While Zitto is being attacked pls read here

While Zitto is being attacked pls read here

Mwenye hoja au maoni mbadala juu ya haya anayopigania Zitto na atoe badala ya kuja na itikadi za kichama,hoja za kumjadili mleta hoja badala ya kujadili hoja.!

Kwani prof kakataa kuweka mikataba wazi? Si amesema atafanya hivyo baada ya wiki mbili? Kuna ubaya gani kama atareview kwanza?
 
Kimsingi hamna m2 mwenye chuki na ZZK ndan ya CDM bali hisia mbaya juu yake zinakuja kw sababu kwa hili la mafuta na gesi na mengine mengi hayasimamii nyuma ya CHADEMA bali kama ZZK nahaneshi nia ya dhati katika kuuondoa mfumo mbovu ulio2fikisha hapa ambao ni wa CCM kazi ya mwanachama au kiongozi wa chama chochote cha upinzan ambacho malengo yake ni kukamata dola ni kuzipinga wazi wazi sera mbovu zilizoshindwa za chama kilichopo madarakani hapa ni lazima ujiulize ni ZZK VS MUHONGO AU NI CHADEMA VS CCM BADO KUNA MASWALI MENGI JUU YA ZZK NDAN YA CHADEMA

Kwenye mambo ya utaalam haihitaji mtu kusimama nyuma,katikati,juu,au chini ya siasa ili uweze kutoa ideas. Na huu ndio uzembe ambao bado watanzania wengi wanaendelea kuufanya. Isitoshe ni uvivu wa kufikiri kuendelea kuamini mtu anatakiwa kufikiri "kama chama" badala ya kufikiri "kama mtu".
Tunachohitaji ni good ideas,kutoka watu wenye uelewa katika sekta hii ya madini,mafuta na gesi,tupate sera na sheria itakayotupa mikataba yenye kutunufaisha Watanzania. Kama Zitto katoa maoni yake,na mwingine atoe tupime. Wakati mwingine tujifunze kufikiri nje ya boksi,hata kama hatujazoea.
Labda nikuulize wewe unaposema asimame "nyuma ya CDM",ni nini sera ya Chadema kuhusu madini,mafuta na gesi(kama ipo),ili ujenge hoja kuwa Zitto ameenda against sera ya chama chake. Na hata kama angepingana na sera ya chama kuhusu jambo husika,hiyo inatosha kwako ku-award credits mbaya kwa mtu anayepingana na sera!
 
Kwani prof kakataa kuweka mikataba wazi? Si amesema atafanya hivyo baada ya wiki mbili? Kuna ubaya gani kama atareview kwanza?

Hatuwezi kufanya review ya kitu ambacho hata sheria wala sera yake hatuna. Mpaka sasa hatuna sheria wala sera ya mafuta na gesi,bado unatusadikisha tujadili mikataba ya mafuta na gesi,ndo hivi unavyosema/anavyosema?
 
Hatuwezi kufanya review ya kitu ambacho hata sheria wala sera yake hatuna. Mpaka sasa hatuna sheria wala sera ya mafuta na gesi,bado unatusadikisha tujadili mikataba ya mafuta na gesi,ndo hivi unavyosema/anavyosema?
Huhitaji uwe na sheria kufanya hii review inayoongelewa hapa. Kumbuka prof Muhongo hana muda mrefu kwenye hiyo wizara na wakati hiyo mikataba inafanyika hakuwepo. Pia bodi ya TPDF ni mpya. Kuna ubaya gani wakiperuzi ili kujiandaa na maswali mijadala itakapoanza?
 
Hatuwezi kufanya review ya kitu ambacho hata sheria wala sera yake hatuna. Mpaka sasa hatuna sheria wala sera ya mafuta na gesi,bado unatusadikisha tujadili mikataba ya mafuta na gesi,ndo hivi unavyosema/anavyosema?
hivi mwl alivyo fanya miaka ileeee, tulikuwa hatuna sera wala sheria?
 
Huhitaji uwe na sheria kufanya hii review inayoongelewa hapa. Kumbuka prof Muhongo hana muda mrefu kwenye hiyo wizara na wakati hiyo mikataba inafanyika hakuwepo. Pia bodi ya TPDF ni mpya. Kuna ubaya gani wakiperuzi ili kujiandaa na maswali mijadala itakapoanza?

Being new to the system does not give one the privillage to make mistake(s). Haya anayofanya au anachosema Waziri lazima yatazamwe kwa uangalifu mkubwa. Vilevile kumbuka ya kuwa kinachotuua kwa sasa ni mikataba mibovu,so waziri anapotaka kupita njia ileile iliyotuzamisha kwenye mikataba mibovu hatuwezi kuchekelea au kusubiri ikishafanyika ndio tukosoe. Turn back immediately no matter how far you have travelled in the wrong direction. We must all shout together,that approach is bad!
Augusthivi mwl alivyo fanya miaka ileeee, tulikuwa hatuna sera wala sheria?
Ni mikatab ipi aliyosaini mwalimu ya mafuta ,gesi au madini..tukumbushe.


 
atuwezi kuwaacha wamchafue mkombozi wa taifa letu..


wapendwa ZITO yule wa kumbananisha karamagi na buzwag yake pale dodoma alishatutoka cku nyingi sana adi masalia yake pia hatunayo tena tuwategemee kina mnyika slaa mbowe lisu na wengineo huyo hayupo wakuu, understand wala c chuki!
 
ulitakiwa ujue hapa ni ishu za maana kabla hujaanzisha ligi ya kombe la samaki.

Mswazi humjua mswazi mwenzie, fair?

Kwa hiyo umekimbia TZ sababu yangu? Unanipa credit sana aisee, punguza basi kidogo.

Eti 'kubwa' anapambana na 'dogo' kwa pumba badala ya hoja.
acha mipasho 'dogo' hapa tunashusha ishu za maana...porojo zako za uswazi na usupastaa wako wa jukwaa la chitchat hazina nafasi hapa.

eti supastaa wa chichat,aibu!!sasa sisi tunaoikimbiza TZ tusemaje!!
 
Mbona wacha ngiaji kwenye mambo ya lugha za kigeni wanapungua, naamini asilimia kubwa ya mawazo aliyonayo Zitto ni mazuri kwa maendeleo ya Taifa letu ila kuna watu ambao wamefundishwa na wamelelewa na makundi ya watu fulani kubisha BUT Hon Zitto dont give up, you will overcome all tyranny.
Eeh ni kidhungu!, hivi jamaa anathema zito kafanya nini?. Lakini huyu jamaa anafaa kuwa kiongozi!
 
Dear the great thinkers of JF,As much as i was suspicious of Hon. Zitto motives on the assigned review process on the Production Sharing Agreements (PSAs)and energy contracts by the Minister of Energy and Minerals; i was forced to backtrack from my Prio-stand and right-off any attempts to have anything significant out of this review process when i came across this:
Tanzania will not revoke any oil and gas PSAs -Energy Minister,Tue Sep 18, 2012 5:13pm GMT Print | Single Page[-] Text [+] DAR ES SALAAM, Sept 18 (Reuters) - Tanzania will not alter or revoke existing oil and gas contracts, its energy minister said on Tuesday, two days after he was widely reported in local media saying unfavourable deals would be scrapped."We are not trying to stop any business. We will not revoke any contract, we will respect all contracts," Energy and Minerals Minister Sospeter Muhongo told Reuters.Muhongo said he had been misquoted in Tanzania's local media.© Thomson Reuters 2012 All rights reserved
 
kwaio wewe kama kiongozi wa chama unakub ali kwamba zito anachukiwa ndani ya cdm...bora wewe umeongea ukweli maana kosa lake atokei kaskazini.
Kaskazini source ya viongozi ndani ya sisiemu. Tangu uhuru mawaziri wakuu 6 kati ya kumi walitoke kaskazini. kibaya zaidi watatu kati yao walitoka Arusha, tena wawili kabila moja!. Kibaya saaaaana 8 kati ya 10 ni dini moja!..
 
Ni mikatab ipi aliyosaini mwalimu ya mafuta ,gesi au madini..tukumbushe.


[/QUOTE]
hivi songo songo project ilianza lini? kama sio wakati wa Mwl? aliye anzisha stamico ni nani? au TPDC why Tanzania? na si kenya au Uganda kuwa na mashrika kama hayo? maana Dalili zilisha anza kuonekana
 
I conquer with you sir that Hon Zitto need our support over this,but ZZK need not to walk alone on issues like this of huge public interest.Why not channel it through party and whetever comes come through party?

Surely, it is not easy for Zitto to fight a lonely battle.
 
so waziri anapotaka kupita njia ileile iliyotuzamisha kwenye mikataba mibovu hatuwezi kuchekelea au kusubiri ikishafanyika ndio tukosee.
Hayo wasema wewe, alichosema yeye ni kwamba anareview kwa maana ya kuperuzi halafu baada ya wiki mbili wananchi wataweza kuijadili. BBC
 
Moja ya matatizo yetu kama nchi na wananchi ni kuchukia watu wanaofikiri tofauti. Tumezoea mazoea; ukiona mtu anaenda tofauti na mazoea tunaanza kumpa majina kibao: kanunuliwa, msaliti, anajipendekeza, hana ushirikiano, n.k.. Lazima tubadilike na kujua kwamba binadamu tu tofauti kimwili, kiakili na kila kitu. Ili tutoke hapa tulipo lazima turuhusu akili zifikirii sawasawa na tena tuhangaike kufikiri kitofautitofauti. Kama tunataka kila mtu afikiri kama sisi ni kuendeleza utamaduni wa kutumia akili za kuazima. Zitto ni miongoni mwa watu wachache hapa nchi aliyeamua kujipambanua na kuamua kufikiri kitofautitofauti. "Kosa" lake ni kwamba ameamua kuacha kufanya mambo kwa mazoea na ameamua kuhangaika kufikiri kitofautitofauti. Zitto analaaniwa kwa kudiriki kwake kuhangaika kufikiri na kuachana na mazoea. Atabambikizwa majina yote ya ovyo kama usaliti, kujipendekeza, n.k. Tunamtia moyo aendelee kuhangaika kufikiri, wapo watakaomuelewa.


Sidhani kama kuna mtu anamchukia Zitto kwa mawazo anayotoa au juhudi anazozionesha katika sekta ya nishati na madini. Kitu kinachojitokeza kwa sasa ni yeye kujiendesha kama Taasisi huru nje ya chama chake.Amekuwa kama Mwanasiasa wa kujitegemea asiyeamini uwepo wa chama chake cha siasa. Ni wazi kuwa huko nyuma enzi za Zitto kuwa kwenye siasa za Majukwaani, kuibua kashfa dhidi ya Serikali (Mf.Buzwagi), kuwa mstari wa mbele kukijenga chama chake hakukuwa na hali hii ya Zitto kupingwa na idadi kubwa ya watu.

Binafsi siko kwenye Chama chochote cha Siasa lakini kila ninapowaona viongozi wa CDM wakimenyeka na maandamano, kufanya mikutano ya hadhara, kupigwa mabomu na Polisi na hata wengi wao kukumbwa na kesi kadhaa mahakamani kitu cha kwanza kinachonijia ni ukweli kuwa wako tayari kujitoa muhanga ili kuwaeleza wazi Watanzania juu ya uozo unaoendelea nchini, mfumo mbovu wa Utawala ikiwa ni pamoja na upuuzi ulioko kwenye sekta ya Gesi, mafuta, madini na nishati kwa ujumla wake ambao Zitto amekuwa akiushikia kidedea.

Sasa kinachomzuia Zitto kutumia platform ya CDM na movement zake (M4C, Vua gamba vaa gwanda nk.) katika kueleza uozo ulioko Serikalini hasa kwenye Sekta za nishati na madini ni nini hasa? Kwa nini amekuwa na personal platforms na mbaya zaidi haonekani kabisa kwenye mihenyeko inayowakumba viongozi wenzake ndani ya CDM? Kwa mtu yeyote makini lazima ahoji haya na kwa kweli Wananchi wanashindwa kumuelewa.

Sasa mambo kama haya yakiongezwa na taarifa (Binafsi sina hakika nazo) za Zitto kuwa na uhusiano wa karibu na watu wa aina ya Rostam Aziz,tetesi za yeye mwenyewe (Zitto) kumiliki mali zisizooana na kipato chake, kutetea wabadhirifu wa aina ya William Muhando ndani ya TANESCO na zaidi kutetea ununuzi wa mitambo ya Dowans nk. nk. yanawafanya watu wengi si tu wahoji Uhalali wa Zitto Kabwe katika hoja anazotoa bali pia uhalali wa hoja zenyewe.

Nakumbuka kipindi fulani kampeni za uchaguzi mdogo wa Arumeru East zilikuwa zimepamba moto na CDM ilikuwa imepigwa kwelikweli na propaganda chafu za CCM (Rejea propaganda za Wassira dhidi ya CDM/Dkt. Slaa) ghafla Zitto akaibuka kuutaka urais. Watu wengi walishtuka, wakahoji inakuwaje Mheshimiwa huyu viongozi wenzake wako kwenye mapambano Arumeru yeye anaibuka kusikojulikana na kutangaza nia ya kugombea urais kupitia CDM? Hili pekee liliwafanya watu wengi kumuona Zitto katika jicho tofauti.

Dkt. Kitila Mkumbo unaweza ukasema huku ni kufikiria tofautitofauti lakini ni wazi hii ni aina ya kufikiri inayolenga kudhoofisha taasisi ya kisiasa uliyomo.
 
Hivi kwanini jamii inachukulia kama kubadili msimamo ni weakness? Mtu anaweza kubadili msimamo baada ya kupata taarifa zaidi juu ya swala husika, na hilo ni jambo jema na lenye manufaa.

Cha msingi ni mtu aliyebadili msimamo kutoa sababu ya kubadili msimamo na hivyo basi mijadala ielekezwe kwenye uzito au wepesi wa hiyo sababu.

Kuhusu Zitto - anachohubiri Zitto sasa hivi kuwa kinachohitajika zaidi ni transparency sio kitu kipya Tanzania. Labda tukumbushane tu kuwa katika awamu ya tatu serikali ilikuwa na kauli mbiu ya UWAZI NA UKWELI. Zitto alichobadilisha ni lugha tu lakini anazungumzia uwazi na ukweli uleule aliouhubiri Rais Mkapa. Sasa kila mtu apime mwenyewe kama uwazi na ukweli wa awamu ya tatu ulifanikiwa kudhibiti ubadhilifu wa mali ya umma. Kama jibu ni ndio basi Zitto anapigania kitu sahihi, kama jibu ni hapana basi Zitto anaelekea siko (kwa makusudi au kwa kutojua: I dont know!).

Uwazi gani unaousema wewe wakati waandishi waliambiwa kua hawana uwezo wa kufikiri. Uwazi anaousema Zito sio huo.
 
I think it is important to clarify this issue. Is ZZK attacked because of his ideas or due to his personalities traits as a means in achieving his political ambitions and long term insatiable gains? The latter remains true.
ZZK is talented with good ideas, often suggesting practical solutions and a gifted politician, nevertheless ZZK uses his charisma for egoism and corruption. There are many examples but let me mention the Buzwagi issue which brought him to the peak of public attention and appreciations and there after had been even climbing higher. We all know how he ended up as we say "he ended up swallowing his own vomitus" by succumbing to corruption tricks. And today we know he is a professional in this game.
In a nutshell, ZZK is a very bright person, has unquenchable thirst of power and wealth, which he is striving to achieve both by ALL means. He is not attacked of his ideas but they are cherished and supported, though those who know him well hate his other part of him and attack the intentions.
 
wapendwa ZITO yule wa kumbananisha karamagi na buzwag yake pale dodoma alishatutoka cku nyingi sana adi masalia yake pia hatunayo tena tuwategemee kina mnyika slaa mbowe lisu na wengineo huyo hayupo wakuu, understand wala c chuki!

Mbowe anataka kutuandamanisha tu mbona hana hoja.
 
Hapa si mahala sahihi pa kujadili watu tunapaswa kujadili hoja japokuwa muda mwingine ni ngumu kutenganisha hoja na mtoa hoja!!!!!!!! Binafsi sina imani hata kidogo kama zito ana uzalendo wa kweli kwa sasa hivi na hata huko nyuma alikwa mpambanaji wa kweli si kwasababu ya uzalendo bali alikuwa akitafuta nafasi ya kuaminiwa na kufanya ayafanyayo sasahivi anaweza kuwa anahoja sahihi kabisa kwa maslahi ya Taifa lakini kinachomsukuma si uzalendo bali ni maslahi binafsi ya kiuchumi na kisiasa,Pamoja na hayo wazo lake la Transparency kwa mikataba ya gesi na mafuta ni wazo zuri sana tunalopaswa kuliunga mkono lakini bila Kumpinga Prof Muhongo kwa kufanya review ya hiyo mikataba tumsupport Muhongo afanye hiyo review then aiweke wazi (nadhani ndo dhamira yake hiyo) then nguvu ya Umma ichukue nafasi yake kama kuna kitu kibaya kwa maslahi ya umma kwenye hiyo mikataba tuipinge kwa nguvu zetu zote kwa umoja wetu kama wananchi tusikubali tena kuingizwa mkenge kama wa kwenye madini "God has given us a second chance let's not misuse it guys" ugomvi wangu na Zitto hapo ni kwenye kupinga hiyo review kwanini anapinga? nadhani alipaswa kuunga mkono lakini akapigania sana iwekwe wazi.
 
Back
Top Bottom