Wezi wa BoT - EPA warejesha bilioni 50 hadi leo

Jamani mnisaidie mimi sijaelewa. Mabillion yakirudishwa what next? Is it the end of the story au ndiyo Tz inabadili sheria ya wizi!!!Sijui kule Keko, Segerea, Ukonga na magereza mengine wanasemaje!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kwanza hawa wezi wetu sijui kwanini tunawabembeleza warudishe hela tena kimyakimya, sheria zipo na hiyo kamati imeagizwa kutumia sheria zilizopo na madaraka yao kuhakikisha siyo kubembeleza kuwa pesa zilizoibiwa zinarudishwa! Kwa mantiki hiyo hakuna haja ya kuwasubiri na kuwabembeleza warudishe hela unless ndio danganya toto inaendelea, wewe mwizi wako unamjua eti unambembeleza arudishe alichokuibia wakati uwezo wa kumsweka ndani na kupata mali yako pamoja na kumwadhibu unao! Haiingii akilini kabisa! Wadanganyika tumeliwa! Mafisadi hapo wametufunga goli, yaani tumepigwa kanzu halafu tobo!!
 
Kitu walichofanya hao waliochota pesa EPA ni uhujumu wa uchumi hivyo wanatakiwa wakamatwe, mali zao zote pia zikamatwe kisha kibano mahakamani. Hii ndivyo wafanyavyo kwenye nchi ambazo zimeendelea bila kujali una-rank gani katika system au tycoon mkubwa kiasi gani. China huwa mjadala unafungwa kwa hukumu ya kifo, America and nchi za ulaya ni kifungo lakini Africa unarudisha fedha tena bila aibu unaendelea kuvinjari mitaa kwa nafasi tu na respect! Mabadiliko makubwa yanahitajika kwa nchi zetu za Afrika na mtazamo wetu katika kuhakikisha serikali inawajibika ipasavyo kwa wananchi na si kwa watu wachache tu. Kwa sasa ni kama serikali yetu ni ya wateule fulani na wao ndio wana maamuzi ya kila kitu. Mwanaharakati mmoja alishawahi kusema inabidi wananchi waamke na kuiwajibisha serikali. Hebu fikiria, wanafunzi wangapi wanahangaika na mikopo ya kwenda vyuoni tena vya hapa nchini ambayo gharama yake haizidi Shs 5 million kwa mwaka, huduma za afya mbovu kupita kiasi, miundombinu ya kusuasua! wakati kwa upande mwingine watu wachache wakivinjari na kodi yetu ambayo wale wanaolipa wanajua uchungu wake. Hebu viongozi waonyeshe na wonekane ni wafuasi wa dhati wa 'Good Governance'
 
kusema ukweli ni kuzuri pale tu ukweli utakaposemwa utaleta faida kwa sehemu husika, lakini kama kusema ukweli kutaletea matatizo na machafuko, basi kusema ukweli si kuzuri, na kama kusema uongo kutaleta furaha au amani sehemu husika basi kusema uongo ni bora kuliko kusema ukweli.Mwandishi : Anon

Friday,

Uongo siku zote hauwezi kuleta amani hata siku moja na Ukweli hauwwezi kusababisha vurugu. embu tupe mfano ni wapi hiyo kauli yako inaweza kutumika kama sio kutetea mafisadi.
 
Nacho jua mimi ni kwamba walio chukua pesa za EPA na zinginezo ni wale wachache ambao wamesha jihesabu kama wenye Nchi .Utakuja hata JK yumo na mashikaji wake zote so is hard to leave them naked na ndiyo maana usanii unafanyika .Lakini hili jambo ni kubwa na la hatari sana.
 
Nacho jua mimi ni kwamba walio chukua pesa za EPA na zinginezo ni wale wachache ambao wamesha jihesabu kama wenye Nchi .Utakuja hata JK yumo na mashikaji wake zote so is hard to leave them naked na ndiyo maana usanii unafanyika .Lakini hili jambo ni kubwa na la hatari sana.

Makamba alisema kwamba sisiemu haikuchukua hata senti tano kwenye fwedha za EPA kwa ajili ya kampeni 2005.....akaendelea kusema mwenye mashaka akakague mahesabu ya fwedha ya chama twawala!

Sasa sijui nimwamini mgosi? Kwamba fwedha za dili kama hizi zingewekwa kwenye mahesabu ya chama twawala...kwa uwazi na ukweli. kwamba wangeweza kurekodi 'bilioni 52 kutoka EPA' then matumizi yake ni haya na haya....

Kwa dhati kabisa naamini kiasi fulani cha hizi bilioni 133 zilitumika kwa shughuli za kisiasa kwa hiyo kinachofanyika sasa ni michango ya kimyakimya. Watu wanachangishana ila chama twawala kisiadhirike..kimyakimya. NITAENDELEA KUAMINI HIVI HADI SIRIKALI ITAKAPOTHIBITISHA VINGINEVYO.
 
Wanapozirudisha hizo pesa, wanazitolea maelezo gani? wanaziingiza kwenye account gani? na Risiti zake zinaandikwaje? RIBA? KODI? na mwengineyo? kwanini wanafanya siri?
 
Kwani Warudishe Au Wasirudishe Zitatusaidia Nini Au Zitaongeza Kitu Gani Mimi Naona Nyimbo Ni Zile Zile Tu Miaka Nenda Rudi Mpaka Roho Zitakapoacha Miili
 
Kama Ingekuwa Serikali Yangu, Na Ili Kuonyesha Kweli Nimekichukia Kitendo Hiki, Nisingeangalia Mambo Ya Haki Za Binadamu Wala Nini Ningewatoa Hadharani Tena Ningealika Vyombo Vya Habari Itv Tvt Dtv Live. Nakata Kichwa Mmoja Mmoja Ili Iwe Fundisho Kwa Wengine Na Najua Wananchi Wangenishangilia Hatuwezi Kuwa Tunaendekeza Mambo Ya Kupuuzi Tu Kila Siku Ni Longo Tuu Hadithi Ni Zile Zile Mbona Alipoiba Kasusura Tena Dola M 2 Tu Mlitaka Kumtoa Korodani Na Kosa Kosa Lakini Jela Miaka Kibao Yaani Sawa Na Kumuua Maana Kwa Umri Alio Nao Na Miaka Mli Yomfunga Ni Sawa Na Mmemuua. Ina Maana Hawa Ni Nani Na Kasusura Ni Nani
 
Wakuu,

Hebu turudi kwenye ile taarifa ya vyombo vya habari kuhusiana na EPA kama ilivyo hapo chini

Baada ya kuipitia Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali na ya Mkaguzi wa Nje, yaani, Kampuni ya Ernst and Young, Mhe. Rais amesikitishwa na kukasirishwa na taarifa ya kuwepo vitendo vya ukiukwaji wa makusudi wa sheria, kanuni na taratibu za uuzaji wa madeni ya nje vilivyofanywa katika taasisi muhimu na nyeti kama vile Benki Kuu. Kwa hiyo, ameamua kuwa hatua za kisheria na kiutawala zichukuliwe dhidi ya makampuni na watu waliohusika na vitendo hivyo viovu.
"

Katika maneno hayo mekundu, ni wazi kuwa JK kama rais karidhika kuwa pesa hizi hazikuwa za MKOPO kama baadhi wanavyotaka tuamini. Sasa kama hazikuwa za mkopo ni dhahiri watu hawa waliiba, either wizi wa kuaminika, wizi wa kugushi nyaraka, utapeli, lakini wote ni WIZI.
Je, ukishagunduliwa kuwa wewe ni mwizi, unaombwa kurudisha pesa au mali uliyoiba?? Au sheria inaanza kufanya kazi yake, ikiwa ni pamoja na kunyang'anywa kile ulichoiba sio kuombwa na kisha kupelekwa mahakamani.

Kwa ajili hiyo Rais ameamua yafuatayo:-

1. Ametengua uteuzi wa Dkt. Daudi A. Balali kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania.

2. Ameagiza Bodi ya Wakurugenzi ya Benki Kuu ikutane mara moja kujadili taarifa ya ukaguzi na kuchukua hatua zipasazo za kinidhamu dhidi ya Maofisa wote wa benki, walio chini ya mamlaka yake waliohusika na kusababisha hasara hii kwa taifa.

Hii bodi ni bodi ipi?? Ni kwa nini hii bodi inaendelea kuwepo? Hawakujua nini kinaendelea ndani ya sehemu waliyopewa kuangalia?? Kama jibu ni "NDIYO", inamaana hawaelewi wajibu wao na hawafai kuendelea kuwepo tena. Kama jibu ni kuwa walikuwa wanajua,walichukua hatua gani?? Hakuna hatua waliyochukua then hawafai pia kwani walifumbia uhalifu au nao walinufaika na uhalifu huo. Hawa hawastahili kuendelea kuwa wakurugenzi wa bodi ili wawachukulie hatua za kinidhamu na zinazostahili wafanyakazi kwani wao pia ni wahusika.
4. Rais amewaagiza; Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Inspekta Jenerali wa Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, kuchunguza na kuchukua hatua zipasazo za kisheria kwa makampuni na watu waliohusika na uhalifu huu. Rais amewataka watumie ipasavyo mamlaka na madaraka waliyo nayo kwa mujibu wa sheria. Aidha, amewataka wakamilishe kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita. Amemuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali awe kiongozi wa kazi hii. Amewataka wahakikishe kuwa fedha zilizolipwa isivyo halali zinarudishwa.

"Wachukue hatua za kisheria kwa mujibu wa mamlaka na madaraka yao kisheria"Jamani hivi hatua zipasazo zakisheria kwa mtu mwizi na muhujumu wa uchumi ni kumwomba arudishe kile alichokwiba huku akiendelea kudunda mitaani??!!Hii ni sheria au matakwa?
Mie nadhani sheria ziko wazi kwa wezi wa mali ya umma na uhujumu.Ni kukamatwa na kupelekwa mahakamani na kufilisiwa mali.

Anapowataka wahakikishe kuwa fedha zinarudishwa, haina maana kwenda kuwabembeleza na kuwaomba warudishe.Bali ni kushirikiana na jumuia za kimataifa kukamata mali na fedha zao na kuhakikisha mali waliyoiibia Tanzania inarudi, either kwa kupiga mnada mali walizonazo.
Haya mengine yanayofanyika ndo yanatufanya tusiamni kitu.
 
I Believe Kuna Jambo Zito Sana Lililojificha Ndani Ya Sakata Hili Ila Mungu Yupo Mambo Yatajiweka Wazi Tu Ipo Siku
 
Kwani Warudishe Au Wasirudishe Zitatusaidia Nini Au Zitaongeza Kitu Gani Mimi Naona Nyimbo Ni Zile Zile Tu Miaka Nenda Rudi Mpaka Roho Zitakapoacha Miili

Hizo pesa zikirudi na kutumika ipasavyo zinaweza kumuongezea mzazi wako siku chache za kuishi kwa kupata matibabu na maji safi ya kunywa, lakini pia zinaweza kumsomesha mtoto wa ndugu yako yeyote ambaye hawezi kwenda shule kwa sasa kwa sababu tu hana ada ya kulipia.
 
JK anakwepa mada, jana ameongelea mambo ya misaada tu ktk hotuba yake. Omba omba kwa Bushi na kusolve mgogolo wa kenya mambo ya ndani yaliyo na madhara kabisa hajagusa hata chembe. Anaogopa nini kama yeye hakuwemo ktk madudu haya.
 
Nimepata mail hii, eti majibu mnayotafuta yako humu, ndio maana hampati kitu.

Disclaimer - ‘The events depicted in this conversation are fictitious. Any similarity to any person living or dead is merely coincidental.’

This conversation took place to background music of Handsome by Dully Sykes;

Dubya – ‘Whats that cool stuff you are listening to?’
Mr. Handsome – ‘That’s bongoflava ma maaan, you should come and visit and bob your head to it like a Masaai. We can cut a couple deals in between’
Dubya – ‘Bongoflava? Is that like our cowboy music?’
Mr. Handsome – ‘Yea yeah that’s wassup ma mein. But its like washed down hip-hop. Bongo is brains…here in Bongo life is so hard we constantly churn our brains for a quick buck…..not as bad as Nigeria though.’
Dubya – ‘Personally not into that hip-hop folks music. But I hold you black folks dearly’
Mr. Handsome –‘So can we cut some deals or what’?
Dubya – ‘You know, there are some good news and bad news’
Mr. Handsome – ‘Eeh?? Let me turn down the music….’
Dubya – ‘I know about your folks drying out your Bank….is that Bank of Tazmania devil…whatteva, some radical elements in your banks. Democracy is possible for your banking opportunity system and economic blackmail can affect our war against terror especially in Iraq’.
Mr. Handsome – ‘You losing me Mr. Prez’
Dubya – ‘I can commit more soldiers from the IMF and World Bank so we make sure the money gets where it needs to the malaria hiv people of the great people of Africa’
Mr. Handsome – ‘Are we talking 10% or what? Mr Prez you pulling my cojones…3% my people are killing me’
Dubya – ‘what is the story about your Banking thing?’
Mr. Handsome – ‘The truth is…..’ swallows, some ukwaju juice ‘If you follow up on that, then we wont be able to cut deals Mr. Prez. And I cant say much cos, there is a chap called Mwanakijiji in your country and he is giving us a run for our ufisadi money’
Dubya – ‘We have freedom of speech in my country… we are not a banana republic.so how can I help you’?
Mr. Handsome – ‘Please come to my country. You know we are dealing with this issue. Make some phone calls along the way, get me some recognised promotion, I will fire some big fish in my Team to show I am serious about corruption, after you come, send your IMF or World Bank people after you….tell them not to ask too many questions and we make them smile. We will make some effort…..5% my country is on offer’
Dubya – ‘You bad mama jamma, I like bongo already. I have always wanted to dance with those masai folks…..they don’t have WMDs? I love their bling bling on the neck’
Mr. Handsome (smiling) – ‘Haaaa you is kraazyyy maaan. You soo cool’
Dubya – ‘Yeah, that’s what Condi says……’
Mr. Handsome – ‘Speaking of Condi….I wanna play her a tune called ‘She got Gwaan by Mangwair’…’
Dubya – ‘Lets no go there buddy. Stick to business. Your country is like Russia now……they have Oligarchs, you have Mineralgarchs….is that a word?’
Mr. Handsome – ‘Hahaaa, we call it Karamagiarchs’
Dubya – ‘Ok, I gotta go. So what should I bring you from our great nation of freedom, liberty and blah blah?’
Mr. Handsome – ‘Some bling bling, Flavor Flav dizaini…I wear that in my big house. I will print Khangas with you face….and our beautiful women can wear them on their beautiful round bottoms….how you like that….’
Dubya – ‘Haahaaaa, back that thang up…..’ shouts to the side of the phone ‘Condiiiii, I think I have a pimp for a…….….’.

Disclaimer - ‘The events depicted in this conversation are fictitious. Any similarity to any person living or dead is merely coincidental.’
 
Kama Ingekuwa Serikali Yangu, Na Ili Kuonyesha Kweli Nimekichukia Kitendo Hiki, Nisingeangalia Mambo Ya Haki Za Binadamu Wala Nini Ningewatoa Hadharani Tena Ningealika Vyombo Vya Habari Itv Tvt Dtv Live. Nakata Kichwa Mmoja Mmoja Ili Iwe Fundisho Kwa Wengine Na Najua Wananchi Wangenishangilia Hatuwezi Kuwa Tunaendekeza Mambo Ya Kupuuzi Tu Kila Siku Ni Longo Tuu Hadithi Ni Zile Zile Mbona Alipoiba Kasusura Tena Dola M 2 Tu Mlitaka Kumtoa Korodani Na Kosa Kosa Lakini Jela Miaka Kibao Yaani Sawa Na Kumuua Maana Kwa Umri Alio Nao Na Miaka Mli Yomfunga Ni Sawa Na Mmemuua. Ina Maana Hawa Ni Nani Na Kasusura Ni Nani

Mara moja moja kitu kama hicho hata mimi nakiunga mkono, unajua haya mambo ya Demokrasia yanategemea situation, kwa hili hawa wezi wanastahiki.Unajua wakati wa Lenin alimtwanga raia risasi kwa kutolipa nauli ya Basi - basi hadi hii leo Mrusi akiingia katika basi nakata tiketi na kuigonga - wamepata funzo.
 
JK anakwepa mada, jana ameongelea mambo ya misaada tu ktk hotuba yake. Omba omba kwa Bushi na kusolve mgogolo wa kenya mambo ya ndani yaliyo na madhara kabisa hajagusa hata chembe. Anaogopa nini kama yeye hakuwemo ktk madudu haya.

Nafikiri JK inabidi abanwe. Ila tatizo waandishi wa habari wengi bongo ni wazushi na wako very cheap kuonga vihela mbuzi. Lakini kwenye press conference na waandishi wa habari inabidi abanwe aelezee interest za watu wengi kama EPA. Wananchi tumechoshwa na maneno matamu inabidi tuambiwe wapi tumefikishwa na hii mijizi, na itajwe watu tuijue hata kama itapita na migari yao ya bei mbaya tujue kuwa ni pesa yetu ndo imenunua hiyo migari. Ni wakati muafaka umefika sasa watz tuwe kitu kimoja na tuwe na nationa interest--achilia mbali watu wakisema ni ubaguzi wala nini lakini hatuwezi kuvumilia mijitu inakuja TZ inatuibia na tukisema tunaonekana wabaguzi.
 
Mafisadi wa BoT warudisha bilioni 50/-
Faraja Mgwabati
Daily News; Friday,February 29, 2008 @06:10

*Mkullo asema fedha hizo zimekusanywa kwa mwezi mmoja
*Amwambia bosi wa IMF zitakazorudishwa ni bilioni 121/-
KAMPUNI zilizohusika na ufisadi wa kuchota mabilioni ya fedha ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), zimerudisha serikalini Sh bilioni 50 hadi sasa, imefahamika.

Fedha hizo zimerejeshwa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamuru mwezi uliopita kampuni 22 zilizohusika na ufisadi wa Sh bilioni 133 kupitia EPA, kurudisha fedha hizo na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mustapha Mkullo, aliwaambia waandishi wa habari leo wakati akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha Duniani (IMF), Dominique Strauss-Khan, kuwa fedha hizo zimepatikana ndani ya mwezi mmoja uliopita.

"Tumeweza kukusanya Sh bilioni 50 ndani ya mwezi mmoja tu na tunatarajia kukusanya fedha na mali zaidi ambazo ziliibwa BoT," alisema Mkullo. Mkullo alisema Serikali pia imefanikiwa kukamata mali za wahusika, zikiwamo zilizofichwa nje ya nchi na wamiliki wa kampuni hizo.

Hata hivyo, hakutaka kutaja thamani ya mali na majina ya kampuni zilizorudisha mali na fedha hizo.

"Tumekamata mali nyingi tu na nyingine zilikuwa nje," alisema Mkullo na kuongeza kuwa, lengo na matarajio ya Serikali itafanikiwa kurejesha asilimia 80 ya fedha zote zilizoibwa, yaani Sh bilioni 106.4.

Suala la ufisadi ndani ya BoT liliibuka mwaka jana baada ya Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kuonyesha upungufu katika akaunti ya EPA na hivyo Serikali kuamuru uchunguzi zaidi kufanyika kwa kutumia kampuni ya nje.

Serikali iliiteua kampuni ya Ernst & Young kufanya uchunguzi wa kasoro zilizokuwapo kwenye ulipaji wa EPA na ikagundua ubadhirifu mkubwa wa fedha ukiuhusisha uongozi wa BoT na kampuni 22.

Rais Kikwete alimfukuza kazi aliyekuwa Gavana wa BoT, Dk. Daudi Ballali na akaamuru akaunti ya EPA kufungwa. Pia aliunda kamati iliyojumuisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kufanya uchunguzi na kuwashughulikia wa husika.

Wakati huo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa IMF, Strauss-Khan, ameipongeza Serikali kwa namna ilivyoshughulikia masuala ya ufisadi wa BoT na Richmond. Strauss-Khan alisema jana kuwa nchi zote duniani zina matukio ya vitendo vya rushwa ila kitu muhimu ni kuhakikisha kwamba nchi husika zinapambana na ufisadi huo.

Bosi huyo wa IMF alitanguliwa na ujumbe mzito wa maofisa wa IMF ambao walikuwapo nchini tangu Jumanne wiki hii ambako walikutana na viongozi mbalimbali wa Serikali na taasisi akiwamo Gavana wa BoT, Profesa Beno Ndulu.
 
Mafisadi wa BoT warudisha bilioni 50/-
Faraja Mgwabati
Daily News; Friday,February 29, 2008 @06:10

“Tumekamata mali nyingi tu na nyingine zilikuwa nje,” alisema Mkullo na kuongeza kuwa, lengo na matarajio ya Serikali itafanikiwa kurejesha asilimia 80 ya fedha zote zilizoibwa, yaani Sh bilioni 106.4.

Why the target of 80% and not 100%? :confused:
We need more details and evidence please. Something is very wrong with this picture. I think they would like to use this as part of the campaign during 2010 elections. We won't believe you without more evidence that can be verified by independent party.
 
Back
Top Bottom