Why TTCL is not the leading Cellular and internet Operator?

MSI(MOBILE SYSTEM INTERNATIONAL AKA MOHAMED SAID IBRAHIM).Ni kampuni ambayo ni mali ya mo ibrahimu aliyewalaghai serikali wakakubali kuuuza ttcl kwa nusu bei na baadaye akakataa kulipa na pesa yote aliyonunua ttcl akarudishiwa na akaanzisha Celtel badala ya Celnet ambayo ilikuwa tayari imesajiliwa na huku mitambo ya gsm ikiwa bandalini kilichofanyika ni kumuuzia mobitel(buzz) na TTCL kuwa na hisa Mobitel )(tigo) ambazo mpaka sasa haijulikani ziko wapi.Mo anahusika sana kuiangamiza TTCL na yeye ati anajifanya ndiye bingwa wa uadilifu ati anawapa zawadi viongozi wa afrika waliostafu wakiwa waadilifu.Sumaye,Walioba na salimu wanajua vizuri habari yote na aliyetolewa kafara na kuachishwa uongozi wa TTCL ni Adolar mapunda natumaini ana mtandao na ni mwanajamii anaweza kueleza mengi.Huu ni wakati wa ukweli na uwazi wafanyakazi wa TTCL amkeni muikomboe ttcl yenu.


Ndigu zetu, hivi kumbe habari zote zinafahamika na sie tumekaa kimya tuu.

it's good kwamba zinaanza kujulikana..... Tunaomba akina Said Kubenea na waandishi wengine wenye uzalendo wazifanyie kazi zianze kuunguruma.
 
The TTCL story doesn’t end here,it still continues. From reliable sources it is said that the same CELTEL/ZAIN owners in collaboration with Government officials they put a condition that TTCL NOT BE ALLOWED GO MOBILE as they,TTCL shall paralyze other MOBILE OPERATORS in Tanzania especially ZAIN. You may notice that in ZAIN the following big heads have a good number of shares: SALIM AHMED SALIM, ROSTAM AZIZI, JOSEPH SINDE WARIOBA,MO IBRAHIM,EDWARD LOWASSA and JK !
As that is not enough, The Tanzania government owes TTCL about 7 billion Tshs. BUT the Government is reluctant to settle the debt!!Reasons??The government coffers have no monie!!???But they are ready to pay the Ghost RICHMONDULI alias DOWANS Company a total of 94/= billion Tshs.

Sheeewww!!
Kumbe sie wajinga ndio tuliwao!! Wakati wakubwa wanakula nchi .. sisi makelele tu.
Haya mambo sasa yako wazi ... ina maana hawa akina JK hawaoni hata aibu wajiuzulu? wanasubiri nini?
 
Wanandugu,

Nashukuru kwa mkubwa hapo juu kwa kutoa ufafanuzi wa undani, mimi nilibahatika kufanya kazi pale kwa muda mfupi,na sasa nipo kwenye upande mwingine wa dunia, niligundua mambo mengi sana.

Kwanza tuwe wakweli, suala la utaalamu upo wa kutosha, na kuna watu wana vichwa vikali huwezi kuamini, na ukitaka kuamini hilo, strategies nyingi zinabuniwa pale, lakini kutokana na uchelewesho wa utekelezaji na ule mwimbo wa ukosefu wa fedha, utashangaa zimeibuka kwa makampuni mengine binafsi (si ajabu kwa sababu kwenye bodi yao Zain wapo ndani).

Kuna miradi ambayo najua ilipangwa pale, kwa ajili ya masuala ya kitaifa, nimeshangaa plan zile zile wamepewa makampuni binafsi (na wanazitekeleza), utajiuliza zimetoka wapi?. sasa hawa tutawaita ma ' Idiot' kweli?. Idiot ataigwa mikakati na ufundi wake?.Sishangai sana kwa sababu ya mchanganyiko wa bodi na utaratibu wa kupeleka 'strategies' wizarani kwa approval...., hapo sasa!.

Hivi hamjiulizi kuwa hao tunaodhani wanaakili (WAZUNGU) waliishapewa TTCL kuiongoza, wakaamua kuingia mitini, wakijua kuwa itakuja kuwafia mbeleni baada ya kukosa ushirikiano toka serikalini?

Suala kubwa kwa TTCL ni uwezeshwaji, haya makampuni tunayoyasifia, jiulize yamepata mikopo mara ngapi toka yameingia kwa ajili ya new investments (mengine yalikuwa yanakufa kabisa, mikopo ikayasaidia) na shughuli za kimasoko. Lakini nilishangaa kuwa TTCL haipewa nafasi hata mara moja ya kupata mkopo, tena hawataki 'fadhira' za bure, ni mkopo lakini tumejiuliza kwanini hawapewi?. kwa kipindi chote hicho wamekuwa wakijiendesha kwa pesa zao wenyewe, bila msaada.

Leo hata ukiwambia TTCL wajitangaze, hawana uwezo wa kutosha kumudu soko bila kuwekeza kuongeza mtandao, kwa kudunduliza billi za kila mwezi hawawezi kwenda popote, na hata ukimpeleka MALAIKA aongoze hapo, bila uwezeshwaji atakimbia tu, kila kitu atakiona cha moto.Kuna fikra potofu kuwa TTCL ipo kila sehemu, si kweli, haijafika sehemu nyingi, na hata kule walipo utakuwa ina uwezo wa kutoa huduma kwa wateja wachache tu. Pia dhana ya kuchanganya kuwa sehemu yeyete waliopo mobile itafanya kazi si kweli, inahitaji uwekezaji mpya kabisa kwani ni technologia ambazo haziingiliani na fixed lines.

Wakati umefika watanzania kuamka na kuacha uvivu wa kufikiri, tujaribu kuyachunguza mambo kwa undani. Makampuni ya umma yenye roho ngumu kama TTCL pengine yanatakiwa YAFE, ndiyo maana hayana support, pengine kama alivyosema mchangiaji hapo juu kuwa "hata kile kidogo walichonacho kinamendewa"


Uzalendo Kwanza,
 
Hi Great thinkers,

I am back again as I promised.

As I have already said ealier and I say it again,the KILLERS of TTCL is the CCM government under leadership of KIWETE and his henchmen. Most of government leaders are either SHARE HOLDERS or CHAIRMAN/CHAIRPERSON/BOARD MEMBERS in Foreign MOBILE operators.We have live examples:
  1. Pius Msekwa,the former Speaker of Tanzania Parliament was Chairman Board of Directors Vodacom Tanzania.
  2. Salim Ahmed Salim,the former AU Secretary General,PM and Minister is ZAIN/AIRTEL shareholder and Board Member.
  3. Joseph Sinde Warioba,the former PM and Minister is ZAIN/AIRTEL shareholder and Board Member.
  4. Rostam Aziz,the MP for Igunga Constituency is Vodacom shareholder and Board Member.
  5. Basil Pesambil Mramba is Board member and shareholder in Zain/Airtel.
This is just a list of some few Government leaders who are fully engaged in Mobile operators business and therefore making all possible means to make SURE that TTCL is no longer there.
About 2 years ago 2009/10 a secret letter from ZAIN to the Deputy Minister(by then Doctor Maua Daftari) was revealed at the Ministry of Science and Technlogy headquarters STATING A STRATEGIC PLAN TO STOP TTCL FROM OPERATING AND EXPAND THEIR TTCL MOBILE PHONES as it will adversely affect other Mobile operators!

The strategic plan was to make sure that TTCL MOBILE network be controlled and limited! In this plan TCRA wa involved in such a way that TTCL can not expand its Mobile phones without the TCRA authority. TTCL was allowed under special LICENCE to expand its network ONLY by 100,000 customers per year! While other Mobile operators are talking of a Customer base of 4m to 6m like Vodacom TTCL have to expand by 100,000 per year. That means, by just simple arithmetic TTCL can achieve a 1m customer base after 10 years!!!.

This can be proved by poor coverage of TTCL MOBILE. There is only one BTS(a Microwave system which connect mobile customers) in most Regions or Districts to cater for TTCL mobile customers. I know one region where there is ONLY ONE BTS!!!!!! Other companies like Vodacom,Tigo,Zain/Airtel have 30-50 BTS systems approximately in the same region.

The cost of 1 BTS ranges between 200-300m Tshs. which TTCL can afford.

I shall come later on more stories about TTCL.
Please kama inawezekana tupate scanned copy ya hiyo barua!
Anyway CCM must go!
 
Ndugu Ndibalema,

Ukisoma post zangu huko nyuma nilisema sababu ya TTCL kuingiza CDMA badala ya GSM. Watendaji wazalendo ndani ya TTCL walielewa limitations za CDMA na faida za GSM. Isingewezekana kuingiza GSM kwani board ilikataa TTCL kufanya biashara ya simu za mkononi kwa sababu biashara hiyo hiyo ilikuwa ikifanywa na kampuni dada (wakati huo) Celtel. Kwa hiyo wataalam hao hata hiyo CDMA waliingiza kwa mgongo wa kuingiza Fixed Wireless na si Mobile.

Baada ya board kugundua kuwa kilichoingizwa ni Mobile solution, board ikazuia fedha zaidi kuingizwa huko. Viongozi wapya walipokuja (management contract) kutoka Canada, waliona kuwa solution ya wazalendo ilikuwa inafaa. Wakaitaka board iruhusu uwekezaji kwenye eneo hilo, board na serikali wakazuia fedha. Wa Canada wakaamua kujitoa.

Kwa hiyo Matendo ya Board ya TTCL pamoja na SERIKALI yanazuia kiongozi yeyote anayeendesha kampuni hii kufanikiwa. Hakuna kampuni inayoendeshwa bila uwekezaji. Umeshauliza Tigo, Zain, Vodacom wamewekeza kiasi gani hadi wakafikia hapo walipo? Unafikiri hizo fedha walizowekeza walitoa wapi? Walikopa kwenye mabenki hayo hayo ambayo yalikuwa tayari kuikopesha TTCL iwekeze.

TTCL inazuiwa kuwekeza. Wanaoizuia kuwekeza ni Board yake (imbayo ndo uongozi wa TTCL) na Serikali. Board na serikali wameshindwa kuweka uongozi wa kampuni wa kudumu. Kampuni inaendeshwa na viongozi wa ku-act ambao hawana mamlaka kamili ya kiutendaji. Na hili utawalaumu wafanyakazi??

Be fair
CCM must go and the whole top TTCL leadership must follow!
 
Wanandugu,

Nashukuru kwa mkubwa hapo juu kwa kutoa ufafanuzi wa undani, mimi nilibahatika kufanya kazi pale kwa muda mfupi,na sasa nipo kwenye upande mwingine wa dunia, niligundua mambo mengi sana.

Kwanza tuwe wakweli, suala la utaalamu upo wa kutosha, na kuna watu wana vichwa vikali huwezi kuamini, na ukitaka kuamini hilo, strategies nyingi zinabuniwa pale, lakini kutokana na uchelewesho wa utekelezaji na ule mwimbo wa ukosefu wa fedha, utashangaa zimeibuka kwa makampuni mengine binafsi (si ajabu kwa sababu kwenye bodi yao Zain wapo ndani).

Kuna miradi ambayo najua ilipangwa pale, kwa ajili ya masuala ya kitaifa, nimeshangaa plan zile zile wamepewa makampuni binafsi (na wanazitekeleza), utajiuliza zimetoka wapi?. sasa hawa tutawaita ma ' Idiot' kweli?. Idiot ataigwa mikakati na ufundi wake?.Sishangai sana kwa sababu ya mchanganyiko wa bodi na utaratibu wa kupeleka 'strategies' wizarani kwa approval...., hapo sasa
!.

Hivi hamjiulizi kuwa hao tunaodhani wanaakili (WAZUNGU) waliishapewa TTCL kuiongoza, wakaamua kuingia mitini, wakijua kuwa itakuja kuwafia mbeleni baada ya kukosa ushirikiano toka serikalini?

Suala kubwa kwa TTCL ni uwezeshwaji, haya makampuni tunayoyasifia, jiulize yamepata mikopo mara ngapi toka yameingia kwa ajili ya new investments (mengine yalikuwa yanakufa kabisa, mikopo ikayasaidia) na shughuli za kimasoko. Lakini nilishangaa kuwa TTCL haipewa nafasi hata mara moja ya kupata mkopo, tena hawataki 'fadhira' za bure, ni mkopo lakini tumejiuliza kwanini hawapewi?. kwa kipindi chote hicho wamekuwa wakijiendesha kwa pesa zao wenyewe, bila msaada.

Leo hata ukiwambia TTCL wajitangaze, hawana uwezo wa kutosha kumudu soko bila kuwekeza kuongeza mtandao, kwa kudunduliza billi za kila mwezi hawawezi kwenda popote, na hata ukimpeleka MALAIKA aongoze hapo, bila uwezeshwaji atakimbia tu, kila kitu atakiona cha moto.Kuna fikra potofu kuwa TTCL ipo kila sehemu, si kweli, haijafika sehemu nyingi, na hata kule walipo utakuwa ina uwezo wa kutoa huduma kwa wateja wachache tu. Pia dhana ya kuchanganya kuwa sehemu yeyete waliopo mobile itafanya kazi si kweli, inahitaji uwekezaji mpya kabisa kwani ni technologia ambazo haziingiliani na fixed lines.

Wakati umefika watanzania kuamka na kuacha uvivu wa kufikiri, tujaribu kuyachunguza mambo kwa undani. Makampuni ya umma yenye roho ngumu kama TTCL pengine yanatakiwa YAFE, ndiyo maana hayana support, pengine kama alivyosema mchangiaji hapo juu kuwa "hata kile kidogo walichonacho kinamendewa"


Uzalendo Kwanza,


GIS,

Kwanza nikupongeze kwa mchango wako mzuri kuhusu TTCL.
Ulichosema mkuu ni a 100% correct. Napenda tu nizungumzie hii sehemu niliyo-bold kwa rangi 'damu ya mzee'.

Kwamba maeneo yote ambako Mtanzania yoyote anayetumia simu za Zain/Airtel AJUE KUWA ILE MINARA ILIFANYIWA KAZI YA UPEMBUZI YAKINIFU na ENGINEERS WA TTCL. Upembuzi yakinifu ninaozungumzia ni DETAIL SURVEYS kwa ajili ya kuweka hiyo minara(i.e Towers+Power supply+BTS).

Kazi hiyo ilifanyika wakti Zain wakijiita Celtel Tanzania as a SISTER COMPANY or subsidiary company to TTCL. Kwa hiyo ma-engineers wa TTCL walishirikishwa kama vile WANAFANYA KAZI YA TTCL. Baada tu ya survey ile PESA YA TTCL NDIYO ILIYOTUMIKA KUAGIZA/KUNUNULIA MITAMBO HIYO GSM NA ILIKUWA IKIINGIZWA NCHINI KWA JINA LA TTCL NA SI CELTEL TANZANIA!

Ni baada tu ya hawa Celtel kumwaga BTS zao kwa mgongo wa TTCL na kuanza kutengeneza FAIDA KUBWA, ndipo wakatangaza NDOA YA CELTEL na TTCL kuvunjika. Hakuna kigogo yoyote aliyehoji uhalali wa Celtel kufanya vile. Ukiuliza ni kwanini jibu liko wazi: Vigogo walipanga iwe hivo.

Nakumbuka wakti uke Mwandosya akiwa Waziri wa Mawasiliano alikwenda kuzindua kituo cha Celtel/Zain huko mikoani na BILA AIBU AKAWAAMBIA WANANCHI KUWA WATU WAACHANE NA SIMU ZA TTCL ZA MEZANI MAANA ZIMEPITWA NA WAKTI!!!Think about that statement, a government Minister anaiponda Kampuni ya Serikali tena iliyokuwa inaibeba hiyo Celtel aliyokuwa akiipigia debe. Shame!!!

Mr. Mwandosya wakti huo akiwa Waziri wa Mawasilianao alichangia kwa sehemu kubwa sana kuimaliza TTCL! Nitaeleza baadaye ni vipi Mwandosya alichangia KUIANGAMIZA TTCL. Kwa sasa naishia hapa.
 
Kwa msio jua, ni afadhali msiendelee kujua; ila mambo ni kama hivi,
  • Wakati Mobitel inaingia TTCL ilikuwa na share mle kama asilimia 40. Baadaye serikali ikazibeba. Walichofanya na hizo hisa hakijulikani, ila leo serikali haina hisa Tigo
  • Mwaka 1999 TTCL iliamua kuanzisha mradi wake wa simu za Mkononi (kwa fedha zake), wakati huo ilikuwepo Tigo na Tritel peke yake. Serikali kupitia TCRA wakauzuia mradi huo kwa madai kuwa kampuni iko kwenye mchakato wa ubinafsishaji - Mwaka 2000 Vodacom wakaingia.
  • Mwaka 2001 akaingia Mbia kwa madai ya kununua asilimia 35 kwa Dola million 120. Akaishia kupewa hizo hizo kwa dola million 65.
  • Mbia huyo akatumia leseni ya biashara za simu za mikononi ya TTCL (mradi ulisimamishwa haukufutwa) kuanzisha celtel Tanzania, TTCL ikawa imenyang'anywa rasmi uwezo wa kufanya biashara za simu za mikononi, si kwa sababu ya uwezo wa watendaji, sababu ya uamzi wa mezani (serikali)
  • Celtel international (aliyekuwa na hisa ndani ya TTCL) ndo akaanzisha Celtel Tanzania ikiwa kama subsidiary company ya TTCL
  • Baadaye TTCL ikanyang'anywa shea zote ndani ya Celtel, zikahamishiwa hazina, TTCL ikabaki haina shea na haina biashara ya simu za mkononi na ikazuiwa kuanzisha ya kwake kwa sababu masharti ya leseni hayakuiruhusu kuanzisha
  • Mwaka 2005, serikali ikaondoa masharti ya leseni, ila mbia mwingine wa serikali; Celtel international (ambaye sasa ni mshindani wa TTCL - lakini akiwa na share ndani ya TTCL) akakataa TTCL isijiingize kwenye biashara ya simu za mikononi.
  • Wafanyakazi wazalendo ndani ya TTCL wakaamua kuingiza biashara hizo kwa mgongo wa nyuma, ndivyo ilivyoingia TTCL Mobile na Technolojia ya CDMA. Hawa wazalendo waliidanganya bodi kuwa wanaingiza CDMA kufanya fixed wireless (WLL) ila kwa siri wakanunua full mobile solution. Bodi ingejua isingiruhusu asilani.
  • Hata hivyo baadaye bodi iligundua kuwa kilichoingia ni Mobile si WLL. Ikaamua kuzuia uwekezaji zaidi katika mradi huo, hivyo TTCL mobile ikashindwa kujitanua kama ilivyotarajiwa.
  • Mwaka 2007, serikali ikaleta menejinti nyingine ya wazungu, kutoka Canada. Hawa walivyokuja wakaiambia serikali tiba ya TTCL ni kuuendeleza ule mradi wa TTCL mobile ulioanzishwa na wazalendo. Serikali ikakubali, lakini ikishirikiana na Celtel international (wakati huo Zain) wakazuia TTCL kukopa kwa ajili ya kuuendeleza mradi wa TTCL Mobile - Kwa hiyo mradi ukabaki bila kuendelezwa.
  • Mwaka 2009, baada ya kusuguana sana na serikali kuhusu kuendeleza mradi huo (serikali na Zain wakikataa), wa Canada waliamua kujitoa rasmi wakaondoka mwezi July 2009.
  • Toka hapo ni dana dana tu. Serikali wanashangaa kwa nini TTCL haifi? Wao wanataka ife, wauze mbao! Menejimenti ya wazalendo na wafanyakazi wao, wanapambana kulinda ajira zao. Ila serikali kwa kushirikiana na Zain (sasa airtel) wanataka hiyo kampuni ife, waipeleke kwa mufilisi ili viongozi wa serikali wajichotee masalia (TTCL inazo mali nyingi sana - Ikiwemo majengo, viwanja katika maeneo muhimu katika miji yote ya Tanzania, n.k.)
  • Ni dharau kwa watanzania kuwasema vibaya wafanyakazi wa TTCL, ni kampuni ngapi zingeweza kuhimili hujuma kutoka kwa wamiliki wake? Ni wafanyakazi pekee wanojua kuwa wanaohujumiwa pale ni watanzani, si wafanyakazi wa TTCL!! Watanzania ndo wenye mali serikali ni msimamizi tu.
  • Serikali dhaifu inashirikiana na matapeli wa nje kuhakikisha hii kampuni itakufa. TTCL ikifa, atakayenufaika ni watendaji wa serikali waliokaa mkao wa kula, wakisubiri kujichotea ma properties yatakayotelekezwa. Atakayenufaika ni Makampuni ya nje yatakayojichukulia biashara kubwa ambazo bado TTCL inazo.
  • TTCL ikifa atakayeumia ni mtanzania atakayekosa kazi. Mapato ya serikali yatashuka kwani TTCL pamoja na hali yake bado ni mlipa kodi mkubwa (waulize TRA watakuambia). TTCL hawafanyi lolote kukwepa kodi. Kodi zote za serikali wanalipa bila matatizo (bado wanalipa kodi kubwa kuliko makampuni mengi ya simu yanayokwepa kulipa kodi). Kushuka kwa mapato ya serikali kutawaumiza watanzania, si wawekezaji kutoka nje.
  • Ni vizuri tuujue ukweli, kwani ukweli utatuweka huru!

Daah, hii inauma sana. Imenitoa chozi!!!
 
Nope! Wamekwisha!....just wait n see. God have not forsaken us yet!

Nashukuru kuwa una matumanini kwenye mazingira ya kukata tamaa kabisa. Tumaini lako lienee kwa kila mtu anayesoma ili tuchukue hatua zinazostahili. It is just pathetic. Uozo wa nchi hii umekithiri mno hata hatujui tutajinasuaje. We need a miracle.
 
Ukisoma habari za Shingo na Gis.., kwakweli machozi yanakulengalenga unless wewe una-matatizo ya Uzalendo..., wapi waandishi wetu wa habari.., haya mambo si ya kufichaficha, Ugonjwa haufichwi bali huwekwa wazi ili tuutafutie dawa am sure wazalendo wangejua haya huenda wateja wa hizi network za kifisadi zingekosa wateja
 
Hakuwahi kukanusha.
Ilisemekana mwane alipelekwa kusomeshwa of all places South Africa, na Mwandosya akakirimiwa kwa kulipiwa safari ya kwenda matembezi huko majuu. (This is how cheap our leaders are)
(Habari hii ni according to magazeti wakati huo. Ni muda mrefu umepita, hivyo facts naweza nikawa nimezisahau zingine au kuzichanganya as they were thenreported).
Halafu huyu ndie some tout as presidential material !! poor tanzania

Ni kweli. Hizi habari zilitoka pia kwenye former forum i.e BCS. Hata jina la binti huyo liliwekwa kwenye mtandao.
 
So what should we do ili tuiokoe kampuni yetu?

Hapa ni kujiuliza, kati ya watu unawaowafahamu ukiwamo wewe mwenyewe, ni wangapi wanatumia ttcl mobile? Wengi wetu tumedandia mitandao ya mafisadi na kuwaneemesha hao mafisadi, huku shirika letu lenyewe likifa. Tubadilike tutumie ttcl
 
Hapa ni kujiuliza, kati ya watu unawaowafahamu ukiwamo wewe mwenyewe, ni wangapi wanatumia ttcl mobile? Wengi wetu tumedandia mitandao ya mafisadi na kuwaneemesha hao mafisadi, huku shirika letu lenyewe likifa. Tubadilike tutumie ttcl
Tatizo hata tukitumia TTCL hawa jamaa bado wataziibe huko huko dawa na kuwaondoa hao wezi
 
NDIO HUYO HUYO MSUDANI UNAYEMFAHAMU NA OMARY ISSA NDIO ALIKUWA MWENYEKITI WA BODI YA TTCLAMBAYE SASA HIVI KAINGIA NA KAMPUNI NYINGINE(ICL) YA KUOMBEA MISAADA SERIKALI NA TRA NA POLICE OMARY ISSA KAINGIA TAYARI HII NI BAADA YA KUIUZA CELTEL.Watanzania wataliwa mpaka lini????????
Huyo kwenye rangi nyekundu ndiye aliyeua TTCL kwa ushirikiano na makaburu weupe na weusi(akina Nigel na Makenzie)
 
Strategy, mission and vision of TTCL Tanzania still relies on the old model of business unlike other MPSP who work to ensure they co-exist with the modern environment in case of marketing and stiff competition from outside. TTCL can advance from the old model of service providing to the contemporary way only if the company`s public relations officer would work to adapt with changing environment and from there they can be the leading in providing good services as other companies do.

Ukimsoma Kishongo na Gis hapo kwenye post za juu, am sure utabadilisha kauli...,
 
Hii issue inafanana sana na ile ya TANESCO. Wengi wamekuja hapa na majibu kama yale ya Ngeleja juu ya TANESCO na DOWANS. Tusiubebeshe mzigo uongozi wa TTCL, tuangalie mazingira wanayofanyia kazi. Ni wangapi, kwa mfano, wanajua TTCL wanalipa kodi kiasi gani, na haya makampuni mengine yanalipa kiasi gani? Tatizo ni waroho wachache tulionao, na hii ya TTCL, sawa na ile ya TANESCO, ni vema yakapelekwa bungeni ili tuone kama kuna njia ya kufanya ili yamnufaishe mwananchi kwa kuwa ni mashirika ya umma.
 
Nasikia Ephraim Mafuru aliyekuwa Vodacom amehamia TTCL kama Mkurugenzi Mkuu,
Je ni kweli na anaweza kuleta mabadiliko chanya na kuifufua TTCL?
 
The TTCL story doesn't end here,it still continues. From reliable sources it is said that the same CELTEL/ZAIN owners in collaboration with Government officials they put a condition that TTCL NOT BE ALLOWED GO MOBILE as they,TTCL shall paralyze other MOBILE OPERATORS in Tanzania especially ZAIN. You may notice that in ZAIN the following big heads have a good number of shares: SALIM AHMED SALIM, ROSTAM AZIZI, JOSEPH SINDE WARIOBA,MO IBRAHIM,EDWARD LOWASSA and JK !
As that is not enough, The Tanzania government owes TTCL about 7 billion Tshs. BUT the Government is reluctant to settle the debt!!Reasons??The government coffers have no monie!!???But they are ready to pay the Ghost RICHMONDULI alias DOWANS Company a total of 94/= billion Tshs.

Sheeewww!!
Kumbe sie wajinga ndio tuliwao!! Wakati wakubwa wanakula nchi .. sisi makelele tu.
Haya mambo sasa yako wazi ... ina maana hawa akina JK hawaoni hata aibu wajiuzulu? wanasubiri nini?

Rostam Aziz na Lowasa siyo shareholders wa Airtel ( Celtel, Zain) ila wako VODACOM na Rostam Aziz alikuwa major shareholder ila sasa nasikia kapunguza share kwa kuwauzia Vodafone
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom