Whatsapp na picha za kutisha..

Whatsapp na picha za kutisha..

Kadri muda unavyokwenda binadamu anakosa utu kwa spidi ya kutisha.Juzi Kuna mtu kanitumia picha za yule kijana WA Arusha,aliyekula ubongo WA mtoto,pamoja na picha ya ubongo huo.Jana picha za viungo vya binadamu Kule Bunju,zimesambaa kwa Kasi Sana.

Mimi kinachonishangaza ni kwamba.. wewe unapokuta tukio kama hilo limetokea.. harakaharaka unachomoa simu na kupiga picha kisha unashea kwenye mtandao.. lengo lako ni nini hasa? Oke.. unataka watu waone.. ili iweje? wakishaona wafanye nini? Au inawasaidia nini? Suppose mmoja wa watakaopata picha hizo ni ndugu labda wa mhanga..? Atajiskiaje? Ah..!
 
miiko aka norms za picha sasa inatakiwa zifahamike si tu kwa waandishi wa habari, bali kwa wote hasa ukizingatia wingi wa mitandao ya kijamii na wingi wa simu zenye huo uwezo
 
Mandla JR vipi ndugu yangu mbona unaanzisha mjadala wako wa ushabiki wa ccm na chuki yako ya kijinga kwa Chadema hata bika kuelewa hoja iliyowekwa mezani. Mtoa hoja anazungumzia usambazaji wa picha kwa kutumia whatsap ambazo zina athari kijamii. Sasa wewe sijui umeathiriwa na siasa, unaona kila jambo baya inafanywa na chadema? Ukiendelea na mtizamo huo utakuwa mwehu kabisa. Jitahidi kuwa nutral bwana, huzi siasa zisikufanye uchukie kila mwanajamii, pia huo upande unaoutetea hawakujui hata jina, we fanya yako jitahidi kuwa raia mwema.
Back to topic; ni kweli hii tabia imekuwa kubwa sasa wakati mwingine mtu anakutumia picha zingine za matusi hadi unaogopa kufungua karibu na watu. Tujitahidi jamani kujidhibiti wenyewe. Hii kazi ya kutoa taarifa nibtaaluma za watu, wanahabari waliosomea wanajua wachuje nini na watujulishe nini. Sasa sikuhizi kwasababu ya mitandao ya jamii kila mtu anajifanya mwanahabari. Mtaharibu jamii kwa mikono yenu, chujeni taarifa.
 
Kwanini kuwa na namba ya mtu anayekuumiza?

Ndio maana nikasema wengine huwa tunafowadi bila hata kufikiria kama huyo unaemtumia atajiskiaje? Yaani ni kama tabia tu imejengeka kwamba ukifowadiwa kitu na wewe unafowadi fasta.. Na mara nyingi picha hizi tuna fowadiwa na watu wetu wa karibu tu ambao hatuwezi kufuta namba zao..
 
Mandla JR vipi ndugu yangu mbona unaanzisha mjadala wako wa ushabiki wa ccm na chuki yako ya kijinga kwa Chadema hata bika kuelewa hoja iliyowekwa mezani. Mtoa hoja anazungumzia usambazaji wa picha kwa kutumia whatsap ambazo zina athari kijamii. Sasa wewe sijui umeathiriwa na siasa, unaona kila jambo baya inafanywa na chadema? Ukiendelea na mtizamo huo utakuwa mwehu kabisa. Jitahidi kuwa nutral bwana, huzi siasa zisikufanye uchukie kila mwanajamii, pia huo upande unaoutetea hawakujui hata jina, we fanya yako jitahidi kuwa raia mwema.
Back to topic; ni kweli hii tabia imekuwa kubwa sasa wakati mwingine mtu anakutumia picha zingine za matusi hadi unaogopa kufungua karibu na watu. Tujitahidi jamani kujidhibiti wenyewe. Hii kazi ya kutoa taarifa ni taaluma za watu, wanahabari waliosomea wanajua wachuje nini na watujulishe nini. Sasa sikuhizi kwasababu ya mitandao ya jamii kila mtu anajifanya mwanahabari. Mtaharibu jamii kwa mikono yenu, chujeni taarifa.

Mkuu watu kama hao hapo juu dawa yao ni kuwachunia tuu..
Bahati mbaya sioni kitufe cha "like" hapo kwenye bold
 
Weka japo chache za mfano ili nasisi tupate kupima maoni yako.
 
mbona hamjadili picha za ngono mnazotumiana kwenye hizo Whats app ama hizo ni sawa.?


Picha za ngono wanatumiana wale wanaojuana wanapenda ngono. Si rahisi kumtumia mtu yeyote tu aliyoko kwenye simu yako maana ni za aibu na zinatumwa kiaibu aibu. Sasa hizi za mauaji mtu anatuma tuuuu kwa kigezo cha kutaka uone tu uovu unavyoenea bila kujali utazipokeaje... ile ya ubongo wa mtoto ulinifanya nisile dinner siku ile ... niliamua kulala tu.... iliniumiza sana TheChoji kwa kweli si matumizi sahihi. Idimi asante kwa ushauri wako... nitaweka kwenye status kabisa loooh
 
Last edited by a moderator:
whatsapp haijaweka limitation ya picha/video za kushea so walaumu wao,siye utuwache tujiachie
 
Kama hii?
 

Attachments

  • 20140717_223650.jpg
    20140717_223650.jpg
    7.1 KB · Views: 1,604
Binafsi sjaipenda hii ya msichana wa tarime aliyeunguzwa na moto sehemu za siri na mumewe, ni udhalilishaji jamani

Fanya kama nifanyavyo mie. Waambie hao watumaji kwamba hupendi picha za aina fulani (ziweke wazi), hivyo wasikutumie. Kama bado wanaendelea, simply block akaunti zao ili usizione kamwe!
 
Kweli zinaudhi sana,lakini nimepata somo kuwa hata madaktari wetu na manesi wa sasa wanakiuka sana maadili...picha ya huyo aliyechomwa na sururu inaonekana kabisa imepigwa ndani ya chumba cha upasuaji,sasa ni nani amezipiga kama sio madaktari/nesi?
 
Back
Top Bottom