwa mtazamo wenu, ila ilikuwa nzuri. Kitendo cha kuwakemea mtandao kilikuwa cha kishujaa!

Mzee FD, nilidhani alishaanza kukemea hata kabla hajawa Rais, nakumbuka vizuri alichosema Ngurdoto, na kwa hakika nakumbuka alipozungumza na viongozi wa Halmashauri na Serikali za Mitaa pale Dodoma.

Jambo moja nina uhakika nalo, Rais Kikwete ni mkemeaji mzuri sana!! Kwa hili sina ubishi.
 
Mwanakijiji,

Mpeni benefit of doubt jamani. Kuongoza nchi ni ngumu sana kaka. Ukishaingia ndani kuna mengi ya ajabu sana. We acha tu.
 
Mwanakijiji,

Mpeni benefit of doubt jamani. Kuongoza nchi ni ngumu sana kaka. Ukishaingia ndani kuna mengi ya ajabu sana. We acha tu.

I agree with you that is why I doubt him..
 
Kuna pointi mbili muhimu ambazo nimeziona na kwa namna fulani zinahusiana.

a. Kwanini Kikwete aliutaka Urais? Kitila naona amelijibu swali hilo kwa maneno machache lakini ukweli wake unaweza kujaza vitabu. Kikwete kuutaka Urais kama an end in itself, ni sawa sawa kabisa na bondia ambaye sifa zake, jinsi alivyotunisha misuli na anavyozungumza "dirty" juu ya wabaya wake anavyopania kuingia ulingoni. Wakati watu wanaamini kuwa bondia huyo anataka kuingia ulingoni ili kuuthibitishia umma kuwa yeye ni bondia bora kuliko wote, kumbe bondia huyo anataka kuingia ulingoni ili aweze kusema "alipanda katika ulingo wa fainali za ngumi duniani".

Na anapoingia ukumbini kwa kushangiliwa na kupigiwa miluzi bondia wetu anaanza kampeni yetu dhidi ya bondia ambaye jina lake hata halijulikani na hakuna chombo cha habari kilichomfuatilia. Kipenda kilipopigwa bondia watu akawa anajirusha rusha kwa mbwembwe na kabla hajakaa sawa Richmond puu! na kabla hafungua macho kuanglia kilichompiga Buzwagi puu!! na anabakia ameshikilia kamba akiweweseka..!!

Watu wanajiuliza kama sifa za bondia yule kabla ya kuingia ulingoni zilikuwa na msingi?

Hili linanileta kwenye hoja ya Kyoma. Kama bondia ana rekodi ya kupigana toka huko nyuma na kushinda basi hata apige porojo vipi watu wanaamini anaweze kuthibitisha maneno yake kwa vitendo, kwani watu wanajua anayo rekodi. Vinginevyo itakuwa kama kisa cha yule Bondia wa Uingereza Prince Naseem ambaye alikuwa na mbwembwe sana hadi siku ile alipokiona cha moto!

Hata hivyo hili linanipeleka kwenye point nyingine kuwa kuna wakati ambapo bondia hata asiye na rekodi ya kutisha anaweza kujijengea jina inapotokea nafasi ya kupambana na bingwa wa dunia! Douglas Douglas hakuwa anajulikana na hakupewa nafasi ya kufanya vizuri hadi pale alipombumunda (notthe same as mabumunda) Mike "Iron" Tyson! Kuna wakati ambapo mpigani uoneshe kuwa unasimama kwa nguvu zako mwenyewe na siyo ahadi, sifa, au majina ya kujipachika au kupachikwa.
Rais Kikwete amepewa nafasi nyingi ndani ya miaka hii miwili kuweza kuonesha kuwa he is a fighter! Suala la Richmond, Buzwagi, na mambo mengine yanayoendelea sasa zimekuwa ni nafasi zilizopotezwa na sidhani atapata nafasi nyingine ya kuonesha kuwa "hana ubia" katika Urais. Watanzania wamemshangilia na walifurahia yeye kuingia ulingoni, lakini hadi hivi sasa salamu za ushindi zimesitishwa, kwani watu wanamuona ni mpiga porojo. Hotuba yake ya Mkutano Mkuu yaweza kuwa ni defining moment, na akaziachia kamba za ulingo na kuanza kujibu mashambulizi, siyo dhidi ya wapinzani kama alivyofanya bali ndani ya serikali yake na watu wa karibu ambao wana sabotage his efforts.

Ni mpaka pale atakapoonesha kuwa anaweza kupigana katika ulingo wa Taifa letu, basi atabakia kuwa ni bondia mtarajiwa! na hii ni raundi ya kwanza, asipoangalia wananchi hawatataka arudi tena ulingoni kwenye raundi ya pili na ya mwisho 2010! Wakati timu yake inajiuliza kama ni bondia aliyestahili, ni lazima akumbushwe kuwa kuna wato wako gymn wanafanya mazoezi!!

Nadhani Kyoma ameelezea kwa ufasaha mzuri sana kuhusu mazingira yanayopelekea kiongozi kutoa hotuba nzuri, ya dhati, yenye mafunzo mazuri na itayokumbukwa kwa vizazi na vizazi vijavyo.

Mfano wa bondia ni mzuri. Buster Douglas hakuwa bondia mzugaji (Journeyman). Katika circles za boxing alikuwa tayari keshajijengea jina. Wapenzi wa ndondi walikuwa wanamfahamu lakini kwa mashabiki ndio alikuwa hajulikani kama alivyokuwa akijulikana Tyson. Katika ngumi za kulipwa, mara nyingi bondia huwa hawezi kupata fursa ya kupigania ubingwa wa dunia tena na bingwa asiyepingika (undisputed) bila kuwa na rekodi ya nzuri dhidi ya mabondia bora. Kupata fursa ya kupigana na Tyson, Buster alikuwa keshashinda mechi za kutosha na hatimaye kujipatia hiyo fursa ya kutwangana na Tyson. Na kwa vile hayo mapambano ya mtoano yalikuwa dhidi ya mabondia wazuri, basi yalimwezesha kujiandaa vizuri kukabiliana na bingwa (Tyson) na siku ya siku ilipofika jamaa akafanya kweli na akaandika historia itakayokumbukwa kwa miaka mingi ijayo.

Sasa unajiuliza,huu mfano unahusiana vipi na Kikwete? Huyu jamaa amekuwa kifelong member wa CCM. Ameshika nyadhifa kadhaa serikalini na kwenye chama. Katika mfano wa ndondi hizo nyadhifa ni sawa na amateur career, golden gloves championship, undercard fights, elimination bouts, nk. Sasa amepata nafasi ya kuwa kwenye main card katika main event. He is now on primetime to show us that he is the real deal: ready to fight for the title and become champion.

Lakini kwa wapenzi wa ngumi kama mimi tunawajua mabondia bora na ambao wanastahili kupigania ubingwa kulingana na rekodi zao kwa vile tunafuatilia kwa ukaribu mchezo wa boxing. Sasa Kikwete ktk hizo nyadhifa alizowahi kushikilia alikuwa na rekodi gani iliyomfanya apate fursa ya kupigania huo ubingwa? Alikuwa mbunge kwa muda mrefu tu, je is there any piece of legislation that he sponsored or co-authored? Did he deliver at least some if not most or all of his promises to the constituency that he represented? While a deputy minister and ultimately minister, what was his record? What was he for and what was he against? Does he have a proven track record with results? If he did what is that record and what are those results?

In boxing you start off as an amateur. You probably win several local competitions then you go on to the golden gloves (in the US at least). If you do well there you go to the Olympic trials. If successful at the trials you get selected to represent your country. If successful at the Olympics you win a medal ( bronze, silver, or gold). Then you most likely turn pro. In the pro ranks you work your way up the ladder then eventually you fight for the championship. But you don't just get the opportunity to make big bucks and fight for the championship without an impressive pedigree. That amateur career is what primes you to later become champion and write history.

Sasa nirudi kwenye hoja ya Mzee Kyoma kwamba hotuba kama "I Have A Dream" au kama ile ya Mandela au ile ya Nyerere hutanguliwa na matendo. Kikwete hawezi kutoa hotuba kama hiyo. Hata kama akija kutoa hotuba nzuri kiasi gani haitakuwa na impact kubwa wala kukumbukwa na vizazi vijavyo kwa sababu hakuna rekodi yoyote huko nyuma itakayowafanya watu waoanishe matendo na maneno yake. Na mara nyingi hotuba kama hizo huwa zinatoka moyoni na maneno yake huwa ni ya dhati na si tu kwa kutaka sifa ya eti na wewe umetoa hotuba nzuri. Nadhani watu wote waliowahi kutoa hotuba za namna hiyo nia au kusudi lao halikuwa kumbukumbu bali lilikuwa ni kutoa kile kilichokuwa moyoni mwao.
 
kikwete ndio amemaliza speech yake ya mwezi hapa TBC na as usual hakuna cha kukumbuka (really sad)

I wish ange-focus kwenye operations aache policies and politics akiongea na wananchi kwani wengi tuko desperate
 
Mwanakijiji,

Mpeni benefit of doubt jamani. Kuongoza nchi ni ngumu sana kaka. Ukishaingia ndani kuna mengi ya ajabu sana. We acha tu.
kwani alikua haijui wakati anaomba kazi!!!??? please give me a break, aliomba kazi ili aondoe huo ugumu sasa nini kinashangaza

we are missing mtendaji au kiranja wa watendani, tunae mtu wa sera na itikadi... that is the weakest link
 
Ndugu zangu niaminini JK akija na hotuba ya dhati, iliyojaa maneno ya kujaza watu imani kwao binafsi na yenye kuchochea jitihada, na kuwapa njozi inayofikika nawahakikisha moto utakaowaka Tanzania hautakuwa na mfano katika bara la Afrika. We just need a spark.. to light the fire...!

Mkuu Mkjj si alishafanya hivyo 2005 ndiyo maana Watanzania wakamuita "Kikwete ni mkombozi wetu" na wengine hata kudiriki kusema ni "Chaguo la Mungu" In my opinion I think it is too late to expect anything to spark or light the fire from this guy...I maybe wrong....but I doubt it.
 
Back
Top Bottom