Wezi wenye 'leseni ya kukuibia' Kariakoo

Wezi wenye 'leseni ya kukuibia' Kariakoo

Hivi huko Dar hamjui kutumia panga, yaani mulisya anakuibia unaona kwanini usimkate panga la makalio.
 
Nadhani kabla ya kununua simu si unapaswa uingie kwenye ile ‘about device’ uone ni aina gani au?
 
Unaandika under assumption kila mtu anajua hilo
Kama hujui sinu unapoenda kule bora umshirikishe mtu mwenye uzoefu mana hata ukisema ununue ipo kwny boksi maboksi mbona yapo tu yanatengezwa mzigo unaekwa...

NB
UNAPOENDA KUNUNUA SIMU KULE EPUKA SANA YALE MATOLEO YA SIMU YALIYOTOKA MIAKA MITATU NYUMA MFANO SAMSUNG S8 2017, SAMSUNG S9 2018, IPHONE 7, 8,6 HIZI SIMU USIJE ENDA POPOTE HII 2020 UKADANGANYWA NI MPYA.
 
Unaandika under assumption kila mtu anajua hilo
Okay, ila ndio tunajuzana sasa, though seems quite obvious, maana simu ni computer siku hizi, lazima uingie kuona details kama unavyokagua RAM, OS, Storage, Resolution ya PC kabla hujainunua
 
Kama hujui sinu unapoenda kule bora umshirikishe mtu mwenye uzoefu mana hata ukisema ununue ipo kwny boksi maboksi mbona yapo tu yanatengezwa mzigo unaekwa...

NB
UNAPOENDA KUNUNUA SIMU KULE EPUKA SANA YALE MATOLEO YA SIMU YALIYOTOKA MIAKA MITATU NYUMA MFANO SAMSUNG S8 2017, SAMSUNG S9 2018, IPHONE 7, 8,6 HIZI SIMU USIJE ENDA POPOTE HII 2020 UKADANGANYWA NI MPYA.


Hebu panua upeo wako..

Watu wangapi wanaenda kkoo kila siku?
Wageni wangapi kutoka nchi jirani??

Nini maana ya Duka na mtu kupewa leseni ya biashara??

Unafikiri nimeandika hapa kulalamika?

Nimeandika hapa ili wanaohusika na policies
Waone ...kuanzia polisi hadi wizara ya biashara na taasisi zingine...

Kunahitajika mabadiliko makubwa kudhibiti
Hizi organised crimes..

Sijui hata kama umenielewa
 
Okay, ila ndio tunajuzana sasa, though seems quite obvious, maana simu ni computer siku hizi, lazima uingie kuona details kama unavyokagua RAM, OS, Storage, Resolution ya PC kabla hujainunua

Simu kama ni LG mfano
Na huijui umeiona Tu ukavutiwa
Nayo ukakuta ndani kila kitu kiko sawa
Ni 4g .. storage size sawa n.k
Kumbe ule utumbo ni itel.
Wameweka covers za juu na box Tu ndo LG..

Nakupa mfano mmoja..

Je ambayo ni used na sio mpya??Kila kitu Sawa lakini kumbe used hujui??
 
Derikali ikichukua hatua mnasema ni ya kidikiteta. Watanzania sijui waganyiwe lipi ili waridhike.
Kuna mengi yanasononesha kwenye hii nchi polisi vituo vyote Tanzania nzima kumejaa rushwa lakini serikali Ni Kama vile haioni huu mchezo
 
Simu kama ni LG mfano
Na huijui umeiona Tu ukavutiwa
Nayo ukakuta ndani kila kitu kiko sawa
Ni 4g .. storage size sawa n.k
Kumbe ule utumbo ni itel.
Wameweka covers za juu na box Tu ndo LG..

Nakupa mfano mmoja..

Je ambayo ni used na sio mpya??Kila kitu Sawa lakini kumbe used hujui??
Hapo kwenye used ndio shida
 
Ukitaka kitu OG nenda kwa maduka makubwa Kama n simu nenda maduka ya mitandao ya simu au maduka ya kampuni husika na hakikisha risiti ya EFD unayopata inasoma tarehe na muda husika ulionunua bidhaa.

Nenda maduka makubwa sikuhizi maisha magumu Bei zinatofautiana 20-10 alafu kule unanunua bila jasho
 
Jamani na mm nilishapigwa hapohapo maduka yanayotizamana na Shule ya Uhuru nikawaonesha risiti ya Jina la Duka wakanikatalia kabisa
Hawa wauzaji wao wana simu aina nyingi sasa mm nikaletewa aina mojawapo inaitwa Bundy kwa manjonjo na promotion ya kupewa fulana na Betri wakadai niwape 250,000/
wanapenda kukaa kwenye Noah kwenye choo cha kulipia kule Samora baada ya Clock Tower tumebishana wakashuka hadi 175,000/ fulana na Betri wananinyang'anya eti wanatangazia.
Jamani nusu saa hamna kitu simu haina Network, kwa vile nina risiti iliyoelekeza kuwa wapo Plot na Block mitaa ya Uhuru nikaipata, Boss akaniruka nikajua nimepigwa
Baada ya mwezi nikawaona tena wapo Dodoma mitaa ya Nyerere square, wakanivaa na uongo wao basi kwa hasira nikawakoromea na kuwaonesha imeo chao cha Bundy tena imekufa kabisa,
wakaniomba msamaha wakalala kona na mm nikawaambia bora wafungashe naifuata risiti nikawakamate.
Nashangaa mpaka leo bado wanaziuza tu na hawakamatwi
Jamani simu tununue maduka ambayo unaweza hata kuirudisha ukabadilishiwa
Tahadhari na wizi huu. Aina za simu ambazo wanaziuza hata hazieleweki. Kuna simu zinaitwa VITU na K-mouse. Wanawatumia mabinti kufanya uhalifu huo. Ukinasa tu umeumia.

Bei zao ni shilingi 250,000 lakini huwa zinapoa kwa makubaliano. Wanadanganya kwamba wanafanya promotion na pia wanakuahidi kupata zawadi ya T-Shirt.

Utaambiwa uchague kikaratasi ambacho kimeandikwa aina ya zawadi utakayopewa. Nilinasa kwa zile aina ya VITU lakini walivyorudi na K-mouse niligoogle na kugundua nini nilikuwa kinaendelea.

Wanapendelea kukaa maeneo yaliyo karibu na benki na wapo tayari kukusubiri utoe fedha ya malipo. Pia wanakubali malipo ya fedha kwa njia ya mitandao. Tahadhari kabla ya hatari.
 
Kizamani ile Eti unamkopesha mtu akikataa kulipa unataka kwenda polisi kushtaki, upuuzi huu siku hizi polisi hawa muda na kesi za kijinga kama hizi oooh nimeuziwa mchee wa sabuni,
Mimi niliuziwa simu feki na nikapewa risiti feki yaani sio ya duka hilo. Nilienda polisi na muuzaji alikamatwa, na pesa aliirudisha sasa unaposema eti hawasikilizi hizo kesi cjui nikueleweje!!

Mind you sikuhonga hata senti tano!!! Ni haki ya kisheria kuripoti crime yoyote polisi ila eti kesi ya madai unaita ya kipuuzi!! Ssa kesi gani watapokea?
 
Mkuu wizi na utapeli ni kila kona na mamlaka hazijaamka. Kuna wauza magari wengi matapeli na wana show rooms utafikiri ni watu wa maana kumbe wahuni tu.

Kuna uhuni dawa yake ni kudeal nao kihuni tu maana sheria haitokusaidia kuna mapungufu mengi.
Eeeh Yani unateka ata wawili mnaenda kuwatawazisha mafuta ya kula ya uvuguvugu...Yani lazima wakasimuliane
 
Back
Top Bottom