MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 793
siko hapa kubishana kisiasa kama hakuna mantiki tupotezee kwa herini naondoka zangu.
nauliza tu hivi halima mdee ameshaolewa?
kama unaweza kunirudishia fedha yangu ndio inafanya niseme hayo ardhi naweza kupata popote lakini hakuna fidia kwa ujanja janja. Kauli ya Halima Mdee ingekuwa na mwongozo yeye ni mbunge wa wote bila kujali chama so far sheria inamtambua hivyo.
nauliza tu hivi halima mdee ameshaolewa?
Hivi Harima mdee ndio nani tena?
Mimi siwasemei wengine hii ni shida yangu na wananchi walioomba nipaze sauti kwa niaba yao kule Madele.
Bado Kesi iko mahakamani lakini tumebomolewa nyumba na kunyang'anywa ardhi tulitegemea mbunge ungekuja kusaidia namna ya kutafuta haki mahakamani lakini uko kimya. Wananchi masikini wamefungua kesi lakini kabla ya hukumu tumeondolewa kwa nguvu.
siko hapa kubishana kisiasa kama hakuna mantiki tupotezee kwa herini naondoka zangu.
Nilikuwa na imani kuwa wabunge wa upinzani ni wabunge mbadala. Mimi ni mmoja wa waathirika wa bomoa bomoa ya Madale ambayo kuna kila aina ya ujanja ujanja lakini tangu tupate matatizo hayo sijawahi kuona mbunge wangu HALIMA MDEE akisema lolote au hata kuwatembelea waathirika kujua shida zao na namna ya kuwasaidia kwani ni wapiga kura wake.
wapo wanaolala nje hadi sasa, wapo walionyang'angwa ardhi kwa nguvu ya fedha lakini Halima ambaye ni mjumbe wa baraza la madiwani la Kinondoni nilitegemea angekuwa na kauli ya kutueleza wananchi tulioathirika na bomoa bomoa hiyo katika eneo la Madale nakalekwa, madale tuaroho na madale nakasangwe. Ni zaidi ya mwezi sasa tangu kupita kwa bomoa bomoa hiyo.
Halima anajua ukweli kwa sababu yuko kwenye vikao vya manispaa ya kinondoni lakini pia niliambiwa kasomea sheria ( i stand to be corrected) ni sheria ipi inaruhusu kumnyang'anya mwananchi aliyekaa eneo kwa miaka kumi bila kuendelezwa hao wamiliki halali akina Michael Chacha na wenzake walikuwa wapi miaka yote. Sheria inatoa miaka mitatu tu kwa ardhi ambayo haijaendelezwa kunyang'anywa au kuwa mali ya yule anayelindwa na sheria hiyo kwa maana kwamba kama mwananchi ameishi hapo kwa zaidi ya miaka mitatu bila mmiliki halali kutokea sheria inatambua na kumpa umiliki yule aliyopo kwa wakati huo.
My take: Halima Mdee acha kukimbilia kigamboni kuwalilia wananchi wake kutokakana na hofu ya mji mpya anza na jimbo lako. Bado tunakusubiri uje kuongea na sisi wananchi wa Madale ingawa umechelewa.
source: Mimi mwenyewe nilikuwa na kiwanja cha nusu heka Madale.
Mbunge wangu wa kawe kupitia chadema
Kwa hao waliokutuma kawaambie wamebomolewa kwa mabavu kutokana na kiranga chao cha kuiweka serikali lege lege na dhaifu madarakani. Wewe hatuna cha kukushauri kutokana na kuujua ukweli ulivyo ila unafanya makusudi kulitumia vibaya jina la Mdee kisa ni mbunge wa Chadema. Hiyo amri ya nyie kubomolewa aliitoa Mdee au imetoka serikalini? Kabla ya kumlaumu Mdee, serikali imefanya lolote kuwasaidia msibomolewe?........................Mimi siwasemei wengine hii ni shida yangu na wananchi walioomba nipaze sauti kwa niaba yao kule Madele.
hebu tuongee ukweli wakuu,Mh Halima Mdee yuko wapi??naombeni jibu hapo,vilevile tunaomba record ya utendaji kazi jimboni mwake,tusiwe tunabisha kila hoja inayoletwa hapa bila kuwa na ushahidi!