Wengine hatumpendi Mungu tunajilazimisha tu

Wengine hatumpendi Mungu tunajilazimisha tu

Umejenga nyumba,

Hapo ndani kwako anaingia nyoka,

unawaambia wanao kuna nyoka humu msimsogelee kaeni mbali atawauma,

nyoka anawauma wanao mmoja mmoja,

nyoka uwezo wa kumwondoa unao ila humwui unasubiri siku ya mwisho uchome wote wanao waliumwa na nyoka kwa kosa la kuruhusu nyoka awaume na nyoka mwenyewe.

Hizi hadithi za wachungaji kuna mambo hayapo sawa.

MUNGU yupo ila nina wasiwasi na haya mahubiri tunayohubiriwa.

Kuna uwezekano huyu MUNGU si huyu wanayemuhubiri.
Nadharia zako umeziweka kwa kuelemea upande mmoja kuonyesha kana kwamba binadamu ni kiumbe dhaifu na si kweli. Embu turudi kwenye mfano wako kwa kusema Mungu kakwambia kabisa kuna nyoka msimsogelee na akiamua kuwasogelea amewapa na uwezo wa kumwondoa huyo nyoka kwakuwapa kila aina ya silaha ya kumuua huyo nyoka, nyoka mwenyewe ni mmoja na nyie mpo wengi tena mna silaha hapo mnamwitaji mungu wa nini tena ikiwa uwezo huo kawapa mnao wenyewe
 
Na ndio maana nimeomba unipe tafsiri ya neno uhuru ili tuone uwepo wa mikingamo kunaweza kumpa mtu uhuru ilihali hajapewa uhuru kamili.

Sasa utaumbaje kiumbe au mtu bila ridhaa yake? Kama ni uhuru ilipaswa kiumbe kiridhie, huo ndio uhuru kamili.

Nilikuuliza kuhusu utashi kabla sijaenda mbali zaidi naomba kwanza tuwekane sawa nini maana ya utashi? Kisha tuje tujadili kwenye uumbaji wa Mungu kwa binadamu kwanzia kwenye akili na huo utashi.

sasa kila kitu hujui mkuu,huoni kama tutaanzia mbali sana,halafu tutakuvuruga njiani,maana kutakuwa na maswali pia.

neno uhuru kwa tafisir ya moja kwa moja,ni nafasi ya mtu kufanya mambo yake bila kuingiliwa.

sasa hapa kwenye ridhaa ya kiumbe kabla ya kiumbe kuumbwa ndiko shida ilipo,kuumbwa haikuwa option ya kiumbe ambacho hakikuwepo,ila kuishi na kutokuishi ni chaguo la kiumbe baada ya kupata pumzi.ndio maana kuna njia za kufata.

utashi ni akili za kawaida kabisa kutambua mazingira yanayokuzunguka.
 
neno uhuru kwa tafisir ya moja kwa moja,ni nafasi ya mtu kufanya mambo yake bila kuingiliwa.
Kwenye hiyo maana ya uhuru uliyotoa hakuna neno masharti wala
Vigezo vya kuzingatiwa. Hivyo kama Mungu angekuwa ametoa uhuru kusingekuwa na sheria.
 
Kwenye hiyo maana ya uhuru uliyotoa hakuna neno masharti wala
Vigezo vya kuzingatiwa. Hivyo kama Mungu angekuwa ametoa uhuru kusingekuwa na sheria.

uhuru ukiwa na mashart au mipaka unaitwaje???
 
uhuru ukiwa na mashart au mipaka unaitwaje???
Hakuna uhuru ulio na masharti. Ukipewa masharti au mipaka inaitwa ni maamrisho au maagizo nawala sio uhuru. Uhuru maanake unafanya unavyotaka au unavyojisikia pasipo na katazo lolote.
 
Kwanini Mungu aliunda lile tunda? Kwanini Mungu asingemuangamiza shetani kabisa asitudanganye? Kwanini Mungu alimuaxha huru shetani ili hali akijua atakuja kumdanganya mwanadamu? Pamoja na hayo nampenda sana Mungu wa kweli,mwenye huruma na nguvu kushinda nguvu yoyote.
 
utashi ni akili za kawaida kabisa kutambua mazingira yanayokuzunguka.

Mungu wakati anamuumba binadamu A si anajua fika kuwa huyu mtu A nayemuumba kutokana na akili na utashi alionao, akienda duniani atakuwa ni mwizi je inawezekana vipi mtu huyu A akaja dumiani akawa tofauti na vile Mungu alivyotaraji?

2) je mtu A aliyekuja duniani akawa muovu na mtu B ambaye kaja duniani akawa mwema wanazidiana kipi kwenye vichwa vyao mpaka kila mmoja afanye chaguzi tofauti ilihali wote wameumbwa na mmoja?
 
Hakuna uhuru ulio na masharti. Ukipewa masharti au mipaka inaitwa ni maamrisho au maagizo nawala sio uhuru. Uhuru maanake unafanya unavyotaka au unavyojisikia pasipo na katazo lolote.

kumbe concept nzima ya neno uhuru ni feki.
hata nyerere aliishawahi kusema hakuna uhuru usio na mipaka.

maana katika asili yake A&B side uhuru ni kulia na kushoto ni utumwa ama mateka.
ukisema uhuru hautakiwi kuwa na katazo la aina yoyote umekataa kwamba hakuna mbadala wake,yaani side B.
kitu ambacho hakiwezekani hata physics inakata,kutokuwepo kwa negative energies.
 
Mungu wakati anamuumba binadamu A si anajua fika kuwa huyu mtu A nayemuumba kutokana na akili na utashi alionao, akienda duniani atakuwa ni mwizi je inawezekana vipi mtu huyu A akaja dumiani akawa tofauti na vile Mungu alivyotaraji?

2) je mtu A aliyekuja duniani akawa muovu na mtu B ambaye kaja duniani akawa mwema wanazidiana kipi kwenye vichwa vyao mpaka kila mmoja afanye chaguzi tofauti ilihali wote wameumbwa na mmoja?

mimi nimesema utashi wa binaadamu wote ni sawa,labda mmoja awe na matatizo ya akili.

Mungu alitupa akili za kutambua mema na mabaya mara baada ya adam kula tunda,tulikabidhiwa haki hiyo ambayo haikuwa yetu.maana yake sasa hapa kila aliyechuma janga ikaanza kuhesabiwa kwamba ni kwa akili zake zote kafanya kosa husika akijua kabisa.

kwa sasa wewe ni rahisi sana kuvunja sheria ya mamlaka kwa kutojua lakini sheria za Mungu siku akili imekomaa tu zote umeshazijua.
 
mimi nimesema utashi wa binaadamu wote ni sawa,labda mmoja awe na matatizo ya akili.

Mungu alitupa akili za kutambua mema na mabaya mara baada ya adam kula tunda,tulikabidhiwa haki hiyo ambayo haikuwa yetu.maana yake sasa hapa kila aliyechuma janga ikaanza kuhesabiwa kwamba ni kwa akili zake zote kafanya kosa husika akijua kabisa.

kwa sasa wewe ni rahisi sana kuvunja sheria ya mamlaka kwa kutojua lakini sheria za Mungu siku akili imekomaa tu zote umeshazijua.
Hili swali haujanijibu. je mtu A aliyekuja duniani akawa muovu na mtu B ambaye kaja duniani akawa mwema wanazidiana kipi kwenye vichwa vyao mpaka kila mmoja afanye chaguzi tofauti ilihali wote wameumbwa na mmoja?
 
mkuu kumbuka wakati Mungu anamuumba mwadamu haikuwa lengo lake mwanadamu kufa ila alimwambia utakapo kula mtu huo ni hakika utakufa.

Na mimi na wewe tunajua kabisa kuwa shetani ndio sababu ya mwanadamu kula lile tunda kwa maana yeye ndie alie washawishi hivyo ni Lucifer anapaswa kulaumiwa juu ya vifo vya wanadamu.
Ina maana Mungu alipomuumba Lucifer hakujua kuwa ataharibu mpango wake mwema?
Je, hakuweza kuondoa hiyo changamoto kwenye uumbaji mapema ili watu wasiwe na mioyo migumu?
 
Mungu alitupa akili za kutambua mema na mabaya mara baada ya adam kula tunda,tulikabidhiwa haki hiyo ambayo haikuwa yetu.maana yake sasa hapa kila aliyechuma janga ikaanza kuhesabiwa kwamba ni kwa akili zake zote kafanya kosa husika akijua kabisa.
.
Kwahiyo unamaana wakati Adam wakati anaumbwa hakuwa na utambuzi wa mema na mabaya ila baada ya kula tunda ndio akapewa hiyo akili. Inamaana Mungu anabahatisha hakujua yaliyo mbele yake kuwa itatokea nini ili ampage kabisa binadamu hizo akili kabla hata ya kula tunda.
 
Nadharia zako umeziweka kwa kuelemea upande mmoja kuonyesha kana kwamba binadamu ni kiumbe dhaifu na si kweli. Embu turudi kwenye mfano wako kwa kusema Mungu kakwambia kabisa kuna nyoka msimsogelee na akiamua kuwasogelea amewapa na uwezo wa kumwondoa huyo nyoka kwakuwapa kila aina ya silaha ya kumuua huyo nyoka, nyoka mwenyewe ni mmoja na nyie mpo wengi tena mna silaha hapo mnamwitaji mungu wa nini tena ikiwa uwezo huo kawapa mnao wenyewe

Shetani ni mtoto wa MUNGU maana alimuumba, sisi ni watoto wa MUNGU maana alituumba, huu ni ugomvi wa ndugu...

Sababu zipi za msingi zinazosababisha BABA awaue watoto wote walioteleza kwa kulubuniwa na ndugu yao? Ndugu ambaye ni mmoja tu? Kwanini maelfu wafe sababu ya ndugu mmoja mkorofi aliyepewa uwezo wa ushawishi na nguvu kubwa ya ulaghai na BABA mwenyewe?

Na ukumbuke hii ni mara ya pili, ya kwanza aliua wote kwa maji, akaacha wachache sana ili wazaliane. Sasa ataua tena kwa moto wa milele, Kwann BABA anafanya hivi?
 
Shetani ni mtoto wa MUNGU maana alimuumba, sisi ni watoto wa MUNGU maana alituumba, huu ni ugomvi wa ndugu...

Sababu zipi za msingi zinazosababisha BABA awaue watoto wote walioteleza kwa kulubuniwa na ndugu yao? Ndugu ambaye ni mmoja tu? Kwanini maelfu wafe sababu ya ndugu mmoja mkorofi aliyepewa uwezo wa ushawishi na nguvu kubwa ya ulaghai na BABA mwenyewe?

Na ukumbuke hii ni mara ya pili, ya kwanza aliua wote kwa maji, akaacha wachache sana ili wazaliane. Sasa ataua tena kwa moto wa milele, Kwann BABA anafanya hivi?
Mungu hakuzaa sisi ni viumbe vyake. Mwenyez Mungu anahuruma na viumbe vyake ndo mana anatupa nafasi ya kutubia matendo yetu na hakika ni msamehevu. Moto ni adhabu kwa wale wenye kuasi na kwenda kinyume, ukomo wa adhabu hiyo anaijua mwenyewe Muumba.

Kwa fikra za kawaida hata hapa dunia fikiria kungekuwa hakuna mahakama watu wajiamulie ukiamua kuuwa, Kuiba, Kupiga mtu, kudhalilisha na hakuna Kifungo wala adhabu yoyote unafikiri maisha yangekuwaje?
 
Hili swali haujanijibu. je mtu A aliyekuja duniani akawa muovu na mtu B ambaye kaja duniani akawa mwema wanazidiana kipi kwenye vichwa vyao mpaka kila mmoja afanye chaguzi tofauti ilihali wote wameumbwa na mmoja?

hakuna wanachozidiana,wanatofautiama maamuzi tu.


wewe ukiona mtu kaangusha simu,unaona ni sawa kumpelekea,mwingine anaona kapata ya kutumia,mwingine anaona akauze apate hela.

lakini nyinyi wote mna utashi unaoendana,anayefanya vibaya wazo la kwanza humjia,ni taarifa kwamba unachofanya si chema,ila hulipuuza.
 
Kwahiyo unamaana wakati Adam wakati anaumbwa hakuwa na utambuzi wa mema na mabaya ila baada ya kula tunda ndio akapewa hiyo akili. Inamaana Mungu anabahatisha hakujua yaliyo mbele yake kuwa itatokea nini ili ampage kabisa binadamu hizo akili kabla hata ya kula tunda.

haya sasa unasema wewe mkuu.

mwanao anazaliwa ukimwona kwamba mtoto,mnalala naye akiwa busy sana na mambo na michezo yake inayohusu utoto pekee,siku atakayoangalia sehemu yako na kukuhoji baba mbona ya kwako kubwa zaidi,hapa utampa tiketi kwamba sasa anatakiwa akalale peke yake.si kweli kwamba ulikuwa hujui atakuja kukua.

Mungu kamuumba binaadam akijua kabisa siku moja atakuja kudanganywa,ushindi kwa adam ulikuwa kukataa,akashindwa.
 
Back
Top Bottom