Holla,
Msimu wa sikukuu za Christmas na Mwaka Mpya ndo umeingia.
Sijajiunga na kifurushi chochote cha kimiminika ila nasikia tuu ulimi unataka kutereza kimalkia. Ngoja nishindane nao, ila kichwa cha uzi kitabaki hivyo hivyo, laah nikifika mwisho naweza kubadili lugha.
Haya twende pamoja...
Utamaduni wa kimagharibi leo tarehe 23 November wanaita Black Friday yaani Ijumaa Nyeusi. Hii ni mahsusi kwa wafanyabiashara wanaouza vitu kushusha bei ya bidhaa zao ili kuwapa nafasi watu wenye uwezo wa chini/ mdogo kununua vitu kwa ajili ya wapendwa wao kama zawadi ya Christmas.
Akina sie tuliobahatika kuishia modern nursery school za wakati ule wa mkoloni tunafundishwa na Waingereza wenyewe, hadi lafudhi tuliipata ya Kiingereza sema baada ya darasa la nne ndo ikawa basi tena shule ikaishia hapo ila si haba ulimi bado unatereza utasema nimepitia Cambridge kumbe grade four, aahahahahaaa!
Tulishasikia kuhusu hii Black Friday yote ikiwa na lengo la kusambaza upendo during the Festive Season.
Kasie Matata mie maneno mengii ngoja nipunguze, turejee kwenye lengo la uzi.
Sasa leo nilienda duka moja hivi nao walikuwa na punguzo la bei za bidhaa zao si haba nikapata wasaa wa kujinunulia vitu ntavyovihitaji wakati wa Christmas.
Nikiwa nazunguka kwenye mashelf ya hizo bidhaa nikakumbuka wana JF, siko tajiri, sina uwezo sanaa wala sina pesa ya ziada ambayo haina matumizi ila, ningependa pale ulipo unaposoma uzi huu useme...
Ni kitu gani unatamani ungekipata au ungekuwa nacho kipindi cha Christmas ya mwaka huu 2019, ambacho kiko nje ya uwezo wako kukipata?! Huwezi jua naweza kuwa Granny Christmas to you au memba yeyote humu JF...
Taja kile kitu kweli unahitaji na si kuwa ni mie tuu ndo ntakupatia hicho kitu, kupitia huu uzi anaweza akaja mtu mwingine ana hivyo vitu vya ziada akagawana na wewe au akavinunua mahsusi kwa ajili ya uhitaji wako na wote tukajikuta tunasherehekea Christmas kwa tabasamu.
Sambaza upendo, eneza amani kipindi hiki cha msimu wa sikukuu za Christmas na Mwaka Mpya.
Mie nshapamba mti wa Christmas, wewe je?
Wishing all MMU members a Merry Christmas and Happy New Year 2020 mmuuah!!
Mahaba matata kwa Captain.
Kasinde.