Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,803
- 11,257
Fundi Mchundo,
Imebidi nirudi tena kukufahamisha kile nilichokuwa nikisema toka mwanzo... Kuwa sanctions zote ni siasa za Biashara!.. toka mwanzo nimelisema hili sijui unatazama wapi mkuu... hukutaka kunielewa bali kila wakati huongeza maswali tu kwa kila nilichoandika badala ya kutazama the big picture.
Ni hivi pamoja na kwamba vikwazo vinajieleza wazi katika nchi tofauti ukweli wa hali halisi sivyo kama ilivyoandikwa...Hizi ni siasa za nchi za magharibi siku zote..
Nikatoa mfano wa Cuba, Iran na kadhalika.. hata Mugabe kuwepo New York na majuzi Italia bado hukujibu kitu ila kutafuta njia ya kutokea.. Sheria zinasema tofauti na vile vinavyoendelea humo. Vitu vinaingia pamoja na vikwazo vyote as a fact Canada wapo wafanya biashara wamewekesha Cuba na dunia haitambui kisheria ushirikiano kama huo ambao upo..best destination ya Wa -Canada ktk tourism ni Cuba.. na kwa mwaka mmoja tu Cuba inapata zaidi ya watalii 500,000 toka North America peke yake... hawa wote wanaingia Marekani na kutoka bila kufuata hizo sheria za sanction unazozizungumzia. Cigar za Cuba hadi kesho zinaingia Marekani kinyume cha sheria hizo unazozungumzia...Hii ndio hali halisi mkuu, sio kilichoandikwa.
Kitu kingine labda nikwambie tena kuwa kama wewe ni Muislaam na jina lako lina majina yote matatu ya Kiarabu basi mkuu huwezi kutuma fedha hata iwe Africa kirahisi fedha hizo zinarudishwa! Je, ipo sheria ya namna hiyo!.. Mimi nafikiria tunachozungumza hapa ni kile kinachotendeka na sio sheria! Mugabe anayoyafanya sidhani kama yamo ktk katiba ya Zimbabwe ama yanatambuliwa kisheria!..tunachozungumzia ni ubabe wa Mugabe na huo wa wazungu hasa Waingereza..na binafsi nafikiria hofu yao kubwa ni MCHINA ambaye anaingia Afrika kwa kasi ya ajabu.
Mugabe kasimamiwa na wahuni ambao hawajali sheria inasema nini! wao upinzani hukumu yake ni kifo tu yaani unauza nchi.. Huu ni uharamia kama alioufanya Saadam Hussein wakati wale Ma Qurdish walipotumiwa na Marekani...Na siku Saadam alipokianzisha kwa hao Qurdish - Wamarekani waliingia mitini, waliwaacha Qurdish ktk mataa wakauawa kama ndama. hiki ndicho nachozungumzia kuwa wazungu wanafiki, washenzi na siku zote watu kama Morgan ambao wanataka kubebwa na mzungu ni hatari sana...
Leo hii Iraq nchi nzima wanalipa kosa la uongozi wa Saadam as a fact sababu kubwa ni Marekani na uongoi wa Bush hata kama tunaweza kusema Saadam was brutal and he had to go!.Hii ndio hofu yangu kubwa na nawaomba tujihadhali nayo zaidi ktk kila tunapojaribu kulitazama swala la Zimbabwe!
Sheria zilizoandikwa kuhusiana na Zimbabwe ni kama ulivyozieleza na kama unakumbuka niliwahi kuyasema haya toka mwaka 2004 ktk ubishi kama huu...Na nyie kwa kutofikiria mnakubali kabisa kwamba Wa - Zimbabwe hawajui kulima isipokuwa mzungu..Na inazidi kunishangaza unapotumia vigezo zvizito kama Utaalam wa ujenzi wa nyumba ktk kilimo ambacho ni jadi ya Mbantu. yaani wazungu ndio wametufundisha kweli kulima ati wao ni architectures wa ukulima!..kiasi kwamba Wazimbabwe washindwe kujua la kufanya hata chakula chao wenyewe washindwe kulima!..
Pengine msichoweza kufahamu ni impact ya kufungiwa kiuchumi, wazungu ni zuga wakubwa sana inapofikia maslahi ya nchi zao ama haki ya mwafrika..
Well, nitarudia kusema kwamba siwezi kuendelea kubishana..kwani nakumbuka wakati wa kuivamia Iraq nilisema wazi ktk kijiwe hiki (Bcstimes) kuwa Marekani wamevamia nchi hiyo kwa sababu ya Mafuta (OIL)mkanibishia sana na kusema yote mabaya ya Saadam including WMD kama ndio sababu kubwa..lakini mkashindwa kuelewa kwamba sikubisha kabisa mabaya ya Saadam isipokuwa kuwashutumu Westerners ktk hatma ya Iraq ni ukweli usiofichika!..
Leo tena najikuta ktk mjadala kama ule ule ambao baada ya miaka mtakuja kaa kimyaaaa msikubali makosa yenu ya kutoona mbali.
Nimesema tunaongea lugha tofauti. Nimekujibu hoja zako lakini pengine kwa vile majibu yangu hayakuendana na uliyoyataka unakazania kuwa sikukujibu! Mfano wako wa Cuba nimeujibu na kukuelezea kuwa hata wakati wa mapambano dhidi ya utawala wa makaburu Afrika Kusini, wanafunzi na makanisa huko Marekani(na wengine) walisusia bidhaa za Afrika Kusini wakati nchi yao ilikuwa haijaweka vikwazo! Nikakueleza kuwa hata sisi tulipofunga mpaka na Kenya, bidhaa kutoka Kenya ziliendelea kupatikana. Hivyo hivyo hakuna kitu kinachomzuia mCuba kwenda Brazil au China, kuingia dukani, kununua jozi mia za Nike na kwenda kuziuza dukani kwake Havana. Hii haimaanishi kuwa Nike wana uhusiano wa kibiashara na Cuba. Kwa kifupi, matendo ya watu binafsi, mashirika binafsi n.k. si msimamo wa serikali.
Huop mfano wako wa Canada nao batili. Nitakusaidia. Kuna wanafunzi wengi wa kimarekani wanasomea udaktari Cuba, lakini hii haina maana kuwa sanctions hazipo! Watu kulazimika kwupitia Canada au Mexico ili waende Cuba ni ishara kuwa hizo sanctions zipo. Kupatikana kwa Cuban cigars, mwenyewe unakiri illegally, si dalili kuwa sanctions hazipo. Kupatikana kwa crack katika mitaa ya New York hakuhalalishi matumizi yake. Wakati tumefunga mpaka na Kenya, watu walikuwa wakienda kenya kwa kupitia Addis. Hii haikuwa na maana kuwa mipaka imefunguliwa? Na kama nilivyokueleza, sabuni za Imperial zilikuwa zinapatikana kama kazi kwenye mitaa ya Darisalama.
Haya,Mkuu, haya ya uislaamu nayo yametokea wapi. Kuna watu wataapa kuwa kama wewe si mchaga hupati kazi TRA lakini hii haimaanishi kuwa ni msimamo wa TRA kuajiri wachaga tu! Unfortunately, racial, ethnic profiling zipo kila mahali. Hata kwetu.Ukiingia kwenye supamaketi Dar umevaa ndala, utakuta unamsindikizaji lakini akiingia mzungu amevaa hivyo hivyo anachangamkiwa. Kinachoendelea kwa wenye majina ya kiislamu ni hivyo hivyo. Uamuzi wa benki binafsi au Western Union kukataa au kukusumbua kwa vile tu wewe ni mwislamu au una jina linalodhaniwa ni la kiislamu, ni wao na si wa serikali. Kuna avenues za kufuata kama unaona haukutendewa haki.
Mugabe si mhudumu wa benki, ni rais wa nchi. Yeye ameonyesha kuwa ana utter contempt na whatever passes as a constitution. Amesimama kwenye kadamnasi na kuwa'mock' kwa kusema anayeweza kumtoa pale ni Mungu tu. Huyu ni mhuni. Na ndicho tunachokisema lakini hutaki kuelewa. sasa kwa vile George Bush senior aliwatosa waKurd, leo anayoyasema mwanae kuhusu huyu mhuni yanakuwa hayana ukweli? Kuna tofauti gani na sisi ambao tulisimama tukiangalia wakati jirani zetu Rwanda wakiuana kikatili? Ambao tunaendelea kuikumbatia serikali ya Sudan wakati ikiendelea na mauaji na unyama huko Darfur? Wakati Bush ameishayaita yanayoendelea huko kuwa ni genocide, nani katika sisi REAL Africans ametoa tamko kulani yanayoendelea? Badala yake tulitaka kuwatuza kwa kuwapa uenyekiti wa AU! Toa kibanzi katika jicho lako kwanza. Sisi hatumkemei Mugabe kwa vile wamarekani na wazungu wanafanya hivyo. La, hasha, tunamkemea kwa sababu aliyowafanyia wazimbabwe ( kuanzia wa matebele, na ndio hata wale Wazimbabwe weupe n.k) goes beyond the pale. Huyu bwana ni muovu, period. Kama wananchi wa Zimbabwe wakiamua kumchagua Morgan wewe una tatizo gani? Akiendeleza hayo ya Mugabe, nae atakemewa na hopefully atatemwa na watu wake. Kama ilivyotokea kwa Chiluba.
Nani amesema waZimbabwe weusi (inaelekea mwenzangu waZimbabwe weupe wewe huwahesabu kama ni raia wa nchi ile) hawajui kulima? On the contrary, mara baada ya zoezi la kwanza la kuwagawia wakulima mashamba ya waZimbabwe weupe, uzalishaji ulipanda. Tatizo ni hapo alipoamua kuwapa kmakada na cronies wake ambao hawajui lolote kuhusu kilimo. Wale wanachi waliokuwa wakifanya kazi katika mashamba ya wazimbabwe weupe walionekana kuwa ni potential wasaliti, wakatemwa. Uendeshaji wa mashamba makubwa unahitaji expertise ambayo si wote waliyokuwa nao. Nilikueleza kuwa, Fundi mchundo au Fundi muashi si sawa sawa na Mhandisi ingawa inawezekana kabisa kuwa wanamzidi katika upangaji wa matofali! Sisi wenyewe tulinyang'anya plantations na ranchi kutoka kwa wale tuliowaita makabaila na tumeshindwa kuyaendesha. Mbona wamasai wako kibao , kwa nini basi tumeshindwa kuendesha ranchi za Kongwa n.k.? Si tungewapa wakina Ole ? Naam, kilimo ni jadi ya mbantu. Ndio maana kila kukicha tuna kibakuli tukiganga njaa! Kilimo cha kiamba si sawa na kilimo cha plantation. Ndiyo maana Nyerere alipoenda Marekani kama mgeni wa Carter, alitembelea Georgia, kuangalia wenzetu wanalimaje. Ukisikia kuwa Carter alikuwa analima karanga si sawa na mkulima wetu wa zao hilo hilo kule Dodoma. Kila utaalamu una kikomo chake. Mkandarasi wa Class 5 haruhusiwi kujenga jengo lenye ghorofa kumi. Matokeo yake tumeyaona. Wengi wetu tunaweza kujenga kibanda lakini inapokuja kaghorofa tunawaachia wataalamu. Ndivyo inavyotakiwa.
Tusiopendana ni sisi. Muuaji mkubwa wa mtu mweusi ni mtu mweusi mwenzake. Wazungu wana mchango wao lakini kwanza inabidi tubanane wenyewe kwa wenyewe ama sivyo hatutajikomboa. Hakuna mtu anayemheshimu mtu asiyejiheshimu. Tutamtegemeaje mzungu atujali wakati wenyewe hatujijali?
Sasa unaondoka Somalia unakimbilia Iraq! Wakati huo huo ukinishutumu kwa kusogeza magoli!!!!! Mimi sikuweko Bcstimes ( nimegundua kitu kinachoitwa internet mwaka jana tu) kwa hiyo nisingeweza kukubishia. Lakini kama ningekuweko, ningekubishia. Sio kwa sababu ulizoziweka bali kwa vile hoja yako ilikuwa simplistic na kwa msamiati wako, ya kutoka kwa kinyozi.
Mkandara, arguments zako ni convoluted bila sababu. Kama nilivyosema awali, naona tunaongea lugha tofauti.
Amandla.......