Kuna watu wao wanaona ya kawaida tu hiyo picha.
Kama wameweza kupiga za huyu ndani ya chumba cha upasuaji,watashindwa nini kupiga picha za mama akijifunfua?
shemeji umewahi kukumbana na hizo picha???
Yaani mda huu niko hapa nadumisha uzi, huku kuna mtu kanitumia sijui za mwanaume singida kakata kata familia yake yote vipande vipande.. arghhh..!
Nazipata sana shemeji na leo nimetumiwa moja ya mtoto kacharangwa mapanga na mzazi wake huko singida. Imebidi nipoteze muda kutoa somo kwa aliyenitumia, sijui kaelewa....!!
Zinatumwa na bavicha, vijana wasiokuwa na kazi wa chadema!!
Inategemea na jinsi unavyojiweka kwao. Kwangu mimi huwa hawanitumii hata iweje kwasababu siwatumii.
Kama unawatumia its obvious watakutumia
Hiyo ya shoka limezama ni balaa
kila saa inakuja kichwani..... hili group langu hili
Ndio maana nikasema wengine huwa tunafowadi bila hata kufikiria kama huyo unaemtumia atajiskiaje? Yaani ni kama tabia tu imejengeka kwamba ukifowadiwa kitu na wewe unafowadi fasta.. Na mara nyingi picha hizi tuna fowadiwa na watu wetu wa karibu tu ambao hatuwezi kufuta namba zao..
Funnie videos and pictures....wewe jamaa nakujua wewe
Nahisi nawe uko kwenye grupu nililo mimi ambalo jana wajumbe tulistukia mida ya jioni tunaletewa mapicha ya hatari