Wezi wa BoT - EPA warejesha bilioni 50 hadi leo

Ili kurudisha mali ya wizi, ni lazima kwanza kukubali umeiba. Sasa kuna aliyekubali kaiba?

Mkulo anadai wamekamata nyumba ndani na nje ya nchi. Nchi zipi? Kwanini hata hizo nchi ziwe siri? Na nchi moja "inakamataje" nyumba ndani ya nchi nyingine? Tanzania haiwezi "kukamata nyumba" Marekani.

Tukumbuke vile vile serikali imekataa kuchunguza wizi kwenye akaunti zilizobaki BoT. Mtu unaambiwa kuna aliyeiba kwenye nyumba, unatazama chumba kimoja unakuta kweli kuna wizi, kisha unakataa kuangalia vyumba vilivyobaki? Kuna kitu unaficha. Umeiba mwenyewe?

Mkulo aache usanii wa hali ya chini namna hii.
 
Back
Top Bottom