Wema Sepetu atupwa lupango

"Mheshimiwa hakimu naomba nikachukue barua za kumdhamini kwani nimezisahau kwenye gari nilipoitwa mimi nikaja bila kuzichukua, "alisema mdhamini wa mtuhumiwa wa kwanza

Baada ya muda kupita hakimu Mchauru alisema, "Yaani mahakama imsubiri mtu aenda nyumbani kuchukua barua za kumdhamini mtu, kesi hii naiahirisha hadi hapo itakapotajwa tena Machi 18".
Kauli ya huyo mdhamini imejaa tabia ya kifisadi, ni kauli inayoonyesha jinsi gani ufisadi unavyoweza kuondoa umakini hata kudharau mahakama.

Hakimu mwanzoni aliweza kuingia mtegoni, lakini aliweza kujirudi na anastahili pongezi...!
 
kuna habari kwamba yule miss TZ 2006, Wema Sepetu ameanza kuchanganyikiwa. Wiki iliyopita alimfanyia fujo mpenzi wake wa zamani ambaye ni msanii wa maigizo nchini Steven Kanumba na kuvunja vioo vya gari lake.
inasemekana kwa sasa mrembo huyu anatumia kilevi aina ya Bangi na wazazi wake wameshamshindwa wanamwachia Mungu tu.

Walimshindwa zamani, kudata na bangi hajaanza leo. Angekuwa mzima na ana akili zake timamu asingekwenda kujitembeza nusu uchi mbele ya halaiki ya watu, si utamaduni wa Ki-Zanzibari huo, amabako ana asili nako.

Atembeae uchi ni chizi tu! Mungu amuondoshee!
 
Duh! Yaani laki 5 imekosekana! Ukizingatia na mastaa wote anaokaaga nao karibu?
 
wholly crap...huyu wema hata hao waliompa umiss TZ walichemsha vibaya mno, sijui wanatumia vigezo gani lakini nadhani inabidi vetting ya hali ya juu!

wasidhani wako majuu hapa na hata huko majuu ukifanya ivo ni sheria tu..sasa alishindwa kumlipa mpenzi wake wa zamani hicho kioo cha 1m au ndo alidhani sheia haipo? Angemwuliza TID kwanza....
 
kweli inasikitisha, inamaana hana hata ndugu wa kumdhamini jamani? dah namuonea huruma, anyway wakati wa matatizo ndio utajua nani rafiki wakweli.
 
Kule kwenye ukumbi wa burudani tayali kuna bandiko hili...Itakuwa jambo la busara na mbolea iwapo zitaunganishwa
 
Kamezidi kuwa na skendo kibao, mwanzoni nilidhani barehe lakini sasahivi kakubwa tu kanapaswa acha upuuzi huu mara moja!


halafu vi skendo vyake vyote vya kipuuzii, kweli ni ka binti kazuri sema tu tabia ndio inamuangusha!dhamana yenyewe aliyopewa hata sio ya kivileee hadi impeleke huko, watu wameona ka issue ka kijinga tu.
 
"wazazi wake wameshamshindwa wanamwachia Mungu tu"

hivi ni watu wangapi wanaamini katika hii dhana ya "WAZAZI WAMEMSHINDWA MTOTO". Bahati mbaya sana mimi sio muumini wa dhana hii. Kwanini nasema hivyo, ni kwa sababu chanzo cha kuharibika kwa binti kama Wema sio Kanumba wala hao wengine washikaji na masela wake na wala sio bangi na pombe. Chanzo ni sapoti aliyokuwa anapewa na wazazi wake toka alipoanza kushiriki kwenye masuala ya urembo na uigizaji. This is what i believe. Kwa hiyo wazazi wake waache kusema wanamuachia MUNGU, MUNGU na yeye ana mambo ana-deal nayo. Mengine yako ndani ya uwezo wetu tuyatatue. Kama ingekuwa Wema ana ugonjwa wa Kisukari, Moyo, Kifafa, na mengineyo tungesema tunamwachia MOLA ila sio ili. Kimsingi huyu binti ndie anaonekana kama muhuni tu sijui ana wanaume watano ila yeye ni kwasababu tu yameanikwa hadharani, mbona kun wengine wanao hata kumi ila hawajakamatwa tu na vyombo vya habari.
 
If we have people who believe in God and Pray in JF - then its time to pray for the lady - God changes people - if we pray for her God will change her -

Naamini Mungu anamuwazia mema - na anaweza kumbadilisha akawa dada mzuri tena - siku moja labda - mtumishi - mhubiri wa Mungu - au mwanamke mwema aliye fahari ya mumewe -

LETS PRAY FOR HER - NOTHING IS IMPOSSIBLE FOR GOD

May God comfort her parents, relatives and friends - najua wanaumia wamwonapo mpenzi wao anapotea - :(


Ni kweli anahitaji maombi ya hali ya juu sana.
 
Walimshindwa zamani, kudata na bangi hajaanza leo. Angekuwa mzima na ana akili zake timamu asingekwenda kujitembeza nusu uchi mbele ya halaiki ya watu, si utamaduni wa Ki-Zanzibari huo, amabako ana asili nako.

Atembeae uchi ni chizi tu! Mungu amuondoshee!
Huko Zenj si kuna mashindano ya urembo vilevile?
 
Hata mimi nimejiuliza laki 5 tu na ustaa wote?

Kwa nini hakwenda mahakamani na wazazi au ndugu zake?

Laki tano! Ndugu yangu si mchezo hiyo 5laki unayosema. Usione wanatoka wamependeza,,,, waulize mchana wamekula nini,,,, ndo utashangaa,,, ama hawajala kabisa ama wamekula chipsi dume hapo mta wa pili. Ndo maana ukitaka kuwajua wee agiza bia tu bila chakula uone watu watakavyotapika hewa. Nguo wavaazo ni za mtandao!! Leo ni Wema inafuliwa asubuhi anachukua mwingine naye anampa mwingine. Ndo maana saa ingine ukiangalia mara leo nguo imembana fulani kesho imempwaya yule. Bongo darisalama ndugu yangu! Laki gwara shughuli pevu!!!! Du!
 
Laki tano! Ndugu yangu si mchezo hiyo 5laki unayosema. Usione wanatoka wamependeza,,,, waulize mchana wamekula nini,,,, ndo utashangaa,,, ama hawajala kabisa ama wamekula chipsi dume hapo mta wa pili. Ndo maana ukitaka kuwajua wee agiza bia tu bila chakula uone watu watakavyotapika hewa. Nguo wavaazo ni za mtandao!! Leo ni Wema inafuliwa asubuhi anachukua mwingine naye anampa mwingine. Ndo maana saa ingine ukiangalia mara leo nguo imembana fulani kesho imempwaya yule. Bongo darisalama ndugu yangu! Laki gwara shughuli pevu!!!! Du!

Hii kali kabisa, nguo mtandao !
 
"wazazi wake wameshamshindwa wanamwachia Mungu tu"

hivi ni watu wangapi wanaamini katika hii dhana ya "WAZAZI WAMEMSHINDWA MTOTO". Bahati mbaya sana mimi sio muumini wa dhana hii. Kwanini nasema hivyo, ni kwa sababu chanzo cha kuharibika kwa binti kama Wema sio Kanumba wala hao wengine washikaji na masela wake na wala sio bangi na pombe. Chanzo ni sapoti aliyokuwa anapewa na wazazi wake toka alipoanza kushiriki kwenye masuala ya urembo na uigizaji. This is what i believe. Kwa hiyo wazazi wake waache kusema wanamuachia MUNGU, MUNGU na yeye ana mambo ana-deal nayo. Mengine yako ndani ya uwezo wetu tuyatatue. Kama ingekuwa Wema ana ugonjwa wa Kisukari, Moyo, Kifafa, na mengineyo tungesema tunamwachia MOLA ila sio ili. Kimsingi huyu binti ndie anaonekana kama muhuni tu sijui ana wanaume watano ila yeye ni kwasababu tu yameanikwa hadharani, mbona kun wengine wanao hata kumi ila hawajakamatwa tu na vyombo vya habari.

Ndugu yangu Sipo,

Wala usiulize wazazi wake maana i know the family. They were my neighbours and its a shame that they are not owning up to their own mistakes, Shame on them!
Kwa kweli ni story ndefu ila kwa ufupi, wazazi wake pia wana walakini fulani. Wasijikoshe kwenye magazeti au kwa watu. this was expected kwa jinsi walivyokuwa wanawalea watoto wao especially huyo Wema.
 
Mungu wa mbinguni naomba msaidie sana Wema,naomba watu badala ya kumlaumu tumwombee Mungu ambadilishe,na kwa maombi hayo naamini atabadilika,kwani si yeye peke yake sio mkamilifu hata wewe pia,usiangalie leo fikiria na kesho kwako.WEMA nakuombea sana Mungu akubadilishe na kukusaidia maishani mwako naamini iko siku utapata heshima iliyopotea na utakuwa na familia bora na mume mzuri mwenye maadili mema na kuzaa watoto wazuri wenye tabia nzuri.na ukitoka huko nenda nyumbani kawaangukie wazazi wako jua hao ni Mungu wa pili.NAKUPENDA SANA MDOGO WANGU!
 
Mungu wa mbinguni naomba msaidie sana Wema,naomba watu badala ya kumlaumu tumwombee Mungu ambadilishe,na kwa maombi hayo naamini atabadilika,kwani si yeye peke yake sio mkamilifu hata wewe pia,usiangalie leo fikiria na kesho kwako.WEMA nakuombea sana Mungu akubadilishe na kukusaidia maishani mwako naamini iko siku utapata heshima iliyopotea na utakuwa na familia bora na mume mzuri mwenye maadili mema na kuzaa watoto wazuri wenye tabia nzuri.na ukitoka huko nenda nyumbani kawaangukie wazazi wako jua hao ni Mungu wa pili.NAKUPENDA SANA MDOGO WANGU!

Taib and Ameen.

Naona majority ya watu hapa wanashangilia kiaina kuona mtu anapatwa na majanga. Sijui inawasaidia nini, hawajui kuwa mtu anapotupwa selo, hiyo inamaanisha gharama za lile basi la kijani na 'utunzaji' vinakula kwako, via kodi yako.

Lets get back to work.
 
Mungu wa mbinguni naomba msaidie sana Wema,naomba watu badala ya kumlaumu tumwombee Mungu ambadilishe,na kwa maombi hayo naamini atabadilika,kwani si yeye peke yake sio mkamilifu hata wewe pia,usiangalie leo fikiria na kesho kwako.WEMA nakuombea sana Mungu akubadilishe na kukusaidia maishani mwako naamini iko siku utapata heshima iliyopotea na utakuwa na familia bora na mume mzuri mwenye maadili mema na kuzaa watoto wazuri wenye tabia nzuri.na ukitoka huko nenda nyumbani kawaangukie wazazi wako jua hao ni Mungu wa pili.NAKUPENDA SANA MDOGO WANGU!
Unajua kila kitu kitaenda vizuri endapo utakuwa mtulivu na nidhamu katika kufanya yale mema yanayostahili wewe kuyafanya;unajua huyu binti baada tu ya kupata U-Miss TZ ndiyo akapagawa badala ya kuongeza nidhamu na utulivu maradufu ili aweze kutukeleza yanayotakiwa katika maisha.
Unajua,hata kama hujitambui basi waone watu wenye busara zao ili wakupatie ushauri.Sijui kama hata alikuwa anajali katika hayo!
 
Taib and Ameen.

Naona majority ya watu hapa wanashangilia kiaina kuona mtu anapatwa na majanga. Sijui inawasaidia nini, hawajui kuwa mtu anapotupwa selo, hiyo inamaanisha gharama za lile basi la kijani na 'utunzaji' vinakula kwako, via kodi yako.

Lets get back to work.

Nashukuru kwa kulitambua hili,inabidi watu wabadilike wote tumeumbwa na Mungu ni vizuri kusaidiana kuliko kuchekana,je wafahamu laweza kukupata kubwa zaidi ya hili katika familia au ukoo wako kwa ujumla.TUBADILIKE!
 
Unajua kila kitu kitaenda vizuri endapo utakuwa mtulivu na nidhamu katika kufanya yale mema yanayostahili wewe kuyafanya;unajua huyu binti baada tu ya kupata U-Miss TZ ndiyo akapagawa badala ya kuongeza nidhamu na utulivu maradufu ili aweze kutukeleza yanayotakiwa katika maisha.
Unajua,hata kama hujitambui basi waone watu wenye busara zao ili wakupatie ushauri.Sijui kama hata alikuwa anajali katika hayo!
Hivi mtu hajitambui atawezaje kutafuta mtu amshauri kama si wewe unaeona hajitambui ndio umtafute na kumpa ushauri....?acheni lawama zisizo na msingi kwani wangapi wana machafu ambayo hata ukiambiwa, nini kuona utaumia sembuse Wema jamani, kinachotakiwa ni msaada hapa lawama wekeni kando,na wale wanaoona anavuta bangi wamsaidie kumpeleka kwenye vitengo vinavyohusika na maswala hayo apate msaada,kusaidia mtu si lazima awe maskini hata Wema ni maskini wa tabia anastahili kusaidiwa.
 
Huyu Wema anaonewa. Kwanza wanasema ni mwehu,halafu wanamfunga. Huyu alishinda Miss Ta nzania bila mizengwe.












It is time for those who say they have control over things to pass it to someone who really does.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom