Asante my sijaongeanae kabisa kuhusu hiyo picha, nimeshaongeanae kuhusu vituko vya familia ni mtu wa kuitikia tu, yani like aaah basi, sijaona akichukua action yoyote, siongei nae sana mambo ya familia yake kwa kuhofu kuwa ataona siwapendi au vipi japo nina mengi ya kuongeanae
Okey my dear,pole kwanza kwa kuumia,pili usiogope huyo ndo mumeo huwezi jua kasimama vipi bila kuongea naye,umesema huwa anaitikia tu usijali wanaume ndivyo walivyo siyo wepesi sana katika kutoa judgement hupenda kujiridhisha kwanza ndipo afanye maamuzi.
Unahitaji muda sana kumsoma mumeo,kwasasa naomba nisimjudge vibaya mumeo,umesema huwa anapokea malalamiko yako anaitikia tu ni dhahiri hata wewe hujajua huwa inamgusa au haimgusi,na yeye hajataka kujidhihirisha kwako yupo upande gani(hii ni tabia ya wengi)lets think positively kabla ya kurusha mawe,nikiangalia jicho la tatu naweza sema mumeo yuko kwenye uchunguzi na hiyo group kaiweka kimakusudi kabisa na ndo maana mara ya kwanza ulivyojitoa alikurudisha ana sababu zake anataka kujua yeye mwenyewe kati yenu ninyi wote mkorofi ni nani, hata hiyo picha kaiweka kimtego aone ndugu zake watarespond vipi na wewe je utalichukuliaje hilo. Huyo yupo kiupelelezi zaidi.
Cha kufanya mumy take it positively waache wajifangulue weeee wewe kaa kimya tu wakuongea naye ni mumeo,najua imekuuma lakini jikaze mumy kaa na mumeo tena ukiwa katika mood nzuri naye yuko vizur ongea bila jazba muulize kwa upendo alimaanisha nini kuweka hiyo picha kadri anavyokujibu maswali yako yambane kulingana na majibu yake lakini jicontrol sana usipandishe hasira,hiyo atleast itakupa mwangaza kujua mume naye yuko upande gani.
Kuhusu wakwe na hao wake wenzako wala usishindane nao uzuri wewe hauko nyumba moja nao pengine nayo ni sababu wanakuonea uwivu,wanatamani hata waume zao wangefanya hivyo sasa wanashindwa iliyobaki ni kufanya vita nawe,mume wako anakupenda na anakujali sana na anapenda uwe safe ndo maana hakuona ulazima wa yeye kuendelea kuwa nyumbani kwao.
Mambo mengine mydear hayaihitaji ulalamike sna bali uonyeshe action,utaheshimiwa na kuthaminiwa kwa matendo yako,ili upate heshima hiyo kuna kamsoto fulani kwa kudharauliwa lazima ukapitie,wafundishe wakwe na wake wenzako upendo,wafundishe kwamba wewe si wa mambo ya umbea kwa yeyote yule atakeyukuja kwako hata awe mnapatana,endelea kuwakarimu usisubiri asante yao wala hata kusifiwa maana makubwa yatakukuta,tenda wema nenda zako.
Naongea haya sababu nimeshayapitia mumy siongei from nowhere,ajishushae atakwezwa na ajikwezae atashushwa,tunza ndoa yako mama utaona mafanikio kila mmoja atakupigia salute,nina yangu mengi nikihadithia ntajaza ukurasa.