Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,815
- 4,565
Katika ulimwengu wetu wa leo matumizi ya Intanet yamekuwa ni miongoni mwa hitaji la msingi kwa kila mtu.
Katika mazingira mbalimbali tumejikuta tukiwa katika maeneo ya umma ambapo kuna wifi za bure na kwa namna fulani tumekuwa tukifurahia na kuunganisha vifaa vyetu kwa na mitandao hiyo. Maeneo ya umma hapa yanaweza kuwa vituo vya basi, super market n.k.
Je, jambo hili linafaa?
Wataalamu wa masuala ya mitandao wameonya na kuweka bayana kuwa kujiunga wifi za bure kunaweza sababisha data zetu binafsi kuwa katika hatari ya kuibiwa au kushambuliwa.
- Miongoni mwa hatari kuu za Wi-Fi za umma ni kuvijisha data binafsi za mlengwa au kifaa chako kuambukizwa virusi (Melware) hatarishi zinavyoweza kuharibu data zako binafsi.
Katika suala la kuvujishwa kwa data zako inatokea pale ambapo unajiunga wifi fulani wakati data zako binafsi zilizopo kwenye kifaa chako zinakuwa hazijalindwa vyema. Hivyo, wadukuzi wanaweza kutumia mwanya huo kuingilia kifaa chako kisha kuiba data zako.
Katika hali ya pili ya kuambukizwa virusi kwenye kifaa chako, wahalifu wa mtandao wanaweza kutumia mwanya wako wa kujiunga wifi kukutumia link fulani na kukuhadaa upakue data zenye virusi hivyo kuharibu data zako.
Nini chakufanya ili kuwa salama unapotumia Wi-Fi ya umma
1. Tumia VPN
2. Zima Bluetooth na file transfer ili kuepusha kuhamisha taarifa zako
3. Usifungue au kutuma data zako nyeti uwapo maeneo hayo
4. Tumia antivirus itayokusaidia kupambana na hatari za kuibiwa data zako
Katika andiko lijalo nitafafnua kwa undani namna ya kutumia mbinu hizo kujilinda
Katika mazingira mbalimbali tumejikuta tukiwa katika maeneo ya umma ambapo kuna wifi za bure na kwa namna fulani tumekuwa tukifurahia na kuunganisha vifaa vyetu kwa na mitandao hiyo. Maeneo ya umma hapa yanaweza kuwa vituo vya basi, super market n.k.
Je, jambo hili linafaa?
Wataalamu wa masuala ya mitandao wameonya na kuweka bayana kuwa kujiunga wifi za bure kunaweza sababisha data zetu binafsi kuwa katika hatari ya kuibiwa au kushambuliwa.
- Miongoni mwa hatari kuu za Wi-Fi za umma ni kuvijisha data binafsi za mlengwa au kifaa chako kuambukizwa virusi (Melware) hatarishi zinavyoweza kuharibu data zako binafsi.
Katika suala la kuvujishwa kwa data zako inatokea pale ambapo unajiunga wifi fulani wakati data zako binafsi zilizopo kwenye kifaa chako zinakuwa hazijalindwa vyema. Hivyo, wadukuzi wanaweza kutumia mwanya huo kuingilia kifaa chako kisha kuiba data zako.
Katika hali ya pili ya kuambukizwa virusi kwenye kifaa chako, wahalifu wa mtandao wanaweza kutumia mwanya wako wa kujiunga wifi kukutumia link fulani na kukuhadaa upakue data zenye virusi hivyo kuharibu data zako.
Nini chakufanya ili kuwa salama unapotumia Wi-Fi ya umma
1. Tumia VPN
2. Zima Bluetooth na file transfer ili kuepusha kuhamisha taarifa zako
3. Usifungue au kutuma data zako nyeti uwapo maeneo hayo
4. Tumia antivirus itayokusaidia kupambana na hatari za kuibiwa data zako
Katika andiko lijalo nitafafnua kwa undani namna ya kutumia mbinu hizo kujilinda