Why TTCL is not the leading Cellular and internet Operator?

Why TTCL is not the leading Cellular and internet Operator?

TTCL ilikuwa na mali nyingi sana wakati inabinafsishwa. Ni pamoja na nyumba za wafanyakazi zilizoko kwenye strategic areas. Baada ya ubinafsishaji nyumba hizo ziliuzwa kama njugu kwa bei za kutupwa kwa kupitia kampuni iliyokuwa inaongozwa na Peter Maro wakati ule ya Simu 2000. Nyingi ya nyumba hizi wamejiuzia viongozi wa serikali. TTCL ilikuwa na shares katika jengo la International House wakati ule lilipojengwa. Share hizi sasa hivi haziisaidii TTCL tena. Sina hakika kama zimehamishiwa Hazina au zimechukuliwa na mafisadi. TTCL ina mali zake ambazo wala haziwasaidii wao ila watu wengine.
 
MSI(MOBILE SYSTEM INTERNATIONAL AKA MOHAMED SAID IBRAHIM).Ni kampuni ambayo ni mali ya mo ibrahimu aliyewalaghai serikali wakakubali kuuuza ttcl kwa nusu bei na baadaye akakataa kulipa na pesa yote aliyonunua ttcl akarudishiwa na akaanzisha Celtel badala ya Celnet ambayo ilikuwa tayari imesajiliwa na huku mitambo ya gsm ikiwa bandalini kilichofanyika ni kumuuzia mobitel(buzz) na TTCL kuwa na hisa Mobitel )(tigo) ambazo mpaka sasa haijulikani ziko wapi.

Mo anahusika sana kuiangamiza TTCL na yeye ati anajifanya ndiye bingwa wa uadilifu ati anawapa zawadi viongozi wa afrika waliostafu wakiwa waadilifu. Sumaye, Warioba na Salimu wanajua vizuri habari yote na aliyetolewa kafara na kuachishwa uongozi wa TTCL ni Adolar mapunda natumaini ana mtandao na ni mwanajamii anaweza kueleza mengi. Huu ni wakati wa ukweli na uwazi wafanyakazi wa TTCL amkeni muikomboe ttcl yenu.
 
MSI(MOBILE SYSTEM INTERNATIONAL AKA MOHAMED SAID IBRAHIM).Ni kampuni ambayo ni mali ya mo ibrahimu aliyewalaghai serikali wakakubali kuuuza ttcl kwa nusu bei na baadaye akakataa kulipa na pesa yote aliyonunua ttcl akarudishiwa na akaanzisha Celtel badala ya Celnet ambayo ilikuwa tayari imesajiliwa na huku mitambo ya gsm ikiwa bandalini kilichofanyika ni kumuuzia mobitel(buzz) na TTCL kuwa na hisa Mobitel )(tigo) ambazo mpaka sasa haijulikani ziko wapi.Mo anahusika sana kuiangamiza TTCL na yeye ati anajifanya ndiye bingwa wa uadilifu ati anawapa zawadi viongozi wa afrika waliostafu wakiwa waadilifu.Sumaye,Walioba na salimu wanajua vizuri habari yote na aliyetolewa kafara na kuachishwa uongozi wa TTCL ni Adolar mapunda natumaini ana mtandao na ni mwanajamii anaweza kueleza mengi.Huu ni wakati wa ukweli na uwazi wafanyakazi wa TTCL amkeni muikomboe ttcl yenu.
Huyu huyu Mo Ibrahim???
 
labda tutofautishe mambo haya mawili: kutokuwa competent na kuhongwa na wamiliki wa kampuni za simu za binafsi

wireless modem ya ttcl inauzwa 75000.

bundle ya 1gb inauzwa 70000

wakubwa wa ttcl wanayajua haya. na wanajua bei za modems na bundles zilivyo cheap kwenye private firms, ila wanafanya makusudi ili kuuwa shirika

nchi hii ni ya rushwa jamani au mumesahau?

Please dont mislead people in this forum.

1. Wireless modem ni TSH 50000/=
TTCL has best rates for internet services. Check out this
2. 2Gb bundle for only 30000/= Broadband adsl
3. 4gb bundle for only 60000/=

Lakini from the orignal thread, matatizo ya TTCL yameletwa na serikali yenyewe na sio management wala wafanyakazi. Serikali imefanya utapeli na MSI-Detecom kwa kuuza hisa 35 kwa dola mil 65 badala ya 120.

Ni serikali iliyodhoofisha juhudi za kuanzisha kampuni ya mobile ya TTCL iliyokuwa na jina la Celnet na mtaji ukatumika kuanzisha Celtel wakitumia rasilmali za TTCL.

Ni serikali iliyoleta management ya kigeni Saskatel ya Canada ambayo iliishia kuchota fedha za wazalendo na kuondoka bila kuleta ufanisi hata kidogo.

Haya yote ni matokeo ya viongozi wasiokuwa wazalendo wenye ubnafsi na wanaotaka TTCL ife ili makampuni ambayo wao wana hisa kubwa kubwa yashamili.

Someni vizuri hiyo habari kamili.
Wakati Mobitel inaingia TTCL ilikuwa na share mle kama asilimia 40. Baadaye serikali ikazibeba. Walichofanya na hizo hisa hakijulikani, ila leo serikali haina hisa Tigo

Mwaka 1999 TTCL iliamua kuanzisha mradi wake wa simu za Mkononi (kwa fedha zake), wakati huo ilikuwepo Tigo na Tritel peke yake. Serikali kupitia TCRA wakauzuia mradi huo kwa madai kuwa kampuni iko kwenye mchakato wa ubinafsishaji - Mwaka 2000 Vodacom wakaingia.

Mwaka 2001 akaingia Mbia kwa madai ya kununua asilimia 35 kwa Dola million 120. Akaishia kupewa hizo hizo kwa dola million 65.
Mbia huyo akatumia leseni ya biashara za simu za mikononi ya TTCL (mradi ulisimamishwa haukufutwa) kuanzisha celtel Tanzania, TTCL ikawa imenyang'anywa rasmi uwezo wa kufanya biashara za simu za mikononi, si kwa sababu ya uwezo wa watendaji, sababu ya uamzi wa mezani (serikali)

Celtel international (aliyekuwa na hisa ndani ya TTCL) ndo akaanzisha Celtel Tanzania ikiwa kama subsidiary company ya TTCL
Baadaye TTCL ikanyang'anywa shea zote ndani ya Celtel, zikahamishiwa hazina, TTCL ikabaki haina shea na haina biashara ya simu za mkononi na ikazuiwa kuanzisha ya kwake kwa sababu masharti ya leseni hayakuiruhusu kuanzisha

Mwaka 2005, serikali ikaondoa masharti ya leseni, ila mbia mwingine wa serikali; Celtel international (ambaye sasa ni mshindani wa TTCL - lakini akiwa na share ndani ya TTCL) akakataa TTCL isijiingize kwenye biashara ya simu za mikononi.

Wafanyakazi wazalendo ndani ya TTCL wakaamua kuingiza biashara hizo kwa mgongo wa nyuma, ndivyo ilivyoingia TTCL Mobile na Technolojia ya CDMA. Hawa wazalendo waliidanganya bodi kuwa wanaingiza CDMA kufanya fixed wireless (WLL) ila kwa siri wakanunua full mobile solution. Bodi ingejua isingiruhusu asilani.

Hata hivyo baadaye bodi iligundua kuwa kilichoingia ni Mobile si WLL. Ikaamua kuzuia uwekezaji zaidi katika mradi huo, hivyo TTCL mobile ikashindwa kujitanua kama ilivyotarajiwa.

Mwaka 2007, serikali ikaleta menejinti nyingine ya wazungu, kutoka Canada. Hawa walivyokuja wakaiambia serikali tiba ya TTCL ni kuuendeleza ule mradi wa TTCL mobile ulioanzishwa na wazalendo. Serikali ikakubali, lakini ikishirikiana na Celtel international (wakati huo Zain) wakazuia TTCL kukopa kwa ajili ya kuuendeleza mradi wa TTCL Mobile - Kwa hiyo mradi ukabaki bila kuendelezwa.

Mwaka 2009, baada ya kusuguana sana na serikali kuhusu kuendeleza mradi huo (serikali na Zain wakikataa), wa Canada waliamua kujitoa rasmi wakaondoka mwezi July 2009.

Toka hapo ni dana dana tu. Serikali wanashangaa kwa nini TTCL haifi? Wao wanataka ife, wauze mbao! Menejimenti ya wazalendo na wafanyakazi wao, wanapambana kulinda ajira zao. Ila serikali kwa kushirikiana na Zain (sasa airtel) wanataka hiyo kampuni ife, waipeleke kwa mufilisi ili viongozi wa serikali wajichotee masalia (TTCL inazo mali nyingi sana - Ikiwemo majengo, viwanja katika maeneo muhimu katika miji yote ya Tanzania, n.k.)

Ni dharau kwa watanzania kuwasema vibaya wafanyakazi wa TTCL, ni kampuni ngapi zingeweza kuhimili hujuma kutoka kwa wamiliki wake? Ni wafanyakazi pekee wanojua kuwa wanaohujumiwa pale ni watanzani, si wafanyakazi wa TTCL!! Watanzania ndo wenye mali serikali ni msimamizi tu.

Serikali dhaifu inashirikiana na matapeli wa nje kuhakikisha hii kampuni itakufa. TTCL ikifa, atakayenufaika ni watendaji wa serikali waliokaa mkao wa kula, wakisubiri kujichotea ma properties yatakayotelekezwa. Atakayenufaika ni Makampuni ya nje yatakayojichukulia biashara kubwa ambazo bado TTCL inazo.

TTCL ikifa atakayeumia ni mtanzania atakayekosa kazi. Mapato ya serikali yatashuka kwani TTCL pamoja na hali yake bado ni mlipa kodi mkubwa (waulize TRA watakuambia). TTCL hawafanyi lolote kukwepa kodi. Kodi zote za serikali wanalipa bila matatizo (bado wanalipa kodi kubwa kuliko makampuni mengi ya simu yanayokwepa kulipa kodi). Kushuka kwa mapato ya serikali kutawaumiza watanzania, si wawekezaji kutoka nje.

Ni vizuri tuujue ukweli, kwani ukweli utatuweka huru
 
Nilishawahi kufanya kazi TTCL zaidi ya miaka kumi iliyopita chini ya utawala wa Mapunda. Kwa wakati huo tuliamini kuwa ufumbuzi wa matatizo yetu ulikuwa chini yetu wenyewe.

Nimekuwa nikiongea na wafanyakazi wa TTCL wa sasa, wao wanaamini kuwa chimbuko la matatizo ni serikali kupendelea makampuni binafsi. Nikiwauliza ni upendeleo gani? Wanashindwa kujibu. Kimsingi TTCL wanaogoja kivuli chao wenyewe.

Naamini tatizo kubwa ni la uongozi, mzee Said na wenzie wameshindwa kuiongoza TTCL.
 
simple and straight forward......conflict of interest...TTCL ikiendelea manake kampuni za wakubwa zitapata hasara sababu wamewekeza huko....hivyo mwendo ni huu mpaka milele
 
Thanks Shingo.
Tatizo kubwa ni conflict of interest. Mwl Nyerere alionana mbali sana ndo maana alianzisha/fanikisha Azimio la Arusha.

Picha hii inawakilisha mambo mengi sana ndani ya serikali yetu. Mfano EPA, ndege ya rais na rada.
 
Nilishawahi kufanya kazi TTCL zaidi ya miaka kumi iliyopita chini ya utawala wa Mapunda. Kwa wakati huo tuliamini kuwa ufumbuzi wa matatizo yetu ulikuwa chini yetu wenyewe.

Naamini tatizo kubwa ni la uongozi, mzee Said na wenzie wameshindwa kuiongoza TTCL.

Mkuu afadhali nimepata mtu mwenye inside information.., kulingana na aliyosema Shingo hapo juu, wewe unadhani ni hatua gani ingebidi ichukuliwe ili kunusuru hili janga? au inatakiwa wafanye nini sasa ili watoke kwenye hili janga?
 
Azimio la Arusha ni gumu kutekeleza lakini naanza na mie kuliona kama solution. Watu kwa ujumla ni GREEDY, inabidi wananchi tuwe aead of time kujiandaa kuwabana wote wataotokezea kujimegea fungu la kodi yetu tunayotokea jasho la damu.
 
Huyu huyu Mo Ibrahim???

Ndio huyo huyo msudani unayemfahamu na Omary Issa ndio alikuwa mwenyekiti wa bodi ya TTCL ambaye sasa hivi kaingia na kampuni nyingine(ICL) ya kuombea misaada serikali na TRA na Police Omary Issa kaingia tayari hii ni baada ya kuiuza celtel

Watanzania wataliwa mpaka lini?
 
Mkuu afadhali nimepata mtu mwenye inside information.., kulingana na aliyosema Shingo hapo juu, wewe unadhani ni hatua gani ingebidi ichukuliwe ili kunusuru hili janga? au inatakiwa wafanye nini sasa ili watoke kwenye hili janga?

Biashara ya mobile services ni matangazo, ubunifu wa kutoa product mpya kila mara pamoja na kumsikiliza mteja - vyote hivi havipatikani TTCL. Hivi karibuni Kampuni ninayofanyia kazi ilipatwa na matatizo ya FIBRE kati ya point A na B ambayo imekodi TTCL. Tuliripoti tatizo TTCL usiku huohuo na kufuatilia kila baada ya nusu saa lakini ilibidi tutume gari asubuhi yake ili waje kumaliza tatizo, hii haikubaliki na hivi sasa tumeshaanza kujenga fibre network yetu wenyewe to get rid of TTCL poor service.

Unaweza ukatembea DSM mzima si ajabu usilione hata bango moja la matangazo la TTCL.

Nadhani shirika lingepewa viongozi wenye VISION na wanaojali maslahi ya taifa kama Mzee Ole Kambainei lingepaa.
 
Biashara ya mobile services ni matangazo, ubunifu wa kutoa product mpya kila mara pamoja na kumsikiliza mteja - vyote hivi havipatikani TTCL. Hivi karibuni Kampuni ninayofanyia kazi ilipatwa na matatizo ya FIBRE kati ya point A na B ambayo imekodi TTCL. Tuliripoti tatizo TTCL usiku huohuo na kufuatilia kila baada ya nusu saa lakini ilibidi tutume gari asubuhi yake ili waje kumaliza tatizo, hii haikubaliki na hivi sasa tumeshaanza kujenga fibre network yetu wenyewe to get rid of TTCL poor service.

Unaweza ukatembea DSM mzima si ajabu usilione hata bango moja la matangazo la TTCL.

Nadhani shirika lingepewa viongozi wenye VISION na wanaojali maslahi ya taifa kama Mzee Ole Kambainei lingepaa.
Mkuu ukimsoma Kishongo, sio kwamba viongozi hawataki kufanya hivyo..., ni Kwamba Mkono kutoka nje unawazuia kufanya hivyo kwa manufaa yao wenyewe.... true huenda kuna kauzembe katika taasisi zote za serikali..., lakini from Kishongo's Post hii imenifanya nione hata kama ukiwa the best CEO in the world hii taasisi huiwezi sababu hapo wanataka " yes man " Kwahiyo hapa our enemy sio TTCL ni people above / outside TTCL na ndio hao hao watu ambao wanakula nchi yetu katika kila industry madini, kilimo etc
 
Mkuu ukimsoma Kishongo, sio kwamba viongozi hawataki kufanya hivyo..., ni Kwamba Mkono kutoka nje unawazuia kufanya hivyo kwa manufaa yao wenyewe.... true huenda kuna kauzembe katika taasisi zote za serikali..., lakini from Kishongo's Post hii imenifanya nione hata kama ukiwa the best CEO in the world hii taasisi huiwezi sababu hapo wanataka " yes man " Kwahiyo hapa our enemy sio TTCL ni people above / outside TTCL na ndio hao hao watu ambao wanakula nchi yetu katika kila industry madini, kilimo etc
Sounds like CCM have to go!
 
Very true, Could not put it any better myself.
They have failed us, and they must leave for somebody else. I think we better have Chadema now and see what they can do. 50 years are enought to test them.....and they have failed
 
Executives are not competent enough to to make the strategic plans for new developments. They are just idiot - business as usual.

TCCL could have been very successfull PLC in the country.



Blue Balaa, Point of correction,it's NOT TCCL it IS TTCL=Tanzania Telecommunications Company Limited-TTCL

Thanx for this vital thread to be discussed by Great Thinkers. First of all I do not concur with your comments here!
Let me say this concerning TTCL,The Tanzania Telecommunications Co. Limited being one of the giant Telecommunication companies in Tanzania despite being disregarded by the Government.

What is happening in TTCL now has no difference to what is happening in other Parastatol Organizations in Tanzania. Look at TANESCO, look at ATCL, look at TRL, look at NIC, etc etc. There is no difference at all. Every Organization is in a very bad shape financially, economically and operationally. But who is behind all theme mess up in our Organizations? It is the GOVERNMENT; I am saying this with big letters to insist my point.FOREIGNERS coming in the name of INVESTORS in collaboration with Greedy and Corrupt government officials are KILLING OUR ORGANISATIONS,TTCL included.

We can remember very well back in year 1995 when the Government under CCM introduced the so famous Policy of PRIVATISATION in Tanzania. The policy was implemented with a supersonic speed whereby all Parastatols were privatized to FOREIGNERS like nobody's business. Initially the Policy stated that only those LOSS making Organizations were to go private.

Besides the gear was changed or engaged to another direction. The Policy was directed to PROFIT making corporations like NBC Bank separated to NMB/NBC, TTCL,TBL, CEMENT Factories like Tanga Cement,Twiga Cement etc,etc.

Now,back to TTCL. It was in 2001 when the so called STRATEGIC INVESTORS going by the name M/S MSI/DETECON took over TTCL. They took over TTCL by that time making a huge profit CL turnover was 90Billion Tshs. Per annum. The MSI/DETECON agreed to pay 120m/-USD equivalent to 120Billion. Tshs , by that time (1 USD =1000 Tshs 120B/-to acquire 35% shares in TTCL.They first paid half amount at 60B/-Tshs before entering TTCL offices and promised to pay the other half after entering TTCL offices.That was a cheat to the government. Immediately after they grabbed office they just started a dilly dallying of payments. Do you what they last paid? It was only 4.5/- USD equivalent to 4.5 B/-Tshs.That was the end of the story. Instead of paying 120B/-Tshs they ended paying a total of 64.5B/- I am not sure if by that Time the ICC was not there!

After paying the 64.5 Billion T.shillings they assured the Government that all the monie paid for shall be invested in expanding TTCL network i.e TTCL infrastructure to increase the customers Base. In year 2001 the TTCL customer stood at 250,000 for both Data and Voice. The investor promised to increase the same to 805,000. Believe me, by the time MSI/DETECON pulls out of TTCL the CUSTOMER BASE was staggering at 160,000 OR less!!!!

Everybody knows what really happened. These guys were conmen! Instead of expanding TTCL network and Customer base as they agreed as per MOU between Government and MSI/DETECON, they just started a MOBILE company within TTCL going by the name of CELTEL by capitalizing on TTCL resources! Initially they said the same company CELTEL shall be owned by TTCL 100%. But as time goes on it was revealed that CELTEL was owned by MSI/DETECON 100%.It was then baptized with a new name as CELTEL INTERNATIONAL , after few years it was changed to ZAIN and now AIRTEL. It is known that Zain was owned by Government at 40% while the other 60% owned by Celtel International. It is very interesting to note that during the sale of ZAIN share by 100% to AIRTEL at a tune of almost 10Billion USD (NOT MADAFU)theTanzania Government was not involved/informed despite the 40% share they own in Zain. NO BODY QUESTIONED THIS RUBBISH, NEITHER IN OUR MJENGO AT IDODOMYA NOR IN THE ICC COURT!!!!!!!!!REASONS? Best known to JK and his CABINET!!

The TTCL story doesn't end here,it still continues. From reliable sources it is said that the same CELTEL/ZAIN owners in collaboration with Government officials they put a condition that TTCL NOT BE ALLOWED GO MOBILE as they,TTCL shall paralyze other MOBILE OPERATORS in Tanzania especially ZAIN. You may notice that in ZAIN the following big heads have a good number of shares: SALIM AHMED SALIM, ROSTAM AZIZI, JOSEPH SINDE WARIOBA,MO IBRAHIM,EDWARD LOWASSA and JK !

As that is not enough, The Tanzania government owes TTCL about 7 billion Tshs. BUT the Government is reluctant to settle the debt!!Reasons??The government coffers have no monie!!???But they are ready to pay the Ghost RICHMONDULI alias DOWANS Company a total of 94/= billion Tshs.


The TTCL story still continues……………………

I will come later,by now let me say guten nacht!
 
Unataka kubisha kwamba viongozi siyo competent? Kama ni competent basi wafanye changes kwenye organization.
Pole sana unazungumza mambo bila utafiti na hutajua ukweli! Nakupa pole zaidi. Tukiwa na watanzania wakurupukajikama wewe hatufiki mbali. Fanya utafiti kidogo na kama umefanya ukaja na conclusion hii basi umepata zero kwenye project yako!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom