Wengine hatumpendi Mungu tunajilazimisha tu

Wengine hatumpendi Mungu tunajilazimisha tu

Ona ulivyopendelewa.
Umeumbwa Bure kabisa, wala hukuingia mkataba na yeyote.

(kama anavyodai Manara wa Yanga)

Umepewa Class ya juu kabisa ya kuwa Binadamu, ( ungeumbwa Nzi sijui ungemlaumu nani)

Nadhani umezawadiwa utimamu wa akili na mwili, bure kabisa.

Umewekewa chakula cha kila aina bure kabisa (mashamba yapo panda mazao ule free of charge)

Umepewa maji ya kutumia, bure kabisa.

Umepewa hewa ya kuvuta, bure kabisa.

Ukaumbiwa Wanawake uchague wa kuishi naye, bure kabisa

Umepewa Uzima wa mwili, bure (kuna watu wana miaka mingi wamelazwa hospitali)

Umepewa namna ya kujitegemea na kujiletea maendeleo binafsi, bure kabisa

Umepewa uwezo wa kuzalisha watoto wa kike na wakiume, bure kabisa.

Yaani umepewa mamilioni ya faida zako binafsi bila kuingia mkataba na mtu.

Tena umeumbwa kwa thamani kubwa sana.
(Eg, kiungo chako kimoja kikiharibika mfano Jicho au Jino, hata ukiuza madini yote ya ulimwengu huu na sio kadunia kamoja, huwezi kukipata kwa kukinunua au kukifanya upya, hata uuze ulimwengu wate hupati, na una viungo vingi sana)

Na wewe ni mmoja tu, hata tokea mwingine na wala hakupata kutokea kama wewe.

Na zaidi na zaidi.

Je hupaswi kukaa mahali na kujiuliza maswali japo madogo tu kama.
Mimi ni nani
Kwanini nipo
Nani kahusika kwa uwepo wangu
Anataka nini hasa
Nini hatima yangu ya baadae

Binadamu anayefanana uwezo na mnyama siku zote.
Yupoyupo tu
Haelewi kwanini yupo
Bora siku ziende
Ilimradi ale na kushiba
Na kulala usingizi
Na kupata marafiki
Siku zinakwenda
Yupoyupo tu

Mimi sikuzote lazima nimshukuru aliyeniweka hapa duniani.
Na bado namtafuta ili nimfikishie asante yangu.
Kwa kipindi nilichokaa hapa duniani hakika nimeflahia maisha
Ni sehemu nzuri ya kuishi.

Huyo ndiye tegemeo langu namba moja.
Na kwakuwa nimetafakari sana na kuuliza uliza kwa walionitangulia sasa hivi nimemtambua.

Na nimefurahi sana kumtambua.
Na nimemwomba mambo mengine mengi tu.
Kwakuwa najua uwezo wake ni zadi yangu na watu na viumbe wote wa Ulimwengu huu.

Hii ndiyo Hekima ambayo haipo katika viumbe wengine isipokuwa Binadamu.
Bila hekima unafanana tu na mdudu Nzi.
Ilimradi yupo anafikiria kushiba na kulala tu basi.
Siku zinaenda.
 
Umejenga nyumba,

Hapo ndani kwako anaingia nyoka,

unawaambia wanao kuna nyoka humu msimsogelee kaeni mbali atawauma,

nyoka anawauma wanao mmoja mmoja,

nyoka uwezo wa kumwondoa unao ila humwui unasubiri siku ya mwisho uchome wote wanao waliumwa na nyoka kwa kosa la kuruhusu nyoka awaume na nyoka mwenyewe.

Hizi hadithi za wachungaji kuna mambo hayapo sawa.

MUNGU yupo ila nina wasiwasi na haya mahubiri tunayohubiriwa.

Kuna uwezekano huyu MUNGU si huyu wanayemuhubiri.
mkuu baada ya kuona kuna nyaka ndani Baba mwenye hekima aliamua kujenga nyumba nyingine na kisha kuwahamasisha wanae kuwa kutokana na nyumba hii kuwa na nyoka basi hamieni nyumba mpya niliyo wajengea ili msipatwe na madhara. Lakini kwa kuwa baba yeye ni mwenye uhuru hawezi mladhimisha mwanae kuwa toka humo ndani kwa lazima badala yake kajenga nyumba nyingine na kuwambia wanae wahaimie huma lakini kawe hawezi walazimisha kuhamia nyumba mpya.

Baada ya mwanadamu kuanguka dhambini Mungu hakuishia kumtazama mwandamu ateketee badala yake aliandaa mpango wa ukombozi. Na ametupatia uhuru wa kuchagua sisi wenyewe either tukombolewe(kuhamia nyumba mpya) au kuendelea kubaki dhambini(Kubaki kwenye nyumba ya zamani yenye nyoka).
 
Wengine hatuna tu option kulingana na vitisho tulivyopandizwa tangu utotoni ila huyu Mungu hatumpendi haswa
Sikushauri uendelee kutokumpenda Mungu lakini angalau nafurahi kujua kuwa humpendi Mungu na unakiri kuwa humpendi. Hii ni hatua moja nzuri sana kwako kwa sababu Mungu kawaida huwa hapendi watu wanafiki, wenye sura mbili. Ninavyoona mimi, wewe una uafadhali mara mia zaidi kuliko yule ambaye ni mnafiki, anajifanya kumpenda Mungu wakati kumbe siyo.
Nakuombea Neema ya Mungu ikuangazie na Mungu akuokoe kama alivyowahi kumuokoa Sauli aalikuwa anataabisha watu wa Mungu kwa kuwaua. Mungu akiujalie hekima yake kwa kiwango kinachohitajika ndani ya roho yako
Ubarikiwe tena na Bwana
 
mkuu baada ya kuona kuna nyaka ndani Baba mwenye hekima aliamua kujenga nyumba nyingine na kisha kuwahamasisha wanae kuwa kutokana na nyumba hii kuwa na nyoka basi hamieni nyumba mpya niliyo wajengea ili msipatwe na madhara. Lakini kwa kuwa baba yeye ni mwenye uhuru hawezi mladhimisha mwanae kuwa toka humo ndani kwa lazima badala yake kajenga nyumba nyingine na kuwambia wanae wahaimie huma lakini kawe hawezi walazimisha kuhamia nyumba mpya.

Baada ya mwanadamu kuanguka dhambini Mungu hakuishia kumtazama mwandamu ateketee badala yake aliandaa mpango wa ukombozi. Na ametupatia uhuru wa kuchagua sisi wenyewe either tukombolewe(kuhamia nyumba mpya) au kuendelea kubaki dhambini(Kubaki kwenye nyumba ya zamani yenye nyoka).
Usilainishe lainishe uhalisia wenye walakini kwa kuusifia kama raia na serikali zetu za duniani, huko ni kuwa mnafiki kwa MUNGU wako...

option ni kuamia nyumba mpya au kuchomwa moto sio kubaki ndani ya nyumba na nyoka kama unavyosema.

Swali: kwanini kuchoma watoto wako moto? Huyo nyoka ana ukuu kiasi gani? Hawezi ondolewa?
 
Katuondolea vipenzi vyeti ametuacha na majonzi yasiyoisha.
kazi yake hainaga makosa,
Mara zote Mungu hutuwazia mema tu(yeremia 29:11-14)
kwa bahati mbaya, kutokana na utoto wetu tumekuwa hatuwezi
kuu'define' wema wa MUNGU , hasa pale tunapopitia changamoto mbalimbali.
Yeye kama baba kwetu amekuwa makini kuhakikisha tunapata kinachotustahili, na
si tunachokihitaji.
Na huu ni mfano ambao hata sisi wababa wa duniani tumekuwa tukifanya kwa watoto wetu.
Wababa wa duniani hapa tuseme ukweli na tujiulize:
Hivi kila tunachowafanyia watoto wetu japo ni kwa faida yao mara zote wanakifurahia?
mfano kuwataka waende shule, kuwataka wakati mwingine wajisomee badala ya kucheza,
kuwataka wahudhurie nyumba za ibaada, kuwataka washiriki kazi mbalimbali za nyumbani,
kuwaadhibu wanapokosea,
nk.(unaweza kufikiria mambo mengi ambayo watoto wengi wakati mwingine wamekuwa
hawayapendi japo yanakuwepo kwa faida yao)
Katika haya wakati mwingine watoto huwaona baba zao kama vile wanawatesa, lakini kadri
akili ya mtoto inavyozidi kukua, huona faida ya mambo haya humwelewa baba na hata kum
shukuru kwa kumwelekeza njia sahihi.
kadri ufahamu wa ki-MUNGU unavyozidi kuongezeka kwa mwanadamu, mwanadamu huyu
huona faida ya kila jambo alitendalo Mungu maishani mwake, na humshukuru(1wathesolanike 5:18)
 
Swali: kwanini kuchoma watoto wako moto?
Mungu hamchukii mwenye dhambi lakini anaichukia dhambi hiyo ndio sababu lazima aiteketeze dhambi.

Swali: Hawezi ondolewa?
Shetani madai yake toka kule mbinguni ni kuwa Mungu ni dikteta. na hivyo basi Mungu angeweza muangamiza moja kwa moja baada ya kuasi kwake lakini jee wale malaika wengine si wangeamini madai ya shetani ni sahihi. Badala yake Mungu kamwacha kwanza ili kila mmoja ajionee matokeo ya kile alichokifanya shetani ili pale atakapo kwenda kutoa hukumu basi kila kiumbe aseme kuwa hukumu zake ni za kweli na haki.
 
mkuu kumbuka wakati Mungu anamuumba mwadamu haikuwa lengo lake mwanadamu kufa ila alimwambia utakapo kula mtu huo ni hakika utakufa.

Na mimi na wewe tunajua kabisa kuwa shetani ndio sababu ya mwanadamu kula lile tunda kwa maana yeye ndie alie washawishi hivyo ni Lucifer anapaswa kulaumiwa juu ya vifo vya wanadamu.

Kwani yeye si mungu alipaswa kujua mbeleni mwanadamu atakuja kosea. Kwanini aliendelea kumuumba. Na kama alikuwa hataki mwanadamu apotee kwanini amruhusu shetani kumshawishi mwanadamu. Na kipindi shetani anamlaghai mwanadamu yeye mungu alikuwa wapi? Kuna maswali bado hayajibiki
 
Mungu hamchukii mwenye dhambi lakini anaichukia dhambi hiyo ndio sababu lazima aiteketeze
Ukikutana na mzazi asiyependa kinyesi na anaua mtoto anayejinyea sababu ana kinyesi utamsifia kuwa hapendi uchafu?

Embu achana na unafiki kwa MUNGU wako.
Toa sababu za msingi ni kwann lazima ndugu zetu, watoto, marafiki walioteleza na kuanguka dhambini wauwawe kikatili kwa moto. Tena moto wa milele

Au na wewe ukifikiria moto wa milele unakosa nguvu inabidi ujifanye kuwa ni sahihi wakiuwawa? Anaona sirini usipoteze muda kumnafikia.
 
Ina
unadhani hata ana shida!!!

yeye mwenyewe katika maagizo yake anasema huwezi kunipenda mimi kama jirani yako unayemwona humpendi,so kama unampenda jirani imetosha.
Hakika mkuu na pia ni watu wengi wanasema wanampenda Mungu lakin kiuhalisia wengi hawana Upendo huo,ukitaka ujue uhalisi wa mtu ni akiwa nyumbani kwake ndio utajua kuwa huyu anampenda Mungu au la
 
Kwani yeye si mungu alipaswa kujua mbeleni mwanadamu atakuja kosea. Kwanini aliendelea kumuumba. Na kama alikuwa hataki mwanadamu apotee kwanini amruhusu shetani kumshawishi mwanadamu. Na kipindi shetani anamlaghai mwanadamu yeye mungu alikuwa wapi? Kuna maswali bado hayajibiki
Huyu akiona maswali magumu anayakwepa. Kuna swali nimemuuliza juu hakulijibu. Ukifuatilia maneno ya kwenye vitabu vya hizi dini halafu ukifanya reasoning unaona kabisa kuna shida mahali.
 
Huyu akiona maswali magumu anayakwepa. Kuna swali nimemuuliza juu hakulijibu. Ukifuatilia maneno ya kwenye vitabu vya hizi dini halafu ukifanya reasoning unaona kabisa kuna shida mahali.

kama yapi embu uliza hapa.

NOTE,hakikisha una nia ya kuelewa sio unataka kubishana.
 
Back
Top Bottom