What happens, sielewi..!

What happens, sielewi..!

Mkunde Original wewe ni katika wale wanawake wasiokuwa na shukrani kwenye ndoa na mwisho wa siku huwa mnaishia kwenye majuto.
 
Umeeleza vizuri everlenk, it's a lifetime commitment na sio vinginevyo, ups and downs lazima ziwepo vile hamna mkamilifu lakini inabaki kuwa ndoa na lazima wanandoa waiheshimu.

Kwani hata kama ni life commitment....mtu huwezi kuchepuka na ndoa ikaendelea?

Mbona watu kibao tu, wake kwa waume, kila siku wanachepuka na ndoa zao bado zipo hai......
 
Kwani hata kama ni life commitment....mtu huwezi kuchepuka na ndoa ikaendelea?

Mbona watu kibao tu, wake kwa waume, kila siku wanachepuka na ndoa zao bado zipo hai......


Ukichepuka umeweka viraka ndani ya ndoa, it will never be the same again hata ufanyeje. Unasikia scenario kibao humu, mtu anakiri kabisa kuwa anaishi kwa ajili ya watoto, hapo kuna ndoa tena...?
 
Kwani hata kama ni life commitment....mtu huwezi kuchepuka na ndoa ikaendelea?

Mbona watu kibao tu, wake kwa waume, kila siku wanachepuka na ndoa zao bado zipo hai......

Zinakuwa hai ila hoi bin taabani
 
Ukichepuka umeweka viraka ndani ya ndoa, it will never be the same again hata ufanyeje. Unasikia scenario kibao humu, mtu anakiri kabisa kuwa anaishi kwa ajili ya watoto, hapo kuna ndoa tena...?

Hahahaaaa duuh basi ndoa nyingi sana zina viraka aisee. Manake si wanawake si wanaume...wote wanachiti kwa kwenda mbele.

Na hiyo yote ni kwa sababu si kawaida kwa binadamu kuwa na sex partner mmoja tu. Hatukuumbwa hivyo lakini tunataka kulazimisha na ndo maana humu watu walio kwenye ndoa mfu ni wengi.
 
Hahahaaaa duuh basi ndoa nyingi sana zina viraka aisee. Manake si wanawake si wanaume...wote wanachiti kwa kwenda mbele.

Na hiyo yote ni kwa sababu si kawaida kwa binadamu kuwa na sex partner mmoja tu. Hatukuumbwa hivyo lakini tunataka kulazimisha na ndo maana humu watu walio kwenye ndoa mfu ni wengi.


Ni kweli, ndoa nyingi zinatumia life supporting machine, manake mda wowote zinakufa. Lakini hilo halifanyi niamini kuwa niliumbwa kuwalala wanawake tofauti kila nitakapo. Haya ni madhaifu tu ya bin adam, sikubaliani na usemi wa "cheating is inevitable" kama ambavyo wengi wetu tumeuhalalisha.
 
Hilo la life commitment ni la kufikirika zaidi kuliko uhalisia wenyewe.

Wanandoa kibao tu wanatoka nje ya ndoa zao.

Kubaki na mtu mmoja milele ni ngumu mno...kwanza naona kama vile haiwezekani.

At some point utataka tu kuonja mwingine.

Ni uhalisia kabisa na tunaishi kwazo.......

Inawezekana iwapo tutaweka tamaa nyuma na kulidhirika na tulichonacho.

Tamaa ipo siku zote na halikwepi ila kinachotakiwa ni kuitiisha tamaa,utajikuta kila siku utajitahidi kutafuta utoshelevu wa nafsi ifurahi kwa kuonja hapa na pale mwisho utajikuta ni nafsi tupu isiyo na furaha yenye majuto ndani yake.

Kutamani kupo kabisa pamoja na vishawishi kibao ila tunapaswa kuvishinda na unapokuwa unamfikiria mwenzako zaidi kuliko wewe mwenyewe hakika unashinda.

Utashangaa haya mambo yalivyo mfano mwanaume au mwanamke ni mchepukaji sana siku akimfuma mwenzie live atahuzunika sana na itamuuma mno kwanini mwenzie kamsaliti, kinachomuuma ni nini wakati yeye naye anamsaliti? Kuna siri kubwa hapo.
 
Wakati mwingine ni vizuri kupeana likizo, yeye akuruhusu na wewe umruhusu, wazungu wanaita Open Marriage, japo mwezi mmoja mtaona tofauti!
 
aisee ukisikia ana mtu nje au anataka aoe tena utamlaumu au? unajua maana ya kuoana kuwa mwili mmoja? unajua mahitaji ya mwanaume.....? nenda kaombewe kwa kuwa si kawaida au kama uko busy na mipango yako go ahead ila outcomes usijiblame.....psychological side effects labda ..we don knw
 
Uzi unatuhusu huu, huoni Eli79 kakubali kuchepuka kidogo ili aweke mambo sawa, sasa sijui akinogewa namfanyaje!

Kuna namna kwa huyu Eli79 najikuta sikubali matokeo. Halafu wax anakaa fungu gani? Manga ML kesho anavunja jungu naye sijui atakaa wapi? Mmmmhhh!!! Niishie hapa nisikuweke hadharani....lol
 
Last edited by a moderator:
Mkunde Original kuna wanawake wengi sana wanatafuta mtu wa kuwafanyia hayo unayoyaona kero lakini hawapati. Siku akichoka kukufanyia na wewe ndio kwanza umeamka kutoka usngizini ndio utajua alikuwa anajisikiajje. Usijitafitie upweke mwenyewe.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom