Why TTCL is not the leading Cellular and internet Operator?

YeshuaHaMelech

JF-Expert Member
Oct 12, 2010
2,597
37
I had time to talk with Some TTCL members/staff in previous time and were not happy that TTCL is not leading.

TTCL is the first company to have the biggest network web ever in Tanzania (I believe it still leads).

TTCL have independent Internet gateway, TTCL mobile, the news goes on saying, was planned to release its cheapest mobile service in form of TTCL mobile but its release was late and hence missed the business timing.

TTCL was tricked into producing enemy of its own by its own costs, that is Celtel then Zain then Airtel Tanzania.

Let us discuss, why is TTCL not leading, who are marring it to the current status and what should be done.

I hope there are TTCL members here to make it hot for the good of Tanzania.
 
Executives are not competent enough to to make the strategic plans for new developments

TCCL could have been very successfull PLC in the country.

Mkuu sio kwamba hawawezi kuwa successful bali hawataki kuwa successful, they are not running a company as profit oriented no one cares..., and no one is accountable..., so long they get their salaries.

Its the same reason why Air Tanzania is not the leading Airline Company...
 
Executives are not competent enough to to make the strategic plans for new developments.

TCCL could have been very successfull PLC in the country.

Musikurupuke tu na kuita wenzenu ****** jamani! hiyo ndiyo lugha gani isiyo ya kistaarabu?
 
Hilo shirika lina matatizo makubwa kwenye uongozi.. viongozi wao wengi ni analogy type.. upeo mdogo wa uongozi wa biashara wa kisasa, hawana uwezo kustrategize chochote. Na wasipoangalia wataingia kwenye matatizo makubwa hivi karibuni kutokana na kushindwa kujiendesha bado vilevile kuna politics yaani wafanyakazi wanajiona kama wanastahili nyingi sana ndani ya hilo shirika kwa kutumia hicho kitu kinaitwa tewuta wakati wao ndo chanzo cha hilo shirika kuporomoka kwa kufanya kazi chini ya kiwango.

Vilevile hilo shirika lina wafanyakazi wengi makao makuu wakati wangeweza kutumia technology na kupunguza matumizi ya uendeshaji.. anatakiwa CEO mwenye upeo wa kimataifa wa uendeshaji wa biashara za IT..bwana Said am afraid ataizamisha hiyo kampuni unless awaambie wafanyakazi ukweli pamoja na Tewuta yao.
 
hapa shida siyo TTCL mi nadhani shida ni hujuma za viongozi wenye hisa kwenye makampuni mengine ya simu, hawa jamaa wanajua kabisa TTCL ikiacha itawale soko ni nini kitatokea kwa makampuni yao. mi nafkiri tukipata viongozi wanaojua wajibu wao kwa taifa basi shilika hili litakuwa ni moja ya mashirika wanayojivunia watz.
 
Executives are not competent enough to to make the strategic plans for new developments. They are just idiot - business as usual.

TCCL could have been very successfull PLC in the country.

It reminds me about the story of Mramba, Air Tanzania and PrecisionAir. Once you get to know all the details of the 3, ndio utaelewa hii habari ya TTCL
 
yup! Niliambiwa na moja ya staff kuwa hata TTCL mobile ilicheleweshwa kwa makusudi ili kampuni nyingine zisiende mrama maana ingekuwa cheap sana. Je inawezekana uongozi wa juu kuna mapandikizi yaliyopo kwa interest ya kampuni nyingine?
Hata wafanyakazi wa chini hawapo motivated sana! So what should we do ili tuiokoe kampuni yetu?
 
Executives are not competent enough to to make the strategic plans for new developments. They are just idiot - business as usual.

TCCL could have been very successfull PLC in the country.


Labda tutofautishe mambo haya mawili: kutokuwa competent na kuhongwa na wamiliki wa kampuni za simu za binafsi

Wireless modem ya ttcl inauzwa 75000.

Bundle ya 1gb inauzwa 70000

Wakubwa wa ttcl wanayajua haya. na wanajua bei za modems na bundles zilivyo cheap kwenye private firms, ila wanafanya makusudi ili kuuwa shirika

Nchi hii ni ya rushwa jamani au mumesahau?
 
It is in my belief kwamba tatizo ni uongozi kuanzia ngazi za juu hadi chini. Kuna siku nilinunua simu ya mobile kwenye tawi mojawapo la Mikoani. At 15,000 unapata simu. Nikamuuliza mbona hamjitangazi? Akasema tatizo ni hela. Nilimkatalia na kumwambia kuwa hela si tatizo bali ni utashi wa staff to make business
 
Tatizo sio ttcl, tatizo mkataba ambao serikali ili ingia na celtel (msi) ambao unaifanya celtel kuwa na share ya 40% ndani ya ttcl, wakati wote wanafanya biashara zinazofanana yaani internet na simu. Prof Msola alikuwa anataka kuvunja mkataba huo wenye share waliopo serikalini wamehakikisha haludi pale wizarani.( msi) ni Warioba, Salim, Maua daftari, Ttcl kila ikifanya mipango yake MSI wanapinga au wanachelewesha inapitwa na wakati, dawa ni kvunja mkataba kati ya TTCL na MSI ili ttcl ijiendeshe yenyewe
 
Binafsi sipendi haya makampuni ya umma yawe na monopoly....mara nyingi yanakuwa inefficient na mwishowe gharama inakuwa kubwa kwa watumiaji. Wakati TTCL ipo dominant wengi mnajua simu ilivyokuwa ishu... ni kama Tanesco ilivyo sasa hivi. Sasa hivi ukiomba servive line ya Tanesco... inakubidi kusubiri mwezi mzima ukiwa na bahati... La sivyo ni kuanzia miezi mitatu na kuendelea. Hivyo ndio ilivyokuwa TTCL wakati ikiwa na monopoly kwenye soko la simu.
 
Binafsi sipendi haya makampuni ya umma yawe na monopoly....mara nyingi yanakuwa inefficient .

Mkuu hatuongelei monopoly ni kwamba private companies ziingie pia ila TTCL nayo iwe kwenye ushindani..., competing on the same level field lakini cha ajabu ni kwamba they have everything lakini hawataki kabisa ku-compete kwenye mobile phones..., na sio kwamba hawawezi. Which brings some people to think probably wana share kwenye hizo private companies au they gain something by TTCL not doing well. labda wabadilishe mfumo na waanze kuwalipa ma CEO wao kulingana na performance na profit
 
Mkuu hatuongelei monopoly ni kwamba private companies ziingie pia ila TTCL nayo iwe kwenye ushindani..., competing on the same level field lakini cha ajabu ni kwamba they have everything lakini hawataki kabisa ku-compete kwenye mobile phones..., na sio kwamba hawawezi. Which brings some people to think probably wana share kwenye hizo private companies au they gain something by TTCL not doing well. labda wabadilishe mfumo na waanze kuwalipa ma CEO wao kulingana na performance na profit

Labda sikusoma vizuri title ya thread!

Anyway, TTCL ina watu, culture na structure ambayo inatokea kwenye monopoly (or let's call it a dominant position in the market)...hivyo hawawezi hawawezi ushindana katika soko la simu lilivyo sasa (hata kama kusingekuwa na 'mkono wa mtu' kama baadhi ya watu wanavyotaka tuamini)! Ni lazima kufanyike revolution. Ni kama leo hii ukitokea ushindani kwenye nishati ya umeme, kwa watu, culture na structure ya Tanesco hawataweza kushindana.
 
labda tutofautishe mambo haya mawili: kutokuwa competent na kuhongwa na wamiliki wa kampuni za simu za binafsi

wireless modem ya ttcl inauzwa 75000.

bundle ya 1gb inauzwa 70000

wakubwa wa ttcl wanayajua haya. na wanajua bei za modems na bundles zilivyo cheap kwenye private firms, ila wanafanya makusudi ili kuuwa shirika

nchi hii ni ya rushwa jamani au mumesahau?
Ni sawa kabisa. Mmeona shirika gani la serikali linalopiga hatua nchini? Nitajieni moja tu. Mashirika yote ya serikali yanaendeshwa kwa hasara, seuze kuweza kuongoza mbele ya mashirika mengine. Kwa mfumo wa sasa wa biashara za ushindani, serikali haikupaswa kulibakisha hili. Cha kufanya ni kulivunja kabisa, kwani nina wasiwasi kuwa hata likibinafsishwa, mizimu ya Richmond, Dowans, Rada, Ndege, Migodi, EPA, ATC, Kiwira, Bandari, Songosongo.... orodha haishii hapa, itahamia hapo. Inaniuma kusema lakini Tanzania imelaaniwa!, na laana hii itaendelea mpaka pale Watanzania tutakapoamua, tutakaposema (na kutenda) kuwa MPAKA HAPA BASI, INATOSHA.
 
Mimi ningeshauri hili shirika lifanywe kama ilivyokuwa crdb bank. Wananchi wauziwe hisa lijiendeshe kibiashara. Hawa MSI hisa zao zinunuliwe na serikali na kuiziwa wananchi. Haya yakifanyika mabadiliko yatakuwa ya kutisha!
 
Kwa msio jua, ni afadhali msiendelee kujua; ila mambo ni kama hivi,

Wakati Mobitel inaingia TTCL ilikuwa na share mle kama asilimia 40. Baadaye serikali ikazibeba. Walichofanya na hizo hisa hakijulikani, ila leo serikali haina hisa Tigo

Mwaka 1999 TTCL iliamua kuanzisha mradi wake wa simu za Mkononi (kwa fedha zake), wakati huo ilikuwepo Tigo na Tritel peke yake. Serikali kupitia TCRA wakauzuia mradi huo kwa madai kuwa kampuni iko kwenye mchakato wa ubinafsishaji - Mwaka 2000 Vodacom wakaingia.

Mwaka 2001 akaingia Mbia kwa madai ya kununua asilimia 35 kwa Dola million 120. Akaishia kupewa hizo hizo kwa dola million 65.
Mbia huyo akatumia leseni ya biashara za simu za mikononi ya TTCL (mradi ulisimamishwa haukufutwa) kuanzisha celtel Tanzania, TTCL ikawa imenyang'anywa rasmi uwezo wa kufanya biashara za simu za mikononi, si kwa sababu ya uwezo wa watendaji, sababu ya uamzi wa mezani (serikali)

Celtel international (aliyekuwa na hisa ndani ya TTCL) ndo akaanzisha Celtel Tanzania ikiwa kama subsidiary company ya TTCL
Baadaye TTCL ikanyang'anywa Hisa zote ndani ya Celtel, zikahamishiwa hazina, TTCL ikabaki haina hisa na haina biashara ya simu za mkononi na ikazuiwa kuanzisha ya kwake kwa sababu masharti ya leseni hayakuiruhusu kuanzisha

Mwaka 2005, serikali ikaondoa masharti ya leseni, ila mbia mwingine wa serikali; Celtel international (ambaye sasa ni mshindani wa TTCL - lakini akiwa na share ndani ya TTCL) akakataa TTCL isijiingize kwenye biashara ya simu za mikononi.

Wafanyakazi wazalendo ndani ya TTCL wakaamua kuingiza biashara hizo kwa mgongo wa nyuma, ndivyo ilivyoingia TTCL Mobile na Technolojia ya CDMA. Hawa wazalendo waliidanganya bodi kuwa wanaingiza CDMA kufanya fixed wireless (WLL) ila kwa siri wakanunua full mobile solution. Bodi ingejua isingiruhusu asilani.

Hata hivyo baadaye bodi iligundua kuwa kilichoingia ni Mobile si WLL. Ikaamua kuzuia uwekezaji zaidi katika mradi huo, hivyo TTCL mobile ikashindwa kujitanua kama ilivyotarajiwa.

Mwaka 2007, serikali ikaleta menejimenti nyingine ya wazungu, kutoka Canada. Hawa walivyokuja wakaiambia serikali tiba ya TTCL ni kuuendeleza ule mradi wa TTCL mobile ulioanzishwa na wazalendo. Serikali ikakubali, lakini ikishirikiana na Celtel international (wakati huo Zain) wakazuia TTCL kukopa kwa ajili ya kuuendeleza mradi wa TTCL Mobile - Kwa hiyo mradi ukabaki bila kuendelezwa.

Mwaka 2009, baada ya kusuguana sana na serikali kuhusu kuendeleza mradi huo (serikali na Zain wakikataa), wa Canada waliamua kujitoa rasmi wakaondoka mwezi July 2009.

Toka hapo ni dana dana tu. Serikali wanashangaa kwa nini TTCL haifi? Wao wanataka ife, wauze mbao! Menejimenti ya wazalendo na wafanyakazi wao, wanapambana kulinda ajira zao. Ila serikali kwa kushirikiana na Zain (sasa airtel) wanataka hiyo kampuni ife, waipeleke kwa mufilisi ili viongozi wa serikali wajichotee masalia (TTCL inazo mali nyingi sana - Ikiwemo majengo, viwanja katika maeneo muhimu katika miji yote ya Tanzania, n.k.)

Ni dharau kwa watanzania kuwasema vibaya wafanyakazi wa TTCL, ni kampuni ngapi zingeweza kuhimili hujuma kutoka kwa wamiliki wake? Ni wafanyakazi pekee wanojua kuwa wanaohujumiwa pale ni watanzania, si wafanyakazi wa TTCL!! Watanzania ndio wenye mali serikali ni msimamizi tu.

Serikali dhaifu inashirikiana na matapeli wa nje kuhakikisha hii kampuni itakufa. TTCL ikifa, atakayenufaika ni watendaji wa serikali waliokaa mkao wa kula, wakisubiri kujichotea ma properties yatakayotelekezwa. Atakayenufaika ni Makampuni ya nje yatakayojichukulia biashara kubwa ambazo bado TTCL inazo.

TTCL ikifa atakayeumia ni mtanzania atakayekosa kazi. Mapato ya serikali yatashuka kwani TTCL pamoja na hali yake bado ni mlipa kodi mkubwa (waulize TRA watakuambia). TTCL hawafanyi lolote kukwepa kodi. Kodi zote za serikali wanalipa bila matatizo (bado wanalipa kodi kubwa kuliko makampuni mengi ya simu yanayokwepa kulipa kodi). Kushuka kwa mapato ya serikali kutawaumiza watanzania, si wawekezaji kutoka nje.

Ni vizuri tuujue ukweli, kwani ukweli utatuweka huru!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom