Whatsapp na Mgogoro wa Familia

Whatsapp na Mgogoro wa Familia

Maisha bana ......

Dada pole kwa changamoto ambayo unakumbana nayo,hakuna changamoto ambayo inasumbua kama hii yako kwasababu iko pale ambapo unatarajia kutuliza misongo na vurugu za mawazo ambazo unaweza kuzipata mahali pengine,hapa panapokuwa ndio kikwazo maisha huwa magumu kidogo

Kwanza labda nianze kukuambia tu kuwa mumeo ameshindwa kutimiza jukumu lake kama baba na kiongozi wa familia anazoziongoza,baba unatakakiwa uwe mtu wa kuondoa matatizo kwenye familia na sio wa kuongeza matatizo kwenye familia,huyu wako inaonekana ni wa kuongeza matatizo badala ya kuyaondoa

Mumeo inaonekana kuna mambo mawili,huenda amekuchoka na ndio sababu ya kuacha yatokee yanayotokea na kama ukiamua kuondoka basi pakacha litakuwa limevuja na faida imekuwa kwa mchukuzi,nasema hivi kwasababu ni ngumu sana mtu kufurahia kuona mtu ambae aliapa kumlinda maisha yake yote awe ana huzuni kwenye mambo ambayo anaweza kabisa kuyaondoa,wakeze pamoja na mama yake wako chini ya himaya yake na anaweza kukemea na hayo yakaisha,lakini kwasababu hii ya kukuchoka [kama ndio sababu] anaamua tu kukuacha na utaamua wewe mwenyewe

Jambo la pili ambalo naliona hapa ni mumeo kuwa na malezi ya kipwani hivi,yaani hapa namaanisha kuwa amelelewa nae kuwa na tabia kama za kike za kupenda umbea na kupashana,huyo angekuwa huku usukumani kwetu tungemuona kama ana tabia za kike kabisa,sasa basi wewe unaona ni tatizo wakati mwenzako anaona ni kawaida tu,hapo kazi ipo sana tu,lakini pia inawezekana pia hajui hata daraka la mume kwenye familia ni lipi na mwanaume anatakiwa aweje hii nayo inasababishwa na malezi na kama ni hivi huyu kuwa sawa ni kazi kidogo

Sasa basi kwasababu hiyo kila jambo huwa lina namna yake ya kulitatua,kama mumeo ana tatizo la kwanza hapo unatakiwa ukague ni kwasababu gani amekuchoka na ukijua sababu naamini utajua cha kufanya,tatizo linaweza kuwa halijaanzia kwake [kama amekuchoka] bali limeanzia kwako na unashindwa kuliona kwasababu unatazama upande wake zaidi,chunguza na ukijua sababu utajua na na namna ya kufanya

Kama ana tatizo la pili la kulelewa kike hapo itakubidi umkubali kama alivyo kama misingi ya ndoa inavyoagiza na uwe unajitahidi sana kumpenda kwa namna alivyo,tafuta masomo ya utambuzi ujifunze namna ya kuishi na watu wa namna hiyo na utakuwa na amani na hata kusumbua,lakini pia kama utafanikiwa kujua namna ya kuishi nae taratibu utamvuta kujifunza namna ya kujitabua nae atabadilika tu

Kama atakuwa ni mt ambae ameathiriwa na malezi na kushindwa kujua majukumu yake utaweza kumsaidia kwa kumpenda zaidi na kuwa unajaribu kmuelekeza kwa upendo na utulivu nae atakusikia

Pole sana dada ....!!
 
Kwenye settings za WhatsApp kuna kitufe kimeandikwa "Mute".

Wewe bonyeza kitufe hicho kisha waache waendelee na maneno yao, wapoteze muda wao. Kwani wahenga walisema "Maneno matupu hayavunji mfupa!"

Mungu atakusimamia na mwisho huyo mume wako atajirudi mwenyewe.

Daima usibishane na mjinga!

Heko Mkuu mhem. Mwanahaki, wewe mtu kweli.... umemsihi vilivyo !! " Mungu akubariki uwe una advise hivyo " naima79 sikia eenh
 
Last edited by a moderator:
pole sana dada yangu kwa matatizo yanayokukuta, mm nakushauri ujitoe tu whatsApp ili ujaribu kupunguza hizo stress kwan bila
hata ya kutumia whasApp maisha yanaenda tuu..
 
Pole sana kwa yanayokupata maana kimbilio lako ndio huyo hajielewi.Kama vipi jiondoe whatsapp uendelee na message za kawaida kuepusha mengineyo maana mume mwenyewe ambaye angekuwa faraja kwako naye ndio hajielewi
 
Maisha bana ......

Dada pole kwa changamoto ambayo unakumbana nayo,hakuna changamoto ambayo inasumbua kama hii yako kwasababu iko pale ambapo unatarajia kutuliza misongo na vurugu za mawazo ambazo unaweza kuzipata mahali pengine,hapa panapokuwa ndio kikwazo maisha huwa magumu kidogo

Kwanza labda nianze kukuambia tu kuwa mumeo ameshindwa kutimiza jukumu lake kama baba na kiongozi wa familia anazoziongoza,baba unatakakiwa uwe mtu wa kuondoa matatizo kwenye familia na sio wa kuongeza matatizo kwenye familia,huyu wako inaonekana ni wa kuongeza matatizo badala ya kuyaondoa

Mumeo inaonekana kuna mambo mawili,huenda amekuchoka na ndio sababu ya kuacha yatokee yanayotokea na kama ukiamua kuondoka basi pakacha litakuwa limevuja na faida imekuwa kwa mchukuzi,nasema hivi kwasababu ni ngumu sana mtu kufurahia kuona mtu ambae aliapa kumlinda maisha yake yote awe ana huzuni kwenye mambo ambayo anaweza kabisa kuyaondoa,wakeze pamoja na mama yake wako chini ya himaya yake na anaweza kukemea na hayo yakaisha,lakini kwasababu hii ya kukuchoka [kama ndio sababu] anaamua tu kukuacha na utaamua wewe mwenyewe

Jambo la pili ambalo naliona hapa ni mumeo kuwa na malezi ya kipwani hivi,yaani hapa namaanisha kuwa amelelewa nae kuwa na tabia kama za kike za kupenda umbea na kupashana,huyo angekuwa huku usukumani kwetu tungemuona kama ana tabia za kike kabisa,sasa basi wewe unaona ni tatizo wakati mwenzako anaona ni kawaida tu,hapo kazi ipo sana tu,lakini pia inawezekana pia hajui hata daraka la mume kwenye familia ni lipi na mwanaume anatakiwa aweje hii nayo inasababishwa na malezi na kama ni hivi huyu kuwa sawa ni kazi kidogo

Sasa basi kwasababu hiyo kila jambo huwa lina namna yake ya kulitatua,kama mumeo ana tatizo la kwanza hapo unatakiwa ukague ni kwasababu gani amekuchoka na ukijua sababu naamini utajua cha kufanya,tatizo linaweza kuwa halijaanzia kwake [kama amekuchoka] bali limeanzia kwako na unashindwa kuliona kwasababu unatazama upande wake zaidi,chunguza na ukijua sababu utajua na na namna ya kufanya

Kama ana tatizo la pili la kulelewa kike hapo itakubidi umkubali kama alivyo kama misingi ya ndoa inavyoagiza na uwe unajitahidi sana kumpenda kwa namna alivyo,tafuta masomo ya utambuzi ujifunze namna ya kuishi na watu wa namna hiyo na utakuwa na amani na hata kusumbua,lakini pia kama utafanikiwa kujua namna ya kuishi nae taratibu utamvuta kujifunza namna ya kujitabua nae atabadilika tu

Kama atakuwa ni mt ambae ameathiriwa na malezi na kushindwa kujua majukumu yake utaweza kumsaidia kwa kumpenda zaidi na kuwa unajaribu kmuelekeza kwa upendo na utulivu nae atakusikia

Pole sana dada ....!!


Asante sana mkuu nimekuelewa vilivo ubarikiwe sana
 
Za siku wana MMU?

Ni hivi; kwa kifupi mimi na familia ya mume wangu hatuko vizuri sana kama mwanzoni, na hii yote imesababishwa na fitina ya mmoja wa mke wa mdogo wa mume wangu kuwa na mambo ya umbea, urongo na unafiki na anapenda kutupaka matope wake wenzake siku zote.

Kwa vile ni familia ya kusikiliza maneno, huwa wanampokea vizuri na wanamfurahia, sasa mimi sikulelewa katika maisha hayo nilichoamua kuwa mbali kidogo na maneno yao yaani ni pamoja na kupunguza sana visiting ya ukweni maana wenzangu wengine watatu wote wanakaa pamoja na mama mkwe yaani bado hawajaamua kutoka nyumbani.

Sasa nyumba imekuwa na matatizo, yaani wengine hapo hatufai kabisa na anaefaa ni huyo mwenye hulka ya maneno, hii imeweza kutujengea ukorofi kwa kila tunalolifanya liwe zuri liwe baya utaonekana mbaya tu mzuri ni huyo mmoja.

Tukija katika point ni hivi, mume wangu ame-create family group whatsapp. Hiyo group ni mipasho, manyanyaso na masimango tu, sio group ya kupeana taarifa muhimu. Kukiwa na shida ndani basi sehemu ya kukusemea ni katika group. Sasa jana ka-share hiyo picha hapo na ndugu zake wote wakawa wanaisupport na kuifurahia, na hiyo yote kwasababu pia hawanipendi na wananisemea vibaya kila siku japo nasikia ila nanyamaza kwa vile sitaki shari.

Mume wangu anafahamu hayo yote, mimi binafsi nimeona hii ni kejeli kubwa kwa sababu waliomo kwenye group ni watu ambao wanatamani nipate shida, watafurahia wakisikia nanyanyasika, watafurahia wakisikia nimeyumba.

Sasa kwa mfano ningeweka mimi picha labda inasema husbands are always selfish and cheaters, vipi yeye asingeona namdhalilisha? Na je, hii ndio kazi ya group ya familia? Nilishatoka katika hii group kwa vile yeye ni creator akanirudisha tena, sasa nashindwa kumuelewa ananilazimisha kukaa kwenye hii group ili kunipa stress?

Hivi wenzangu mnamtafsiri vipi mwanaume mwenye tabia hizi? Naona yuko tayari niwe stressed na yeye kwake ikawa burudani.

Naombeni mtazamo wenu, lakini nahisi maisha ya ndoa yananishinda maana hayana starehe zaidi yana stress.

======================

Hii ndio picha iliyotumwa kwenye hilo Group la Whatsapp:
attachment.php
View attachment 204120

Hivi?
Kipindi kile cha zile simu zenye mikonga, yalikuepo hayo?
Achana na smart4ne, Rudi kule kwenye vitochi,
Maisha bila stress mbona yanawezekana!
 
Nimeshajitoa katika hiyo group najua atanirudisha tena maana ana makusudio yake

Haya Sasa un-install whatssap application kwenye simu yako.simple like that utaondokana na kero..Au yeye ndio ana mamlaka na simu yako pia
 
Za siku wana MMU?

Ni hivi; kwa kifupi mimi na familia ya mume wangu hatuko vizuri sana kama mwanzoni, na hii yote imesababishwa na fitina ya mmoja wa mke wa mdogo wa mume wangu kuwa na mambo ya umbea, urongo na unafiki na anapenda kutupaka matope wake wenzake siku zote.

Kwa vile ni familia ya kusikiliza maneno, huwa wanampokea vizuri na wanamfurahia, sasa mimi sikulelewa katika maisha hayo nilichoamua kuwa mbali kidogo na maneno yao yaani ni pamoja na kupunguza sana visiting ya ukweni maana wenzangu wengine watatu wote wanakaa pamoja na mama mkwe yaani bado hawajaamua kutoka nyumbani.

Sasa nyumba imekuwa na matatizo, yaani wengine hapo hatufai kabisa na anaefaa ni huyo mwenye hulka ya maneno, hii imeweza kutujengea ukorofi kwa kila tunalolifanya liwe zuri liwe baya utaonekana mbaya tu mzuri ni huyo mmoja.

Tukija katika point ni hivi, mume wangu ame-create family group whatsapp. Hiyo group ni mipasho, manyanyaso na masimango tu, sio group ya kupeana taarifa muhimu. Kukiwa na shida ndani basi sehemu ya kukusemea ni katika group. Sasa jana ka-share hiyo picha hapo na ndugu zake wote wakawa wanaisupport na kuifurahia, na hiyo yote kwasababu pia hawanipendi na wananisemea vibaya kila siku japo nasikia ila nanyamaza kwa vile sitaki shari.

Mume wangu anafahamu hayo yote, mimi binafsi nimeona hii ni kejeli kubwa kwa sababu waliomo kwenye group ni watu ambao wanatamani nipate shida, watafurahia wakisikia nanyanyasika, watafurahia wakisikia nimeyumba.

Sasa kwa mfano ningeweka mimi picha labda inasema husbands are always selfish and cheaters, vipi yeye asingeona namdhalilisha? Na je, hii ndio kazi ya group ya familia? Nilishatoka katika hii group kwa vile yeye ni creator akanirudisha tena, sasa nashindwa kumuelewa ananilazimisha kukaa kwenye hii group ili kunipa stress?

Hivi wenzangu mnamtafsiri vipi mwanaume mwenye tabia hizi? Naona yuko tayari niwe stressed na yeye kwake ikawa burudani.

Naombeni mtazamo wenu, lakini nahisi maisha ya ndoa yananishinda maana hayana starehe zaidi yana stress.

======================

Hii ndio picha iliyotumwa kwenye hilo Group la Whatsapp:
attachment.php
View attachment 204120

Block to hlo group ndg yangu
 
Miss Chagga nimeshajitoa huko lakini najua atanirudisha tena, ila hii hali tu inanikwaza sana, yaani sijui niseme nini nieleweke lakini maisha ya ndoa yamekuwa magumu

Exactly naima79.. Maisha ya ndoa yanaambatana na changamoto nyingi sana.. Ukitilia maanani unaenda kuishi na mtu ambae ana tabia tofauti na zako.. Na ndo maana unapoingia kwenye ndoa unatakiwa uwe unajua toka moyoni mwako kwamba ndoa ni ndoano.. Uvumilivu ni tunu muhimu sana ndani ya ndoa.. Uwe unajitoa kila anapokuingiza ili kupunguza karaha kwako..
 
Last edited by a moderator:
Ngoja tumpatie mhanga hiki kiburudisho.
Pole mdada.

Digital wakae mbali na mambo haya
acha kabisa na Marijani Rajabu

Halafu kuna ile ya kuitwa uke wenza
 
Kuolewa na familia ya kiswahili shida tupu!!!!!!!!! pole sana...........

wajuzi wa ndoa watakupa ushauri
 
Kuna wanaume waswahili duniani kaaah!!
Pole sana mpendwa huyo kashikiwa akili wallah mbona hajielewi hajui umeacha familia yako, baba na baba, na ndugu zako wengine, mkaamua kuwa mwili mmoja as mume na mke leo hii akuona kama mpira anauchezea atakavyo, mungu amsamee bure maana iposiku atakuja kushtuka akutendeayo sio mazuri na hapo itakuwa too late
 
Mmmhhh
Wanaume wengine? majanga!!!!
Pole
Vumilia
Jitoe tena kwenye hilo group then mwambie kuwa hutaki kuwe na mipaka sometimes!!!!heegh
Kwani ndoa jehanam!?
 
Mmeo hana msimamo, tena hawezi kusimama yy km yy peke yake bila hao ndg zake, angalia anytime utasikia wamemtafutia mke mwingine, jiandae kisaikolojia dada'ngu
 
Back
Top Bottom