Wezi wenye 'leseni ya kukuibia' Kariakoo

Wezi wenye 'leseni ya kukuibia' Kariakoo

Mm sim nanunua maduka yanayoeleweka kama Mlimani City pale au mara nyingine naagizia toka nje ya nchi.

Japo zamani nilinunua sim duka la Airtel Mcity nikapata ka usumbufu upande wa softwate wakanambia nipeleke science nikatengenezewa bure .Ila kariakoo sinunui simu japo mm ni mtoto wa DsM .

K/koo kuna mambo ya kishenzi sana pale tena siku hizi wamepunguza sana.
Mkuu sayansi kuna mafundi simu wa kueleweka?
 
Jamani na mm nilishapigwa hapohapo maduka yanayotizamana na Shule ya Uhuru nikawaonesha risiti ya Jina la Duka wakanikatalia kabisa
Hawa wauzaji wao wana simu aina nyingi sasa mm nikaletewa aina mojawapo inaitwa Bundy kwa manjonjo na promotion ya kupewa fulana na Betri wakadai niwape 250,000/
wanapenda kukaa kwenye Noah kwenye choo cha kulipia kule Samora baada ya Clock Tower tumebishana wakashuka hadi 175,000/ fulana na Betri wananinyang'anya eti wanatangazia.
Jamani nusu saa hamna kitu simu haina Network, kwa vile nina risiti iliyoelekeza kuwa wapo Plot na Block mitaa ya Uhuru nikaipata, Boss akaniruka nikajua nimepigwa
Baada ya mwezi nikawaona tena wapo Dodoma mitaa ya Nyerere square, wakanivaa na uongo wao basi kwa hasira nikawakoromea na kuwaonesha imeo chao cha Bundy tena imekufa kabisa,
wakaniomba msamaha wakalala kona na mm nikawaambia bora wafungashe naifuata risiti nikawakamate.
Nashangaa mpaka leo bado wanaziuza tu na hawakamatwi
Jamani simu tununue maduka ambayo unaweza hata kuirudisha ukabadilishiwa
Hawa walinitapeli mwaka jana Samora Avenue mkabala na maktaba ya British Council. Waliniuzia simu mbovu aina ya Vituz kwa 250,000 na t-shirt ya bure. Wanatembea na Noah.
 
Polisi kumejaa rushwa
uwezo wapolisi wengi kutafakuri ni zero
Mkuu inabidi tuanze na hawa jamaa wa k/koo na mizizi ya polisi wachafu wanaochafua jeshi letu

Siku watakapokagua vyeti vya shule vya Polisi wetu ndipo litageuka na kuwa safi vinginevyo ni kutwanga maji kwenye kinu
 
Ile safisha vyeti fake ilipaswa kupita huku pia. Naamini Polisi wa Tanzania ni moja ya corrupt organization, na wameshaona hawana la kufanywa. Ushauri wangu, Jeshi la Polisi lisukwe upya.
Haitoshi kulisuka upya bila kuboresha mishahara yao! Mishahara midogo wanayopata nadhani ndiyo inawafanya wapokee rushwa kirahisi ukizingatia na kazi wanazofanya ambazo nyingine ni hatarishi.
 
Jukumu la mwananchi wa kawaida ni tu ku report crime imetendeka,

Sio kwamba leo amelizwa aende TBS..

Kesho aende tena police..

NO!

Police wana wajibu, to work cooperatively na other Agencies,kuhakikisha uhalifu hautendeki,na kama umetendeka na kuwa reported kwao..then wawajibike kuchunguza by involving other agencies wanaoweza kusaidia investigation...period,

Simply usiwatetee, police hawajui wajibu wao katika kumlinda mwananchi...
Wanajua wajibu wao ila hawataki kufanya kazi.
 
Jamani na mm nilishapigwa hapohapo maduka yanayotizamana na Shule ya Uhuru nikawaonesha risiti ya Jina la Duka wakanikatalia kabisa
Hawa wauzaji wao wana simu aina nyingi sasa mm nikaletewa aina mojawapo inaitwa Bundy kwa manjonjo na promotion ya kupewa fulana na Betri wakadai niwape 250,000/
wanapenda kukaa kwenye Noah kwenye choo cha kulipia kule Samora baada ya Clock Tower tumebishana wakashuka hadi 175,000/ fulana na Betri wananinyang'anya eti wanatangazia.
Jamani nusu saa hamna kitu simu haina Network, kwa vile nina risiti iliyoelekeza kuwa wapo Plot na Block mitaa ya Uhuru nikaipata, Boss akaniruka nikajua nimepigwa
Baada ya mwezi nikawaona tena wapo Dodoma mitaa ya Nyerere square, wakanivaa na uongo wao basi kwa hasira nikawakoromea na kuwaonesha imeo chao cha Bundy tena imekufa kabisa,
wakaniomba msamaha wakalala kona na mm nikawaambia bora wafungashe naifuata risiti nikawakamate.
Nashangaa mpaka leo bado wanaziuza tu na hawakamatwi
Jamani simu tununue maduka ambayo unaweza hata kuirudisha ukabadilishiwa


Tanzania kuna vituko sana kuanzia hao wauzaji hadi wanunuaji. Utanunuaje simu imeandikwa bundy (Bundi?) Ulisikia wapi?
 
Hii nchi viongozi wameishalemaa hadi haki itendewe ni eti namba moja hadi aseme, wengine wote ni kama wapo kwenye usingizi wa pono
 
Nimeuza simu Kkoo kwa zaidi ya miaka 5 kwa alichokisema mtoa mada ni kweli mtupu na tatizo ni watanzania kupenda vitu bei rahisi kwa Kariakoo asilimia 90 ya smart phone zinazouzwa ni used na za wizi.
Na unaweza ondoka Kkoo endapo ukiwa mkuda au kutokula pamoja na aliowataja mtoa mada.

Ushauri wangu unapoenda kununua simu Kkoo mwambie akupe simu ambayo iko ndani ya boksi ambalo halijafunguliwa na ujiridhishe kuwa imei iliyopo kwenye simu na na boksi ziko sawa.
 
Watu mkija kariakoo mje na wazoefu, sisi tunajua michezo yao yote tena hata mafundi simu wanawapiga sana dada zetu hasa wale wenye wameweka miamvuli kwa nje aisee, utawaonea huruma ila unakausha ndio maisha
Kweli mkuu, wale jamaa ukiwaachia simu imekula kwako hadi baadhi ya vifaa wanaiba wanakuwekea feki
 
Kwa brand kama LG au Sony wakikuwekea
Ndani itel huwezi jua kama sio mjanja

Ni wezi sana sana hapo kkoo na polisi wanajua kila kitu
ohoo hii balaa ... Sasa utafaham baada ya kufungua cover au hata kwa kuiangalia tu mkuu! Maana ni ngumu sana kupigwa kwa namna hiyo labda simu kama hautoiwasha hapohapo mbele yao. na kila brand ya simu ina namna yake ya ku display once inapokuwa ON
 
Mkuu nakubaliana na wewe kabisa, kuna kisa kingine ngoja nikiweke hapa, kuna jamaa mmoja alinunua iphone kwenye duka fulani k/koo pia na risiti kapewa kila kitu sasa ile simu ametumia kitambo tu sasa hivi juzi juzi kapigiwa simu na polisi kuwa anatuumiwa kwa kununua simu ya wizi jamaa akawauliza ni nani uyo anasema hii ni simu yake polisi hawana cha kusema sasa kesi imeenda hadi jamaa akawaambia polisi twendenj niwapeleke dukani sasa cha ajabu walivyofika k/koo walikuta lile duka limefungwa jamaa mwenye iPhone akijaribu kumcheki mwenye duka aeleweki sasa kumbe jamaa mwenye iPhone akagundua kuna mchezo mchafu unaendelea kati ya muuza duka na polisi, wito wangu kuweni makini sana na hawa wauza simu haka kamchezo sio powa kabisa watu wanalizwa wengi sana
Wabongo ni tatizo kubwa sana, kwanini msiende kununua simu kwa wahindi au mlimani city.
 
Mimi niko mbali kweli kwenye maisha yenu ya kula vumbi la mavi..yaani mbali mno....
Inaonekana nyie wote mazwazwa mmepigwa na hamtaki kuambiwa ukweli
Unaleta utopolo wako hapa Jf, na ushaambiwa leta vielelezo ndio polisi watahusika
Kizamani ile Eti unamkopesha mtu akikataa kulipa unataka kwenda polisi kushtaki, upuuzi huu siku hizi polisi hawa muda na kesi za kijinga kama hizi oooh nimeuziwa mchee wa sabuni,
Ndio maana nakwambia Nyie Dawa yenu nikusomewa visomo na kufukiwa mbuzi mzima ili uoze utumbo.


Unafurahia kula hela za wanaume.
 
Back
Top Bottom