WikiLeaks: Tanzania official fears for his life!

Tanzania, on Africa's east coast, is one of the poorest states in the world, formerly controlled in turn by Arab slavers, German colonists and the British.At the time of the radar deal, life expectancy was 45.
Tanzania was forced to apply for debt relief from the west and was heavily dependent on aid. It is ravaged by HIV/Aids and its GDP per head is just $723 (£465).
President Benjamin Mkapa, whose regime did the deal, was succeeded in 2004 by his political colleague Jakaya Kikwete.
Tanzania, which has no air force, bought the military air defence radar from BAE in 2001 for £28m.
It was claimed the Commander system, which was portable and festooned with anti-jamming devices, could also be used for civilian air traffic control.
The country borrowed the cost from Barclays, adding to its debt burden. Both the World Bank and the International Civil Aviation Organisation called the purchase unnecessary and overpriced.
In London, the then development secretary, Clare Short, temporarily blocked aid payments in protest. "It stank," she now says of the sale.
She urged an export licence be withheld, but was overruled by Tony Blair himself. Robin Cook, then foreign secretary, recorded bitterly in his diary that Dick Evans [of BAE] seemed to have "the key to the garden door of No 10 [Downing St]".
In January 2007 the Guardian disclosed that BAE had used an offshore front company, Red Diamond, to secretly pay £8.4m, 30% of the radar's ostensible price, into a Swiss account.
The account was controlled by Tanzanian middleman Sailesh Vithlani. His "consultancy" agreement was, it is alleged, formally signed off in London by Evans
.

Hii aibu ya kitaifa Mkapa na JK wake watajitokeza lini na kutuomba msamaha kwa ulafi wao?
 
Mambo ya wikileaks yanakiweka kiti cha Hoseah hatarini sasa.


 
More to come...nadhani kwa sasa viongozi matumbo joto maana hawajui what will come next. Unaweza kukuta zikamwagwa data ambazo zitawavua nguo viongozi wetu na unafiki wao uliokubuhu. Natamani ziwepo habari za wizi wa EPA, meremeta, deep green na juu ya Balali. Jamaa wanaweza kuthibitisha kuwa balali hajafa.....uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii, wikileaks mwaga mpunga kwenye kuku wengi please
 
Hosea aache unafiki na asitufanye Watanzania wapumbavu kwamba tunasahau kiraisi ivyo,wote tunakumbuka maneno ya Jk alipokuwa analizindua bunge mwaka 2005 juu ya kuwaacha viongozi Wastaafu akimlenga Mkapa kwamba waachwe wa pumzike kwa Amani hata kama waliiba nakuifilisi Nchi.

Juzi hapa kwenye Kampeni amemnadi Mramba kwenye Campaign kwamba ni Mtu safi wakati Takukuru inamshtaki Mahakamani.

Hivi huu Udokta wa Hoseah ni wa kupewa nin? Siamini kama Msomi kama yeye anaweza kuwa Unprofessional ivi kwakuongea pasipo kuamini anachokisema so anamdanganya nani maybe Jk but to we Great Thinkers he 'll never succeed at all na akae mkao wa Kula wakutidoliwa kama Boss wake atamshtukia anampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
 
Hosea hajui hata kusema uongo. Akajifunzie kwa wife wake akiona ameiva aje hapa, maana watu wanaamini uongozi huanzia nyumbani.
 
Hosea Vs JK

http://http://www.guardian.co.uk/world/2010/dec/19/wikileaks-cables-tanzania-bae-fears

President-Jakaya-Kikwete--007.jpg
 
“Nilichosema ni kwamba Rais hataki kuruhusu uchunguzi wa maofisa waandamizi wa serikali au mtu yeyote yule kufanywa kwa kuegemea katika minong’ono au ushahidi dhaifu, kwa sababu kwa kufanya hivyo, serikali inaweza kuwa katika hatari ya kulipa fidia kubwa kama watuhumiwa watashinda kesi mahakamani,” alidai Dk. Hoseah katika taarifa yake jana.

Hivi huyu Hosea anafikiri sisi mabwege kiasi hiki!!! Serikali italipa fidia gani kwa kumfanyia mtuhumiwa uchunguzi????!! Anasema uchunguzi hauwezi kufanyika kwa ushahidi dhaifu... kama wangepata ushahidi wa uhakika uchunguzi ungekuwa wa nini tena???!!! Uchunguzi unafanywa pale ushahidi unapokua si wa uhakika!!! Ushahidi wa uhakika ukipatika mtu anapelekwa mbele ya PILATO!!! Mtu anaweza kupelekwa mahakamni kabla ya uchunguzi kukamilika?????!!!! This gringo is nothing but chicken head!!!!! Hiyo ndo Serikali ya CCM! They are nothing but PLUNDERERS!!!
 
TAARIFA zilizovuja za mtandao wa Wikileaks, ambazo zilizotoka kwa Serikali ya Marekani, zimemgusa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), Dk. Edward Hoseah, na kwa haraka, amekanusha kuwa Rais Jakaya Kikwete amekuwa ni kikwazo cha utendaji wa taasisi hiyo, kama alivyonukuliwa humo.

Dk. Hoseah, anadai katika taarifa za mtandao huo zilizoripotiwa jana na gazeti la The Guardian la Uingereza kueleza kuwa Rais Kikwete alikuwa anakwamisha kuchunguzwa kwa vigogo wa serikali wanaotuhumiwa kwa vitendo vya rushwa, na pia madai kuwa anahofia maisha yake kama Mkuu wa Takukuru.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Dk. Hoseah anakiri kukutana na ofisa wa Marekani ofisini kwake Julai 2007, lakini katika mazungumzo yake, anakanusha kuwa hakuna mahali popote alipoeleza kuwa Rais Kikwete alikuwa hataki sheria ichukue mkondo wake katika kuwachunguza vigogo wanaotuhumiwa kwa rushwa.

“Nilichosema ni kwamba Rais hataki kuruhusu uchunguzi wa maofisa waandamizi wa serikali au mtu yeyote yule kufanywa kwa kuegemea katika minong’ono au ushahidi dhaifu, kwa sababu kwa kufanya hivyo, serikali inaweza kuwa katika hatari ya kulipa fidia kubwa kama watuhumiwa watashinda kesi mahakamani,” alidai Dk. Hoseah katika taarifa yake jana.

Kuhusu madai ya ‘hofu ya maisha yake’, alisema anakumbuka kuulizwa na ofisa huyo kama anahofia uhai wake au la, akiwa ni Mkuu wa Takukuru, na kwamba jibu lake lilikuwa rahisi, “ndio, wakati unaposhughulika na vigogo au matajiri, ni lazima uwe mwangalifu na tahadhari na maisha yako.”

“Lakini hakuna mahali popote nilipotamka kuwa nina mpango wa kukimbia nchi kwa sababu maisha yangu yalikuwa hatarini. Ni jambo la kushangaza kwa mara nyingine, Ofisa huyo wa Ubalozi wa Marekani amenikariri kinyume na ukweli na sijui nia yake hasa ilikuwa nini.”

Dk. Hoseah alisema kupokea vitisho ni sehemu ya kazi yake kwa sababu anawachunguza watu matajiri na wenye nguvu, lakini kwa kuwa kila kitu kinafanyika kulingana na sheria iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, “hakuna cha kuhofia sana kwa sababu kila kitu kiko katika sheria.”

Aliihakikishia jamii kwamba ingawa kazi yao ni ngumu, wataendelea na dhamira yao ya kupambana na rushwa katika ngazi zote kwa kushirikiana na wadau wote nchini.

“Tunaamini kwa pamoja tutashinda vita hii, lakini tukigawanyika, itakuwa kazi ngumu kufikia dhamira yetu.”


"sometime the only solution is execution for some" huyu mtu hata haoni aibu kukanusha na kujidanganyanganya? ningekuwa kikwete ningemsimamisha kazi mpaka atoe maelezo kamili. ile ni kashfa kubwa sana kwa kiongozi wa nchi, kusema Rais anazuia upelezi.... hata kwenye hayo maelezo bado hajakanusha hilo,
sasa utajuaje ushahidi ni dhahifu kama ujauchunguza vya kutosha...... nitamshangaa sana kikwete asipomdiscipline huyu mtu.
 
Tatizo wakuu wetu wanadhani bado tuko stone age (hata sio industrial age) wakati kumbe tuko information age ... kwakweli watakoma maana kujaribu kukanusha taarifa za wikilieaks ambazo hata marekani yenyewe inashindwa kukanusha ni kitu cha kitoto kabisa.
 
Maswali hapa ni kweli aliongea nao? na kama aliongea nao aliongea nao nini? je ni baada ya kushindwa kufanya kazi? tukirudi kwenye hali halisi je watuhumiwa wa ufisadi wanaozungumzwa kila siku wanakamatwa na kushitakiwa? kama hawashitakiwi je kwa nini?
baada ya mtu kujiuliza haya maswali mtu unarudi pale pele na kuona kwamba taarifa kutoka ubalozi ni sahihi.....hata hivyo nchi nyingi zimekanusha taarifa zilizovujishwa na wikileaks Tz haitakuwa ya kwanza lakini kukanusha haina maana kuwa si za kweli.....
 
Kama utakuwa umerejea zile post za wikileak, na kuzielewa vizuri, then utakubaliana nami Hosea amemuaibisha rais, kwa kusema kwamba ni kikwazo katika mapambano na rushwa, na pamoja kwamba amejitetea hakusema, ila kwa kueleweka hivyo na wamerakani ni kashfa tosha, and if he couldn't express himself clearly kwa huyo balozi, then he doesn't deserve to serve in this government. na ni sababu tosha kabisa kwa JK kumsimamisha kazi, kumuomba atoe maelezo au vielelezo zaidi, na pengine kumshtaki. we need some action here from our president. And if Mr. JK atakuwa silence on this issue, then we should all here at JF denounce him.
 
Mimi nampongeza Hosea kwa kusema ukweli, Hakika JK ni kikwazo katika mapambano ya ufisadi, Hebu wewe fikiria anaenda kwa Lowasa, Chenge, Rostam, na Mramba kuwapigia kampeni. Halafu Hosea ndo anenda kwa JK kuripoti taarifa za mafisadi.

Ni kikwazo, tena kikubwa tu
 
hayo majungu sasa kwani Hoseah kakosea kusema ukweli??
na kama kweli ni ni kikwazo? hv mtu mwenyewe unayemsema yupo nchini kweli??
TULISEMA URAIS wa kubaka hauna Amani na yanatokea sasa bado mengi yatakuja!
 
Hosea ndio mwanaume wa kweli na alikua anahaja ya kupinga kuhusu hilo swala,na jk awezi kumshughulikia hosea kwa sababu ataonekana ni mtu wa visasi ukweli upo wazi kua jk ndio kikwazo cha mafisadi(anawalinda)sasa wilieaks ndio hao wanakuja na mada moto moto.
 
to make things better, we need local wikileaks as well

Acid,
Local wikileaks ilikuwepo enzi zileeeeee ikiitwa " MIKINGAMO" SIJUI iliishia wapi na kama ilikuwa na tija yeyote...
Whistleblowing ni kitu kizuri kama itakuwa handled responsibly.Vinginevyo ni kiwanda cha majungu, umbeya na uongo.
 
Kikwete ni kichwa cha mwendawazimu, asie na maamuzi acha dogo Hosea na uozo wake ajiongezee japo credits maana anajua JK hawezi m-hold accountable. Kama angeweza angelishaondoka siku nyingi sana PCCB.

Na wewe mwandishi ulichoandika ni NYODO zako kama jina lako juu ya upenzi wako kwa Kikwete ukiona hakutendewa haki kwa kuambiwa ukweli.
 
Back
Top Bottom