Kaka huo ni mpango mzuri sana muombe mungu atakusaidia katika hilo,mimi nakumbuka nilikuwa na jamaa yangu nimesoma nae,tulikuwa tukiipanga safari 2012 ya kusepa,tulipita mashirika kadhaa kuulizia nauli ya ndege lakini mwenzangu alikuwa anamishe ingawa pesa ilikuwa ndogo sana.
Huwezi amini alivyokuwa ameshika kalamu na karatasi ananipa mipango kama vile tunapiga pindi nilimuona kama anafanya mzaha vile,alizipanga nchi za kwenda,lakini alisema zikifeli hizi naenda hata south afrika lakini hapa nimepachoka.
Alijitoa sadaka akaacha kazi then akalamba nssf yake ilikuwa kama milioni kadhaa hivi,alisepa nchi moja ya kiaarabu mpaka leo anafanya kazi huko,na mipango yake aende kiwanja kirefu zaidi ya hapo.
Mimi aliniacha kwa sababu changamoto kubwa mno ni nauli kazi ngumu kupatikana na ukipata unapata pesa ya kula tuu.
Ila bado ndoto ninazo katika hilo na hatua mojawapo nimepiga namshukuru mungu kitabu ninacho tayari.
Ila namkumbuka broo mmoja huwa ananiambia safari haipo mdomoni ipo moyoni...weka nia madhubuti muombe mungu,tafuta fursa uchange nauli sepaaaaa.