Wewe ungemfuta yupi?

Wewe ungemfuta yupi?

Ningefuta yote nikabakiza la mama...huyu ndio mtu pekee ambae tatizo langu ni lake,anakubali na kuvumilia mapungufu yangu..
 
Unajua kwa kuwa ni kufuta tu ubaoni inakuwa simple lakini kama ingekuwa ukifuta anakufa duh!
 
Huyo Dada ni bonge la fala nyumbu wa ngorongoro haswaaa....!!!! me huniambii kitu kwa wazazi wangu hasa my mom!
 
Mama tu, hizo nyingine ni hadithi za kusadidika kwangu, japokuwa nampenda sana Rey wangu lakini hatofikia hadhi ya Mama Peter, sijui kwa nini wakati mwingine nawaza nife mimi kabla yake, kiukweli sitaki kuhisi yale machungu ninayowaona nao jamaa zangu walipowapoteza Mama zao, ila najisemea nikiondoka mama yangu akiwa kikongwe nani atamsaidia, yaani sielewi mwenzenu, I LOVE U SO MUCH MAMA PETER
 
Aisee its my mum....ts my mom,its my mom. Paradise lies at the feet of my mother,hakuna kiumbe wa kufikia daraja ya mama yangu,hakuna kama mama,mama mtamu jamani,siku ikitokea umempoteza ndio utajua shimo la upweke linalobaki moyoni mwako halizibiki kwa mke/me au mtoto. Na ziada siku zote maamuzi yetu juu ya mambo kadha wa kadha ktk maisha yetu huwa yanachagizwa na uhalisia unaozunguka jambo husika. Mfano yawezekana Cathy hakuwa na mahusiano mazuri na mama/baba yake na kubwa zaidi majibu yetu yanareflect mafunzo ya imani zetu
 
Mama tu, hizo nyingine ni hadithi za kusadidika kwangu, japokuwa nampenda sana Rey wangu lakini hatofikia hadhi ya Mama Peter, sijui kwa nini wakati mwingine nawaza nife mimi kabla yake, kiukweli sitaki kuhisi yale machungu ninayowaona nao jamaa zangu walipowapoteza Mama zao, ila najisemea nikiondoka mama yangu akiwa kikongwe nani atamsaidia, yaani sielewi mwenzenu, I LOVE U SO MUCH MAMA PETER
kaka peter msiba wa mama usikie kwa mwenzio, siku yaliponifika, sijawahi kupona jeraha la mauti yake. Kifo cha mama ambae mmeshibana ni msiba wa kila siku ndani nyoyo zetu.
 
Nafuta wote na kubakiza jina la MWANANGU..especially kama ni wa kiume.

Sababu
1. baba,mama na mke wote wana wazazi wao..mimi ndiye mzazi wa mwanangu..ni usaliti mkubwa kumwacha mwanao na kuchagua watoto wa watunwengine.
2. Mwanangu ndiye atakayendeleza uzao wangu dunia hii hata nikifa. Mke yeye atasepa kwenda kumzalia bwana mwingine...aargh..
yaani mwanangu tuu kwa kweli.
 
Yeeeees!!!! Una akili sana wewe mungu akubaliki sana. mume/mke kitu gani? wazazi kwanza mengine baadae

Ukute una mtoto mmoja unageuza shingo unamwona then mama daah nitajiua binafsi sioni wakuchagua
 
Swali lingetakiwa liwe hivi:
Wale wanne waliobaki yaani baba,mama mke au mume na mtoto ndio watu wa mwisho duniani waliobaki. Mwenyezi Mungu akakupa nafasi ya kuchagua mtu mmoja wa kubaki naye duniani.
Je,ungemchagua nani?
 
Mzazi wangu,hakuna kama mzazi..mume hatoweza kunivumilia mapungufu yangu lakini mzazi wangu hatochoka kunivumilia..

Kwa ulivyosimulia kwenye ile sredi ya mke kumtuhumu mumewe kumwibia, una haki zote duniani kusema hivyo.
 
Back
Top Bottom