Wengine hatumpendi Mungu tunajilazimisha tu

Wengine hatumpendi Mungu tunajilazimisha tu

Mfano uliotoa ni tofauti na uwezo wa Mungu. Mzazi angekuwa na uwezo asingetaraji mpaka mwanae ahoji maumbile yake kwa kumchungulia, ndio ajue akili yake bali kabla ya chochote kutokea yeye mzazi angeshaanza kutambua na kisha kukiweka sawa. Umetoa mfano ambao unaonesha Mungu ni dhaifu asiyejua kama akili ya binadamu ipoje mpaka pale alipofanya tukio ndio katambua akili ya binadamu ilivyo

nimekupa mfano wa binaadam ili uelewe tu,maana Mungu ni mfano wake ila sio binaadam,kama utamkadiria kwa udhaifu ni sawa pia,acha tumjadili katika udhaifu chini kabisa.
 
hapana mkuu usinipe sifa za ajabu sababu tu akili yako imefikia tamati katika kuchanganua mambo fulani.

baba yako mzazi alikukanya mambo kadhaa,hukufanya sababu ulijua ni kumkosea baba yako na atakuadhibu,ukatili wa baba yako hauko katika adhabu anayokupa bali upendo upo katika njia mbadala anayokuelekeza kabla hujaamua kushika nyingine.

mama kuiba ili mimi nisome inahalalishaje wizi machoni kwangu!!!wizi ni wizi tu hakuna anayeiba bila sababu za msingi kwake.
Hvyo basi wewe umeridhia hayo kuwa sawa, haki na sahihi.

Unajua hata humu duniani kuna viongozi wa aina ya mungu wako walishakuwepo ama wapo.

Viongozi ambao watu walisifia kila watendalo sababu ya woga wa ukatili walionao viongozi hao.

Kwa mtazamo wangu mungu wako si MUNGU ninayejaribu kumfahamu. Kwa mungu wako utapatikana utii wa unafiki na woga.
 
Hvyo basi wewe umeridhia hayo kuwa sawa, haki na sahihi.

Unajua hata humu duniani kuna viongozi wa aina ya mungu wako walishakuwepo ama wapo.

Viongozi ambao watu walisifia kila watendalo sababu ya woga wa ukatili walionao viongozi hao.

Kwa mtazamo wangu mungu wako si MUNGU ninayejaribu kumfahamu. Kwa mungu wako utapatikana utii wa unafiki na woga.

hicho ndicho kitu ambacho hata yeye hapendi.

hataki kumbana mtu amtii kwa vitisho.

wewe mkuu unaitii mamlaka kwa sababu kuna polisi ukijaribu kwenda kinyume,na kisha mahakama,Mungu hajaweka polisi.

kula bata,tafiti mpaka dhambi mpya kwa vitendo,wala hakuna tatizo.
 
Katuondolea vipenzi vyeti ametuacha na majonzi yasiyoisha.
Kama wewe ni mtu mzima mwenye uelewa, utakuwa unajua ubinadamu wetu uko vipi, tuna uwezo gani, tuna mapungufu gani? Kwa hiyo badala ya kuhukumu na kulaumu uasili wetu wa jinsi tulivyo, tunazaliwa , tunakumbana na kila aina ya majanga, na Mafanikio vilevile, Ila tunajua lazima tutakufa.
Kama utajishughulisha na tafiti za kubadili huu mfumo, endeleza juhudi, Ila kama umejikalia tu, usimlaumu mtu, ndivyo tulivyo, kubaliana tu na huu uhalisia, Furahia, pambana mpaka utakapokuwa huna huo uwezo na wakati wa kuiacha dunia umefika.
 
Sasa Naja naja haya malalamiko umeleta huku unataka tukusaidieje?

Afu kuna mada nyingi tu za kipuuzi unaweza kuanzisha na ukapata wachangiaji.
Fanyeni dhihaka na vitu vingine, si Mungu.
Binadamu akishapumua akajamba anajiona kamalizaaa

Hajui kuwa huo ni upendeleo kapewa! Anaona adhihaki tu
 
ni maamuzi tu maana hakuna makundi maalumu ambayo yameumbwa ili kufanya uchaguzi wa aina fulani tu.
Wewe mwenyewe umesema wanatofautiana kwenye maamuzi. Sasa kipi kinachopelekea kuwa na utofauti wa maamuzi ikiwa wote wana kiwango sawa na aina sawa ya package kwenye vichwa vyao?
 
hicho ndicho kitu ambacho hata yeye hapendi.

hataki kumbana mtu amtii kwa vitisho.

wewe mkuu unaitii mamlaka kwa sababu kuna polisi ukijaribu kwenda kinyume,na kisha mahakama,Mungu hajaweka polisi.
Tunarudi palepale, hatutakiwi kutenda mema sababu ya uwepo wa adhabu, tunatakiwa kutenda mema sababu sisi ni viumbe wema.

Polisi, jela isiwe sababu ya utii wa sheria na mamlaka.
Tuzitii sheria tulizojiwekea sababu tusipozitii hapatakuwa na amani wala upendo baina yetu.

Woga una mwisho wake, tunapotii kwa hofu ya adhabu kuna siku kutatokea vita pale uoga utakapoondoka.

Jifunze kwenye tawala za kidikteta za duniani zinapopata machafuko

Fanya tafiti ni kwann shetani alipata wafuasi mbinguni pakatokea vita mbinguni kisha utagundua ni kwann MUNGU hakumuangamiza shetani. Just imagine, malaika wa MUNGU wangepata taswira gani kwa MUNGU endapo angemuua shetani on spot.... wangempenda au wangemwogopa?


kula bata,tafiti mpaka dhambi mpya kwa vitendo,wala hakuna tatizo.
Unadhani nimekuuliza yote sababu nahitaji uhuru wa kufanya dhambi.?
 
Wewe mwenyewe umesema wanatofautiana kwenye maamuzi. Sasa kipi kinachopelekea kuwa na utofauti wa maamuzi ikiwa wote wana kiwango sawa na aina sawa ya package kwenye vichwa vyao?

ilifaaa wawe sawa,wawaze sawa,wachukue hatua sawa si ndio???

hizo kelele ambazo ungepiga kwamba wako programed na Mungu wao zingevumilika kweli???
 
Tunarudi palepale, hatutakiwi kutenda mema sababu ya uwepo wa adhabu, tunatakiwa kutenda mema sababu sisi ni viumbe wema.

Polisi, jela isiwe sababu ya utii wa sheria na mamlaka.
Tuzitii sheria tulizojiwekea sababu tusipozitii hapatakuwa na amani wala upendo baina yetu.

Woga una mwisho wake, tunapotii kwa hofu ya adhabu kuna siku kutatokea vita pale uoga utakapoondoka.

Jifunze kwenye tawala za kidikteta za duniani zinapopata machafuko

Fanya tafiti ni kwann shetani alipata wafuasi mbinguni pakatokea vita mbinguni kisha utagundua ni kwann MUNGU hakumuangamiza shetani. Just imagine, malaika wa MUNGU wangepata taswira gani kwa MUNGU endapo angemuua shetani on spot.... wangempenda au wangemwogopa?



Unadhani nimekuuliza yote sababu nahitaji uhuru wa kufanya dhambi.?

na ndio sababu ya yeye kutojishihirisha,anataka umwamini na kumfuata uokoke.

fikiria siku moja tu itokee ishara ngumu sana hata ya kivuli cha sura yake kikikemea maovu,nani atadhubutu kiendelea na dhambi!!!hataki iwe hivi,anataka wewe,mimi yule.tumfate bila kitisho chochote kwa kutoogopa moto ambao hauna virhibitisho vyovyote kuwepo kwake.
 
ilifaaa wawe sawa,wawaze sawa,wachukue hatua sawa si ndio???

hizo kelele ambazo ungepiga kwamba wako programed na Mungu wao zingevumilika kweli???
Swala la Mungu kuwa program binadamu linabakia pale pale kuwa Mungu amewa program binadamu. Kwanini nasema hivyo kwasababu Mungu ndiye muumbaji kwa mujibu wa imani yako. Huyu muumbaji anamwekea binadamu hardware na pia software. Mungu huyu anajua fika ni yupi kamwekea software ili weak na yupi kamwekea software iliyo strong. Na anajua kabisa huyu mtu kulingana na nilivyomuumba akienda duniani atakuwa ni mzinifu na atakufa akiwa mzinifu na atakuwa wa motoni lakini pamoja na kujua hilo hakurekebisha ili huyu asijekuwa mzinifu je unategemea ni vipi huyu mtu aje duniani na akawa mchamungu badala ya mzinifu?
Au unataka kuniambia anayetenda mema yeye software yake amejiwekea mwenyewe tofauti na Mungu huyo huyo aliyemwekea software mtu muovu?

Mungu amemprogram kila mtu tofauti tofauti na ndio maana kila mmoja anatenda matendo tofauti na mwingine
 
Swala la Mungu kuwa program binadamu linabakia pale pale kuwa Mungu amewa program binadamu. Kwanini nasema hivyo kwasababu Mungu ndiye muumbaji kwa mujibu wa imani yako. Huyu muumbaji anamwekea binadamu hardware na pia software. Mungu huyu anajua fika ni yupi kamwekea software ili weak na yupi kamwekea software iliyo strong. Na anajua kabisa huyu mtu kulingana na nilivyomuumba akienda duniani atakuwa ni mzinifu na atakufa akiwa mzinifu na atakuwa wa motoni lakini pamoja na kujua hilo hakurekebisha ili huyu asijekuwa mzinifu je unategemea ni vipi huyu mtu aje duniani na akawa mchamungu badala ya mzinifu?
Au unataka kuniambia anayetenda mema yeye software yake amejiwekea mwenyewe tofauti na Mungu huyo huyo aliyemwekea software mtu muovu?

Mungu amemprogram kila mtu tofauti tofauti na ndio maana kila mmoja anatenda matendo tofauti na mwingine

pale microsoft kila mwaka zinatoka pc za aina moja zenye sifa sawa na uwezo sawa.

lakini muundaji yule anajua kabisa zinakwenda kufanya kazi tofauti,hivyo kuishi kipindi kifupi au kirefu inategemea?na kuleta ufanisi wa asilimia fulani inategemea pia.hili sio swala la pc hizo wala muundaji yeye kaumaliza mwendo akikukabidhi ni wewe na mashine yako.

lakini kwa binaadm ni tofauti kidogo,baada ya kuja duniani yeye binaadm ndiye mwamuzi aishi vipi,hakuna nguvu inayomuongoza ua kumlazimisha namna bora ya kuishi ili ampendeze Mungu.

wewe unagaka kusema Mungu amewaprograme viumbe wake lakini wanamemshinda tabia,hii inawezekanaje!!!!!
 
Nishetani tu kampitia, shetani anatumia nguvu kubwa sana kuhakikisha hafi peke yake kwenye moto wa jehanamu

Tusali sana wapendwa
hii I'd imehakiwa
Huyu sio Scars naemjua Mimi aaaa hapa Kuna namna wewe huyo?
Hapana hapana!
 
pale microsoft kila mwaka zinatoka pc za aina moja zenye sifa sawa na uwezo sawa.

lakini muundaji yule anajua kabisa zinakwenda kufanya kazi tofauti,hivyo kuishi kipindi kifupi au kirefu inategemea?na kuleta ufanisi wa asilimia fulani inategemea pia.hili sio swala la pc hizo wala muundaji yeye kaumaliza mwendo akikukabidhi ni wewe na mashine yako.

lakini kwa binaadm ni tofauti kidogo,baada ya kuja duniani yeye binaadm ndiye mwamuzi aishi vipi,hakuna nguvu inayomuongoza ua kumlazimisha namna bora ya kuishi ili ampendeze Mungu.

wewe unagaka kusema Mungu amewaprograme viumbe wake lakini wanamemshinda tabia,hii inawezekanaje!!!!!

Kama binadamu ndio mwamuzi je Mungu wakati anamuumba binadamu hajui atakachoenda kuamua huyo binadamu pindi atakapoends duniani?

Unasemaje kuwa Mungu ameshindwa tabia na binadamu ilihali Mungu ndiye mwenye uwezo kuliko binadamu.
 
Kama binadamu ndio mwamuzi je Mungu wakati anamuumba binadamu hajui atakachoenda kuamua huyo binadamu pindi atakapoends duniani?

Unasemaje kuwa Mungu ameshindwa tabia na binadamu ilihali Mungu ndiye mwenye uwezo kuliko binadamu.

mimi sijasema hivyo kwamba Mungu hakujua binaadam anakwenda kutenda nini.

Mungu ndiye mwenye uwezo,kuliko kiumbe wake,ndio maana nikakuuliza unataka kusema Mungu anashindwa tabia na kiumbe wake!!!
 
Mimi swali nalojiuliza waliokufa kipindi ukristo na uislam haujaingia tanzania watahukumiwaje?
Hofu ya uwepo wa Mungu Ipo kwa kila Binadamu ndugu yangu

Ndio maana hata kama Mtu hajawahi kufundishwa au kushuhudiwa habari za Mungu utakuta anajua kabisa kuwa mema ni yapi na mabaya ni yapi, na anajua kuwa kumfanyia mtu hivi ni vibaya na hivi ni vizuri

Mathalani katika jamii za kiafrika hata kabla ya kuja kwa Wazungu na Waarabu tayari walijua kuua ni dhambi, kubaka, kusema uongo, kuroga n.k

Kwahiyo, watahukumiwa kwa kile walichokifahamu wakakaidi.
 
mimi sijasema hivyo kwamba Mungu hakujua binaadam anakwenda kutenda nini.

Mungu ndiye mwenye uwezo,kuliko kiumbe wake,ndio maana nikakuuliza unataka kusema Mungu anashindwa tabia na kiumbe wake!!!
Kama Mungu anajua kipi anaenda kukitenda huyo binadamu wakati hata duniania hajakpeleka, inamaana yeye Mungu ndiye aliyetaka huyo binadamu aende duniani akakitende hiko. Nakupa mfano

Mimi ni fundi ujenzi, nimejenga nyumba lakini inacheki juu kwenye bati nikaona kuna tundu ambalo litasababisha nyumba kuvujisha pindi mvua ikinyesha. Lakini pamoja na kugundua hilo sijafanya chochote kurekebisha. Maana yake nimekusudia nyumba ivuje. Ni hivyo hivyo kwa Mungu, mpaka anaona binadamu akienda duniani atakuwa ni muovu maanake hayupo kamili katika kiumbwaji, laiti kama angekuwa kamili basi angefanya maamuzi yaliyo sahihi. Huyu binadamu asiyekamilika anapelekwa duniani hivyo hivyo unategemea atafanya kipi tofauti na Mungu alivyotaraji?
 
Back
Top Bottom