Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,631
- 3,543
Am sory michele but have to say this. Kumekuwa na wimbi kubwa la kile kinachoitwa vita dhidi ya mfumo dume. Japokuwa kuna sehemu ambazo kweli zina mapungufu na tunahitaji, kama jamii ku-take action, lakini pia tusiache kusema ukweli kwa kuhofia kuonekana tunaendekeza mfumo dume. Hebu tuangalie kwa namna hii. Mary anatekeleza matakwa ya aliyemtuma bila kutumia ubongo wake. Anatekeleza matakwa ya kibosile aliyemwezesha kuwa hapo alipo ambaye pia ni chakula yake. Kama watu wanajua uwepo wake hapo unatokana na fadhila kwake kwa kile anachowafadhili wakubwa, kumsema kwa kuzingatia hizo fadhila sio masuala ya patriachal. Hapo ubongo wake hautenganishwi na namna anavyotumika. Usife moyo. Tuendeleze mapambano huku pia tukielimishana.
Asante kunielewesha Sumuni,sijakataa kabisa kwenye maelezo yangu kuwa wapo wanawake wanawatumikia wale waliowaweka hapo, ninachokisema kama umeangalia post zangu zilizopita ni kuwa,imekuwa desturi sasa kwamba mwanamke akikosea au akiteuliwa au hata akichaguliwa watu wanasema ni chakula ya fulani,there are exceptions,Mary Chitanda might not be one of them. Na huko juu nimesema kuwa namfahamu huyu mama ukiacha suala la yeye sina uhakika kama ni chakula ya fulani,uwezo wake wa kufikiri si mkubwa ndo maana haoni shida.......Ingekuwa ni Tibaijuka kaambiwa akaseme hivi asingeliongea hata kama maana zingefanana kama Mary,ndo maana kwenye post yangu nikasema kuwa chakula ya mzee isiwe kigezo pekee cha kum-disqualify mtu though nimekubali inaweza punguza utendaji na ku-limit decision ambazo mtu anafanya, kuna factors kama exposure ya mtu,elimu,maisha aliyoishi na hata tamaduni alizokulia.kama nilivyotarajia nimetukanwa na kuambiwa nami chakula ya mzee fulani na mtu asiyenijua,simply kwakuwa mi ni mwanamke????Am very sensitive na hii issue kwakuwa imenigusa si kwenye siasa bali kazini.....na sitoacha kusema we should be judged on fair basis si jinsia pekee.