Whatsapp na picha za kutisha..

TheChoji

JF-Expert Member
Apr 14, 2009
4,973
15,304
Mmeshindaje?
Siku za hivi karibuni kumejitokeza tabia ya watumiaji wa Whatsapp ku-forward picha zinazoonyesha matukio ya kutisha kama vile watu waliokatwa mapanga, waliokatwa/unguzwa sehemu za siri, waliokitwa mashoka vichwani, waliopata ajali mbaya na nyingine ambazo kwa maoni yangu sioni kama ni sawa kwa picha za aina hii kusambaa kwenye jamii. Inawezekana kabisa baadhi yetu huwa tunafowadi tu picha hizi bila hata kufikiria mara mbili kwamba zina athari gani katika jamii? Mimi binafsi sioni kama picha hizi zinatusaidia chochote sisi kama Watanzania. Ni kweli tunayo haki ya kupata habari lakini nadhani tuangalie sana aina ya vitu tunavyo izoesha jamii ikizingatiwa kwamba picha hizi zinaweza kuangaliwa hata na watoto maana hamna kizuizi chochote. Nadhani itasaidia zaidi kwa matukio tajwa kuripotiwa polisi badala ya kusambaza kwenye mitandao. Au wadau mnaonaje?
 
yaani kama umeniona.... nimefowadiwa picha za mauaji gani sijui.... watu wamezungushiwa matairi wanachomwa moto... yaani zimeniharibia siku kabisaaaa; na aliyenifowadia namheshimu.. nimebaki naumia tuuuu maana huwa sipendi kabisa kuangualia vitu vya kuchinjana chinjana...
 
Mmeshindaje?
Siku za hivi karibuni kumejitokeza tabia ya watumiaji wa Whatsapp ku-forward picha zinazoonyesha matukio ya kutisha kama vile watu waliokatwa mapanga, waliokatwa/unguzwa sehemu za siri, waliokitwa mashoka vichwani, waliopata ajali mbaya na nyingine ambazo kwa maoni yangu sioni kama ni sawa kwa picha za aina hii kusambaa kwenye jamii. Inawezekana kabisa baadhi yetu huwa tunafowadi tu picha hizi bila hata kufikiria mara mbili kwamba zina athari gani katika jamii? Mimi binafsi sioni kama picha hizi zinatusaidia chochote sisi kama Watanzania. Ni kweli tunayo haki ya kupata habari lakini nadhani tuangalie sana aina ya vitu tunavyo izoesha jamii ikizingatiwa kwamba picha hizi zinaweza kuangaliwa hata na watoto maana hamna kizuizi chochote. Nadhani itasaidia zaidi kwa matukio tajwa kuripotiwa polisi badala ya kusambaza kwenye mitandao. Au wadau mnaonaje?

CCM Ndio wanazisambazaaaaa hizooo
 
yaani kama umeniona.... nimefowadiwa picha za mauaji gani sijui.... watu wamezungushiwa matairi wanachomwa moto... yaani zimeniharibia siku kabisaaaa; na aliyenifowadia namheshimu.. nimebaki naumia tuuuu maana huwa sipendi kabisa kuangualia vitu vya kuchinjana chinjana...

Kwa kweli ni tabia inakera sana.. mi sidhani kama hayo ni matumizi sahihi ya mitandao hiyo
 
Kuna grupu flani la wadau waliohitimu shule flani toka mkoa wa hayati wanatumiana mapicha ya hatari kwa mfano jana binti mmoja wa grupu lile katuma picha ya mtu kakitwa shoka la kichwa, muda mfupi baadaye kijana mmoja akatuma picha ya mwanamke ametega makalio kuonyesha sehemu za siri zilizounguzwa.
 
CCM Ndio wanazisambazaaaaa hizooo

Hoja ya msingi kwenye mada hii sio vyama wanavyotoka watumaji. Ni kwamba tabia hiyo inakera na sisi kama jamii tuna nafasi kubwa katika kuikomesha. Tusione ufahari kuwa wakwanza kuwatumia watu picha hizo tukidhani ni sifa..! Nna uhakika mtu mmoja mmoja tukianza kuacha tabia hiyo itakoma.
 
Haya mapicha yanakera sana sijui.watu wanaona sifa kuharibiana mda tu mi hadi huwa sifungui na delete mara mtu sijui kachomwa sehemu nyeti mtu ana forwad mipicha inakera hawajui kuwa wengne tuna roho nyepesi
 
yaani kama umeniona.... nimefowadiwa picha za mauaji gani sijui.... watu wamezungushiwa matairi wanachomwa moto... yaani zimeniharibia siku kabisaaaa; na aliyenifowadia namheshimu.. nimebaki naumia tuuuu maana huwa sipendi kabisa kuangualia vitu vya kuchinjana chinjana...
Fanya kama nifanyavyo mie. Waambie hao watumaji kwamba hupendi picha za aina fulani (ziweke wazi), hivyo wasikutumie. Kama bado wanaendelea, simply block akaunti zao ili usizione kamwe!
 
Hizo picha zinakukera wewe tu ndugu,sisi wenzenu lazima tuangalie watu wanavyochinjwa na kukatwa shoka IN ALLAH'S NAME!

Nyingi nilizoziona hazina uhusiano kabisa na hicho ulichokitaja.. ni za ajali, mafumanizi, unyanyasaji wa kijinsia n.k
 
wabongo wakiona tu forward utabarikiwa sijui utakuaje ndani ya wiki wanazituma fasta mno... mimi hua siziforward afu naona ndo nafanikiwa badala ya kupatwa na mikosi kama meseji zinavosema...
 
Kadri muda unavyokwenda binadamu anakosa utu kwa spidi ya kutisha.Juzi Kuna mtu kanitumia picha za yule kijana WA Arusha,aliyekula ubongo WA mtoto,pamoja na picha ya ubongo huo.Jana picha za viungo vya binadamu Kule Bunju,zimesambaa kwa Kasi Sana.
 
Back
Top Bottom